Chama cha walimu Tanzania kimeanza mgomo wa walimu nchi nzima july 30 2012 ambao unatokana na walimu laki moja na elfu 53 kuukubali.
Ishu imekua nzito baada ya kushindwa kupata kile walichotaka kwa serikali ndani ya siku 30.
Wanachotaka ni kulipwa malimbikizo, ongezeko la mishahara kwa asilimia 100, posho za kufundishia kwa walimu wa sayansi asilimia 55 na walimu wa sanaa asilimia 50 na posho za mazingira magumu kwa asilimia 30.
Shinyanga walimu waliendelea na kufundisha kama kawaida, ambapo walimu wengi wakuu wamesema hawana taarifa zozote za kuanza kwa mgomo, yani hawakuambiwa chochote na bado wanaendelea na kazi.
Dar es salaam shule nyingi kumekua na mgomo mfano Mbezi Luis ambako wanafunzi walikwenda hadi kituo cha polisi Mbezi Luis kwa maandamano.
Kwenye mkoa wa Tanga shule kadhaa zimeonekana kuwa kimya huku wanafunzi wakiwa wenyewe shuleni, walimu wamegoma na wanafunzi kubaki kucheza tu na wengine wakarudi nyumbani.
Kwenye mkoa wa Pwani mgomo ulikuepo ambapo kwenye shule ya Mkoani wanafunzi walikua nje baada ya walimu kuondoka ambapo mwandishi wa habari Victor kasema kwenye shule ya Mtongani Mlandizi wilayani Kibaha ilikua kimya na imefahamika walimu waliwachapa wanafunzi walioingia darasani.
Amesema kwenye shule ya msingi Maili Moja mgomo ulikuepo ambapo baadhi ya wanafunzi walikua wakipiga mawe kwenye ofisi za walimu ambazo milango yake ilikua imefungwa, walimu hawajafanya chochote toka asubuhi.
Singida na Mbeya pia kumekuwepo na mgomo, kwa upande wa Mbeya kwa mujibu wa mbeyayetu Blog kuna vurugu kubwa ambayo mpaka Polisi waliingilia na kupiga mabomu ya machozi kutawanya wanafunzi walioandamana kushinikiza walimu wawape mitihani kabla ya kufunga shule.
Pamoja na hizo taarifa zote za mgomo, Waziri wa Elimu na mafunzo ya ufundi Dr Shukuru Kawambwa amesema mgomo huo ni batili lakini Serikali inawahakikishia walimu ambao hawajajihusisha na mgomo kwamba Serikali na vyombo vya usalama vitawalinda na kuwahakikishia usalama wao.
Amesema “tunawatahadharisha Walimu wote ambao wamegoma na wamekua wakiwatishia maisha walimu wengine ambao hawako kwenye mgomo, atakaebainika hatua za kisheria zitachukuliwa”
Tuesday, July 31, 2012
KAULI ZA BAADHI YA WABUNGE KUHUSU RUSHWA BUNGENI.
Baada ya kuwepo malalamiko ya rushwa kutembea bungeni na kusababisha kuvunjwa kwa kamati ya kudumu ya bunge ya Nishati na Madini mwishoni mwa wiki iliyopita, baadhi ya Wabunge wametaka majina ya wenzao wanaojihusisha na rushwa yawekwe wazi na wafukuzwe bungeni.
Mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nassari (CHADEMA) amesema pamoja na kwamba kamati ya nishati na madini imetajwa moja kwa moja, zipo kamati nyingine ambazo wabunge wake wanatajwa kuhusika na kuomba rushwa.
