Thursday, November 29, 2012

VIONGOZI WA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI WAZINDUA BARABARA YA ARUSHA-NAMANGA-ATHI RIVER

 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Jomo Kenyatta jijini Nairobi Kenya Jumatano Novemba 28, 2012 tayari kuhudhuria sherehe za ufunguzi wa barabara ya Arusha-Namanga-Athi River pamoja na Mkutano wa Wakuu wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki utaozungumzia maendeleo ya miundombinu. Kiongozi wa Jumuiya ya Waislamu wa Ismailia Mtukufu Aga Khan naye alikuwepo hapo uwanjani.
                            Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipanda mti wakati wa uzinduzi wa barabara hiyo
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete na viongozi wenzie wa nchi wanachama za Jumuiya ya Afrika Mashariki wakikata utepe kwa pamoja kuzindua  rasmi wa Barabara ya Arusha – Namanga – Athi River yenye  urefu wa kilometa 104.4 kwa upande wa Tanzania




 Baadhi ya mawaziri na makatibu wakuu wa Tanzania waliohudhuria sherehe za uzinduzi rasmi wa barabara ya Arusha – Namanga – Athi River yenye  urefu wa kilometa 104.4 kwa upande wa Tanzania
              Rais Jakaya Kikwete akitoaa hotuba yake wakati wa uzinduzi wa barabara hiyo





Rais Jakaya Mrisho Kikwete na viongozi wenzie wa nchi wanachama za Jumuiya ya Afrika Mashariki wakifurahia mara baada ya kuzindua rasmi ujenzi wa barabara hiyo kwa kukata utepe.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na viongozi wenzie wa nchi wanachama za Jumuiya ya Afrika Mashariki  wakiwa katika picha ya pamoja na wadau mbalimbali waliofanikisha ujenzi wa barabara ya Arusha – Namanga      

Makamu Wa Rais Dkt. Bilal Aagana Na Rais Wa Kenya Mwai Kibaki

  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na Rais wa Kenya, Mwai Kibaki, ambaye ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro, mara baada ya ufunguzi wa Jengo la ofisi za Jumuiya hiyo iliyofanyika Jijini Arusha jana, Nove 28, 2012.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipunga mkono kuwaaga wananchi baada ya kumsindikiza Rais wa Kenya, Mwai Kibaki, ambaye ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro, mara baada ya ufunguzi wa Jengo la ofisi za Jumuiya hiyo iliyofanyika Jijini Arusha jana, Nove 28, 2012

Maadhimisho Kupinga Ukatili Dhidi Ya Wanawake

                                                                  Mkuu wa mkoa wa singida
 Kikundi cha nyota njema kikitumbuiza ngoma ya asili ya kabila la Kinyaturu wakati wa maadhimisho ya siku ya kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia

SERIKALI imeyataka mashirika ya kiraia kushirikiana pamoja, ili kupiga vita na hatimaye kutokomeza kabisa vitendo vinavyosababisha ukatili wa kijinsia, hususani wanavyofanyiwa wanawake na watoto wadogo nchini.

Hayo yamebainishwa mjini Singida na mkuu wa mkoa huo, Dk. Parseko Kone, kwenye maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili dhidi ya wanawake, yaliyoadhimishwa kitaifa katika viwanja vya Peoples, mjini Singida, jana.

Maadhimisho hayo, yamefanyika mkoani Singida, kwa ushirikiano wa mashirika 16 hapa nchini, yaliyoipa dhamana ya kusimamia sherehe hizo, shirika la Action Aid-Singida,huku kauli mbiu yake ikiwa ‘FUNGUKA! Kemea ukatili dhidi ya wanawake, sote tuwajibike’.

Dk. Kone alisema kuwa, kutokana na changamoto nyingi zinazowakabili wanawake ikiwemo ukatili wanaofanyiwa na wanaume, serikali kwa kushirikiana na mashirika ya kirai bado yanayo kazi kubwa katika kuungana pamoja ili kutokomeza unyanyasaji huo.

“Madhara yatokanayo na ukatili kwa wanwake katika jamii hupunguza nguvu kazi ya Taifa, baadhi ya madhara ya ukatili huo ni mauaji ya wanawake, ulemavu wa kudumu wa viungo…kupungua kwa uzalishaji kwa kuwa mwanamke ndiye mzalishaji mkuu kwenye kaya nyingi hapa nchini,”alisema Dk. Kone.

