Wednesday, August 22, 2012
TTB yawatunuku Vyeti watanzania waliofanya vyema katika Utalii
Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii nchini Tanzania TTB Dk Aloyce Nzuki wa tatu kutoka kushoto akiwa katika picha ya pamoja na watanzania hao wakiwa wameshika vyeti vyao kushoto ni Wilfred Moshi, Respicius Baitwa wa pili kutoka kulia na Juma K. Nugaz aka Antonio Nugaz wa tatu kutoka kushoto wengine ni Geofrey Meena Meneja Masoko wa TTB na Devotha Mdachi Mkurugenzi wa Masoko wa pili kutoka kushoto.
Bodi ya Utalii Tanzania TTB leo imetoa vyeti kwa watanzania watatu walioipeperusha vyema bendera ya Tanzania katika masuala ya Utalii.
Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii nchini Tanzania Dk Aloyce Nzuki Akizungumza na waandishi wa habari kwa ajili ya tukio muhimu la kuwatunikia vyeti watanzania wa tatu amesema watanzania hao waliweza kupeperusha bendera ya Tanzania vizuri hasa katika masuala ya utalii, kwa hapa Tanzania na nchi za nje.
Watanzania hawa wameweza kufanya mambo makubwa ambayo kwa kiasi kikubwa sana yamechangia kwenye sekta ya utalii.Watanzania ambao tunaowapa tuzo leo ni pamoja na
Mr. Respicias H. Baitwa
Mr. Wilfred Moshi
Mr. Juma K. Nugaz
1. Mr. Respicius BaitwaNi mtanzania wa kwanza ambaye ameweka rekodi ya Afrika kwa mwafrika wa kwanza anatarajia kupanda vilele saba virefu katika mabara yalioko duniani. Mr. Baitwa mpaka sasa ameshapanda vilele 4. Ameshapanda kilele cha kwanza Mt. Kilimanjaro zaidi ya mara 100, amepanda Elbrus kilele kirefu katika nchi za ulaya, Aconcagua, Argentina na Kosciusko Australia.
2. Mr. Wilfred Moshi
Wilfred Moshi amekuwa mtanzania wa kwanza kupanda kilele kirefu kuliko vyote duniani kilele cha mlima Everest. Wilifred Mosha alipanda mlima Everest mwezi may 2012 na amekua mwafrika wa 3 kupanda na kufika kilele cha mlima Everest, na kupandisha bendera ya Tanzania kwa kufanya hivyo Wilifred Mosha ameweza kutangaza jina la Tanzania na kwenye mahojiano mbalimbali na vyombo vya habari duniani ameweza kutangaza vivutio vya utalii wa Tanzania kwa ujumla wake.
3. Mr. Juma K. Nugaz (Antonio Nugaz)
Juma Nugaz mtayarishaji wa kipindi cha utalii cha Kambi Popote kinachorushwa na clouds TV amekuwa mtangazaji bora katika kuhakikisha utalii wa ndani kwa mwaka 2012 tuzo iliytolewa na chama cha waandishi wa habari Tanzania.
Mr. Juma Nugaz amekuwa mstari wa mbele katika kuhamasisha utalii wa ndani kupitia kipindi cha kambi popote na amekuwa akitembelea bila kuchoka vivutio vya utalii na mwaka jana mwezi wa Disemba aliweza kurekodi kipindi maalum wakati wa zoezi la kupanda mlima kwa baadhi ya watanzania katika sherehe za kuazimisha miaka hamsimi (50) wa Tanzania bara ya Uhuru.Tunampongeza sana.
Bodi ya utalii Tanzania inawapongeza watanzania hawa kwa kufanya juhudi kubwa ya kutangaza vivutio vyetu vya utalii wa Tanzania na tutaendea kushirikiana nao kutangaza vivutio vyetu zaidi.
Pamoja na kuwazawadia cheti hiki vilevile tunawazawadia safari ya kitalii kwenda mbuga za wanyama za Selous kwa siku nne na familia zao.
Bodi ya Utalii Tanzania TTB leo imetoa vyeti kwa watanzania watatu walioipeperusha vyema bendera ya Tanzania katika masuala ya Utalii.
Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii nchini Tanzania Dk Aloyce Nzuki Akizungumza na waandishi wa habari kwa ajili ya tukio muhimu la kuwatunikia vyeti watanzania wa tatu amesema watanzania hao waliweza kupeperusha bendera ya Tanzania vizuri hasa katika masuala ya utalii, kwa hapa Tanzania na nchi za nje.