Amesema “zipo kamati kadhaa zinatuhumiwa kwa rushwa, Mh Spika nilikua naomba muongozo wako kwamba kwa nini ofisi yako isiamue kuzivuruga kamati kadhaa ambazo zinatuhumiwa kwa rushwa ikiwemo kamati ya kudumu ya bunge ya Serikali za mitaa inayoongozwa na Mh. Mrema na Kamati ya kudumu ya bunge ya Mashirika ya Umma inayoongozwa na Mh. Zitto Kabwe, hii ni kwa sababu wabunge wengi wamekua wanazikimbilia zile kamati ambazo zina mikataba lakini kamati kama ya maendeleo ya jamii ya huduma za jamii ambazo zina umuhimu mkubwa kwenye nchi kwa sababu hazina mikataba zinakimbiwa”
Mbunge wa Lindi mjini Salum Khalfan na mbunge wa Nkasi kaskazini Ally keissy Mohamed wamelitaka bunge kuwafukuza bungeni wabunge wote watakaogundulika kula rushwa, wanataka watajwe kwa sababu sasa hivi wabunge wengine kila wakipita barabarani wanakosa raha kutokana na hiyo kashfa ya rushwa iliyolichafua bunge.
Baada ya hayo Naibu Spika wa bunge Job Ndugai aliomba kamati ya uongozi wenyeviti wa kamati za bunge kukutana na Spika kulizungumza ili baadae wampe maelekezo zaidi.
Mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nassari (CHADEMA) amesema pamoja na kwamba kamati ya nishati na madini imetajwa moja kwa moja, zipo kamati nyingine ambazo wabunge wake wanatajwa kuhusika na kuomba rushwa.
Amesema “zipo kamati kadhaa zinatuhumiwa kwa rushwa, Mh Spika nilikua naomba muongozo wako kwamba kwa nini ofisi yako isiamue kuzivuruga kamati kadhaa ambazo zinatuhumiwa kwa rushwa ikiwemo kamati ya kudumu ya bunge ya Serikali za mitaa inayoongozwa na Mh. Mrema na Kamati ya kudumu ya bunge ya Mashirika ya Umma inayoongozwa na Mh. Zitto Kabwe, hii ni kwa sababu wabunge wengi wamekua wanazikimbilia zile kamati ambazo zina mikataba lakini kamati kama ya maendeleo ya jamii ya huduma za jamii ambazo zina umuhimu mkubwa kwenye nchi kwa sababu hazina mikataba zinakimbiwa”
Mbunge wa Lindi mjini Salum Khalfan na mbunge wa Nkasi kaskazini Ally keissy Mohamed wamelitaka bunge kuwafukuza bungeni wabunge wote watakaogundulika kula rushwa, wanataka watajwe kwa sababu sasa hivi wabunge wengine kila wakipita barabarani wanakosa raha kutokana na hiyo kashfa ya rushwa iliyolichafua bunge.
Baada ya hayo Naibu Spika wa bunge Job Ndugai aliomba kamati ya uongozi wenyeviti wa kamati za bunge kukutana na Spika kulizungumza ili baadae wampe maelekezo zaidi.
Monday, July 30, 2012
CCM,Chadema Wawatangazia Kiama Wabunge Mafisadi
DK SLAA AONYA HAKUNA HURUMA, MSEKWA ASEMA RUSHWA ADUI WA HAKI, MBATIA ATOA WIKI MOJA SPIKA AWATAJE WOTE
VYAMA vya CCM na Chadema vimetoa onyo kali kwa wabunge wanaotuhumiwa kwa kashfa ya kuhongwa na baadhi ya kampuni za mafuta na kulihujumu Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), vikisema havitasita kuwawajibisha pindi tuhuma hizo zitakapothibitika.
Kauli ya vyama hivyo imekuja siku moja baada ya wabunge watano, watatu wa CCM na wawili wa upinzani kudaiwa kuhusika na vitendo hivyo vya rushwa, ambavyo vimesababisha Spika wa Bunge, Anne Makinda kuivunja Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini na kuagiza uchunguzi wa kina ufanyike ili majina ya wahusika yawekwe hadharani.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti jana, viongozi wa juu wa vyama hivyo walisema wanasubiri kwa hamu taarifa rasmi kutoka bungeni.
