Monday, February 2, 2015
Sunday, January 18, 2015
Wednesday, December 31, 2014
TAARIFA YA UFAFANUZI WIZARA YA NISHATI NA MADINI
Katika gazeti la NIPASHE la Jumatatu tarehe 08 Desemba, 2014 ziliandikwa habari kuhusu Waziri wa Nishati na Madini, Prof. Sospeter Muhongo (Mb) chini ya kichwa cha habari "Wanaomtetea Muhongo Wajibu haya". Hoja zilizotolewa katika gazeti hilo zililenga kupotosha ukweli. Wizara inapenda kutoa maelezo kuhusu hoja zilizotolewa kama ifuatavyo:
Utendaji wa Wizara chini ya Waziri wa Nishati na Madini, Prof. Sospeter Muhongo (Mb)
Taarifa za gazeti hilo zilieleza kuwa utendaji wa Wizara ya Nishati na Madini hasa katika uongozi wa Waziri Muhongo umekuwa ni wa kukatisha tamaa. Moja ya mifano iliyotolewa ni kuendelea kuwepo kwa wachimbaji madini wanaozidi kutorosha madini kwa nia ya kukwepa kodi.
DOKTA AONYA MIMBA YA AUNT!
TABIA za mitoko ya usiku matembezini, uvaaji viatu virefu na unywaji pombe unaofanywa na wamama wajawazito, kama alivyo sasa muigizaji Aunt Ezekiel, zimeelezewa kuwa si nzuri na zina uwezekano mkubwa wa kusababisha madhara kwa mtoto anayetarajiwa kuzaliwa.Akizungumza baada ya kuulizwa na gazeti hili juu ya mwenendo wa muigizaji Aunt Ezekiel ambaye mara kadhaa huonekana akiwa 'viwanja' usiku, daktari mtaalamu wa magonjwa ya kina mama na watoto, aliyejitambulisha kwa jina moja la Dokta Chale, alisema utokaji wa usiku na uvaaji wa viatu virefu unaweza kusababisha matatizo ya nyonga, shida wakati wa kujifungua, miguu kuuma na uvimbe kwenye vifundo vya miguu 'enka'.
Kuhusu unywaji pombe, Dokta Chale alisema endapo mama mjamzito atafanya tabia hiyo, ipo hatari ya uelewa wa mtoto katika ukuaji wake kuwa mdogo na pia kuchukua tabia zote za mama yake."Viatu virefu na mitoko ya usiku kwa mama mjamzito ina madhara makubwa sana kwani mtoto atakuwa na uelewa mdogo, yaani akili yake inakuwa haikui sawasawa, kifupi ana-adapti (kuiga) tabia zote za mama yake anaweza kuwa zezeta kama mama anatumia pombe," alisema.
Katika kudhihirisha kuwa ustaa ni kazi kubwa, licha ya ujauzito wake kuonekana mkubwa, Aunt Ezekiel amekuwa akijirusha kama kawaida sehemu mbalimbali nyakati za usiku huku wakati mwingine akiwa amevaa viatu virefu..
Globalpublishers
Kuhusu unywaji pombe, Dokta Chale alisema endapo mama mjamzito atafanya tabia hiyo, ipo hatari ya uelewa wa mtoto katika ukuaji wake kuwa mdogo na pia kuchukua tabia zote za mama yake."Viatu virefu na mitoko ya usiku kwa mama mjamzito ina madhara makubwa sana kwani mtoto atakuwa na uelewa mdogo, yaani akili yake inakuwa haikui sawasawa, kifupi ana-adapti (kuiga) tabia zote za mama yake anaweza kuwa zezeta kama mama anatumia pombe," alisema.
Katika kudhihirisha kuwa ustaa ni kazi kubwa, licha ya ujauzito wake kuonekana mkubwa, Aunt Ezekiel amekuwa akijirusha kama kawaida sehemu mbalimbali nyakati za usiku huku wakati mwingine akiwa amevaa viatu virefu..