Watanzania hawa wameweza kufanya mambo makubwa ambayo kwa kiasi kikubwa sana yamechangia kwenye sekta ya utalii.Watanzania ambao tunaowapa tuzo leo ni pamoja na
Mr. Respicias H. Baitwa
Mr. Wilfred Moshi
Mr. Juma K. Nugaz
1. Mr. Respicius BaitwaNi mtanzania wa kwanza ambaye ameweka rekodi ya Afrika kwa mwafrika wa kwanza anatarajia kupanda vilele saba virefu katika mabara yalioko duniani. Mr. Baitwa mpaka sasa ameshapanda vilele 4. Ameshapanda kilele cha kwanza Mt. Kilimanjaro zaidi ya mara 100, amepanda Elbrus kilele kirefu katika nchi za ulaya, Aconcagua, Argentina na Kosciusko Australia.
2. Mr. Wilfred Moshi
Wilfred Moshi amekuwa mtanzania wa kwanza kupanda kilele kirefu kuliko vyote duniani kilele cha mlima Everest. Wilifred Mosha alipanda mlima Everest mwezi may 2012 na amekua mwafrika wa 3 kupanda na kufika kilele cha mlima Everest, na kupandisha bendera ya Tanzania kwa kufanya hivyo Wilifred Mosha ameweza kutangaza jina la Tanzania na kwenye mahojiano mbalimbali na vyombo vya habari duniani ameweza kutangaza vivutio vya utalii wa Tanzania kwa ujumla wake.
3. Mr. Juma K. Nugaz (Antonio Nugaz)
Juma Nugaz mtayarishaji wa kipindi cha utalii cha Kambi Popote kinachorushwa na clouds TV amekuwa mtangazaji bora katika kuhakikisha utalii wa ndani kwa mwaka 2012 tuzo iliytolewa na chama cha waandishi wa habari Tanzania.
Mr. Juma Nugaz amekuwa mstari wa mbele katika kuhamasisha utalii wa ndani kupitia kipindi cha kambi popote na amekuwa akitembelea bila kuchoka vivutio vya utalii na mwaka jana mwezi wa Disemba aliweza kurekodi kipindi maalum wakati wa zoezi la kupanda mlima kwa baadhi ya watanzania katika sherehe za kuazimisha miaka hamsimi (50) wa Tanzania bara ya Uhuru.Tunampongeza sana.
Bodi ya utalii Tanzania inawapongeza watanzania hawa kwa kufanya juhudi kubwa ya kutangaza vivutio vyetu vya utalii wa Tanzania na tutaendea kushirikiana nao kutangaza vivutio vyetu zaidi.
Pamoja na kuwazawadia cheti hiki vilevile tunawazawadia safari ya kitalii kwenda mbuga za wanyama za Selous kwa siku nne na familia zao.
Makarani 800 Wagoma Kula Kiapo Cha Sensa
MAANDALIZI ya Sensa ya Watu na Makazi inayotarajiwa kufanyika Agosti 26, mwaka huu yameingia dosari baada ya matukio kadhaa ya kukwamisha kazi hiyo kujitokeza katika mikoa mbalimbali, ukiwamo Dar es Salaam ambako zaidi ya makarani 800 wamegoma kula kiapo cha utii na kutunza siri.Habari zilizopatikana jana zimeeleza kuwa mbali na makarani hao, vipeperushi vyenye ujumbe wa kutaka watu wagomee Sensa vimesambazwa mkoani Arusha, huku mkoani Tanga kukiwa na tukio la Sheikh mmoja kutiwa mbaroni kwa kusambaza vipeperushi vya aina hiyo.
Makarani hao waligoma jana ikiwa ni siku yao ya mwisho ya mafunzo ya kazi ya kuhesabu watu na makazi. Makarani hao kutoka vituo mbalimbali kulikotolewa mafunzo hayo, walisema wameamua kugomea kiapo hicho kutokana na fedha zilizotengwa kwa ajili ya malipo ya kazi hiyo kuchakachuliwa kinyume na makubaliano.
Baadhi ya vituo ambavyo makarani wake wamegoma ni Shule ya Sekondari Makumbusho, Kambangwa, Shule ya Msingi Zawadi na vituo kadhaa vilivyopo maeneo ya Buguruni na Kawe.Baadhi ya makarani hao walionekana wakiwa katika makundi, muda ambao walipaswa kuendelea na mafunzo yao kabla ya kula kiapo cha kushiriki Sensa kwa uaminifu na ukamilifu.Baadhi ya makarani ambao waliomba majina yao yasitajwe gazetini, walisema imekiuka makubaliano ya awali.