Mapema akimkaribisha mgeni rasmi katika maadhimisho hayo, mkuu wa wilaya Singida mwalimu Queen Mlozi aliagiza kuwa ni vema sherehe kubwa kama hiyo inapofanyika mkoani hapa, wahusika wakashirikisha serikali ili iweze kufana zaidi.

Mwalimu Mlozi alilazimika kutoa amri hiyo, baada ya maadalizi, husani hamasa kuwa katika kiwango cha chini sana, hali iliyochangia uwanja kuonekana mtupu kutokana na watu wachache sana kujitokeza, vikiwemo vikundi vichache vya hamasa.

“Jamani ni vizuri maadhimisho makubwa kama haya yanapoletwa mkoani kwetu, basi wahusika wajitahidi kushirikisha serikali washirikiane pamoja kuhamasisha wananchi ili wajitokeze kwa wingi na wafurike kwenye sherehe,”alisema kwa masikitiko Mlozi.

Akizungumzia maadhimisho hayo, Juliana Bwire, afisa usawa na jinsi wa shirika la Concern worldwide kutoka jijini Dar es Salaam alisema siku 16 walizokuwa Singida, walizitumia vijijini kuielimisha jamii madhara ya ukatili, ikiwemo unyanyasaji, ukeketaji, na wanawake kunyimwa haki.

Aidha mmoja wa wanawake waliohudhuria sherehe hizo, Happynes Juma(30) mzaliwa wa Kigoma, alieleza kwa masikitiko ukatili aliofanyiwa na mumewe ikiwemo kudaiwa hajui kufanya mapenzi, hali iliyoleta mgogoro wa kifamilia na suala hilo lipo ustawi wa jamii, tayari kwa ajili ya kutengana.

Alisema maadhimsho hayo yatahitimishwa jijini Dar es Salaam siku ya desemba 8, mwaka huu.

Na Elisante John;Singida
Novemba 28,2012.

Hotuba Ya JK Bunge La Afrika Mashariki

Honourable Speaker;
Invited Speakers here present;
 Honourable Members of the East African Legislative Assembly, Distinguished Guests; Ladies and Gentlemen;

 I thank you, Hon. Speaker for giving me this rare opportunity to address this august Assembly at its 3rd sitting since its inauguration this year. I also thank you for the kind words you have spoken about me and my dear country, the United Republic of Tanzania.

Honourable Speaker; Since I am speaking to Members of East African Legislative Assembly for the first time since you were elected, let me take this opportunity to extend to you all my warm congratulations on your well deserved election. Your election is a testimony of the immense confidence and trust reposed in you. More so I wish to .... Read More... http://www.kwanzajamii.com

Jengo La Jumuiya Ya Afika Mashariki Lazinduliwa

  Rais Jakaya Mrisho Kikwete na viongozi wenzie wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wakiangalia mfano wa jengo jipya la makao makuu ya Jumuiya hiyo pamoja na maelezo yake baada ya kulifungua rasmi  Novemba 28, 2012 jijini Arusha
                     Mfano wa  jengo la Makao makuu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete na viongozi wenzie wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wakifunua pazia  kufungua rasmi jengo jipya la makao makuu ya Jumuiya  Novemba 28, 2012 jijini Arusha
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na wakuu wenzie wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wakiwa katika picha ya pamoja na wadau pamoja na wabunge wa Afrika Mashariki

PICHA NA IKULU

Mkuu Wa Wilaya Na Nape Wamzika Sharobaro

  Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye (Watatu kulia, waliobeba jeneza) akishiriki kubeba jeneza lenye mwili wa aliyekuwa msanii wa muziki wa kizazi kipya na filamu, Hussein Ramadhani maarufu kwa jina la Sharo Milionea, alipokiwakilisha Chama Cha Mapinduzi, kwenye mazishi ya msanii huyo, leo kwenye Kijiji cha  Lusanga, Muheza Tanga.
 Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akitoa pole za Chama Cha Mapinduzi (CCM) alipokiwakilisha Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwenye mazishi ya aliyekuwa msanii wa muziki wa kizazi kipya na filamu, Hussein Ramadhani maarufu kwa jina la Sharo Milionea,leo kwenye Kijiji cha  Lusanga, Muheza Tanga
 Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nauye, akitupa mchanga kaburini, alipokiwakilisha Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwenye mazishi ya aliyekuwa msanii wa muziki wa kizazi kipya na filamu, Hussein Ramadhani maarufu kwa jina la Sharo Milionea,leo kwenye Kijiji cha  Lusanga, Muheza Tanga.
 Mkuu wa wilaya ya Muheza, Subra Mgalu akisoma salam za Shirika la Fursa Sawa kwa Wote (EOTF) la Mama  Anna Mkapa, kwenye msiba huo. Pamoja naye ni Nape

 (Picha na Bashir Nkoromo).

