Tuesday, January 22, 2013
Mapokezi ya jk ufaransa
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikagua gwaride rasmi aliloandaliwa kwa heshima yake mjini Paris Ufaransa leo Januari 21, 2013 ikiashiria kuanza rasmi kwa ziara yake ya kiserikali ya siku tano nchini humo.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikagua gwaride rasmi aliloandaliwa kwa heshima yake mjini Paris Ufaransa leo Januari 21, 2013 ikiashiria kuanza rasmi kwa ziara yake ya kiserikali ya siku tano nchini hum.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa na mwenyeji wake Rais Francois Hollande wa Ufaransa katika Ikulu ya nchi hiyo maarufu kama Champs L’Elyesee (hutamkwa chanz elezee) jijini Paris leo Januari 21, 2013
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisindikizwa na mwenyeji wake Rais Francois Hollande wa Ufaransa baada ya mazungumzo yao rasmi katika Ikulu ya nchi hiyo maarufu kama Champs L’Elyesee (hutamkwa chanz elezee) jijini Paris leo Januari 21, 2013
Gari iliyomchukua Rais Jakaya Mrisho Kikwete ikiondoka Ikulu ya nchi hiyo maarufu kama Champs L’Elyesee (hutamkwa chanz elezee) jijini Paris leo Januari 21, 2013
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na ujumbe wake akiwa katika maongezi rasmi na mwenyeji wake Rais Francois Hollande wa Ufaransa na ujumbe wake katika Ikulu ya nchi hiyo maarufu kama Champs L’Elyesee (hutamkwa chanz elezee) jijini Paris leo Januari 21, 2013
Monday, January 21, 2013
RAIS KIKWETE AWASILI UFARANSA
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete wakiwa na mke wa Rais
wa Mali Mama Touré Lobbo Traoré waliyekutana naye uwanja wa ndege wa
Kimataifa wa Charles de Gaulle jijini Paris, Ufaransa, baada ya kuwasili
tayari kuanza ziara ya kiserikali ya siku tatu.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na mke wa Rais wa Mali Mama Touré Lobbo Traoré waliyekutana naye uwanja wa ndege wa Kimataifa Charles de Gaulle jijini Paris, Ufaransa, baada ya kuwasili tayari kuanza ziara ya kiserikali ya siku tatu.
Mama Salma Kikwete akiongea na mke wa Rais wa Mali Mama Touré Lobbo Traoré waliyekutana naye uwanja wa ndege wa Kimataifa Charles de Gaulle jijini Paris, Ufaransa, baada ya kuwasili tayari kuanza ziara ya kiserikali ya siku tatu.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na mke wa Rais wa Mali Mama Touré Lobbo Traoré waliyekutana naye uwanja wa ndege wa Kimataifa Charles de Gaulle jijini Paris, Ufaransa, baada ya kuwasili tayari kuanza ziara ya kiserikali ya siku tatu.
Mama Salma Kikwete akiongea na mke wa Rais wa Mali Mama Touré Lobbo Traoré waliyekutana naye uwanja wa ndege wa Kimataifa Charles de Gaulle jijini Paris, Ufaransa, baada ya kuwasili tayari kuanza ziara ya kiserikali ya siku tatu.
Maafa stendi ya ubungo

SEHEMU ya ukuta wa kituo cha mabasi ya kwenda mikoani cha Ubungo, jijini Dar es Salaam, leo alfajiri umeanguka na kuyaharibu vibaya magari zaidi ya ishirini yaliyokuwa yameegeshwa nje ya eneo hilo. Akizungumza na waandishi wa habari, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Charles Kenyela alisema kuwa idadi ya magari yaliyopatwa na ajali hiyo yanakadiriwa kufikia 24 ambapo watu watatu wanasemekana wamejeruhiwa.
Baada ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kumtimuwa uwanachamaMwamalala ajiunga nccr mageuzi
Edo Mwamalala, hatimaye mwanachama huyo ametangaza rasmi kujiunga na Chama cha Mageuzi ya Taifa (NCCR- Mageuzi).
Mwamalala, alisema harakati za kisiasa alizianza tangu akiwa kijana, kuwa muumini wa siasa za upinzani na rasmi alijiunga na Chadema.
Alisema ameamua kujiunga na Chama hicho kutokana na ukweli kwamba ndicho chama kinachoonekana kuwa chama chenye utu, misingi bora ya usawa, uheshimu wa haki za wanachama na Watanzania pamoja na mshikamano.
“Kwa furaha kubwa kabisa na penda kuchukua fursa hii kuwatangazia Wanambeya na umma wa Watanzania kwa kuvunja ukimya na sasa natangaza kujiunga na chama cha NCCR-Mageuzi na nisema kuwa huu ni mwanzo tu mimi nimetangulia na wengine watakuja au kufuata hatua kwa hatua”alisema Mwamalala.