“Serikali imesema imetenga Sh141 bilioni kwa ajili ya Sensa. Sisi tayari tuliingia makubaliano nayo kwamba tunatakiwa kulipwa Sh35,000 kwa siku, kwa muda wa siku saba jambo ambalo limegeuka na kuwa kinyume.”
“Ukipiga mahesabu fedha ambazo tungetakiwa kulipwa kwa siku hizo saba ni Sh245,000 lakini wao wamekuja hapa na kutupa Sh140, 000 tu. Hatuwezi kuendelea na kazi mpaka tulipwe fedha zetu.”
Karani mmoja katika Kituo cha Sekondari ya Kambangwa, alisema wameamua kugomea kiapo baada ya kuona kuwa mpaka mafunzo yanahitimishwa jana, baadhi yao hawajalipwa chochote.
RC Dar:Watalipwa
Akizungumzia madai ya makarani hao, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadiki alisema mpaka jana mchana makarani wote walipaswa kulipwa awamu ya pili ya fedha zao. Alisema awamu ya kwanza ya malipo hayo ilifanywa katika siku tano za mwanzo.“Kuna watu wamejichomeka katika zoezi hili, lakini kama kweli karani ameteuliwa lazima atalipwa pesa zake na kama imetokea amesahaulika basi afanye mawasiliano na mratibu wa Sensa wilaya anayotoka ili alipwe,” alisema.
Sheikh mbaroni
Katika hatua nyingine Sheikh Juma Koosa (52) anashikiliwa na polisi wilayani Morogoro akituhumiwa kutumia kipaza sauti kuwatangazia wananchi wasishiriki Sensa.
Sheikh huyo ambaye pia ni mwanafunzi wa mwaka wa pili wa Chuo Kikuu cha Kiislamu Morogoro, alikamatwa Agosti 19 mwaka huu alipokuwa kwenye Msikiti wa Miembeni, Mazinde mara baada ya kukaribishwa na wenyeji wake kuzungumza.Imedaiwa kuwa Koosa alitoa kitabu chenye kueleza sababu za kuwakataza Waislamu kutokushiriki Sensa mwaka huu.
Chanzo: http://www.mwananchi.co.tz
Tuesday, August 21, 2012
Meles Zenawi Is Dead
July 31, 2012 — Prime Minsiter Meles Zenawi passed away from an unspecified aliment in a Brussels hospital, according to Ethiopian Satellite Radio and Television (ESAT) in its nightly raido broadcast.
Citing the International Crisis Group and western diplomatic sources for its claims, the Amsterdam-based news agency said the 57-year-old dictator's death is being covered up by the regime to buy time for a successor.
Meles, whose appearance is the daily diet of the State media, has not been publicly seen in 40 days, fueling speculations that his health has deteriorated. During his absence, he has missed key events, including the two-day AU Summit held in Addis Ababa and a number of state visits.
Last week, unnamed European diplomats told the AFP and the Telegraph news agencies that Meles was in 'critical' condition and may not survive his aliment.
The other day, veteran fighter and Tigrayan Peoples Liberation Front founder, Sehbat Nega, said Meles is still in a European hospital but is not sure to which country. This uncertainty comes two weeks after he said Meles would return within a few days.
Sources say a select few of TPLF bigwigs are in the know of Meles deteroriting health status. Even senior officials within the TPLF party are being kept in the dark to prevent a power struggle from within.
Talk of Meles' health troubles has Addis Ababa on edge. Recently, An Ethiopian court banned distribution of a newspaper that published front-page articles about premier's health on the grounds of endangering 'national security'.
Citing the International Crisis Group and western diplomatic sources for its claims, the Amsterdam-based news agency said the 57-year-old dictator's death is being covered up by the regime to buy time for a successor.
Meles, whose appearance is the daily diet of the State media, has not been publicly seen in 40 days, fueling speculations that his health has deteriorated. During his absence, he has missed key events, including the two-day AU Summit held in Addis Ababa and a number of state visits.
Last week, unnamed European diplomats told the AFP and the Telegraph news agencies that Meles was in 'critical' condition and may not survive his aliment.
The other day, veteran fighter and Tigrayan Peoples Liberation Front founder, Sehbat Nega, said Meles is still in a European hospital but is not sure to which country. This uncertainty comes two weeks after he said Meles would return within a few days.
Sources say a select few of TPLF bigwigs are in the know of Meles deteroriting health status. Even senior officials within the TPLF party are being kept in the dark to prevent a power struggle from within.
Talk of Meles' health troubles has Addis Ababa on edge. Recently, An Ethiopian court banned distribution of a newspaper that published front-page articles about premier's health on the grounds of endangering 'national security'.
