Nchi tatu zimekabidhiwa Tunzo kutokana na ubunifu wao katika Sekta ya Umma .
Nchi hizo zilizoshinda na kupewa Tunzo na Jumuiya ya Utumishi wa Umma katika Afrika na Uongozi AAPAM ni pamoja na Kenya, Mauritius na Ghana
Tunzo hizo zimetokana na kuwa wabunifu katika masuala mbalimbali ambapo Kenya imekuwa mshindi wa Kwanza kwa kupata medali ya dhahabu ikifuatiwa na Mauritius iliyopata Medali ya Fedha na Ghana iliyopata Medali ya Shaba.
Wakati huo huo Mkutano wa 34 wa AAPAM uliomalizika hivi leo hapa Zanzibar na kufungwa rasmi na Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar Balozi Seif Ali Idd umetoa maazimio mbalimbali yanayohusu Mkutano huo.
Miongoni mwa maazimio hayo ni kuwa na Mfumo bora na mzuri wa Utawala, kuimarisha mazingira juu ya nchi na Uongozi, Kuwashirikisha wadau wengine katika kuimarisha Utawala Bora na siyo Serikali kujipangia wao wenyewe tu.
Kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa AAPAM ameeleza kuwa Mkutano huo wa 34 umefanikiwa sana kutokana na mahudhurio ambapo Wajumbe 420 walihudhuria kutoka nchi 35 za Afrika na nje ya Afrika.
Mwaka jana Mkutano kama huo wa AAPAM uliofanyika nchini Malawi nchi 35 zilihudhuria ambapo wajumbe wapatao 210 ndio walioshiriki.
Katibu huyo wa AAPAM ameeleza kuwa tangu kufanyika Mikutano hiyo hii ni mara ya kwanza kwa wajumbe wengi kuhudhuria katika Mkutano huo na kuwa wa mafanikio makubwa.
Mkutano wa AAPAM hapo mwakani umeamuliwa kufanyika mjini Kigali,Rwanda.
Wajumbe kadhaa waliohudhuria Mkutano huo wameshaanza kuondoka hapa Zanzibar kurejea nyumbani.
IMETOLEWA NA IDARA YA HABARI MAELEZO ZANZIBAR.
Saturday, November 17, 2012
Safu ya Mkapa yarejea CCM
KUNA kila dalili kuwa Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete amekirejesha chama hicho katika mikono ya Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa, baada ya kuwateua katika nafasi za juu za CCM waliokuwa wasaidizi wa mtangulizi wake huyo.
Wasaidizi hao ni pamoja na Makamu Wenyeviti, Philip Mangula (Tanzania Bara) na Dk Ali Mohamed Shein (Tanzania Zanzibar) pamoja na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahaman Kinana, ambao walichaguliwa na kuteuliwa katika vikao vya juu vya CCM vilivyomalizika hivi karibuni mjini Dodoma.
Baadhi ya wachambuzi wa masuala ya kisiasa wanasema kwamba lengo la mabadiliko yaliyofanywa ni kujaribu kurejesha utaratibu wa CCM kuisimamia Serikali, utamaduni ambao ni kama ulikuwa umekufa, tangu Serikali ya awamu ya nne ilipoingia madarakani.
Mhadhiri wa zamani wa Chuo cha Ushirika Moshi, Akwiline Kinabo anasema kwamba kuna kila dalili kuwa Mkapa ana ushawishi katika uteuzi wa safu mpya katika sekretarieti ya chama hicho.
“Inawezekana Mangula, Kinana na Dk Shein walifanya vizuri sana enzi za Mkapa hadi akashawishi waingizwe kwenye sekretarieti ya sasa, lakini enzi za Mkapa na sasa ni kama mlima na kichuguu,” alisema.
Endelea nayo...www.kwanzajamii.com/?p=4356
Wasaidizi hao ni pamoja na Makamu Wenyeviti, Philip Mangula (Tanzania Bara) na Dk Ali Mohamed Shein (Tanzania Zanzibar) pamoja na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahaman Kinana, ambao walichaguliwa na kuteuliwa katika vikao vya juu vya CCM vilivyomalizika hivi karibuni mjini Dodoma.
Baadhi ya wachambuzi wa masuala ya kisiasa wanasema kwamba lengo la mabadiliko yaliyofanywa ni kujaribu kurejesha utaratibu wa CCM kuisimamia Serikali, utamaduni ambao ni kama ulikuwa umekufa, tangu Serikali ya awamu ya nne ilipoingia madarakani.
