Thursday, August 2, 2012

Magazeti ya Leo Alhamis 2nd August 2012

ALICHOSEMA NAIBU WAZIRI KUHUSU HASARA YA AJALI YA NDEGE YA AIR TANZANIA KIGOMA.

                Hii ndio ndege pekee inayomilikiwa na Shirika la ndege ATC, moja iliyobaki ni ya kukodi.
                                      Hii ndio ndege mpya iliyokodiwa na shirika la ndege ATC.
Kwenye kipindi cha maswali na majibu Aug 1 2012 bungeni Naibu waziri wa Uchukuzi Charles Tizeba alijibu kuhusu hasara ya ajali ya ndege ya shirika la ndege Tanzania iliyotokea Kigoma tarehe 9 April 2012 pamoja na uhaba wa ndege kwa sababu shirika la ndege Tanzania linazo ndege mbili tu.

Tizeba amesema “ni kweli kwa sasa shirika la Ndege Tanzania linazo ndege mbili tu, moja ikiwa inamilikiwa na shirika lenyewe na nyingine ya kukodi, historia ya hili shirika nadhani inafahamika kwa sababu baada ya kuingia ubia wa aina mbalimbali huduma zilidorora na likaserereka kuelekea huko”


Kuhusu hasara iliyojitokeza kwenye ajali Kigoma, Naibu Tizeba amesema “ndege inayo gharama yake na ndio maana baada ya kupata ile ajali tulilipwa bima kiasi cha shilingi bilioni 10.2 lakini hasara iliyopatikana ilikua kwenye biashara hasaa na sio gharama ya ndege yenyewe.

Gharama iliyopatikana kutokana na kulazimika kuwalipia hoteli abiria walioshindwa kusafiri kutokana na ajali hiyo imetajwa kwamba ni milioni 499 ambayo ilitumika kulipia hoteli pamoja na mambo mengine.

Tayari imetangazwa na waziri wa Uchukuzi kwamba pesa hiyo ya bima itatumika kununua ndege mbili mpya.

BAADA YA MWAKA, PROFESA MWANDOSYA AINGIA BUNGENI KWA MARA YA KWANZA, ALIYOYASEMA NDIO HAYA!

Profesa Mark Mwandosya akiwa na Waziri mkuu Mizengo Pinda alipokwenda kumtembelea wakati akiumwa, hii ilikua May 7 2012.

Jumatano Aug 1 2012 nilikua nimetulia nachek bunge ghafla nikaona wabunge wanapiga meza kama kuna shangwe flani hivi, kuja kushtuka kumbe ilikua ni kutokana na waziri wa ofisi ya Rais aisekua na wizara maalum Profesa Mark Mwandosya kuingia bungeni kwa mara ya kwanza baada ya kuugua kwa zaidi ya mwaka mmoja.

Alisema “naona mkono wake mwenyezi Mungu katika uponyaji wangu, ni zaidi ya mwaka tangu nimekwenda kwa ajili ya matibabu na sijazungumza katika bunge hili tukufu, moja kati ya mambo nilikua nasema mbona ungenirudishia hata kwa dakika tano nije kuongea na wabunge wenzangu na mwenyezi Mungu ameliridhia ombi langu”

Pamoja na kuwashukuru na kuwasifu viongozi wote waliomjulia hali wa chama tawala na upinzani, Profesa Mwandosya amesema “afya ni muhimu sana na tuendelee kupima afya zetu wabunge, mimi miaka 45 sijawahi kuona kitanda hospitali nimekwenda kukikuta huko Hydrebad, nilidhani ni mtu mwenye afya sana mtu wa mazoezi kila siku asubuhi na jioni lakini kumbe mwili wa binadamu Mungu alivyoumba ni maajabu yake yeye mwenyewe”

Thanks kwa : http://millardayo.com/

Wednesday, August 1, 2012

WAKALI WA MAN U MAREKANI NA MAMA OBAMA PAMOJA NA FANS!

 Wachezaji wakongwe wa Manchester United walipokutana na mama Michelle Obama mke wa rais Obama wa Marekani.