Miss World Tanzania 2012 Arejea Kutoka China
Lisa Jensen (kulia) akila pozi ya picha na mmoja wa warembo waliofika
kumpokea Amisa Hassan. Lisa alifanikiwa kuingia Robo fainali za Top
Model na kumi na kumi bora ya Shindano la Multmedia Award 2012.
Miss World Tanzania 2012, Lisa Jensen amerejea jijini Dar es Salaam jana akitokea nchini China alipokwenda kuiwakilisha nchi katika mashindano ya Dunia mwaka huu na kupokelewa na viongozi kadhaa wa Kamati ya Miss Tanzania akiwepo Mkurugenzi wa Kino International Agency waandaaji wa Miss Tanzania, Hashim Lundenga (kulia) aliyefika uwanja wa ndege wa JNIA Dar es salaam kumpokea. Chanzo: www.mrokim.blogspot.com
Miss World Tanzania 2012, Lisa Jensen amerejea jijini Dar es Salaam jana akitokea nchini China alipokwenda kuiwakilisha nchi katika mashindano ya Dunia mwaka huu na kupokelewa na viongozi kadhaa wa Kamati ya Miss Tanzania akiwepo Mkurugenzi wa Kino International Agency waandaaji wa Miss Tanzania, Hashim Lundenga (kulia) aliyefika uwanja wa ndege wa JNIA Dar es salaam kumpokea. Chanzo: www.mrokim.blogspot.com
DK.Dalali Kafumu Avuliwa Ubunge Igunga!.
Kwa habari zilizotufikia hivi punde kutoka mahakamani kuwa mbunge wa Igunga kwa ruhusa ya CCM Dk. Peter Dalali Kafumu Amevuliwa Ubunge na Mahakama, Habari zaidi zitakujia hivi punde usikae mbali na blog hii
Sitta:Msiisubiri Serikali Kutaja Walioficha Mabilioni
WAZIRI wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta amewataka wanaotangaza kuwafahamu vigogo walioficha mabilioni ya fedha nje ya nchi kuwataja mara moja ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yao badala ya kuisubiri Serikali kufanya hivyo.Kauli hiyo ya Sitta ambaye pia ni Mbunge wa Urambo Mashariki (CCM), imekuja wakati baadhi ya wanasiasa, wakiwamo wabunge kutishia kuwataja watu hao, lakini wakisisitiza kuwa ni pale tu Serikali itakaposhindwa kufanya hivyo.
Utafiti uliofanywa na Shirika la Kimataifa la Fedha la Global Financial Integrity, unaonyesha kuwa tatizo la utoroshaji wa fedha nchini limekuwapo katika awamu zote za Serikali zilizoiongoza Tanzania, lakini Awamu hii ya Nne imetia fora.
Utafiti huo uliofanywa kuanzia mwaka 1970 hadi 2009, unaonyesha kuwa katika utawala wa Rais Jakaya Kikwete, fedha zilizofichwa nje ya nchi ni Dola za Marekani 7,967.4 milioni (sawa Sh12.7 trilioni).
Akizungumza katika mahojiano maalumu, kuhusu nini kifanyike ili kuiokoa Tanzania isiendelee kufilisiwa na watu wachache, Sitta alisema anasikitishwa na watu hao kuogopa na kuwaficha watu wanaofisadi mali za nchi na hasa pale inapokuwa wahusika ni vigogo wa Serikali.
Alisema vigogo hao ni sababu ya watu kupata kigugumizi katika hili akihoji : “Kwa nini linapokuwa ni suala linalowahusu hawa wanaoitwa vigogo hawatajwi?”
Sitta ambaye ameshika nyadhifa mbalimbali serikalini katika awamu tofauti, alisema haoni kama kuna kosa kumtaja hadharani mtu aliyeficha fedha nje ya nchi huku akisababisha Watanzania kuendelea kukabiliwa na maisha magumu.
“Watajwe! Kama ni Samuel Sitta ameficha fedha nje atajwe. Kwa kweli mimi sioni kama kuna dhambi yoyote kumtaja,” alisema Sitta huku akisisitiza kwamba huo ni msimamo wake binafsi unaotokana na uzoefu wake kwenye uongozi wa nchi na siyo kwa mamlaka aliyonayo ya Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki.
Alisema njia nzuri ya kukomesha tabia hiyo ni kuwataja na vyombo husika kuwafikisha mahakamani kwa kuzingatia kuwa sheria ni msumeno, haipaswi kubagua aliye mdogo au mkubwa kwa maana ya wadhifa katika nchi.Sitta ambaye pia aliwahi kuwa Spika wa Bunge alisema: “Swali la kwa nini hawatajwi, ni jambo la kushangaza.”