CCM: Rushwa adui wa haki
Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Pius Msekwa alisema chama hicho kimewaapiza wanachama wake wote kutotoa wala kupokea rushwa.
Alisema rushwa ni kosa la jinai hivyo anaamini vyombo husika vya dola vitachukua hatua zinazofaa kwa mujibu wa sheria za nchi.
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye alikazia kauli hiyo akisema rushwa inaelezwa katika katiba ya chama hicho kwamba ni, ‘adui wa haki’ na wanachama wote waliapishwa kuwa hawatapokea wala kutoa rushwa.
Alisema yeyote anayekwenda kinyume na kanuni za CCM, anajiweka katika kundi la wasaliti wa chama.
Alisema wabunge ni kundi maalumu nchini ambalo linalipwa vizuri ili lisimamie vyema misingi ya maendeleo ya nchi pasipo tamaa wala vishawishi hivyo wanapotajwa miongoni mwa kundi la wala rushwa, CCM kinalaani vikali tukio hilo.
Kuhusu tuhuma hizo kutajwa kuwahusisha wabunge watatu wa chama hicho, Nape aligoma akisema habari hizo siyo rasmi, hivyo hawezi kuzizungumzia.
Hata hivyo, alisema CCM kinasubiri uchunguzi ufanyike ambao ndiyo utakaoweka bayana wahusika wa tuhuma... “Tusubiri uchunguzi ukamilike. Idadi inawezekana ikawa hiyo au ikapungua au kuongezeka.”
Dk Slaa: Hatufumbii macho ufisadi
Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa alisema: “Nalaani kitendo cha wabunge kuhusishwa na ufisadi hasa ikizingatiwa kwamba Chadema tumekuwa tukiupinga vikali. Tumekuwa tukipinga rushwa kwa sababu ndiyo inayoielekeza nchi pabaya… Chadema hatufumbii macho rushwa.”
Alisema tangu kuanza Bunge la 10, Chadema kimekuwa kikiona baadhi ya mambo yanayoendelea katika mhimili huo muhimu wa dola yamejaa walakini... “Ndiyo maana sisi Chadema tumekuwa tukisema Bunge limepoteza mwelekeo.”
Alisema akiwa mtendaji mkuu wa chama, anasubiri taarifa kamili kutoka katika kikao cha wabunge wa chama hicho ili kuweka wazi majina ya wahusika na kisha kufuatiwa na kikao cha Kamati Kuu (CC) ambacho kitakaa na kuchukua hatua kali.
“Tunahitaji tupate maelezo ya kina... chama chetu hakikurupuki… Nasubiri taarifa ya kokasi ya chama. Katiba ya Chadema inatambua uwapo wa kikao cha wabunge wetu na kwa bahati nzuri, kiongozi wake mkuu ni Mwenyekiti wa Chadema (Freeman Mbowe) na katibu (David) Silinde ni mbunge wetu. Tunasubiri taarifa yao.”
Alisema Chadema kina kanuni ya kudhibiti rushwa hivyo, mbunge wake akitajwa miongoni mwa wanaohusishwa na rushwa, atawajibishwa kupitia kikao cha CC ya chama hicho.
NCCR-Mageuzi yakoleza moto
Katika hatua nyingine, Chama cha NCCR- Mageuzi jana kilikoleza moto baada ya kumtaka Spika Anne Makinda awataje wabunge hao bungeni ili wafukuzwe na kufungwa kama Sheria ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge inavyotaka.
Chanzo: http://www.mwananchi.co.tz
VYAMA vya CCM na Chadema vimetoa onyo kali kwa wabunge wanaotuhumiwa kwa kashfa ya kuhongwa na baadhi ya kampuni za mafuta na kulihujumu Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), vikisema havitasita kuwawajibisha pindi tuhuma hizo zitakapothibitika.
