Sunday, August 19, 2012

Magazeti ya leo Jumapili 19th August 2012





















MATOKEO YA MECHI ZOTE ZA PREMIER LEAGUE NA WAFUNGAJI WAKE AUG 18 2012.








Rais Jakaya Mrisho kikwete Awasili Kutokea Msumbiji

 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Inspekta Jenerali wa Polisi Saidi Mwema baada ya kuwasili  usiku huu Agosti 19, 2012 kutoka Maputo, Msumbiji alikohudhuria kikao cha viongozi wa Jumuiya Ya Maendeleo Kusini Kwa Afrika (SADC) uliofunguliwa tarehe Agosti 17,  2021 na kumalizika jana jioni  Agosti  18 2012. Katika kikao cha Jana Tanzania imechukua uenyekiti wa Kamati ya Siasa, Ulinzi na Usalama kutoka Afrika ya Kusini ambapo uenyekiti wa SADC umechukuliwa na Msumbiji kutoka Angola. Nafasi hizi ni za mwaka mmoja mmoja

Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiwa na Mkuu wa Wilaya ya Temeke Mhe Sophia Mjema baada ya kuwasili  usiku huu Agosti 19, 2012 kutoka Maputo, Msumbiji alikoambatana na Rais Kikwete katika  kikao cha viongozi wa Jumuiya Ya Maendeleo Kusini Kwa Afrika (SADC) uliofunguliwa tarehe Agosti 17,  2021 na kumalizika jana jioni  Agosti  18 2012. Katika kikao cha Jana Tanzania imechukua uenyekiti wa Kamati ya Siasa, Ulinzi na Usalama kutoka Afrika ya Kusini ambapo uenyekiti wa SADC umechukuliwa na Msumbiji kutoka Angola. Nafasi hizi ni za mwaka mmoja mmoja

Saturday, August 18, 2012

SALAMU ZA EID MUBARAK KUTOKA TANZANIA ASILIALIVE BLOGSPOT.COM


Wadau wa Blog ya Tanzania Asilialive familia pamoja na familia yangu nawatakia Waislam wote Duniani Furaha ya Sikukuu ya EID - MUBARAKA .

TAQABALLAH ALLAHU MINNA WAAMINKUM SWAALIHAL A3MAAL = AMIIN M/MUNGU AZIPOKEE IBADA ZETU NA FUNGA ZETU NA ATUDUMISHE MILELE KATIKA MAMBO YALIYO MAZURI DAIMA

MWANAMKE TAJIRI NA MREMBO KULIKO WOTE UGANDA!!


JARIDA maarufu la Times nchini Uganda limemtaja mama wa watoto wawili Zari Hassan kuwa ndiye mwanamke mrembo na tajiri kuliko wote nchini humo kwa wakati huu.
Kwa mujibu wa jarida hilo Zari (30) ambaye ni Mwanamuziki,Mfanyabiashara na Mtangazaji wa runinga amepata mafanikio makubwa kwenye muziki na pia kipindi chake cha runinga kinachofananishwa na kipindi cha ‘Keeping up with the Kardashians’ kinachoendeshwa na mrimbwende wa kimarekani Kim Kardashian.
Huku likiambatanisha picha za magari na nyumba anazomiliki mwanadada huyo, jarida hilo limeandika kuwa huenda akaingia kwenye orodha ya wanawake matajiri zaidi Afrika baada ya kipindi kifupi kijacho endapo ataendelea na mwenendo wake wa sasa kibiashara.
hata hivyo jarida hilo pia limetaja zari kuwa mmoja wa mstaa wapenda starehe na amekuwa akitumia mkwanja alionao kumnasa mwanaume wa aina yoyote anahisi kuwa anahitaji kumliza kwa wakati huo ingwa tuhuma hizo hazikusibitishwa moja kwa moja.

katika hatua nyingine jarida hilo limesema kuwa Zari mwenye maskani yake pia nchini Afrika ya Kusini, wazazi wake si raia wa uganda kuzaliwa ispokuwa ni wahamiji kwani baba yake ni raia wa Buurundi mwenye asili ya Somalia na mama yake ni raia wa India kutoka kabila la Mutoroo.

Aidha Times limeandika kuwa Zari anamiliki ndinga kibao za kisasa na zenye thamani kubwa kama BMW – 2006, Black Chrysler – 2008, – Audi Q7 2010 Silver Crysler – 2008, JETTA-2006, Mercedes Benz convertible -2008. Range-Rover, Lamborghin, Hummer na mengine mengi huku pia akiwanaumiliki wa maduka, hotel na majumba ya kisasa kwenye miji mikubwa ya Pretoria, Cape Town na Kampala.

Afisa Mwandamizi Baraza La Habari (MCT) Alfred Mbogora Afariki Dunia

Ofisa Mwandamizi  wa Baraza la Habari Tanzania (MCT) Alfred Mbogora,amefariki mapema  tarehe 18/8/2012 katika hospitali ya Taifa Muhimbili alipokuwa amelazwa baada ya kuugua ghafla.

 Taarifa zinasema siku ya jumatano aliuguwa ghafla akiwa safarini kuelekea Bagamoyo kikazi.Ambapo njiani alisema hajisikii vizuri na kupoteza nguvu.

Marehemu Alfred Mbogora aliwahi pia kufanya kazi katika taasisi ya Utafiti na Demokrasia(REDET),amewahi kuwa mwandishi wa habari wa SHIHATA,The Guardian  na  The African.