Safari Ya Mwisho Ya Sharo Milionea

MAELFU ya waombolezaji jana walijitokeza kushiriki mazishi ya msanii Hussein Ramadhan maarufu kwa jina la Sharo Milionea, huku mamia wakizirai baada ya kushindwa kujizuia wakati mwili wake unawekwa kaburini.

Mwili wa msanii huyo ulizikwa jana kijijini kwake Lusanga wilayani Muheza saa 7 mchana, katika tukio lililomshirikisha Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye ambaye alimwakilisha mwenyekiti wa chama hicho, Rais Jakaya Kikwete.

Waombolezaji walianza kumiminika kijijini Lusanga tangu juzi jioni na idadi yao iliongezeka zaidi jana asubuhi. Mkuu wa Wilaya ya Muheza, Subira Mgalu ndiye aliyekuwa mwenyekiti wa Kamati ya Mazishi.Sala ya mazishi iliongozwa na Sheikh Twaha Juma ambaye baadaye aliamuru jeneza hilo kupelekwa makaburini, ambako waombolezaji kadhaa walipoteza fahamu.20 wapelekwa hospitali

Miongoni mwa matukio yaliyojitokeza katika msiba huo ni baadhi ya waombolezaji kupoteza fahamu msibani.Matukio tofauti ya watu kuzirai yalitokea wakati mwili wa msanii huyo ulipokuwa unapelekwa nyumbani kwao kijijini Lusanga ukitokea Hospitali Teule ya Wilaya ambako ulihifadhiwa tangu alipopata ajali Jumatatu usiku na wakati wa mazishi.

Miongoni mwa waliopoteza fahamu katika msiba huo ni wasanii na waigizaji wa filamu waliokuwa wakiigiza na Sharo Milionea wakati akiwa katika kundi la AL Riyam.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na MC wa shughuli hiyo, Steve Nyerere, zaidi ya watu 20 walipoteza fahamu katika msiba huo na kupelekwa katika Hospitali ya Wilaya ya Muheza.

mbolezaji kutokuwa na shaka juu ya waliopoteza fahamu kwa kuwa madaktari maalumu walikuwa wameandaliwa hospitalini hapo kwa ajili ya kuwapa huduma.

Mwananchi lilifika katika hospitali Teule na kukuta waliokuwa wamepoteza fahamu, wengi wao wakiwa ni wasichana, wakipata huduma huku wengine wakiomba kupewa ruhusa ili wakahudhurie maziko.

JK atuma rambirambi
Rais Jakaya Kikwete amemtumia salamu za rambirambi, Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Dk Fenella Mukangara kutokana na vifo vya wasanii watatu vilivyotokea hivi karibuni, kikiwamo cha Sharo Milionea.

Taarifa iliyotolewa jana Dar es Salaam na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu, ilisema kuwa Rais Kikwete ameshtushwa na vifo hivyo vya ghafla.

Wasanii hao ambao walifariki dunia katika mazingira tofauti ni Mwigizaji wa Kundi la Kaole, Khalid Mohamed ‘Mlopelo’ aliyefariki dunia hivi karibuni kutokana na maradhi yaliyokuwa yanamsumbua kwa muda mrefu.

Soma zaidi:  http://www.mwananchi.co.tz/habari

Wednesday, November 28, 2012

"NIKIACHIKA TENA NITAOLEWA UARABUNI...." JACK WOLPE


PAMOJA na kukataa kumwanika hadharani mpenzi wake mpya, staa wa filamu za Kibongo, Jacqueline Wolper Massawe amesema kuwa akipigwa chini na jamaa yake huyo, atatimka nchi na kwenda kuolewa uarabuni.

Wolper amesema anajitahidi kulilinda penzi lake jipya ili lisiweze kuvunjika na ikitokea hivyo, hatataka  tena kuwa na mpenzi wa  Kibongo.

