Saturday, November 10, 2012

MAMBO YALIVYOKUWA EBSS 2012 WALTER CHILAMBO AIBUKA KIDEDEA HAAAAA JAMAA MKALI

    Msanii Barnaba akiimba na mmoja wa washiriki wa shindano la Epiq Bongo Star Search 2012 (EBSS),
                   Mshiriki wa EBSS NshomaNg'hangasamala akiimba moja ya wimbo wake jukwaani.
Mwanadada Salma Albushiri akiimba kwa hisia huku akipiga gitaa mbele ya mashabiki wake waliofika kumshuhudia ndani ya ukumbi wa Diamond usiku huu.
                                         Mapouda.! majaji hawaishi vituko
                                                                 Mashabiki
 Wasanii wa muziki wa kizazi kipya Linah na Amin wakiimbwa kwa pamoja wimbo mpya uitwa Mtima Wangu





                               Mkurugenzi wa kampuni ya Benchmark Productions Limited,
 Mkurugenzi wa kampuni ya Benchmark Productions Limited, na jaji mkuu wa Shindano la  Epiq Bongo Star Search 2012 (EBSS), akiwa amemkumbatia mshindi wa shindano hilo Walter Chilambo ndani ya ukumbi wa Diamond,Chilamba ameibuka na kitita cha shilingi Milioni 50
  Mshindi wa shindano la  Epiq Bongo Star Search 2012 (EBSS),Walter Chilambo (Dar) akiwashukuru wapenzi na msahabiki wake waliompigia kura na hatimaye kuibuka mshindi wa shindano hilo,lililofanyika ndani ya ukumbi wa Diamond jubilee,

 Mshindi wa shindano la  Epiq Bongo Star Search 2012 (EBSS),Walter Chilambo (Dar) akikabidhiwa sanduku lake lenye kitita cha shilingi milioni 50 jana usiku ndani ya ukumbi wa Diamond jubilee,katika shindano hilo lililovuta hisia za wengi,mshindi wa pili ameibuka mwanadada Salma Abushiri  (Zanzibar) na watu ni Wababa Mtuka (Dar)
 Baadhi ya mashabiki wa mshindi wa shindano hilo la EBSS,Walter Chilambo wakishangilia kwa shangwe na vifijo mara baada kutamkwa yeye ndiye kinara katika kilele cha shindano hilo lililovuta hisia za watu wengi

                Huyu ni Salama Jabir  na hapa ni katiak yale ya Look ndani ya fainali za EBSS 2012
 Washiriki wa Washindano la EBSS 2012 ambao wamefanikiwa kuingia fainali ya shindano hilo wakiwa jukwaani usiku huu wakati wa kuanza kwa fainali hizo. Ni ndani ya Ukumbi wa Diamond Jijini Dar es Salaam. Mshindi kuondoka na kitita cha Shilingi Milioni 50 za kitanzania.
  Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Kampuni ya simu za Mikononi ya Zantel, Awaichi Mawalla akiwa katika mahojiano na mmoja wa ma MC wa sho ya leo Caesar Daniel,wakati akingia katika zulia jekundu la Fainali za EBSS nadani ya  Diamond Jubilee.




                                                      Mwasisi akitumbuiza jukwaani

                                                                          Majaji
                                                          Salma Yusufu
Shindano la EBSS usiku huu limefikia patamu baada ya washiriki 3 walio ingia katika fainali hizo kutoka na sasa kubakia washiriki wawili ambao ni Walter Chilambo na Salama Yusufu mwakilishi pekee kutoka kisiwani Zanzibar.

Washiriki waliotoka usiku huu na kuachia kitita chaa Shilingi Milioni 50, kikiwaniwa na Walter na Salama ni pamoja na Nsami Nkwabi, Nshoma Ng’hangasamala Wababa Mtuka.

Shindano la EBSS linafikia tamati yake usku huu katika ukumbi wa Diamond Jublee linapoendea kufanyika.
WALTER CHILAMBO ndiye mshindi wa Shindano la Epic Bongo Star Search (EBSS)  2012. Kufuatia matokeo hayo Kalambo amejinyakulia kitita cha Shilingi Milioni 50 za Kitanzania kutoka kwa wadhamini wakuu wa shindano hilo kampuni ya Simu za Mkononi ya Zantel.

