Monday, July 16, 2012

WACHEZAJI WAPYA WA MANCHESTER UNITED WALIYOZAWADIWA MAGARI.

                                                    Shinji Kagawa na Nick Powell
Mjapan Shinji Kagawa amezaliwa miaka 23 iliyopita na club yake ya mwisho kuichezea ni Borussia Dortmund na kaifungia magoli 21 kwa miaka miwili aliyokaa nayo na amezichezea timu za taifa toka mwaka 2006, Powell yeye ameichezea Crew Alexandra kwa miaka miwili na kuondoka na magoli yake 16, Timu za taifa za England amejiunga nazo toka 2009.
                                        Waandishiwa habari wakipata picha

Ebenezer Hair Food Products Registered By Tanzania Food and Drugs Authority (TFDA).

Tunapenda kuwajulisha wateja wote wa nje na ndani ya Tanzania kua Ebenezer Hair Food, Ebenezer Shampoo, Ebenezer Conditioner na Ebenezer 2 in 1 Shampoo Conditioner vyote vimeshasajiliwa na Tanzania Food and Drugs Authority (TFDA).

Tunaahidi kuendelea kuthamini nywele zetu, nywele za Mwafrika kwa kuendelea kukuwezesha kuzipa lishe na matunzo yanayotakiwa.

Usisite kutumia Ebenezer Hair Food kwa nywele zako. Kwa waliopo USA unaweza kununua online at www.ebenezer-arisebeauty.com Kwa waliopo Tanzania jipatie Ebenezer Hair Food toka ARISE Beauty Supply @0714311283.

                                Asanteni na karibuni

Dr Asha Rose Migiro Ateuliwa Kuwa Mjumbe Maalum Wa Katibu Mkuu Umoja Wa Mataifa

Former United Nations Deputy Secretary-General from 2007 to 2012 Dk Asha-Rose Migiro

United Nations Secretary-General Ban Ki-Moon has appointed Asha-Rose Migiro as his Special Envoy for HIV/AIDS in Africa.  “Ms  Migiro’s experience in responding to AIDS as UN Deputy Secretary General, combined with her many years as an advocate for health and social justice in Africa, make her uniquely qualified for this important role,” said  Mr Ban. Ms Migiro served as the United Nations Deputy Secretary-General from 2007 to 2012. In that role, she was integrally involved in promoting the AIDS response globally and within Africa, with special emphasis on reducing the vulnerability of women and girls and ensuring the rights of people living with HIV.

“I am honoured to accept this appointment at this crucial moment in the African AIDS response,” said Ms Migiro. “A decade ago, HIV in Africa was almost entirely an epidemic of despair. Today, we celebrate progress  against AIDS that we never thought possible. Now is the time to take our  efforts to a new level––I am committed to the Secretary-General’s vision  that the beginning of the end of AIDS in Africa starts now.” Ms Migiro served as Tanzania’s Minister of Foreign Affairs and International Cooperation from 2006 to 2007—the first woman to hold that position since the country’s independence.

 She was previously the Minister  for Community Development, Gender and Children for five years. Prior to  Government service, she pursued a career in academia, and, served as a member of Tanzania’s Law Reform Commission in 1997 and as a member of the United Nations Committee on the Elimination of Discrimination against Women in 2000. “I look forward to working closely with Ms Migiro in helping African countries reduce their AIDS dependency and provide universal access to HIV prevention, treatment, care and support services,” said UNAIDS Executive  Director Michel SidibĂ©. “Her experience and leadership will promote African ownership of the AIDS response at the highest levels and reduce the inequities of people affected by AIDS in the continent.” Africa remains the continent most affected by HIV. In 2010, about 68% of  all people living with HIV resided in sub-Saharan Africa. The region also accounted for 70% of all new HIV infections worldwide.

Kwa Wale Wanaotafuta Ajira Kwenye Database Maalumu Ya Serikali


Kwa wale wanaotafuta Ajira au kuhitaji kuweka CV zao kwenye Database Maalumu ya Serikali basi watembelee  Tovuti hiyo, bado inaendelea na matengenezo madogo madogo lakini utaweza kuweka taarifa na mambo mengine pamoja na kutafuta kazi zinazohusiana na Serikali ya Tanzania. http://www.ajira.go.tz

Magazeti ya leo 16th July 2012


Benki KKKT Yalizwa 250m Kupitia ATM





WATEJA zaidi ya 50 wa Benki ya Uchumi Commercial Bank Ltd (UCB) ya Dayosisi ya Kaskazini ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) wanasakwa na polisi kufuatia wizi wa karibu Sh250 milioni.

