Wilfred Lwakatare ameitwa Makao Makuu ya Polisi sasa hivi kwa mahojiano na jeshi hilo kufuatia video clip iliyowekwa mitandaoni ikionesha jinsi alivyokuwa akipanga mbinu za utekaji....
WILLIFRED LWAKATARE NI MKURUGENZI WA ULINZI NA USALAMA WA CHADEMA...
Kwa taarifa ni kuwa atawakilishwa na wakili Nyaronyo Kicheere na baadaye kama watafungua kesi watakuwa na Mabere Marando.
Je, hii sio double standard ndani ya taifa?
Mbona Mwigulu hajakamatwa baada ya kusema ana mkanda wa njama za kufanya mauaji?
MAELEZO YOTE NI KWA HISANI YA JAMII FORUM
Thursday, March 14, 2013
HATIMAYE PAPA MPYA APATIKANA HUKO VATICAN
Jorge Mario Bergoglio(Pope Francis) akipewa salamu na Papa aliyejiuzuru Benedict 16
Kadinali Bergoglio anakuwa mtu wa kwanza kutoka Amerika kusini kuchaguliwa kuwa Papa. Mara tu baada ya kuchaguliwa alichagua jina la Papa Francis I. Awali moshi mweupe ulishuhudiwa ukifuka kutoka bomba la kutolea moshi katika kanisa la Sistine Chapel na kufuatiwa na kengele kupigwa.
Hii ilikuwa ni ishara kwa walimwengu kuwa makadinali ambao walianza mchakato wa kumchagua Papa mpya hatimae walikuwa wamefaulu katika kazi yao. Kadinali Bergoglio anachukuwa mahali pa Papa Benedict XVI, ambaye alijiuzulu mwezi uliopita akisema hana nguvu na uwezo wa kuendelea kuliongoza Kanisa Katoliki. Makadinali 115 wamekuwa faraghani tangu siku ya Jumanne alasiri na wakaanza mchakato wao kwa kupiga kura mara nne kwa siku.
Ilikuwa inahitajika kuwa angalau Makadinali 77 yaani theluthi-mbili wangeliweza kumpigia kura mmoja wao ili aweze kutangazwa kuwa Papa mpya. Na kabla ya mchakato huo kuanza kulikuwa hakuna dalili za kuonyesha nani angelichaguliwa.
Maelfu ya watu kutoka sehemu mbali mbali duniani walikuwa wamekusanyika katika ukumbi wa Kanisa la St Peter tangu siku ya Jumanne. Muda mfupi kabla ya Kadinali Bergoglio kujitokeza , maelfu ya watu walionekana wakikimbia kuelekea ukumbi wa St Peters ili kuweza kumshuhudia Papa mpya akitangazwa
Kadinali Bergoglio anakuwa mtu wa kwanza kutoka Amerika kusini kuchaguliwa kuwa Papa. Mara tu baada ya kuchaguliwa alichagua jina la Papa Francis I. Awali moshi mweupe ulishuhudiwa ukifuka kutoka bomba la kutolea moshi katika kanisa la Sistine Chapel na kufuatiwa na kengele kupigwa.
Hii ilikuwa ni ishara kwa walimwengu kuwa makadinali ambao walianza mchakato wa kumchagua Papa mpya hatimae walikuwa wamefaulu katika kazi yao. Kadinali Bergoglio anachukuwa mahali pa Papa Benedict XVI, ambaye alijiuzulu mwezi uliopita akisema hana nguvu na uwezo wa kuendelea kuliongoza Kanisa Katoliki. Makadinali 115 wamekuwa faraghani tangu siku ya Jumanne alasiri na wakaanza mchakato wao kwa kupiga kura mara nne kwa siku.
Ilikuwa inahitajika kuwa angalau Makadinali 77 yaani theluthi-mbili wangeliweza kumpigia kura mmoja wao ili aweze kutangazwa kuwa Papa mpya. Na kabla ya mchakato huo kuanza kulikuwa hakuna dalili za kuonyesha nani angelichaguliwa.
Maelfu ya watu kutoka sehemu mbali mbali duniani walikuwa wamekusanyika katika ukumbi wa Kanisa la St Peter tangu siku ya Jumanne. Muda mfupi kabla ya Kadinali Bergoglio kujitokeza , maelfu ya watu walionekana wakikimbia kuelekea ukumbi wa St Peters ili kuweza kumshuhudia Papa mpya akitangazwa
Wednesday, March 13, 2013
LULU USO KWA USO NA MAMA YAKE KANUMBA KWENYE KABURI LA KANUMBA
WEMA SEPETU AAMUA KUZITIA MKASI NYWELE ZAKE...
