Saturday, February 9, 2013

Tanzania yashiriki utalii hispania

 Ujumbe wa Tanzania ukiwa katika picha ya pamoja na Youssou Ndour Waziri wa Utalii na Utamaduni nchini Senegal  ambaye pia ni mwanamuziki maarufu duniani wakati alipotembelea banda la Tanzania katika maonyesho hayo , Youssou Ndour amewahi kufanya ziara ya kimuziki mara tatu nchini Tanzania kabla ya kuteuliwa kuwa Waziri wa Utalii na Utamaduni nchini mwake.

Miss Utalii Tanzania 2013 kutembelea Hifadhi za Taifa na vivutio vya utalii





    Miss Utalii Tanzania 2012/13 wiki ijayo wataanza ziara ndefu ya kutembelea Hifadhi za Taifa na vivutio vya utalii katika mikoa ya Dar es salaam,Morogoro,Mtwara,Lindi na Pwani. Vivutio hivyo ni pamoja na Hifadhi za Taifa za Mikumi, Udizungwa, Saadani, Selous, pia maeneo ya kihistoria ya Bagamoyo, Amboni, Kijiji cha makumbusho,Makumbusho ya Taifa, Pugu sekondari,maeneo mengine ni ufukwe wa kigamboni, soko la kimataifa la Magogoni, Uwanja wa Taifa, uwanja wa ndege wa  J.K.Nyerere Air Port, Soko la Kariakoo, Mashule ya sekondari na msingi, pia watatembelea manispaa za Ilala, Temeke na Kinondoni ambapo watakutana na viongozi wakuu wa wilaya, mikoa, na wabunge katika majimbo ya mikoa hiyo.

JK atua msumbiji Jana

 Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya nchi jumuiya ya Maendeleo ya Uchumi Kusini Mwa Afrika SADC Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akikagua gwaride la heshima muda mfupi baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Maputo.Rais Kikwete yupo nchini Msumbiji kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi za SADC

MAgazeti ya leo Jumamosi ya 9th February 2013




YALIYOJIRI BUNGENI

 Mh Kigwangalla alimalizia kwa kusema “naomba atumie uungwana yeye mwenyewe kusimama katika bunge hili.. aidha kuwaomba radhi Watanzania kwa kudanganya ama kutimiza wajibu aliousema hapa yeye mwenyewe wa kujiuzulu, uongo aliousema ni mkubwa sana.. naomba nitoe hoja kwamba Mh Mbatia aadhibiwe kwa mujibu wa kanuni ya 63, asihudhurie vikao visivyozidi 20 na aombe radhi kwa maandishi kwa Watanzania kwa kusema uongo bungeni”

Friday, February 8, 2013

MSIKUBALI KUDANGANYWA ANGALIENI MAFANIKIO YENU- PALANGYO

WANACHAMA wa Chama cha Mapinduzi wilaya ya Meru,mkoani Arusha,wameshauriwa kutokukubali kudanganywa na Vyama vya kisiasa ambavyo vinaeneza Propaganda chafu  kuwa hakuna kilichofanyika tangia Uhuru,badala yake wachukie siasa zinazosababisha uvunjifu wa amani

KAMPUNI YA NDEGE YA fastjet YAKANUSHA UVUMI KUWA IMEFUTIWA LESENI YA BIASHARA

Jean Uku Meneja Masoko na Mauzo wa Kampuni ya ndege ya Fastjet akizungumza na waandishi wa habari kwenye hoteli ya Hyyat Regency Dar es salaam kukanusha uvumi wa habari zinazosema kampuni hiyo imenyang’anywa leseni ya kufanya biashari nchini Tanzania, Kushoto ni Givaldine Dawe Meneja Utawala.

Pamoja na habari zilizoandikwa na kusemwa kwenye vyombo vya habari leo, biashara ndani ya kampuni ya fastjet inaendelea kama kawaida. Madai yanayotukabili ya kunyang’anywa leseni hayana ukweli wowote. Tunaendelea kufanya kazi na ndege zetu nchini Tanzania kama kawaida na bado tunazidi kuzindua vituo vipya kama ilivyopangwa. Huu ni uzushi wa baadhi ya watu au kampuni zenye chuki dhidi ya kampuni ya fastjet, kusudi lao ni kudhoofisha uaminifu na kuharibu sifa ya jina la biashara na bidhaa zetu za fastjet.