“Kwa kweli siwezi kuachika tena sasa hivi! Ikitokea sitakuwa na amani moyoni mwangu na sitataka kuwa na mpenzi mwingine hapa nchini, nitaenda kuolewa nje ya nchi,” alisema Wolper ambaye hivi karibuni alimwagana na aliyekuwa mpenzi wake, Abubakar Mtoro ‘Dalas’.

JENEZA LILOBEBA MWILI WA MAREHEMU SHARO MILIONEA.

                           Hili ndilo jeneza lililobeba mwili wa marehemu sharo milionea.
                                     Nyumba ya Milele ya ndugu yetu Sharo Milionea Apumzike kwa Amani
Marehemu Sharo milionea Akiondolewa Hospitalini Kuelekea Katika Nyumba yake Ya milele

Hatimae Baba Mdogo wa Mwigizaji wa Filamu Marehemu John Maganga Aeleza Mkasa Mzima toka Alipoanza kuumwa Mpaka kifo chake

Muigizaji wa tasnia ya Bongo Movie John Stephan Maganga ambaye filamu yake ya mwisho inayoweza kuwakumbusha watu wengi taswira yake, kwa wale wanaotaka kumjua ni “BAR AHMED” iliywashirikisha Nice na Irene Uwoya, ambapo Marehemu Stephano ali act kama Boss wa bar ambaye alimwambukiza gonjwa la ukimwi Irene Uwoya.
Baba yake mdogo na marehemu, ambaye pia naye ni mwigizaji, ameelezea mkasa mzima toka Stephan alipoanza kuumwa mpaka siku ya kifo chake jumamosi asubui ya wikiendi iliyopita.

Baba mdogo wa Stephano anasema, kabla ya kufikwa na umauti mwigizaji John alikuwa akisumbuliwa na homa ambapo alimpigia simu na kumweleza jinsi anavyojisikia ndipo akamwambia amngojee, kisha alimfuata na kumpeleka Hospitali ya Mwananyamala.

Aidha anaendelea na kusema siku ya pili yake John alimpigia simu na kumwambia bado anaumwa na wala hajisikii vizuri, kuona hivyo, baba yake mdogo akaenda nyumbani kwake na kumkuta amelala kwenye kochi anatoka jasho sana, akamuuliza, John vipi tena?, John akamjibu, tumbo linamuuma sana, ikabidi nimpigie simu Baba yake mzazi nimwambie tumpeleke Hospital Mwananyamala.

Tulipofika pale hospitali, kutokana na maelezo ya Stephano, madaktari wakaamua wampige X Ray na Utra Sound kwa sababu alikuwa na maumivu makali sana tumboni mwake. Baada ya majibu ya vipimo kutoka, madaktari, wakasema ana matatizo kwenye utumbo hivyo wanatakiwa wamfanyie upasuaji wa haraka.

Stephano aliingizwa chumba cha upasuaji, wakati sisi kwa maana ya mimi na baba yake tukiwa tumekaa, dokta alitoka na kutuambia mashine za kupumulia zina matatizo kwa hiyo tunafanya transfer ya kwenda Muhimbili kwa matibabu zaidi, hivyo zilifanyika taratibu na Stephano aliingizwa kwenye gari la wagojwa na kupelekwa hospitali ya Muhimbili.

Baada ya kufika Muhimbili, Stephano aliingizwa chumba cha dharura (emergence room), na baada ya dakika kama 10 hivi, alitoka Doctor ambaye tunafaamiana naye na kusema kuwa, kwa tatizo alilonalo John, hatakiwi kufanyiwa upasuaji kama walivyofikiria madaktari wa Mwananyamala ambapo walidhani kuna utumbo umekatika.
Daktari huyo wa Muhimbili aliendelea kutuambia sehemu ambayo inaonekana kuleta matatizo ni sehemu ya kongosho ambapo vipimo vinaonesha ina matatizo, ime fell kwa hiyo ina mwaga maji kwenye tumbo ndiyo maana anapata maumivu kwenye tumbo na tumbo kujaa.

Baada ya maelezo hayo Dokta tunayejuana naye alitueleza kwamba mtaalamu wa tatizo hili hayupo na kwamba anategemewa kuja kesho yake asubuhi na kutuasa tuende nyumbani na kwamba watammwekea mashine ya kupumua na sisi turudi kesho.
Kesho yake asubuhi, ilikuwa ni siku ya jumamosi nilifika Muhimbili na kuonana na yule Dokta kama tulivyokubaliana usiku wa jana yake. Nilipokutana naye akaniambia nisubiri atanijulisha kinachoendelea.

