Tuesday, March 19, 2013

Magazeti ya leo jumanne ya 19th March 2013



RIPOTI MAALUMU KUHUSU KESI YA KUPINGA MATOKEO YA UCHAGUZI KENYA

Taarifa kutoka 254 zinasema tayari kesi iliyowasilishwa na mrengo wa CORD imesajiliwa na mahakama ya upeo nchini Kenya na tayari jopo la majaji watano limeteuliwa kusikiliza kesi hiyo akiwemo rais wa Mahakama ya Upeo Dr. Willy Mutunga huku msajili wa Mahakama akithibitisha kwamba watakaosalia kusikiliza kesi hiyo ni majaji sita kinyume na kawaida ambapo huwa ni saba.

Kesi inatarajiwa kuanza kusikilizwa leo march 19 2013 Nairobi kenya na endapo mrengo wa CORD utatoa uthibitisho kwamba uchaguzi ulikua na dosari, duru ya pili ya uchaguzi itaandaliwa chini ya siku 60 ambapo mrengo wa CORD unawakilishwa na mawakili kama Mutula Kilonzo na Moses Wetangula ukidai tume huru ya uchaguzi haikuzingatia mipangilio wa uchaguzi kama vile kutambua wapiga kura kupitia mitambo ya kielektronik.

TUNDULISU AFUNGUKA KUHUSU SAKATA LA KUJIFUNGIA CHOONI

 ZIPO taarifa kwamba Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu, wiki iliyopita alijifungia chooni kukwepa waandishi wa habari waliotaka kauli yake juu ya video hatari ambayo inadaiwa Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa chama hicho, Wilfred Rwakatare, alirekodiwa akieleza njama za uhalifu.

Tundu ambaye ni Mnadhimu wa Kambi ya Upinzani Bungeni, amesema kuwa maelezo yaliyotolewa kwamba alijificha chooni kwa muda wa saa mbili si kweli, kwani hawezi kufanya hivyo.

“Jamani mimi na umri wangu huu nawezaje kuwakimbia waandishi wa habari? Siku zote mimi nafanya kazi na waandishi wa habari,” alisema Lissu na kuongeza:

RIPOTI MAALUMU TOKA MAHAKAMA YA KISUTU ALIKOSHITAKIWA LWAKATARE WA CHADEMA

HATIMAYE Mkurugenzi wa Mashitaka nchini, Dk Eliezer Feleshi amemfikisha katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Usalama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Wilfred Lwakatare na mwenzake kwa makosa ya ugaidi.

Mbali na Lwakatare mshitakiwa mwingine ni Ludovick Rwezaula Joseph ambao wanatetewa na mawakili wa kujitetemea Profesa Abdallah Safari, Tundu Lissu na Nyaronyo Kicheere.

Washitakiwa hao wakifikishwa jana saa mbili asubuhi mahakamani hapo chini ya ulinzi mkali wa askari kanzu walikuwa wakiongozwa na Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Mkoa wa Ilala, Duwani Nyanda na kuifadhiwa nyuma ya jengo la mahakama hiyo tayari kwaajili ya kufikishwa kizimbani kosomewa mashitaka yanayowakabili.

LWAKATARE ASOMEWA MASHITAKA YA UGAIDI

                       Lwakatare akionesha alama ya vidole viwili wakati akipelekwa kizimbani.
          Wanachama na mashabiki wa Chadema wakionesha alama ya vidole viwili kabla ya kesi kuanza.

LULU MICHAEL ALIKUMBUKA PENZI LA STEVEN KANUMBA.....

Wakati zikiwa zimebaki wiki chache tu hadi kifo cha Stephen Kanumba kitimize mwaka mmoja, aliyekuwa mpenzi wake, Elizabeth Michael aka Lulu kwa mara ya kwanza leo ameandika ujumbe kuhusiana na jinsi anavyomkumbuka.