Kauli ya vyama hivyo imekuja siku moja baada ya wabunge watano, watatu wa CCM na wawili wa upinzani kudaiwa kuhusika na vitendo hivyo vya rushwa, ambavyo vimesababisha Spika wa Bunge, Anne Makinda kuivunja Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini na kuagiza uchunguzi wa kina ufanyike ili majina ya wahusika yawekwe hadharani.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti jana, viongozi wa juu wa vyama hivyo walisema wanasubiri kwa hamu taarifa rasmi kutoka bungeni.
CCM: Rushwa adui wa haki
Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Pius Msekwa alisema chama hicho kimewaapiza wanachama wake wote kutotoa wala kupokea rushwa.
Alisema rushwa ni kosa la jinai hivyo anaamini vyombo husika vya dola vitachukua hatua zinazofaa kwa mujibu wa sheria za nchi.
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye alikazia kauli hiyo akisema rushwa inaelezwa katika katiba ya chama hicho kwamba ni, ‘adui wa haki’ na wanachama wote waliapishwa kuwa hawatapokea wala kutoa rushwa.
Alisema yeyote anayekwenda kinyume na kanuni za CCM, anajiweka katika kundi la wasaliti wa chama.
Alisema wabunge ni kundi maalumu nchini ambalo linalipwa vizuri ili lisimamie vyema misingi ya maendeleo ya nchi pasipo tamaa wala vishawishi hivyo wanapotajwa miongoni mwa kundi la wala rushwa, CCM kinalaani vikali tukio hilo.
Kuhusu tuhuma hizo kutajwa kuwahusisha wabunge watatu wa chama hicho, Nape aligoma akisema habari hizo siyo rasmi, hivyo hawezi kuzizungumzia.
Hata hivyo, alisema CCM kinasubiri uchunguzi ufanyike ambao ndiyo utakaoweka bayana wahusika wa tuhuma... “Tusubiri uchunguzi ukamilike. Idadi inawezekana ikawa hiyo au ikapungua au kuongezeka.”
Dk Slaa: Hatufumbii macho ufisadi
Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa alisema: “Nalaani kitendo cha wabunge kuhusishwa na ufisadi hasa ikizingatiwa kwamba Chadema tumekuwa tukiupinga vikali. Tumekuwa tukipinga rushwa kwa sababu ndiyo inayoielekeza nchi pabaya… Chadema hatufumbii macho rushwa.”
Alisema tangu kuanza Bunge la 10, Chadema kimekuwa kikiona baadhi ya mambo yanayoendelea katika mhimili huo muhimu wa dola yamejaa walakini... “Ndiyo maana sisi Chadema tumekuwa tukisema Bunge limepoteza mwelekeo.”
Alisema akiwa mtendaji mkuu wa chama, anasubiri taarifa kamili kutoka katika kikao cha wabunge wa chama hicho ili kuweka wazi majina ya wahusika na kisha kufuatiwa na kikao cha Kamati Kuu (CC) ambacho kitakaa na kuchukua hatua kali.
“Tunahitaji tupate maelezo ya kina... chama chetu hakikurupuki… Nasubiri taarifa ya kokasi ya chama. Katiba ya Chadema inatambua uwapo wa kikao cha wabunge wetu na kwa bahati nzuri, kiongozi wake mkuu ni Mwenyekiti wa Chadema (Freeman Mbowe) na katibu (David) Silinde ni mbunge wetu. Tunasubiri taarifa yao.”
Alisema Chadema kina kanuni ya kudhibiti rushwa hivyo, mbunge wake akitajwa miongoni mwa wanaohusishwa na rushwa, atawajibishwa kupitia kikao cha CC ya chama hicho.
NCCR-Mageuzi yakoleza moto
Katika hatua nyingine, Chama cha NCCR- Mageuzi jana kilikoleza moto baada ya kumtaka Spika Anne Makinda awataje wabunge hao bungeni ili wafukuzwe na kufungwa kama Sheria ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge inavyotaka.