Mrembo na Miss Tanzania wa zamani, Wema Sepetu ameamua kubaki natural baada ya kuzinyoa nywele zake. Kupitia Instagram, Wema ameshare picha hizo na kuandika, ‘me apa nimenyoa nywele’. Ingia ndani kusoma maoni aliyoyapata baada ya kunyoa.
MOSHI MWEUSI WAFUKA VATICAN KUASHIRIA KUWA BADO PAPA HAJAPATIKANA....
Moshi mweusi ulifuka jana jioni kutoka kwenye dohani huko Vatican ikiwa ni ishara kwamba Baraza la siri la Makadinali bado halijampata Kiongozi mpya wa Kanisa Katoliki baada ya kupiga kura ya kwanza.
Mchakato wa kupiga kura ulianza mapema jana ambapo Makadinali 115 kutoka nchi 48 walikutana kwa faragha ili kumchagua atakaechukua nafasi ya aliyekuwa papa Benedikt wa 16 aliejiuzulu mwishoni mwa mwezi uliopita.
Zoezi la kupiga kura litaendelea hadi hapo mmoja wa Makadinali atakapopigiwa theluthi mbili ya kura yaani kura 77.
Atakaefikia kiwango hicho atakuwa Baba Mtakatifu wa 266.
Ikiwa Makadinali, wanaopiga kura watakubaliana juu ya Kiongozi mpya wa Kanisa Katoliki, moshi mweupe utatoka dohani na kengele zitapigwa kwenye makao makuu ya Kanisa Katoliki, Vatican.
Mchakato wa kupiga kura ulianza mapema jana ambapo Makadinali 115 kutoka nchi 48 walikutana kwa faragha ili kumchagua atakaechukua nafasi ya aliyekuwa papa Benedikt wa 16 aliejiuzulu mwishoni mwa mwezi uliopita.
Zoezi la kupiga kura litaendelea hadi hapo mmoja wa Makadinali atakapopigiwa theluthi mbili ya kura yaani kura 77.
Atakaefikia kiwango hicho atakuwa Baba Mtakatifu wa 266.
Ikiwa Makadinali, wanaopiga kura watakubaliana juu ya Kiongozi mpya wa Kanisa Katoliki, moshi mweupe utatoka dohani na kengele zitapigwa kwenye makao makuu ya Kanisa Katoliki, Vatican.
Huyu Ndio Msanii Anaye Ongoza Kulipwa Hela Nyingi Kutokana na Ringtones za Simu
Mwanzilishi wa kampuni ya Push Mobile inayohusika na uuzaji wa miito ya simu, ringback tone (RBT) amesema Diamond ndiye msanii wa Bongo Flava anayeingiza fedha nyingi zaidi.
Shamte ametoa taarifa hiyo jana alipokuwa akizungumza kwenye kongamano la mchango wa technolojia ya habari na mawasiliano ICT kwenye tasnia ya muziki nchini katika kituo cha ubunifu wa technolojia hiyo cha KINU jijini Dar es Salaam
Shamte ametoa taarifa hiyo jana alipokuwa akizungumza kwenye kongamano la mchango wa technolojia ya habari na mawasiliano ICT kwenye tasnia ya muziki nchini katika kituo cha ubunifu wa technolojia hiyo cha KINU jijini Dar es Salaam
Tuesday, March 12, 2013
MTOTO WA MIAKA 8 AFUNGA NDOA NA JIMAMA LA MIAKA 61...
Kijana huyo Sanele Masilela alisimama mbele ya watu 100 na kufunga ndoa na Bi Shabangu, mama mwenye watoto watano .
WAKENYA WAANDAMANA KUPINGA MATOKEO YA URAIS
Polisi wa kutuliza ghasia, wamelazimika kutumia mabomu ya machozi nchini Kenya, mji wa Kisumu kuwatawanya waandamanaji waliokuwa wakipinga matokeo ya urais ambayo mgombea wao, Raila Odinga alishindwa katika uchaguzi uliofanyika nchini humo.
Vurugu hizo ziliibuka, baada ya kutangazwa kwa matokeo ya urais yaliyompa ushindi Uhuru Kenyatta.
DOKEZO
Mahakama Kuu ya Kenya ndicho chombo pekee chenye uwezo wa kutengua matokeo ya urais yaliyotangazwa IEBC.