Globalpublishers
Hakimu ajitoa kesi ya jumuiya ya Uamsho
Dar es Salaam.Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Kisutu, Hellen Liwa amejitoa kusikiliza kesi ya ugaidi inayowakabili viongozi 23 wa Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu Zanzibar (JUMIKI).
Ni baada ya wakili wa washtakiwa hao wa ugaidi, Abubakar Salim kumtaka ajitoe kuisikiliza kesi hiyo ili iweze kupangiwa hakimu mwingine ambaye atatoa uamuzi juu ya hoja zao walizozitoa mahakamani hapo Septemba 19,2014.
Salim aliiambia mahakama kuwa baada ya kushauriana na wateja wao na uamuzi uliotolewa na Jaji wa Mahakama Kuu, Dk Fauzi Twaib wakaona kuwa ni ukweli kuwa Hakimu Liwa alikwisha toa uamuzi wake juu ya hoja zao Oktoba Mosi, 2014 kuwa mahakama hiyo ya kisutu haina mamlaka ya kuzikiliza.
Alidai Mahakama Kuu katika uamuzi wake uliotolewa na Jaji Twaib umeelekeza kuwa Mahakama ya Kisutu inayo mamlaka ya kuzisikiliza hoja za washtakiwa hao wa ugaidi na hata kuzitolea uamuzi.
Miss Tanzania 2014 asaidia kituo cha New Life Orphans Home,Boko jijini Dar
Miss Tanzania Lilian Kamazima (kulia) akimkabidhi zawadi ya mwaka mpya
Msimamizi wa kituo cha kulelea watoto yatima cha New Life kilichopo
Boko, Mwanaisha Magambo kwa ajili ya watoto 102 waliopo kituoni hapo,
tukio hilo lilifanyika juzi.
HAKIKA WANAWAKE TUNAWEZAAAA "MTUNZI MKONGWE WA VITABU ZANZIBAR AZINDUA VITABU VITATU VYA HADITHI ZA KALE"
Mtunzi mkongwe wa vitabu Zanzibar Bi. Fatma Moh’d Salim (Jinja) akionyesha vitabu vya hadithi za kale alivyovitunga, katika sherehe za uzinduzi wa vitabu hivyo zilizofanyika nyumbani kwake Chukwani Zanzibar.
Mwandishi wa Habari wa Redio Annur Fm Kasim Khamis akimuuliza suali Bi. Fatma Jinja kuhusiana na utunzi wa vitabu vyake alivyo vizindua.…
Baadhi ya waalikwa waliohudhuria sherehe za uzinduzi wa vitabu hivyo wakimskiliza Bi. Fatma Jinja (hayupo pichani) alipokuwa akitoa maelezo juu ya utunzi wa vitabu hivyo .
Waandishi wa Habari wakifanya mahojiano na mtunzi wa vitabu Bi. Fatma Jinja huko nyumbani kwake Chukwani Zanzibar baada ya uzinduzi wa vitabu vyake.
Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar.
SHEIKH SHARIF AZUA MAPYA YA URAIS 2015
Sheikh Shariff Matongo akizungumza leo na waandishi wa habari ofisini kwake jijini Dar es Salaam(hawapo pichani)kuhusu ndoto yake ambayo ameoteshwa kuelekea mwaka 2015.
Sheikh Sharif Matongo amesema ameoteshwa ndoto ya mwaka 2015 na kupata ushauri kwa mashekh mbalimbali duniani ambavyo vitatokea nchini na viongozi wasipuuze ndoto hiyo. Sharif aliyasema hayo leo ofisini kwake alipokutana na waandishi wa habari ,alisema ameoteshwa mambo saba likiwemo la kupata Rais ajaye ambaye kiongozi ambaye muda mwingi ameishi nje ya nchi kwa kufanya kazi.
Alisema katika ndoto nyingine kifo cha kiongozi mkubwa ambaye ameshika nyadhifa mbalimbali na na mwenye kambi katika Chama cha…
Subscribe to:
Posts (Atom)