MUNGU AILAZE  ROHO YA MAREHEMU MAHALA PEMA PEPONI-AMIN

Pata Ratiba za England Premier Leaque

Magazeti ya Leo Jumamosi 18th August 2012

President Kikwete Attends The 32nd Ordinary Summit Of Heads Of State And Government Of SADC In Maputo

 President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete in conversation with the South African President Jacob Zuma  during the 32nd Ordinary Summit of Heads of State and Government of the Southern African Development Community(SADC) in Maputo
 President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete together with Namibian President Hifikepunye Pohamba in intimate conversation during the opening ceremony of the 32nd Ordinary Summit of Heads of State and Government  of SADC in Maputo today.
Presiddent Dr.Jakaya Mrisho Kikwete left front row in a group photo with other SADC Heads of State and Government during the opening session of the 32rd Ordinary Summit of Heads of State and Government of SADC in Maputo   
             
Photos by Freddy Maro

Friday, August 17, 2012

DULLY 'MTOTO WA KARIAKOO' OFFICIAL VIDEO .


KOFFI OLOMIDE JELA KWA KUFANYA FUJO.


Stori kutoka Kinshasa Congo DRC zimetoa uthibitisho kwamba mwanamuziki maarufu ambae jina lake lina uzito ndani na nje ya Afrika Koffi Olomide, amehukumiwa kwenda jela kwa miaka mitatu au kulipa faini.

Kilichomfanya apigwe hizo nyundo ni fujo alizozifanya akiwa kwenye hoteli moja maarufu Congo DRC pamoja na kumpiga meneja wake.

Nimemsikia mwandishi wa DW kutoka Congo akisema Koffi alikua akitetewa na zaidi ya mawakili 15 ambapo mamia ya mashabiki wake walihudhuria Mahakamani kusikiliza kitatokea nini kwenye kesi yake August 16 2012.

kabla  ya kufikishwa Mahakamani Koffi alikamatwa na polisi August 15 jioni muda mfupi tu baada ya kufanya fujo hizo na kuwekwa kwenye rumande ya mahakama ndogo Kinshasa kutokana na makosa aliyofanya hotelini ikiwa ni pamoja na kumpiga meneja wake ambae amekua akiishi Ulaya.

Mwandishi wa DW amesema ugomvi huo umetokana na Koffi kumdai meneja huyo euro elfu sita ambapo mashahidi kwenye eneo la tukio wamekiri kwamba Koffi alimpiga ngumi meneja wake pamoja na kuvunja mlango wa hoteli.

Hata hivyo meneja huyo aliwasilisha Mahakamani hoja ya kuondoa mashtaka yake dhidi ya Koffi na kupendekeza kuwepo kwa maridhiano kati yao lakini majaji walilipiga chini hilo ombi lake.

Baadhi ya wananchi waliotoa maoni kuhusu hiyo kesi ya Koffi wameunga mkono adhabu hiyo na kusema amezidisha, Ulaya ni yeye na kwengine ni yeye, mwingine amesema ni safi kwa sababu hii sio mara ya kwanza kwa yeye kutenda kosa.

Kutokana na adhabu hiyo kiongozi wa mawakili wanaomtetea Koffi amesema wamepanga kukata rufaa lakini wanasubiri maoni ya Koffi mwenyewe.… unaweza kuiskiliza hiyo ripoti ya Dw hapo chini pia.

BELINA AWA BALOZI WA NYWELE

                                                 Mwanamitindo Belina Mgeni.

MWANAMITINDO mwenye mvuto Bongo, Belina Mgeni amelamba shavu la nguvu kutoka kwa kampuni kubwa ya nywele nchini kwa kusainishwa mkataba wa mwaka mmoja kuwa balozi wa kampuni hiyo.

‘Akisemezana’ na Motomoto Newz, Belina alisema anamshukuru  Mungu kwa kupata shavu hilo ambapo sasa picha zake zitakuwa zikionekana katika mabango ya kampuni hiyo, pia atakuwa akisuka bure nywele kwa kipindi cha mwaka mmoja na kutumia bidhaa za kampuni hiyo kama balozi.

Aidha, mwanamitindo huyo alisema ataubeba ubalozi huo kwa umakini mkubwa  kwa sababu heshima waliyompa ni kubwa sana  kwa upande wa warembo  na wanamitindo wa hapa nchini.

Na Imelda Mtema

MAIMARTHA: WAMESHAANZA KUMCHOKONOA MUME WANGU:



MTANGAZAJI wa Kituo cha Runinga cha TBC1, Maimartha Jesse ameeleza kusikitishwa kwake na baadhi ya watu wasioitakia mema ndoa yake kwa kuanza kumchokonoa mume wake kipenzi, Shaa.

 Akizungumza na Ijumaa hivi karibuni Maimartha alisema kuwa, kuna watu ambao mara kwa mara wanamtumia sms za kumponda mume wake huyo wakieleza kuwa, eti hawaendani na ‘ameingia chaka’.
Alisema kuwa, kibaya zaidi mumewe amekuwa akizisoma meseji hizo lakini kwa bahati nzuri ni muelewa hivyo hakasiriki badala yake humtaka kuzipuuza kwani zinatumwa na watu wasiowatakia mema.

“Wapo watu walionitabiria mabaya na sasa yanawageukia, wapo pia wengine bado wananifuatilia wanataka kuivunja ndoa yangu lakini nawaambia watashindwa,nampenda mume wangu na naamini tutadumu,” alisema Maimartha.