Vyanzo vya kuaminika vilidokeza kuwa ingawa taarifa zilizofunguliwa polisi na menejimenti ya UCB zinaonyesha kiasi kilichoibwa ni Sh224 milioni, lakini kinaweza kufikia Sh250 milioni kadri uchunguzi unavyoendelea.

Benki hiyo iliyoanzishwa mwaka 2005 baada ya kupatiwa leseni namba CBA 00031 na Benki kuu ya Tanzania (BoT), inamilikiwa na Watanzania wapatao 330,000 ambao ni waumini wa dayosisi hiyo.

Habari za uhakika zilizolifikia Mwananchi zilisema wizi huo ulifanyika baada ya kuparanganyika kwa mfumo wa kompyuta uliounganishwa na mashine za ATM.

Taarifa nyingine zilisema wizi huo ulitokana na baadhi ya wateja kuusoma mfumo wa kompyuta hiyo na kugundua kuwa kuna nyakati za usiku huchanganyikiwa na kutoa salio lisilo sahihi la wateja.

“Kilichotokea ni kuwa kuna watu walivujisha siri kuwa nyakati za usiku sana ukichomeka kadi kwenye hiyo ATM inatoa pesa hovyo hovyo hata kama hauna salio la kutosha”kilidokeza chanzo chetu.

Uchunguzi wa Mwananchi ulibaini kuwa wateja wa benki hiyo wapatao 50 walijihusisha na wizi wa fedha hizo kupitia ATM hiyo na tayari polisi imeanzisha uchunguzi maalumu wa kuwasaka.

Habari hizo zimedai kuwa baada ya kugundulika kwa dosari katika mfumo huo wa kompyuta za ATM katika benki hiyo, baadhi ya wateja walianzisha kuchukua fedha muda mfumo huo unapoharibika.

“Sio pesa zilizoibwa mara moja hapana yaani unakuta leo anatoa 500,000 kesho hivyo hivyo na ilikuwa ni wateja tofauti tofauti waliokuwa wamegundua siri hiyo”alidokeza mtumishi mmoja wa UCB.

Baadhi ya wanasheria walidai zipo changamoto nyingi katika kesi za aina hiyo hasa katika kuthibitisha kama wakati mtuhumiwa anatoa fedha hizo katika ATM,alikuwa amekula njama ya kutenda kosa hilo.

Meneja mkuu wa Benki hiyo, Angela Moshi alipoulizwa alikiri kuwapo kwa tukio hilo, lakini akasema hakuwa katika nafasi nzuri ya kulielezea kwa vile alikuwa akielekea kanisani kwa ajili ya ibada.

"Naomba uje kesho (leo)tutazugumza vizuri tu juu ya hilo jambo nitakupa taarifa vizuri tu unajua leo ni siku ya ibada na sasa hivi naingia kanisani kwa ajili ya ibada"alisisitiza Meneja mkuu huyo jana.

Kwa upande wake, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro,Robert Boaz alipoulizwa na gazeti hili juzi alisema“ni kweli hilo tukio lipo kwa maana ya wateja ‘wame overdraw’ (wametoa zaidi) kutoka kwenye akaunti zao na uchunguzi wa tukio hilo unaendelea”alisema Kamanda Boaz.
Chanzo:  http://www.mwananchi.co.tz/biashara.

Friday, July 13, 2012

Rais Jakaya Mrisho Kikwete Akishiriki kikao Maalumu.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akishiriki katika kikao maalumu cha maandalizi ya mkutano wa Commonwealth Partnership for Technology Management (CPTM) kwenye makao makuu ya CPTM inayojiandaa kwa mkutano wake mkuu wa Global 2012 International Smart Partneship Dialogue unaotarajiwa kufanyika mwezi Mei Mwakani jijini Dar es salaam.