Nafikiri wakati huo ndipo mambo yaliharibika, kwa sababu yule daktari ambaye alimtaja kutokuwepo jana, alikuwa ndani anamshughulikia hivyo alikuwa anajaribu achomwe sindano ambayo ingeweza punguza makali ya sumu iliovuja toka kwenye kongosho au angewekewa drip ya maji lakini inaonekana jambo hili lilichelewa kufanyika.

Muda mchache baadae Dokta alitoka na kuniambia John hatuko nae tena, amefariki. Hicho ndicho kilichomtokea John kuelekea kifo chake.Alisema baba mdogo wa muigizaji Stephano.

Abiria wa treni Watoa mpya ya kufungia mwaka, wageuzanalo kwaajili ya kuwahi siti.

 Baadhi ya Wakazi wa Jiji la Dar wakiwa wanasubiri treni ya mwakyembe iwasili stesheni ikitokea ubungo maziwa tayari kwa safari ya kuwarudisha Majumbani Kwao. Baadhi ya Abiria wakiwa wamewahi kwaajili ya Kupanga foleni ili waweze kupata siti huku wengine wakichuchumaa kutokana na kulisubiri kwa muda
 Abiria Wakiteremka katika treni linalofanya safari zake ndani ya Jiji la Dar mara lilipowasili Katika Kituo cha Stesheni karibu na central polisi tayari kwa safari ya kurudi tena Ubungo
 Baadhi ya Abiria waliogeuza na treni hilo wakiwa wamepandia Kituo cha Kamata Ili kuwahi Siti ambapo walipelekea sintofahamu kwa baadhi ya abiria waliokuwa kituoni hapo na kutaka kupanda kwenye hilo behewa kukuta likiwa tayari limeshajaa kutoka na abiria kugeuza na treni hilo wakati utaratibu huwa haurusiwi na ikifika mwisho abiria wote wanatakiwa kushuka
 Mmoja wa Abiria aliyegeuza na treni hilo ambapo walipandia Kamata kwa lengo la kuwahi kiti akibishana na mmoja katika ya abiria ambao walikua kwenye foleni muda mrefu wakisubiria treni hilo kufika ili waweze kuingia ndani na kupata siti ambapo alikuta behewa hilo likiwa limeshajaa na kuanza kubishana huku abiria waliokuwa wakisubiri treni hilo wakitaka abiria waliogeuza na treni hilo kushuka
 Wakazi wa Jiji la Dar wakiwa kwenye foleni ya kupanda treni maarufu kwa jina la treni ya mwakyembe jana kwenye majira ya saa 11 jioni katika kituo cha Stesheni tayari kwa kurudi nalo ubungo huku baadhi ya behewa kuwa limeshajaa kabla hata halijafika kituoni hapo kutokana na abiria kugeuza nalo kwa lengo la kuwahi siti. Behewa ambalo lilikuja likiwa limeshajaa ni behewa lenye namba 3644 ambalo abiria wake walikua wamepandia njiani kwa nia ya kugeuza nalo ili waweze kupata siti.
 Abiria wakianza kupanda treni tayari kwa kurejea makwao mara baada ya treni la mwakyembe kuwasili kituoni hapo kwenye majira ya saa kumi na moja na dakika ishirini jana

Katika hali isiyo ya kawaida jana kwenye majira ya Saa 11: 20 Jioni katika kituo cha Treni kilichopo stesheni mkabala na Kituo Cha Polisi Cha Cetral kuliibuka Jambo la kushangaza wakati abiria wanaosubiria treni inayofanya kazi zake ndani ya jiji la dar kuona behewa moja likiwa limeshajaha tayari kutokana na abiria kupandia njiani na kugeuza nalo kwa lengo la kuwahi siti na kupelekea abiria waliowahi kituoni hapo na  kupanga foleni kwaajili ya kuwahi siti kuambulia patupu.