Mhadhiri wa zamani wa Chuo cha Ushirika Moshi, Akwiline Kinabo anasema kwamba kuna kila dalili kuwa Mkapa ana ushawishi katika uteuzi wa safu mpya katika sekretarieti ya chama hicho.
“Inawezekana Mangula, Kinana na Dk Shein walifanya vizuri sana enzi za Mkapa hadi akashawishi waingizwe kwenye sekretarieti ya sasa, lakini enzi za Mkapa na sasa ni kama mlima na kichuguu,” alisema.
Endelea nayo...www.kwanzajamii.com/?p=4356
Friday, November 16, 2012
Sekretarieti Mpya CCM Yapondwa Kila Kona
SIKU moja baada ya Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete kutangaza safu mpya ya wajumbe wa Sekretarieti ya chama hicho, wasomi, wanasiasa na viongozi wa dini wameponda uteuzi huo wakisema chama hicho tawala, kisitarajie jipya kutoka katika safu hiyo.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti na gazeti hili, wadau hao walisema viongozi walioteuliwa wana upungufu, hivyo hawawezi kuwajibishana kwa kuwa wanaogopa kuumbuana.
Katika uteuzi huo Kikwete aliwateua, Abdulrahaman Kinana kuwa Katibu Mkuu wa CCM, akisaidiwa na Mbunge wa Iramba Magharibi, Mwigulu Nchemba upande wa Bara na Vuai Ali Vuai upande wa Zanzibar.
Wengine ni Zakhia Meghji aliyeteuliwa kuwa Katibu wa Uchumi na Fedha, Mohamed Seif Khatib (Oganaizesheni), Dk Rose Migiro (Kimataifa) na Nape Nnauye (Uenezi).
Uteuzi huo ulitanguliwa na uchaguzi ambao ulimrejesha Kikwete kuwa Mwenyekiti wa chama wa Taifa akisaidiwa na Philip Mangula (Tanzania Bara) na Dk Ali Mohamed Shein (Zanzibar).
Hata hivyo, baadhi ya wachambuzi wa masuala ya siasa wanawatizama Mangula na Kinana kama viongozi makini, lakini wasioweza kumudu kasi ya siasa za sasa ambazo zimebadilika kulingana na wakati na aina ya ushindani kutoka upinzani.
Kadhalika wanakiona kikosi hicho kuwa hakiwezi kuisaidia CCM kupambana na rushwa, ambayo inaonekana kuota mizizi kiasi cha kuonekana kama sehemu ya utamaduni wa chama hicho.
Askofu Msaidizi wa Kanisa Katoliki Jimbo la Bukoba, Methodius Kilaini alisema safu hiyo ya uongozi haina jipya akifafanua kuwa, tatizo kubwa la chama hicho ni mfumo wake wa utendaji kazi.
“Ni mfumo ambao wamejiwekea wa kulindana, hivyo uongozi huu hautaleta mabadiliko yoyote CCM,” alisema Kilaini.
Alisema viongozi waliochaguliwa hawatakuwa na sauti kwa kuwa nao wana udhaifu wao hivyo hawawezi kuwachukulia hatua wenzao kwa kuwa nao wataumbuliwa.
Askofu Kilaini alisema viongozi hao wataendeleza mfumo walioukuta na hakuna atakayeweza kumkosoa mwenzake aliyefanya makosa.
“Kati ya viongozi wa CCM waliochaguliwa hakuna atakayemnyooshea mwenzake kidole kwamba amefanya kosa fulani, ni vigumu mno kumwadhibu mwenzake kwa kuhofia kuwa, kwa vile yeye pia ni dhaifu akimwadhibu huyo matendo yake yatagundulika,” alisema.
Alisema licha ya Rais Kikwete kukemea rushwa kwa viongozi wote waliochaguliwa, lakini hakuna hatua yeyote aliyochukuwa kwa wale waliotuhumiwa kujihusisha na vitendo hivyo wakati wa chaguzi za ndani ya CCM.
“Rais wetu anazungumzia rushwa na kukemea lakini hakuna aliyemchukulia hatua yoyote kwa wale waliokutwa wakitoa rushwa katika uchaguzi wa Umoja wa Vijana (UVCCM), Jumuiya ya Wazazi na Ujumbe wa Halmashauri Kuu (Nec),” alisema Kilaini.