Netherland Kuwekeza Sekta Ya Afya Nchini

Kaimu mgaga mkuu wa serikali Dkt. Donan Mmbando akizungumza na ujumbe wa Biashara na Uwekezaji katika huduma za afya kutoka nchini Netherland  mara baada ya ujumbe huo kuwasili makao makuu ya Wizara ya Afya na Ustawi  wa jamii jana jijini Dar es Salaam.
 Watendaji wakuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii wakiwa katika picha ya pamoja na ujumbe wa Biashara na Uwekezaji katika huduma za afya kutoka nchini Netherland .

Dr.Slaa,Mbowe Na Lema Wakamatwa

Kwamba wanashikiliwa Central Dar.Tutawaletea habari kamili tutakapokuwa tumejuwa sababu ya wao kukamatwa.labda madai yao kuuawa na kukataa kupeleka madai polisi.

Taarifa Kwa Umma Juu Ya Hali Ya Utendaji Wa Viongozi Wa Bunge

CIVIL AND POLITICAL RIGHTS WATCH
The Citizens’ Parliament watch
Plot 522 Block E, Sinza Palestina, P. O. Box 522, Dar Es Salaam,
Telephone:0784417307,E-mail:ed.civilrights@yahoo.com; marcossy@yahoo.com Dated 18th JUNE, 2012.

TAARIFA KWA UMMA JUU YA HALI YA UTENDAJI WA VIONGOZI WA BUNGE
Taarifa hii ni matokeo ya ufuatiliaji wa shughuli za Bunge na mijadala ya Wabunge juu ya mahitaji ya umma kwao kwenye maendeleo, uongozi, kuimarisha utawala bora, uwajibikaji wa serikali na haki za binadamu na kuimarisha usimamizi wao kwa serikali kupitia mijadala yao katika vikao vya Bunge. Taarifa hii inahusika na utendaji wa viongozi wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mwaka 2011.

Kwa Ujumla:
Kumekuwa na upendeleo wa vyama katika kujadili na kuchangia hoja na kuonekana Mh Spika na Wenyeviti wa vikao kutumia vibaya kanuni za bunge kuwadhibiti wabunge kulingana na vyama vyao. Mfano ni pale Mh Spika alipomzuia Mh Tundu Lissu kumwuliza swali Mh Mizengo Pinda juu ya mauaji ya raia mikononi mwa vyombo vya dola kwa madai kuwa kuna kesi mahakamani juu ya hoja hiyo. Pamoja na Mh Lissu kujitahidi kufafanua tofauti zilizopo kati ya kesi inayomkabili yeye na wenzake na hoja anayoiulizia, bado Mh Spika ameendelea kuizuia hoja hiyo. Kulingana na maoni ya wabunge 36, Watendaji 22, wachambuzi 11 na wananchi 48 waliohojiwa, ubora wa uongozi wa bunge kwa mwaka 2011 ni kama ilivyo hapa chini:


NAFASI JINA SIFA YA KIPIMO ALAMA WASTANI MAONI YA WASHIRIKI
1 NDUGAI,
JOB
YUSTINO USIKIVU KWA WABUNGE 2.5 Amejitahidi sana kukwepa upendeleo wa kisiasa na kuilinda serikali; haoneshi utashi wake kumiliki mamlaka aliyopewa na Kanuni za Bunge anapoongoza vikao.
UZINGATIAJI KANUNI 2.625
UPENDELEO WA KISIASA 2.5625
UZINGATIAJI HOJA 2.375
USHABIKI BUNGENI 3
JUMLA KIWANGO 13.0625
WASTANI 2.6125
2 SIMBACHAWENE, USIKIVU KWA WABUNGE 2.125 Msikivu kwa Wabunge haswa wenye HOJA zenye maslahi kwa Taifa; Amejitahidi sana kukwepa upendeleo wa kisiasa na kuilinda serikali; Anayumbishwa na makundi au siasa.
GEORGE
BONIFACE UZINGATIAJI KANUNI 2.3125
UPENDELEO WA KISIASA 3.28125
UZINGATIAJI HOJA 2.09375
USHABIKI BUNGENI 3.4375
JUMLA KIWANGO 13.25
WASTANI 2.65
3 MAKINDA,
ANNE
SEMAMBA USIKIVU KWA WABUNGE 3.03125 Imara kwenye kanuni na kuzingatia hoja; Anayumbishwa na ushabiki kisiasa; si msikivu kwa wabunge.
UZINGATIAJI KANUNI 2.65625
UPENDELEO WA KISIASA 3.46875
UZINGATIAJI HOJA 2.75
USHABIKI BUNGENI 2.9375
JUMLA KIWANGO 14.84375
WASTANI 2.96875 Anajitahidi sana kuzingatia kanuni; Anayumbishwa na makundi kisiasa; si msikivu kwa wabunge.
4 MHAGAMA,
JENISTER
JOAKIM USIKIVU KWA WABUNGE 3.21875
UZINGATIAJI KANUNI 3.15625
UPENDELEO WA KISIASA 3.5
UZINGATIAJI HOJA 3.53125
USHABIKI BUNGENI 3.3125
JUMLA KIWANGO 16.71875
WASTANI 3.34375
5 MABUMBA,
SILVESTER
MASELE USIKIVU KWA WABUNGE 4.25 Haoneshi ushabiki wa wazi wa kisiasa; hushindwa kuhimili mivuto ya makundi na upendeleo wa kisiasa; Si msikivu kwa wabunge.
UZINGATIAJI KANUNI 4.25
UPENDELEO WA KISIASA 3.78125
UZINGATIAJI HOJA 3.90625
USHABIKI BUNGENI 3.25
JUMLA KIWANGO 19.4375
WASTANI 3.8875