Abiria waliokuwa wakisubiria treni hilo walianza kulalamika pale ambapo walikuta behewa hilo limeshajaa kabla hata treni hiyo haijafika kwenye kituo chake cha mwisho kwa lengo la abiria hao kuwahi . Baada ya Tukio hilo kutokea kulizuka sintofahamu kwa baadhi ya wafanyakazi na Askari Polisi ambao hawajawahi kuona utaratibu huo ukifanyika na kupelekea Abiria kuhisi tayari wafanyakazi wa treni hiyo waneshaanza kuchakua kitu ambacho utaratibu hauruhusu. Utaratibu uliopo ni kwamba hata kama abiria amepandia katikati anatakiwa kuteremka pindi treni hilo linapofika mwisho wa kituo ndipo akate tiketi kwaajili ya kupanda tena na kurudi nalo lakini hali imekuwa tofauti hapo jana baada ya abiria hao kutokushuka na tiketi kukatiwa ndani na kupelekea abiria waliokuwa wakisubiri treni hilo kusubiri kwa muda mrefu.

Lukaza blog imeweza kunakili sauti za abiria ambao waliokuwa wakilalamika juu ya utaratibu huo uliofanywa na wafanyakazi ambao sio waaminifu na kupelekea usumbufu kwa abiria ambao wamewahi kupanga foleni.

TENGA, WIZARA WATETA KUZUIWA AKAUNTI YA TFF

 Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) lina imani kuwa mazungumzo kati yake, Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) yatamaliza tatizo la kushikiliwa akaunti ya TFF kutokana na malipo ya kodi ya mishahara ya makocha wa kigeni.

Rais wa TFF, Leodegar Tenga alizungumza na waandishi wa habari jana juu ya uamuzi wa TRA kushikilia akaunti ya TFF ikiielekeza Benki ya NMB kukata sh. 157,407,968 ikiwa ni malipo ya Kodi ya Mapato ya Mshahara wa Mfanyakazi (P.A.Y.E) ya makocha Marcio Maximo na wasaidizi wake.

Katika mzozo huo wa muda mrefu, TFF imejitetea kuwa haiwezi kulipa kodi hiyo kwa kuwa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo ndiyo mlipaji wa mishahara ya makocha hao, ikiwa ni ahadi ya Rais wa Tanzania, Jakaya Kikwete ya kulipia makocha wa michezo tofauti, ukiwemo mpira wa miguu.

“Hili ni suala nyeti ambalo linahitaji kumalizwa kwa mazungumzo baina ya pande zote. Ninataka kuwahakikishia kuwa suala hili linazungumzwa na tayari nimeshafanya mazungumzo na maofisa wa Wizara na tumekubaliana kukutana na pande zote  wakati wowote; iwe leo jioni au kesho.

“Ni matumaini yangu kuwa suala hili litakwisha na jana nimetoka Kampala (Uganda kwenye Kombe la Chalenji) moja kwa moja na kwenda kuzungumza na viongozi wa Wizara na wamekubali kwamba tuongee pande zote kulimaliza suala hili.

Precision Air katika Facebook na Twitter

 Baada ya shirika la ndege la Precision Air kununua ndege yao mpya aina ya ATR 42-600 na kuwa shirika la kwanza Africa na duniani kumiliki na kutumia ndege aina hiyo, sasa inawapa fursa mashabiki wake katika mtandao wa facebook na twitter kuwa wa kwanza

kuruka na ndege hiyo.
 Ndege hiyo hiyo ya kisasa ambayo uzinduzi wake rasmi umepangwa kufanywa tarehe 5 ya mwezi December, ina siti 50 na inatarajiwa kufanya safari zake kati ya Dar es salaam na Kilimanjaro.

Katika uzinduzi huo Precision Air itatoa zawadi kwa washindi watatu (3) kutoka katika ukurasa wao wa facebook. Ili kushinda itakubidi utembelee ukura wao wa facebook (www.facebook.com/Precisionairtz), kwanza bonyeza LIKE kama bado hujajiunga na ukurasa huo halafu SHARE picha ya ndege hiyo iliowekwa kwenye ukurasa huo kisha waambie marafiki zako waLIKE na kuCOMMENT kwenye picha yako ulioSHARE, Watu watatu (3) watakaoongoza kwa kua na LIKEs na COMMENTs nyingi kwenye picha yao walioShare moja kwa moja kutoka kwenye ukurasa wa facebook wa Precision Air watakua washindi.