HIVI UMEISIKIA KAULI YA GAZETI LA MWANAHALISI BAADA YA KUFUNGIWA NA SERIKALI? NDIO HII..

Siku moja baada ya Serikali kutangaza kulifungia kwa muda usiojulikana gazeti la kila wiki la MWANAHALISI linalochapishwa na kampuni ya Hali Halisi Publishers kutokana na kulituhumu kuandika habari za uchochezi na zinazoleta hofu, Uongozi wa gazeti hilo umezungumza.

Mkurugenzi mtendaji wa kampuni hiyo Said Kubenea amesema kimsingi hawakupokea barua rasmi kutoka Serikalini inayowataka kusitisha zoezi la kuchapisha gazeti hilo na badala yake hizo taarifa wamezipata kupitia vyombo mbalimbali vya habari.

Kubenea amesema hawakubaliani na madai ya serikali kwamba gazeti hilo limekua likiandika habari za uchochezi na kusisistiza kwamba habari yeyote inayoandikwa katika gazeti hilo ni lazima iwe imefanyiwa uchunguzi wa kina na kamwe gazeti hilo halikuwahi kukurupuka na kuandika habari isiyo ya kweli.

Inaaminika kwamba moja kati ya habari za hatari zilizofanya gazeti hilo kufungiwa kwa muda usiojulikana ni ile ya kuchapisha namba za simu za watu waliowasiliana na Dr Ulimboka mara ya mwisho kabla ya kufanyiwa ukatili.

Kwa kusisitiza, Kubenea amesema “hakuna kosa lolote tulilolifanya na tunastahili kupongezwa badala ya kulaumiwa, tulichofanya sisi ni kitu kidogo sana, tuliangalia tu ni nani aliwasiliana na Dr Ulimboka kwa mara ya mwisho… sasa tumepetaje? hizo ni taarifa zetu, kama kuna uchochezi ambao tumeufanya tulipaswa kuwepo Mahakamani lakini mpaka leo hatujaulizwa, hatujahojiwa, hatujaitwa hivyo ina maana hakuna kesi…. mimi kubenea nimefanya uchochezi ni kosa, naweza kufanya kosa kama hilo alafu natembea barabarani? “

"Diamond Hatunae Tena" anasema ndiyo ingekuwa kichwa cha habari leo

DIAMOND HATUNAE TENA...!!!
"Diamond hatunae tena"....hiyo ndo ingekuwa heading na kichwa cha habari cha media na watu wengi kwenye social networks na simu zao za mikononi kwa siku ya jana....Kiukweli hali yangu ilikua ni mbaya sana,nilizidiwa na homa kali ya ghafla iliyosababishwa na kifua kilichonisumbua kwa takribani wiki mbili mfululizo....hadi kupelekwa Heameda Medical Clinic kwa Doctor Hery M. Mwandolela, Specialist wa Heart and Cough kwa uchunguzi na vipimo vikubwa maana hali haikuwa ya kawaida.....namshkuru Mwenyezi Mungu baada ya vipimo vyote iligundulika ni kifua cha kawaida tu ila kilisababishwa na tour na ziara nyingi nilizozifanya mikoa na nchi mbalimbali kwa mfululizo bila mapumziko ya kutosha..
kwa sasa hali yangu si mbaya sana...nawashukuru wote mliokuwa mkiniombea kupitia Blogs, Twitter, Bbm, Facebook...etc, na Media zote niweze recover

Picha toka kwa http://www.thisisdiamond.com

Dah  nimeweka lakini usirudie tena kuweka kichwa cha habari kama hiki........ Poleni kwa mtakaoshtuka si nia yangu.

JLO ASHEREHEKEA BIRTHDAY YAKE KATIKA BOAT NA KING'ASTI WAKE.

                                                                  Akielekea Kwenye boti
                                                  Hakika amependea red is my best
                            Baba shika mama isianguke bana kwa raha zao raha kupendwa Jamani
                                                              Keki ikielekea kwenye boti