Hata hivyo, Mwamalala alipinga kuwa alifukuzwa chama bali kilichotokea ni kwamba mwanzoni mwa Januari 3 mwaka huu alitangaza kujiuzulu nafasi zote za uongozi ndani ya Chadema ikiwa ni pamoja na kujivua uanachama wa chama hicho.
Pamoja na kudai kuwa hajafukuzwa, taarifa za Chama hicho zinaeleza kuwa Mwamalala alifukuzwa uwanachama tangu mwaka jana.
Mwamalala, alisema harakati za kisiasa alizianza tangu akiwa kijana, kuwa muumini wa siasa za upinzani na rasmi alijiunga na Chadema.
Alisema ameamua kujiunga na Chama hicho kutokana na ukweli kwamba ndicho chama kinachoonekana kuwa chama chenye utu, misingi bora ya usawa, uheshimu wa haki za wanachama na Watanzania pamoja na mshikamano.
“Kwa furaha kubwa kabisa na penda kuchukua fursa hii kuwatangazia Wanambeya na umma wa Watanzania kwa kuvunja ukimya na sasa natangaza kujiunga na chama cha NCCR-Mageuzi na nisema kuwa huu ni mwanzo tu mimi nimetangulia na wengine watakuja au kufuata hatua kwa hatua”alisema Mwamalala.
Hata hivyo, Mwamalala alipinga kuwa alifukuzwa chama bali kilichotokea ni kwamba mwanzoni mwa Januari 3 mwaka huu alitangaza kujiuzulu nafasi zote za uongozi ndani ya Chadema ikiwa ni pamoja na kujivua uanachama wa chama hicho.
Pamoja na kudai kuwa hajafukuzwa, taarifa za Chama hicho zinaeleza kuwa Mwamalala alifukuzwa uwanachama tangu mwaka jana.
MTWARA : SERIKALI INAVUNJA NCHI KWA KUTOSIKILIZA WANANCHI
Mbunge wa Kigoma Kaskazini(CHADEMA)na Mwenyekiti wa kamati ya Bunge Ya Mashirika ya Umma Mheshimiwa Zitto Kabwe
Kwa wiki ya tatu mfululizo kumekuwa na malumbano kuhusiana na suala la ujenzi wa Bomba la gesi kutoka Mtwara mpaka Dar es Salaam. Kumekuwa na madai yenye nguvu ya hoja kutoka kwa wananchi wa Mtwara dhidi ya porojo kutoka kwa viongozi wenye dhamana ya kujibu madai haya ya watu wa Mtwara. Watu wa Mtwara kwa umoja wao na kwa kuungwa mkono na viongozi wa dini zote wamekuwa wakitaka Serikali ifikirie upya suala la mradi wa ujenzi wa Bomba la gesi na badala yake kujenga mitambo ya kufua umeme mkoani Mtwara na kusafirisha umeme huo kwenda maeneo mengine ya nchi. Kwenye moja ya maandishi yangu (Serikali iwasikilize watu wa Mtwara) nimeshauri kuwa Taifa liwe na gridi nyingine ya Taifa ambayo itatokana na Gesi tu na ianzie Mtwara.
Kwa wiki ya tatu mfululizo kumekuwa na malumbano kuhusiana na suala la ujenzi wa Bomba la gesi kutoka Mtwara mpaka Dar es Salaam. Kumekuwa na madai yenye nguvu ya hoja kutoka kwa wananchi wa Mtwara dhidi ya porojo kutoka kwa viongozi wenye dhamana ya kujibu madai haya ya watu wa Mtwara. Watu wa Mtwara kwa umoja wao na kwa kuungwa mkono na viongozi wa dini zote wamekuwa wakitaka Serikali ifikirie upya suala la mradi wa ujenzi wa Bomba la gesi na badala yake kujenga mitambo ya kufua umeme mkoani Mtwara na kusafirisha umeme huo kwenda maeneo mengine ya nchi. Kwenye moja ya maandishi yangu (Serikali iwasikilize watu wa Mtwara) nimeshauri kuwa Taifa liwe na gridi nyingine ya Taifa ambayo itatokana na Gesi tu na ianzie Mtwara.
MABAO 3 DHIDI YA MABAO 2 NDIYO YALIIPA YANGA USHINDI
Wachezaji wa Young Africans wakisalimiana na wachezaji wa Black Leopard kabla ya kuanza kwa mchezo
Mabingwa wa kombe la Vilabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati almaarufu kombe la Kagame, timu ya Young Africans Sports Club imeifunga timu ya Black Leopard ya Afrika Kusini mabao 3-2 katika mchezo wa kirafiki uliofanyika leo jioni katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaaam.