Chilambo ametwaa ubingwa huo baada ya kumwangusha mwana dada kutoka Zanzibar ambaye alikuwa ni mshindani wake wa karibu katika kinyang’anyoro hicho Salma Yusufu.

Wanajeshi Wa Marekani Waadhibiwa

Wanajeshi saba wamarekani wa kitengo cha Elite akiwemo mmoja wa maafisa wa jeshi aliyehusika na kumkamata na kumuua Osama bin Laden wameadhibiwa kwa madai ya kutoa taarifa za siri za marekani kinyume na sheria.

Kuvunjwa kwa usalama huo kunadaiwa kujiri wakati wanajeshi hao walikuwa wakifanya kazi ya kutoa huduma za ushauri katika kutengeneza mchezo wa video inayoonyesha makabiliano ya kijeshi.

Saba hao walipata barua za nidhamu na kupokea nusu ya mishahara yao kwa kipindi cha miezi miwili .

Idara ya usalama ya marekani bado inachunguza iwapo maafisa zaidi wa kitengo cha Seal walihusika

Chanzo:  http://www.bbc.co.uk/swahili/news

Dk. Shein Afanya Mazungumzo Na Balozi Mdogo Wa India Zanzibar


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein akizungumza na Balozi Mdogo wa India wa Zanzibar, Pawan Kumar alipofika Ikulu Mjini Zanzibar Kujitambulisha kwa Rais.

  [Picha na Ramadhan Othman Ikulu]

Magazeti ya leo Jumamosi ya 10th November 2012

Hoja Ya Mdee ‘Kaa La Moto’ Kwa Serikali

MBUNGE wa Kawe, Halima Mdee amewasilisha hoja binafsi bungeni akiitaka Serikali kusitisha ugawaji wa ardhi hadi tathmini ifanyike, huku akimtuhumu Waziri Mkuu kuwa anashiriki katika kuwakumbatia wawekezaji wanaopora ardhi wananchi.

Mdee amesema kuwa bila kufanya hivyo, ardhi yote ya nchi hii itachukuliwa na wawekezaji huku wananchi wakiachwa masikini.

Akiwasilisha bungeni hoja binafsi kuhusu kusitishwa ugawaji ardhi nchini, Mdee aliitaka Serikali kusitisha ugawaji wa ardhi hadi hapo tathmini ya kina itakapofanyika kujua kiasi cha ardhi kilichopo mikononi mwa wawekezaji.

Vile vile, alitaka tathmini ya kina ifanyike kubaini raia wa kigeni na wa ndani waliojipatia ardhi kinyemela kupitia Serikali za vijiji kinyume na matakwa ya sheria ya ardhi namba 5 ya mwaka 1999.

“Kwa mujibu wa Kanuni  namba  54(1), (2)  na (3) ya Kanuni za Kudumu za Bunge, Toleo la 2007 naomba kutoa hoja binafsi ya kuitaka Serikali kusitisha ugawaji wa ardhi kwa wawekezaji wa ndani na wa nje mpaka hapo tathmini ya kina itakapofanyika kubaini ni kiwango gani cha ardhi kiko mikononi  mwa wawekezaji,” alisema Mdee.

Alisema katika miaka ya hivi karibuni, kutokana mtikisiko wa uchumi duniani, tumeshuhudia wimbi la wawekezaji kutoka nje wakingia nchini kuwekeza katika kilimo kwa maelezo kwamba watasaidia kuinua uzalishaji katika sekta ya kilimo.

Hata hivyo, alisema uwekezaji huo wa wageni katika ardhi umegeuka kuwa shubiri kwa wananchi hususan wakulima wadogo.

Alisema wakulima hao wamekuwa wakiondolewa katika maeneo yao ya asili ili kuwapisha wageni huku wakiachwa katika lindi la umasikini mkubwa.

Mdee alisema ardhi hiyo imekuwa ikichukuliwa na Serikali kuwa haina mwenyewe au haitumiki.