Lulu aliachiwa kwa dhamana mwezi January mwaka huu baada ya kukaa mahabusu kwa takriban miezi minane kufuatia kukamatwa kwa kuhusika na kifo cha Kanumba.
Lulu ambaye hivi karibuni amekuwa akitweet mara kwa mara ameandika:

“Ulikuwa zaidi ya baba,kaka,mpenzi,mume,ndugu,rafiki….sitoacha kukulilia katika maisha yangu yote!!R.I.P daddy angu STEVEN KANUMBA.”

Akiambatanisha na picha ya Kanumba, Lulu ameongeza, “I will alwayz love u daddy angu!”

Saturday, March 16, 2013

Uchaguzi wa Kamati za Bunge:Vita Lowassa,Membe yakolezwa

                                              Mbunge wa Jimbo la Monduli, Edward Lowassa

Dar es Salaam. Ofisi ya Bunge jana ilitangaza majina ya wenyeviti na makamu wapya wa Kamati za Kudumu za Bunge huku Mbunge wa Jimbo la Monduli, Edward Lowassa akichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

Kuchaguliwa kwa Lowassa kuongoza kamati hiyo kunaibua upya vita kati yake na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, kutokana na wote kutajwa kutaka kugombea urais katika uchaguzi mkuu ujao mwaka 2015. Awali

RAFIKI WA RAILA ODINGA AMPA TALAKA MKEWE KWA KUMSIFIA UHURU KENYATTA KUWA NI HANDSOME

 Rafiki wa karibu wa waziri mkuu wa Kenya Raila Odinga Jumatatu hii anadaiwa kumpa talaka mke wake baada ya kumsifia Rais mteule wa Kenya Uhuru Kenyatta ni ‘handsome’ mbele yake.

Kwa mujibu wa mtandao mmoja wa Kenya, mwanasiasa huyo wa chama cha CORD anayetokea magharibi mwa Kenya, alikuwa akitazama taarifa ya habari akiwa na mke wake na ndipo alipoonekena Uhuru Kenyatta kwenye TV akizungumza na wawakilishi wa nchi mbalimbali nyumbani wake.

AFYA YA LWAKATARE NI MBAYA.....BADO ANASHIKILIWA NA POLISI

Dar es Salaam. Hali ya afya ya Mkuu wa Usalama na Ulinzi wa Chadema, Wilfred Lwakatare anayeshikiliwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za kuwahamasisha watu kufanya vitendo vya uvunjifu wa amani kupitia mitandao ya jamii, imezorota.

Gazeti hili imemshududia jana akizungumza na wakili wake Nyaronyo Kicheere, huku akilalamikia hali yake kuwa si njema kutokana na ugonjwa wa kisukari alionao.

Alikuwa akitembea kwa kujivuta, na alidai kuwa ameshindwa kula chakula inavyotakiwa.

MGOGORO WA UCHINJAJI NYAMA BAINA YA WAKRISTOB NA WAISLAM HUKO GEITA WAPATA SULUHISHO

Baadhi ya viongozi wa Dini ya Kiislam na Kikristo kutoka Geita wamekaa pamoja na kuondoa tofauti zao hususan katika suala la uchinjaji wa nyama kwa ajili ya kitoweo, miongoni mwa makubaliano waliyofikia ni nyama yoyote inayochinjwa kwa ajili ya biashara wachinje waislamu lakini kwenye sherehe zinazowahusu waislam wachinje waislamu na sherehe zinazowahusu wakristo wachinje wakristo wenyewe. Hivyo sherehe zozote za kidini wasiingiliane kwenye taratibu za kidini kwa kila mmoja.

Shehe Ismail Ibrahim na Mchungaji Isaya Ikiri

Magazeti ya leo jumamosi ya 16th March 2013

                                             


Friday, March 15, 2013

TCRA YAKATAA KURUDISHIA MFUMO WA ZAMANI WA ANALOGIA....