ANGALIZO LA VIWANGO:
1.00 – 1.49 = Uongozi Mzuri Sana,
1.50 – 2.49 = Uongozi Mzuri
2.50 – 3.49 = Uongozi wa Wastani
3.50 – 4.49 = Uongozi Dhaifu
4.50 – 5.0 = Uongozi Dhaifu Sana

Kwa Ujumla
Taarifa hii imeonesha mapungufu kadhaa kwenye uongozi na utendaji wa kazi wa viongozi wa Bunge na hivyo kutoa changamoto kwa viongozi wa Bunge na wabunge kuimarisha utendaji wao iwapo wangependa kutekeleza wajibu wao kwa jamii. Ni matarajio yetu kuwa wabunge watatumia taarifa hii kuimarisha mjadala wa bajeti ya 2012/13 unaoendelea, ikiwa ni pamoja na kendeha na kusimamia vema vikao na mijadala ya Bunge na kutoa changamoto kwa utendaji wa serkali kwa maslahi ya jamii.

Tunakumbusha pia kuwa bado Bunge limeendelea kutumia muda vibaya kwa wabunge kuendeleza vijembe, kebehi, shukrani, pongezi na salamu. Hata baada ya miaka miwili sasa baada ya Uchaguzi na Serikali kuundwa bado wabunge wameendelea kutoa shukrani kwa Rais, wapiga kura wao na wengineo. Matumizi haya ya muda yanapunguza mijadala na mwendelezo wa ushiriki wa wabunge kwa ufasaha.

Mapendekezo
1. Ipo haja ya wabunge kujiangalia kwa karibu uwezo na utayari wao kujadili maswala ya maslahi kwa taifa bila kuingiza ushabiki na maslahi binafsi.
2. Iangaliwe upya akidi ya wabunge katika kupitisha hoja (angalau iwe robo tatu na sio nusu ya wabunge kama ilivyo sasa).Hii iendane na haja kwa Mhe, Spika kujiridhisha bila kuacha shaka juu ya idadi ya kura za wabunge kwenye hoja husika, na haswa walioshiriki mjadala baadala ya kuingia kwa ajili ya kupiga kura tu;
3. Spika atumie mamlaka na kanuni za Bunge ili kudhibiti maudhui, mantiki na maana ya mijadala ya Bunge bila kuathiri maslahi ya taifa. Katika hili Mhe Spika, Naibu na Wenyeviti wa Bunge,wana dhamana ya kuhakikisha ushabiki wa kisiasa haupati nafasi kuvuruga Bunge
4. Tunaona ipo nafasi kubwa kwa Spika kusaidia na kuelekeza bunge ili lifanye kazi zake vizuri zaidi. Spika atumie nafasi hii baadala ya yeye kuangukia kwenye ushabiki na kuilinda serikali.

Imetolewa na Taasisi ya Raia ya Haki za Kisiasa na Mwenendo wa Bunge,

CIVIL AND POLITICAL RIGHTS WATCH
Marcossy Albanie
Mkurugenzi Mtendaji

HAWA NDIO WATOTO WENGINE WA P DIDDY.