Kauli za wasomi
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk Kitila Mkumbo alisema Watanzania wasitegemee mabadiliko katika safu mpya ya uongozi ya CCM kwa kuwa walioteuliwa hawana jipya.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti na gazeti hili, wadau hao walisema viongozi walioteuliwa wana upungufu, hivyo hawawezi kuwajibishana kwa kuwa wanaogopa kuumbuana.
Katika uteuzi huo Kikwete aliwateua, Abdulrahaman Kinana kuwa Katibu Mkuu wa CCM, akisaidiwa na Mbunge wa Iramba Magharibi, Mwigulu Nchemba upande wa Bara na Vuai Ali Vuai upande wa Zanzibar.
Wengine ni Zakhia Meghji aliyeteuliwa kuwa Katibu wa Uchumi na Fedha, Mohamed Seif Khatib (Oganaizesheni), Dk Rose Migiro (Kimataifa) na Nape Nnauye (Uenezi).
Uteuzi huo ulitanguliwa na uchaguzi ambao ulimrejesha Kikwete kuwa Mwenyekiti wa chama wa Taifa akisaidiwa na Philip Mangula (Tanzania Bara) na Dk Ali Mohamed Shein (Zanzibar).
Hata hivyo, baadhi ya wachambuzi wa masuala ya siasa wanawatizama Mangula na Kinana kama viongozi makini, lakini wasioweza kumudu kasi ya siasa za sasa ambazo zimebadilika kulingana na wakati na aina ya ushindani kutoka upinzani.
Kadhalika wanakiona kikosi hicho kuwa hakiwezi kuisaidia CCM kupambana na rushwa, ambayo inaonekana kuota mizizi kiasi cha kuonekana kama sehemu ya utamaduni wa chama hicho.
Askofu Msaidizi wa Kanisa Katoliki Jimbo la Bukoba, Methodius Kilaini alisema safu hiyo ya uongozi haina jipya akifafanua kuwa, tatizo kubwa la chama hicho ni mfumo wake wa utendaji kazi.
“Ni mfumo ambao wamejiwekea wa kulindana, hivyo uongozi huu hautaleta mabadiliko yoyote CCM,” alisema Kilaini.
Alisema viongozi waliochaguliwa hawatakuwa na sauti kwa kuwa nao wana udhaifu wao hivyo hawawezi kuwachukulia hatua wenzao kwa kuwa nao wataumbuliwa.
Askofu Kilaini alisema viongozi hao wataendeleza mfumo walioukuta na hakuna atakayeweza kumkosoa mwenzake aliyefanya makosa.
“Kati ya viongozi wa CCM waliochaguliwa hakuna atakayemnyooshea mwenzake kidole kwamba amefanya kosa fulani, ni vigumu mno kumwadhibu mwenzake kwa kuhofia kuwa, kwa vile yeye pia ni dhaifu akimwadhibu huyo matendo yake yatagundulika,” alisema.
Alisema licha ya Rais Kikwete kukemea rushwa kwa viongozi wote waliochaguliwa, lakini hakuna hatua yeyote aliyochukuwa kwa wale waliotuhumiwa kujihusisha na vitendo hivyo wakati wa chaguzi za ndani ya CCM.
“Rais wetu anazungumzia rushwa na kukemea lakini hakuna aliyemchukulia hatua yoyote kwa wale waliokutwa wakitoa rushwa katika uchaguzi wa Umoja wa Vijana (UVCCM), Jumuiya ya Wazazi na Ujumbe wa Halmashauri Kuu (Nec),” alisema Kilaini.
Kauli za wasomi
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk Kitila Mkumbo alisema Watanzania wasitegemee mabadiliko katika safu mpya ya uongozi ya CCM kwa kuwa walioteuliwa hawana jipya.
RAIS KIKWETE AWASILI ARUSHA, VIONGOZI WA DINI WAMPONGEZA NA KUMUOMBEA MAFANIKIO ZAIDI
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipokelewa na viongozi wa dini mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro jana jioni Novemba 15, 2012 tayari kwa ziara ya siku tatu ya kikazi mkoani Arusha.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiombewa dua na viongozi wa dini mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro jana Novemba 15, 2012 tayari kwa ziara ya siku tatu ya kikazi mkoani Arusha.
(PICHA NA IKULU)
Subscribe to:
Posts (Atom)

























