Ofisi zetu na vituo vyetu vya kuuzia tiketi bado viko wazi kwa ajili ya bookings na Kwa tiketi zilizolipiwa pesa haitarudishwa.

TAMKO RASMI BAADA YA MASAA MACHACHE

MAGUNIA MENGINE 97 YA BANGI YAKAMATWA NA JESHI LA POLISI ARUSHA

 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi wa Polisi Liberatus Sabas akiwaonyesha waandishi wa habari madawa ya kulevya aina ya bangi ambayo yalikuwa kwenye magunia 97 yaliyokamatwa na askari wa jeshi hilo katika eneo la Usa river wilayani Arumeru (Picha na Rashid Nchimbi wa Jeshi la Polisi)

HIVI NDIVYO MATUMAINI ALIVYOPOKELEWA JIJINI DAR

    Matumaini (katikati) akisaidiwa na wasanii wenzake muda mfupi baada ya kutua.
   Matumaini (kulia) akiwa na Bi. Mwenda (wa pili kushoto) na anayefuata (kushoto) ni msanii mwenzake Kiwewe wakisubiri gari la kumpeleka hospitali.
                                     Bi. Mwenda akiwa amembeba Matumaini mgongoni.

Yaliyojiri Magazetini Leo Ijumaa ya 8th February 2013




Thursday, February 7, 2013

Kiongozi wa Chadema alipokwenda kumjulia hali Askofu Thomas Leizer Kabla ya Kifo chake

Askofu Thomas Leizer, katika siku za mwisho za uhai wake, akiwa chumba cha uangalizi maalum (ICU) katika Hospitali ya Selian Hospital Arusha Centre. Pamoja naye ni Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe. Picha hii ilipigwa Tarehe 3 Februari 2013, ambapo viongozi wa CHADEMA (Mbowe na Lema) walifika kumjulia hali, baada ya kuugua kwa muda mrefu na kulazwa

Picha kwa Hisani ya Jamiiforums.

Taswira bungeni leo

 Baadhi ya Maafisa Habari  Mawasiliano Serikalini  wakielekea katika Ukumbi wa Mkutano wa Bunge leo Dodoma. Maafisa hao  wamefanya ziara  Bungeni hapo ili kuona  shughuli za Bunge,
                                                   Aggrey Mwanri akijibu hoja Bungeni
Naibu Waziri, Ofisi ya  Waziri Mkuu (TAMISEMI) Aggrey Mwanri akiwakilisha hati mezani kuhusu Taarifa ya  Mwaka na Hesabu zilizokaguliwa na Mfuko wa Pensheni wa Serikali za Mitaa kwa Mwaka wa Fedha,2010/2011.

(Picha na Mwanakombo Jumaa- MAELEZO

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete azindua vitambulisho vya taifa

 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akibonyesha kitufe kuashiaria kuzindua rasmi mfumo wa usajili na utambuzi wa watu na utoaji wa vitambulisho vya taifa uliofnyika katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam leo.Watatu kushoto ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi Dkt.Emmanuel Nchimbi, kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa NIDA Bwana Mwaimu na kulia nia Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Bwan Said Meck Sadik.
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam wakiangalia bango lenye kitambulisho cha  taifa cha Rais Kikwete muda mfupi baada ya Rais Kikwete kuzindua mfumo wa Usajili na utambuzi wa watu na utoaji wa vitambulisho vya taifa uliofanyika katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam leo.Kushoto ni Waziri wa Mambo ya  Ndani ya Nchi Dkt.Emmanuel Nchimbi

Tanzia; askofu katoliki msarikie amefariki dunia

Askofu Mstaafu wa jimbo Katoliki la Moshi Mhashamu Amedeus Msarikie Amefariki Dunia.

WAMA yakabidhi vifaa tiba vyenye thamani ya milioni 700

Taaasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) imeikabidhi hospitali ya mkoa wa Lindi Sokoine  kontena lenye  urefu wa futi 40 lenye mitambo na vifaa vya huduma ya afya vya kisasa  ilivyochangiwa na Shirika linayoshughulika na utoaji wa huduma za kibinadamu la  Project C.U.R.E la nchini Marekani vyenye thamani  ya shilingi milioni mia saba Makabidhiano hayo yalifanyika jana katika viwanja vya...