Alisema amesikia na kuwasoma baadhi ya wanasiasa wakitishia kuwa watawataja wahusika iwapo Serikali haitafanya hivyo, lakini akasema haoni sababu yoyote ya mtu kusita katika kuokoa taifa dhidi ya wizi wa fedha za umma.
“Haiwezekani kwa mwanasiasa yeyote katika nchi maskini kama Tanzania au kiongozi wa Serikali kuwa na utajiri wa mabilioni ya fedha.”
Alisema hata kama anafanya biashara, siyo rahisi kuwa na utajiri wa kiwango hicho hasa ikizingatiwa kuwa hutumia muda mrefu kulitumikia taifa.
“Sisi tunaofanya kazi serikalini, tunatoka saa moja usiku. Sasa muda huo wa kufanya biashara ni saa ngapi?”
Tuhuma hizo ziliibuka bungeni Jumatano iliyopita baada ya Kambi ya Upinzani kudai kwamba nawafahamu wahusika wa ufisadi huo na kutishia kuwataja ikiwa Serikali haitafanya hivyo.
Chanzo http://www.mwananchi.co.tz
Utafiti uliofanywa na Shirika la Kimataifa la Fedha la Global Financial Integrity, unaonyesha kuwa tatizo la utoroshaji wa fedha nchini limekuwapo katika awamu zote za Serikali zilizoiongoza Tanzania, lakini Awamu hii ya Nne imetia fora.
Utafiti huo uliofanywa kuanzia mwaka 1970 hadi 2009, unaonyesha kuwa katika utawala wa Rais Jakaya Kikwete, fedha zilizofichwa nje ya nchi ni Dola za Marekani 7,967.4 milioni (sawa Sh12.7 trilioni).
Akizungumza katika mahojiano maalumu, kuhusu nini kifanyike ili kuiokoa Tanzania isiendelee kufilisiwa na watu wachache, Sitta alisema anasikitishwa na watu hao kuogopa na kuwaficha watu wanaofisadi mali za nchi na hasa pale inapokuwa wahusika ni vigogo wa Serikali.
Alisema vigogo hao ni sababu ya watu kupata kigugumizi katika hili akihoji : “Kwa nini linapokuwa ni suala linalowahusu hawa wanaoitwa vigogo hawatajwi?”
Sitta ambaye ameshika nyadhifa mbalimbali serikalini katika awamu tofauti, alisema haoni kama kuna kosa kumtaja hadharani mtu aliyeficha fedha nje ya nchi huku akisababisha Watanzania kuendelea kukabiliwa na maisha magumu.
“Watajwe! Kama ni Samuel Sitta ameficha fedha nje atajwe. Kwa kweli mimi sioni kama kuna dhambi yoyote kumtaja,” alisema Sitta huku akisisitiza kwamba huo ni msimamo wake binafsi unaotokana na uzoefu wake kwenye uongozi wa nchi na siyo kwa mamlaka aliyonayo ya Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki.
Alisema njia nzuri ya kukomesha tabia hiyo ni kuwataja na vyombo husika kuwafikisha mahakamani kwa kuzingatia kuwa sheria ni msumeno, haipaswi kubagua aliye mdogo au mkubwa kwa maana ya wadhifa katika nchi.Sitta ambaye pia aliwahi kuwa Spika wa Bunge alisema: “Swali la kwa nini hawatajwi, ni jambo la kushangaza.”
Alisema amesikia na kuwasoma baadhi ya wanasiasa wakitishia kuwa watawataja wahusika iwapo Serikali haitafanya hivyo, lakini akasema haoni sababu yoyote ya mtu kusita katika kuokoa taifa dhidi ya wizi wa fedha za umma.
“Haiwezekani kwa mwanasiasa yeyote katika nchi maskini kama Tanzania au kiongozi wa Serikali kuwa na utajiri wa mabilioni ya fedha.”
Alisema hata kama anafanya biashara, siyo rahisi kuwa na utajiri wa kiwango hicho hasa ikizingatiwa kuwa hutumia muda mrefu kulitumikia taifa.
“Sisi tunaofanya kazi serikalini, tunatoka saa moja usiku. Sasa muda huo wa kufanya biashara ni saa ngapi?”
Tuhuma hizo ziliibuka bungeni Jumatano iliyopita baada ya Kambi ya Upinzani kudai kwamba nawafahamu wahusika wa ufisadi huo na kutishia kuwataja ikiwa Serikali haitafanya hivyo.
Chanzo http://www.mwananchi.co.tz
Subscribe to:
Posts (Atom)







