                                   Hi ndio picha ya shindano unayotakiwa kuSHARE ili kushinde
[ ANGALIZO : Unatakiwa kushare picha moja kwa moja kutoka kwenye facebook page ya Precision Air]

Mshindi wa kwanza kwa kua na LIKEs na COMMENTs nyingi zaidi atashinda tiket ya buuure kwenda kokote ambako ndege za Precision Air zinakwenda, pia atapata fursa ya kuruka na ndege mpya ATR 42-600  na mwisho atahudhuria sherehe za uzinduzi wa ndege hi mpya.

Mshindi wa pili atapata fursa ya kuruka na ndege mpya ATR 42-600  na pia atahudhuria sherehe za uzinduzi wa ndege hi mpya. Na mshindi wa tatu yeye atapata fursa ya kuhudhuria sherehe za uzinduzi wa ndege hi mpya.
Kwa maelezo zaidi tembelea kurasa zao za;

facebook [www.facebook.com/precisionairTz],
Twitter [www.twitter.com/PrecisionAirTz]

na YouTube [www.youtube.com/PrecisionAirTz].

Ndege za fastjet zazinduliwa na Naibu Waziri wa Uchukuzi, yakamilisha makubaliano ya ubia na Swissport

Shirika la kwanza la ndege la nauli nafuu Afrika, fastjet, leo limeizundua ndege yake ya kwanza ikiwa nachapa yake kamili, siku mbili tu kabla ya kuanza safari za anga Tanzania. Kwenye hafla iliyofanyikakwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Kamabarage (JKIA),Dar es Salaam, maafisa wa serikali, watendaji wa fastjet na wataalamu wa safari za anga walishuhudia ndege aina ya Airbus A319 ikipaa kwenye anga ya Dar es Salaam kwa mara ya kwanza.

Kuanzia Alhamisi, 29 Novemba, fastjet itafanya safari mbili kutwa kwenye ruti zake mbili za mwanzo – Dar es Salaam-Kilimanjaro na Dar es Salaam-Mwanza, zote zikiwa ni safari zenye wasafiri wengi wa ndani. Tiketi zilianza kuuzwa wiki mbili zilizopita na fastjet imeshuhudia mahitaji makubwa, zaidi kuliko matarajio ya awali. Mpaka sasa idadi ya tiketi zilizonunuliwa ni sawa na safari 60 za ndege iliyojaa, na mauzo yanaendelea kwa safari za mwakani. Nauli zitakuwa za wastani wa dollar $80, lakini zinaanzia bei ya chni kabisa ya $20 kwa safari ya kwenda, kabla ya kodi za serikali kwa wateja watakowahi kununua tiketi.

Akizungumza mjini Dar es Salaam leo, Afisa Mtendaji Mkuu wa fastjet, Ed Winter, alisema:

“Leo ni siku ya kusisimua sana, na siyo tu kwa fastjet, bali kwa Tanzania na Afrika kwa ujumla. Kwa miaka mingi tasnia ya safari za anga Afrika imekosa huduma bora, na kulegalega nyuma ya kwingine duniani. Ustawi wa mapato umeongeza fursa za watu kuwa na mapato ya ziada, na pamoja na kwamba hilo limeambatana na mahitaji makubwaya usafiri wa anga, bado watu baraniAfrika wamekosa fursa za usafiri wa anga wanaoumudu na kuuamini. fastjet sasa itaziba pengo hilo na kwakuwaletea Watanzania, na hasa bara zima la Afrika, shirika la kwanza la ndege la nauli nafuu, likiwa na safari za kituo hadi kituo, na lenye kujiendesha kwa viwango vya kimataifa vya usalama na ubora.”

Akizungumzia uzinduzi wa leo, Afisa Mwendeshaji Mkuu wa Airbus – Wateja, alisema:

Uamuzi wa fastjet kujikita kwenye ndege aina ya A319 pekee ni kidhihirisha ufanisi, kuaminika na kustahili kwa ndege za aina hiyo kwa ajili ya safari za nauli nafuu barani Afrika na haswa kusini mwa Jangwa la Sahara. Ndege hiyo itakayotumiwa na fastjet inaoongoza kwenye mauzo ya ndege aina ya Airbusna inayo safu mbili za viti,, fastjet imezingatia kuleta viwango vipya vya starehe na unafuu wa gharamakwenye soko la Afrika ambalo linatarjiwa kuongezeka mara dufu karikakipindi cha miaka 20 ijayo .”

Magazeti ya leo Jumatano 28th November 2012