
NYOTA ya Tanzania katika sekta ya Utalii imeendelea kung’ara zaidi badaa ya hivi karibuni kuchaguliwa kuwa ndio nchi bora kwa watu mbalimbali kuweza kufanya safari za kitalii miongoni mwa nchi barani Afrika.
Kwa mujibu utafiti uliofanywa na kutolewa hivi karibuni na katika mtandao wa Kampuni ya marketplace kwa ajili ya safari za Africa (marketplace for African safari tour)
Tanzania imepata kura nyingi zaidi ziliyotolewa kama maoni ya watu kufuatia utafiti huo ambapo Safaribooking .com ilifanya mchanganuo huo kwa kupitia maoni 3061ya zaidi ya watalii na wasafiri waliohusishwa katika utafiti huo na kuhitimisha kuwa katika nchi zote zilizopendekezwaa barani Africa,Tanzania ni zaidi.