                                               Jessie, D’Lila na Chance.
According to blog ya Necole ni kwamba jana ilikua siku ambayo Rapper/Producer wa longtime P DIDDY alipata time ya kuspend na watoto wake mapacha wa miaka mitano baada ya mama yao ambae ni longtime girlfriend wake (Kim Porter) kukubali manake alikua hataki kabisa mapacha wake wakutane hasa na dada yao mwingine aitwae Chance ambae alizaliwa miezi mitano kabla ya mapacha hao lakini kwa mama mwingine ambae ni Sarah Chapman.

P Diddy ni miongoni mwa mastaa wenye watoto wengi lakini ndoa bado haijafungwa, Diddy tayari mpaka sasa ameshapata watoto na wanawake zaidi ya watatu huku November 4 mwaka huu akifikisha umri wa miaka 43.
Pamoja na kwamba ana watoto wengi na kila mmoja ana mama yake, Diddy amevunja rekodi ya kuwa baba anaetimiza mahitaji yote… hataki lawama au mtoto wake kupata tabu anawajibika kila anapohitajika, hii ilikua ni siku nyingine wakati wa birthday ya Chance.

                          PichaYa chini Mama (Sarah Chapman) mtoto na baba.

Huyu wa katikati tena ni mtoto wake mkubwa sasa anaitwa Justine

Thanks Millard Ayo Blog.

MADAKTARI KUANDAMANA TENA?

                              Dr Rodrick Kabangila upande wa kwanza kulia.
Kutokana na kusitishwa kwa ujasili wa madaktari zaidi ya 400 waliokuwepo kazini na wale wa mafunzo kwa vitendo Chama cha Madaktari (MAT) kimesema kimeandaa maandamano ya amani yatakayoshirikisha wanachama wake nchi nzima lengo likiwa ni kudai haki zao.

Katibu mkuu wa MAT Dr Rodrick Kabangila amesema tangu kuanza kwa vuguvugu la mgomo wa Madaktari, mambo mengi  yamekua yakifanywa kinyume na taaluma yao hivyo wameamua kukutana kesho ili kupanga maandamano.

Amesema lengo jingine la maandamano ya amani ni kuiomba serikali kuunda tume huru kufuatilia ishu ya kutekwa na kuteswa kwa Dr Ulimboka ambae kwa sasa yuko Afrika Kusini akipatiwa matibabu kutokana na huo mkasa pamoja na kupinga dhuluma na uonevu unaoendelea dhidi ya taaluma ya udaktari na madaktari wenyewe.

KAULI YA CHAMA CHA WALIMU KUHUSU KAULI YA NAIBU WAZIRI.

Chama cha walimu Tanzania CWT kimesema kimeshangazwa na kauli iliyotolewa jana bungeni na Naibu waziri ofisi ya waziri mkuu TAMISEMI Kassim Majaliwa kwamba chama hicho hakina mgogoro wa kimaslahi na serikali huku akitambua kwamba hiyo ishu iko kwenye majadiliano chini ya tume ya usuluhishi.

Rais wa chama cha walimu Gratian Mukoba amesema hiyo kauli ni ya upotoshaji na ni kulidanganya bunge pamoja na Watanzania na kusisitiza kwamba nchi ya kuendeshwa kwa girba sio hii, kama girba za mwaka  70 zitaendelea kutumika 2012 ni kwamba unaishi na kichwa cha zamani katika ulimwengu mpya.

Amesema ” hizi girba hazitawasaidia kuwapa walimu mshahara, hazitawasaidia waliokata tamaa kurudisha ari ya kazi… kinachotakiwa ni kutafutwa ni ukweli utakaosaidia nchi kwenda mbele”

Kuhusu ishu ya walimu kuingia rasmi kwenye mgomo rais huyo wa Chama cha Walimu amesema hatua hiyo itafikiwa kama majadiliano yanayoendelea sasa hivi kati yao na serikali yatafikia pazuri.

Amesisitiza kwamba “katika mkutano wetu hatukumaliza majadiliano kwa sababu upande wa serikali wameomba siku mpaka tarehe 20 July 2012, ndio tutarudi mezani kuzungumza kama wametuletea tunachokihitaji na kama hatutakubaliana msajili atatupatia cheti kwamba tumeshindwa kukubaliana na tutaendelea na hatua inayofuata ambayo ni kupiga kura na kuingia kwenye mgomo”

Magazeti yaleo13th July 2012