Young Africans iliyokuwa nje ya nchi kwa kambi ya mafunzo takribani wiki ilikuwa ikicheza mbele ya washabiki wake, iliweza kucheza soka safi na la kuvutia kipindi chote cha mchezo huku Black Leopard ikipata wakati mgumu kwa dakika 45 za kipindi cha kwanza.
Didider Kavumbagu alikosa bao la wazi dakika ya 21 ya mchezo akiwa yeye na mlinda mlango wa Black Leopard Ayanda Mtshali, lakini shuti alilopiga lilipaa juu ya lango la timu hiyo.
Mabingwa wa kombe la Vilabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati almaarufu kombe la Kagame, timu ya Young Africans Sports Club imeifunga timu ya Black Leopard ya Afrika Kusini mabao 3-2 katika mchezo wa kirafiki uliofanyika leo jioni katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaaam.
Young Africans iliyokuwa nje ya nchi kwa kambi ya mafunzo takribani wiki ilikuwa ikicheza mbele ya washabiki wake, iliweza kucheza soka safi na la kuvutia kipindi chote cha mchezo huku Black Leopard ikipata wakati mgumu kwa dakika 45 za kipindi cha kwanza.
Didider Kavumbagu alikosa bao la wazi dakika ya 21 ya mchezo akiwa yeye na mlinda mlango wa Black Leopard Ayanda Mtshali, lakini shuti alilopiga lilipaa juu ya lango la timu hiyo.
Sunday, January 20, 2013
MALKIA WA NYUKI: NITASHINDANA NA MANJI
-BILIONEA WA MAFUTA ANAYETAKA KUIFIKISHA SIMBA MBALI
-AISHI JUMBA LA MABILIONI, AELEZA NDOTO ZAKE MSIMBAZI
RAHMA Al Kharusi si jina geni katika mchezo wa soka Tanzania, wengi wanamkumbuka wakati alipoamua kuingia katika kuisaidia Twiga Stars na baadaye akaipeleka nchini Marekani lakini baadaye akapotea.
Akarejea akiwa upande wa African Lyon, akasaidia mambo mengi na kufanya timu hiyo izidi kupata umaarufu, lakini baadaye hakuonekana hadi alipokuja kuibukia Simba na kusema hapo ndiyo nyumbani.
Mfanyabiashara huyo bilionea anasisitiza ametua Simba baada ya kuombwa kukubali uteuzi wa mjumbe wa kamati ya utendaji na anaamini atakuwa mshindani mkubwa wa kuleta maendeleo.
Anataka kuiona Simba ikiwa na mambo mengi yenye mabadiliko, lakini anataka timu ya wanawake pamoja na timu imara ya vijana ambayo itaiwezesha Simba kuwa na msingi hapo baadaye.
“Simba walikuja kuniomba, sikuona kama kuna ubaya wa kukubali kuingia. Wakati tunakua nyumbani nilikuwa nikimuona baba yangu akiisaidia Simba, nasi tukajikuta tunaingia Simba. Tangu nikiwa mdogo, hii ndiyo timu yangu.
Rahma ni Rais wa Makampuni ya RBP Oil ambayo yanafanya biashara mbalimbali katika nchi tofauti za Afrika. Baadhi ya biashara hizo ni uuzaji wa mafuta ya ‘dizeli’ na petrol katika nchi mbalimbali, lakini pia vyakula pamoja na samani za ndani.
Nchi za Afrika ambazo makampuni yake yanafanya kazi ni pamoja na Tanzania, DR Congo, Sudan Kusini na Uganda lakini pia kampuni zake zinafanya biashara katika nchi za Oman na Qatar.
Rahma, maarufu kama Queen of Bees, yaani Malkia wa Nyuki, anataka Simba yenye mabadiliko makubwa huku akitumia msemo wa, “Nikianza jambo, lazima nilimalize.”
Safari Oman:
Ilikuwa Simba wapelekwe sehemu moja inaitwa Nizwa, ni kama kilomita 150 kutoka hapa Muscat, nikaona si sahihi. Natumia kama milioni 80 au zaidi kuihudumia Simba hapa maana wenyeji wao Fanja nao kama hawaihudumii vilivyo.
Sipendi wafike hapa halafu wateseke, ndiyo maana mambo yote ninayafanya kupitia RBP Group. Najua Simba inajiandaa na nina mpango wa kufanya mengi makubwa ikiwezekana.
“Huo ni ushabiki, lakini ninachotaka mimi ni maendeleo. Najua kuna presha kubwa kutoka kwa Yanga, mimi nitaichukulia kama changamoto na nitashindana kuleta maendeleo. Najua Yanga wanaye (Yusuf) Manji, nitashindana naye sana.
“Najua nikishindana na Manji nitaleta maendeleo upande wa Simba, lakini nitapenda uwe ushindani wa kimaendeleo na si zaidi. Kama nitaona ni ushindani wa kutaka kuumizana nitajiweka kando, nataka maendeleo ambayo ndiyo mafanikio.