 Dar es Salaam. Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imesema haitarudi nyuma kwenye suala la kutumia mfumo wa matangazo kupitia njia ya dijitali na kwamba mfumo huo utaendelea kutumika.

Kauli ya TCRA imekuja siku moja baada ya wamiliki wa vituo vya utangazaji vya televisheni nchini kutishia kusitisha kurusha matangazo ndani ya mwezi mmoja kuanzia sasa kutokana na kushindwa kumudu gharama za uendeshaji.

Mwenyekiti wa Chama cha Wamiliki wa Vyombo vya Habari Tanzania (Moat), Reginald Mengi juzi alisema hakuna haja ya kurusha matangazo kwa hasara kwani watangazaji wamesitisha kutoa matangazo kwa sababu wananchi wengi hawana ving’amuzi. Licha ya Moat kutoa kauli hiyo juzi, Mkurugenzi wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Profesa John Nkoma alisisitiza kwamba TCRA haiwezi kurudi nyuma katika suala hilo kwani mfumo huo utaendelea kutumika.

WAGANGA 12 WAJITOKEZA KUPAMBANA NA "JINI MAHABA" LINALOMSUMBUA LADY JAYDEE

WAGANGA wanaodai kuwa ni wataalam na wana uzoefu wa kupambana na jini mahaba linalomsumbua Mwanamuziki Judith Wambura ‘Lady Jaydee’, wamejitokeza huku kila mmoja akiomba apewe nafasi ya kumtibu bure.

Mmoja wa wataalam hao aliyejitambulisha kwa jina la Jumaa wa Magomeni, Dar alisema: “Nimesoma habari kuhusu Jide, mimi naweza kumtibu tena bure, mpe namba yangu na mwambie anipigie.”

Mwingine ambaye hakupenda jina lake liandikwe alisema: “Nimesikitika sana kusoma hii habari ya huyu msanii Lady Jaydee, kwa kifupi naweza kumtibia free of charge.”

Kufuatia maombi ya wataalam hao, mwandishi wetu alijitahidi kumtafuta Jide bila mafanikio lakini juzikati kupitia kipindi chake cha Diary ya Lady Jaydee alionekana akipewa matibabu na ustaadhi mmoja, mazingira yanayoashiria kuwa huenda mambo yametulia.

BENARD MEMBE AGEUKA MBOGO BAADA YA KUHUSISHWA NA UTEKAJI WA ABSALOM KIBANDA

 Ifuatayo ni kauli iliyotolewa na Waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa Bernard Membe kuhusu kilichoandikwa na gazeti la Mtanzania march 13 2013 toleo namba 7255.
 “SAKATA LA KUTESWA KWA KIBANDA: Membe atajwa” na kwamba eti mimi ninahusika na vitendo vya kikatili na unyama alivyofanyiwa Mhariri Mtendaji Mkuu wa kampuni ya New Habari, Bw. Absalom Kibanda”

“Nimeshangazwa na kusikitishwa sana na habari hizo na ningependa kuwahakikishia Watanzania wenzangu kwamba sijahusika, sihusiki na sina sababu ya kuhusika kwa namna yoyote ile. Sina nia, genge wala fedha za kufanya shughuli kama hiyo.

 Katika maisha yangu yote, sijawahi kugombana naye na hajawahi kunifanyia ubaya wowote. Kwa kifupi, sina uhasama na Bw. Absalom KIbanda”
.

"VIDEO YA LWAKATARE NI FEKI,,," HII NI KAULI YA DR. SLAA

  KATIBU  Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Wilbroad Slaa amezungumzia video aliyorekodiwa Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chama hicho, Wilfred Lwakatare na kusema ni ya kutungwa na vyombo vya dola.

Dk. Slaa pia amelituhumu Jeshi la Polisi kufanya mchezo mchafu kwa maslahi ya kisiasa.

Alikuwa akizungumza na waandishi wa habari Makao makuu ya chama hicho kufafanua suala la kushikiliwa kwa Lwakatare.