Chanzo: http://www.mwananchi.co.tz
MZEE SMALL BADO HALI MBAYA
HUJAFA, hujaumbika! Hali ya staa wa vichekesho na filamu Bongo, Said Mohamed Ngamba ‘Mzee Small’ bado hairidhishi tangu mwezi Mei, mwaka huu alipopatwa na ugonjwa wa kupooza ghafla nyumbani kwake Tabata-Kimanga jijini Dar es Salaam, Ijumaa Wikienda linafunguka.
Mzee Small alipatwa na ugonjwa huo wakati akitokea mkoani Mwanza alipokwenda kufanya kampeni ya kupinga mauaji ya albino, safari ambayo aliambatana na mkongwe mwenzie kwenye sanaa, Bi Chau.
TUJIUNGE NA MKEWE
Akizungumza na Ijumaa Wikienda lilipofika nyumbani kwake kumjulia hali, mke wa staa huyo, Fatuma Said alisema siku mumewe alipopata matatizo alifika salama na kuanza shughuli zake za kila siku lakini kesho yake, ghafla alishtuka kumuona mumewe ametokewa na hali hiyo (kupooza) ghafla.
Alisema kuwa mara baada ya kufikishwa kwenye Hospitali ya Amana, Dar, madaktari walimcheki na kugundua alipatwa na stroke (kupooza) ndipo matibabu yakaanza.
BADO HALI TETE
Akizungumzia afya yake, Mzee Small alisema: “Kwa kweli nilitakiwa kurudi hospitali kwa ajili ya kuchekiwa upya na kufanyiwa mazoezi tangu Julai 5, mwaka huu lakini kwa kuwa sikuwa na fedha sikuweza kwenda hivyo bado hali ni mbaya na naomba Watanzania wanisaidie.”
KUTOKA KWA MHARIRI
Kwa kutambua kuwa Mzee Small kwa sasa anashindwa kuendelea na kazi zake kutokana na ugonjwa huo, ni wazi kuwa anahitaji msaada wa kuweza kujikimu kwa matibabu.
Kama unagushwa kumsaidia Mzee Small, basi tuma chochote ulichonacho kwa njia ya M-Pesa kwa namba yake ambayo ni 0754 647265.
chanzo:Globalpublishers
Mzee Small alipatwa na ugonjwa huo wakati akitokea mkoani Mwanza alipokwenda kufanya kampeni ya kupinga mauaji ya albino, safari ambayo aliambatana na mkongwe mwenzie kwenye sanaa, Bi Chau.
TUJIUNGE NA MKEWE
Akizungumza na Ijumaa Wikienda lilipofika nyumbani kwake kumjulia hali, mke wa staa huyo, Fatuma Said alisema siku mumewe alipopata matatizo alifika salama na kuanza shughuli zake za kila siku lakini kesho yake, ghafla alishtuka kumuona mumewe ametokewa na hali hiyo (kupooza) ghafla.
Alisema kuwa mara baada ya kufikishwa kwenye Hospitali ya Amana, Dar, madaktari walimcheki na kugundua alipatwa na stroke (kupooza) ndipo matibabu yakaanza.
BADO HALI TETE
Akizungumzia afya yake, Mzee Small alisema: “Kwa kweli nilitakiwa kurudi hospitali kwa ajili ya kuchekiwa upya na kufanyiwa mazoezi tangu Julai 5, mwaka huu lakini kwa kuwa sikuwa na fedha sikuweza kwenda hivyo bado hali ni mbaya na naomba Watanzania wanisaidie.”
KUTOKA KWA MHARIRI
Kwa kutambua kuwa Mzee Small kwa sasa anashindwa kuendelea na kazi zake kutokana na ugonjwa huo, ni wazi kuwa anahitaji msaada wa kuweza kujikimu kwa matibabu.
Kama unagushwa kumsaidia Mzee Small, basi tuma chochote ulichonacho kwa njia ya M-Pesa kwa namba yake ambayo ni 0754 647265.
chanzo:Globalpublishers
Subscribe to:
Posts (Atom)








