Jopo la majaji watano ndilo litakalosikiliza rufaa ya mgombea wa Cord, Raila Odinga; nao ni Jaji Mkuu, Dk. Willy Mutunga ambaye ni Rais wa Mahakama hiyo, wengine ni Majaji Dk. Smokin Wanjala, Njoki Ndung’u, Philip Tunoi, Jackton Boma Ojwang na Mohamed Ibrahim.
Source: Mwananchi, Jumatatu, Marchi 11, 2013
Vurugu hizo ziliibuka, baada ya kutangazwa kwa matokeo ya urais yaliyompa ushindi Uhuru Kenyatta.
DOKEZO
Mahakama Kuu ya Kenya ndicho chombo pekee chenye uwezo wa kutengua matokeo ya urais yaliyotangazwa IEBC.
Jopo la majaji watano ndilo litakalosikiliza rufaa ya mgombea wa Cord, Raila Odinga; nao ni Jaji Mkuu, Dk. Willy Mutunga ambaye ni Rais wa Mahakama hiyo, wengine ni Majaji Dk. Smokin Wanjala, Njoki Ndung’u, Philip Tunoi, Jackton Boma Ojwang na Mohamed Ibrahim.
Source: Mwananchi, Jumatatu, Marchi 11, 2013
"BILA DIAMOND SINA MVUTO"...WEMA SEPETU
Wema Sepetu amefunguka kuwa anapenda kuvaa urembo wenye madini ya almasi (diamond) kwani humpendeza kuliko madini mengine.
Akizungumza na mwandishi wetu, Wema alisema amekuwa akivaa madini mbalimbali ila tangu alipoanza kuvaa ya ‘diamond’, watu wake wa karibu wamekuwa wakimsifia kuwa anatoka chicha.
“Ukiniambia nichague madini kati ya silver, gold na diamond mimi nitachagua diamond kwani yananipendeza sana, bila kuyavaa nahisi sijapendeza,’’ alisema Wema.
Akizungumza na mwandishi wetu, Wema alisema amekuwa akivaa madini mbalimbali ila tangu alipoanza kuvaa ya ‘diamond’, watu wake wa karibu wamekuwa wakimsifia kuwa anatoka chicha.
“Ukiniambia nichague madini kati ya silver, gold na diamond mimi nitachagua diamond kwani yananipendeza sana, bila kuyavaa nahisi sijapendeza,’’ alisema Wema.
Monday, March 11, 2013
RAIS KIKWETE AMTUMIA SALAMU ZA PONGEZI RAIS MTEULE WA KENYA
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemtumia salamu za pongezi nyingi Rais Mteule wa Jamhuri ya Kenya, Mheshimiwa Uhuru Kenyatta.
Katika salamu hizo zilizotumwa leo, Jumamosi, Machi 9, 2013, saa chache baada ya kuthibitishwa rasmi kuwa Mheshimiwa Kenyatta ameshinda Uchaguzi Mkuu wa Kenya uliofanyika mwanzoni mwa wiki hii Jumatatu, Machi 4, 2013, Rais Kikwete amemwambia Mheshimiwa Uhuru Kenyatta:
“Mpendwa Rais Mteule na Kaka, ilikuwa ni furaha kubwa kwangu kupokea taarifa ya ushindi wako wa kuchaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Kenya. Niruhusu, kwa niaba ya Serikali na Wananchi wa Tanzania, na kwa hakika, kwa niaba yangu binafsi kukupogenza kwa dhati ya moyo wangu kwa mafanikio haya makubwa ya kuchaguliwa kwako.”
Katika salamu hizo zilizotumwa leo, Jumamosi, Machi 9, 2013, saa chache baada ya kuthibitishwa rasmi kuwa Mheshimiwa Kenyatta ameshinda Uchaguzi Mkuu wa Kenya uliofanyika mwanzoni mwa wiki hii Jumatatu, Machi 4, 2013, Rais Kikwete amemwambia Mheshimiwa Uhuru Kenyatta:
“Mpendwa Rais Mteule na Kaka, ilikuwa ni furaha kubwa kwangu kupokea taarifa ya ushindi wako wa kuchaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Kenya. Niruhusu, kwa niaba ya Serikali na Wananchi wa Tanzania, na kwa hakika, kwa niaba yangu binafsi kukupogenza kwa dhati ya moyo wangu kwa mafanikio haya makubwa ya kuchaguliwa kwako.”
Subscribe to:
Posts (Atom)