“Sitaki ugomvi, ndiyo maana utaona nilijiondoa Twiga na African Lyon. Migogoro ni kati ya vitu nisivyopenda kabisa, halafu Manji ni mtu ninayeheshimiana naye sana. Hivyo sitaki malumbano ila ushindani wa kuleta maendeleo.
Bima:
Tayari tupo katika hatua za mwisho, ndani ya siku moja wachezaji wa Simba na viongozi watakatiwa bima ya maisha. Naamini ni kitu kizuri wakiwa na bima hasa hapa ugenini.
Najua fedha nyingi pia zitatumika lakini naona ni jambo la busara kufanya hivyo, maana sisi ni binadamu na hauwezi kujua kitakachotokea kesho.
Familia, kazi, Simba:
Kweli ni kitu kigumu sana, lakini hayo tayari ni majukumu yangu. Ninapenda kufanya kazi kwa kujituma sana. Wakati mwingine nakesha nikifanya kazi hadi asubuhi maana nina ofisi nyingine Marekani, hivyo kuna vitu navifanya nikiwa hapa Oman au Tanzania, unajua tena dunia sasa ni kama kijiji.
Ugumu utakuwepo lakini sipendi kufeli katika lolote, ndiyo maana napenda kujituma ili nifanikishe kitu ambacho nimekianzisha au nimeingia na kuanza kukifanya.
Ubora:
Ninaamini Simba ni timu bora, lakini lazima wajiandae vizuri na kufanya mambo kitaalamu. Kama watajaribu kubahatisha wataharibu kila kitu. Lakini kujituma pia ni msingi wa maendeleo, hivyo lazima kuwe na watu wenye nia ya kupata mafanikio.
Sisemi Simba itashinda kila siku, lakini ikipoteza basi lazima kuwe na hali ya kukubali, pia ni lazima watu wajitathmini kwa nini wamejikwaa. Mimi pia ninapenda kuona timu yangu inashinda kama ilivyo kwa mashabiki.
Malkia wa Nyuki:
Hili jina nimebatizwa na watu kutokana na tabia yangu ya kupenda kufanya kazi kwa ushirikiano, lakini mara nyingi nimekuwa nikizungukwa na watu ambao wanapenda kuniona nipo salama.
Lakini kifamilia kuna jambo moja, karibu nyumba zangu zote, nyuki wamekuwa wakitengeneza mzinga. Hali hii imewashangaza ndugu na marafiki zangu wengi, hata mimi mwenyewe. Tayari nimelizoea hilo jina na ninaona kawaida ingawa sikulikusudia.
Rahma anaishi katika eneo la Al Kheri, moja ya vitongoji maarufu vya Jiji la Muscat, watu wengi wenye uwezo wa fedha wanaishi eneo hilo.
Nyumba yake inaweza kufikia thamani ya zaidi ya Sh bilioni 1.8, imejengwa kisasa huku ikiwa na mambo kadhaa ya kuvutia utafikiri zile nyumba za mastaa wa Hollywood au wanamuziki maarufu wa Marekani.
Ingawa kuna nyumba nyingi bora katika eneo hilo, bado yake inachomoza pekee na kuonekana moja ya nyumba bora kabisa.
Ukiingia getini, gari inapanda hadi juu ghorofa ya kwanza ambako ndiko kuna sebule, kila moja ikiwa imetengenezwa kwa mfumo wake. Ndani kuna sebule tatu huku kukiwa na vyumba zaidi ya vitano vya kulala.
Kuna vyumba viwili tofauti vya kulia chakula, kuna bwawa la kuogelea lililo ndani ambamo hakuna jua na AC zinawashwa ili kuleta kipupwe. Juu ya bwawa hilo kuna maporomoko ya maji ambayo yanaongozwa na umeme na kuna ukuta wa mawe ambao unafanya eneo hilo liwe kama ziwani.
Mbele ya bwawa hilo la kuogelea kuna ukumbi mdogo ambao bendi au kikundi cha taarabu cha watu kinaweza kutumbuiza na watazamani hadi 70 wakaingia na kuburudika kwa raha zao.
Ndani ya nyumba hiyo kuna ofisi kubwa ikiwa na chumba kidogo cha mikutano ambayo mara nyingi huitumia kufanya kazi zake kama anaamua kutotoka nje.
Kwa kuwa nyumba hiyo inajitosheleza kwa kila kitu, wakati mwingine Malkia huyo wa Nyuki, mama wa watoto pacha, hujikuta akiishi ndani ya nyumba hiyo hata mwezi mzima bila kutoka nje.
Subscribe to:
Posts (Atom)












