“Hii inatokana na ukweli kwamba kumekuwa na tafsiri ambayo sio sahihi, kwamba ardhi wanayopewa wawekezaji haina wenyewe, haina mtu, haitumiki. Wakati ukweli ni kwamba maeneo mengi kama sio yote yalikuwa yanatumiwa na wakulima wadogo,” alisema.

Mdee alisema wawekezaji wamechukua maeneo makubwa ambayo wameshindwa kuyaendeleza na hata yale ambayo wanayaendeleza ni kwa kiasi kidogo.

Alisema baadhi ya waewekezaji wengine baada ya kumilikishwa ardhi kwa bei ya kutupa wamekuwa wakikaa nayo na baadaye kuiza kwa wawekezaji wengine.

Mdee aliliomba Bunge kukubali Serikali kusitisha ugawaji wa ardhi ili kuangalia wapi ilipokosea kwa manufaa ya nchi.

Mbunge huyo kupitia Chadema, alisema hata wizara ya ardhi na maendeleo ya makazi wakitakiwa leo kutoa taarifa sahihi ya ardhi kiasi gani iko chini ya miliki ya wageni hawana taarifa hizo.

Alisema kutokana na waewekezaji kupewa ardhi bila ya kufuata taratibu, hivi sasa migogoro mingi ya ardhi iliyopo nchini inatokana na wananchi kuporwa ardhi kwa kisingizio cha uwekezaji.

Alitoa mfano wa Kampuni ya Kigoma inayofahamika kama Agrisol na FELISA ambayo imenunua hekari 3,000 katika Kijiji cha Basanza Kata ya Uvinza wilayani ya Uvinza.

Alisema wawekezaji hao ambao wanakingiwa kifua na Waziri Mkuu, wamewakuta wakulima na wafugaji katika maeneo haya.

Alisema mwekezaji kwa kushirikiana na vyombo vya dola aliwatoa kwa nguvu wananchi akitumia askari mgambo kupiga wananchi, kuchoma nyumba, kuharibu mazao na halikadhalika kuwafungulia wananchi mashtaka.

Alitaja maeneo mengine yenye migogoro kuwa ni wananchi na wawekezaji kuwa ni Rufiji, Kilombero, Bagamoyo, Kisarawe, Muheza, Pangani, Katavi ,Meatu, Kinondoni, Njombe na Ngorogoro.

Moto wa hoja hiyo uliwafanya baadhi ya mawaziri kuinuka kuchangia akiwamo, Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi, Profesa Tibaijuka, Waziri Nchi ofisi ya Waziri Mkuu, (Uwekezaji na Uwezeshaji), Mary Nagu na Waziri wa Nchi ofisi ya Rais (Mahusiano), Steven Wassira.

Akichangia hoja hiyo, Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi, Profesa Tibaijuka alikubali kufanya marekebisho katika sheria ya ardhi ili iweze kuwanifaisha watanzania.

Alisema hakubaliani na hoja ya Mbunge Mdee ya kutaka kusitisha utoaji wa ardhi kwa wawekezaji akisema hali hiyo inaweza kuleta matatizo zaidi.

Profesa Tibaijuka alisema ni aibu kwa nchi yenye ardhi kubwa na yenye rutuba kushindwa kujitosheleza kwa chakula.

Hivyo, alisema kuwapa wageni wenye mitaji ardhi kwa ajili ya kilimo kutasaidia kuongezeka kwa uzalishaji wa mazao na hivyo kujitosheleza kwa chakula.

Profesa Tibaijuka alisema ili watanzania waweze kunufaika na uwekezaji mkubwa wa ardhi nchini, Serikali itakuwa inachukua hisa katika mshamaba hayo na kuziuza kwa wananachi.

“Serikali hii haiwezi kukukbali wananchi wake kuporwa ardhi na wawekezaji,” alisema.

Alisema anakubalina kufanyiwa marekebisho sheria hiyo ili iweze kumsiadia mwananchi.

Waziri Nagu, alisema hatuwezi kusitisha uwekezaji kwa wageni kwa sababu itasabisha kurudisha nyuma maendeleo katika sekta ya kilimo.

Chanzo: http://www.mwananchi.co.tz/habari/siasa