Friday, June 22, 2012
Mtoto Mchanga akutwa ametupwa akiwa amefariki karibu na Msikiti wa Soweto jijini Mbeya Asubuhi hii
Katika hali ya kutatanisha wananchi wa Soweto jijini Mbeya wamekutana na Kifurushi ambacho ndani yake kulikuwa na mtoto mchanga amewekwa na kutupwa akiwa amefariki, ikiwa ni tukio la pili kutokea eneo hilo baada ya tukio kama hilo kutokea wiki mbili zilizopita.
Hata hivyo akiongea na baadhi ya wananchi ambao hawakupenda kutaja majina yao wamedai kwamba kuna dispensary jirani hapo ambayo hawakutaka sema ni hospital ipi ambapo wana wasi wasi kwamba hutoa Mimba mabinti na kuwatupa eneo hilo. Jamani Binadamu tumekuwa wanyama huu ndio mwisho wa dunia, wanawake tunataka nini Jamani??
Kwa picha na habari zaidi tembelea Mbeya yetu Blog
LULU AKAANGWA NA MAWAKILI WA SERIKALI JUU YA UMRI WAKE
MAWAKILI wa Serikali jana waliwasilisha vielelezo Mahakama kuu kuthibitisha kwamba umri wa msanii wa filamu Elizabert Michael ni zaidi ya miaka 18.Habari zilizolifikia gazeti hili na kuthibitishwa na mawakili wawili; mmoja wa Lulu na mwingine wa Serikali ambao hawakutaka kutajwa, zimeeleza kuwa vielelezo hivyo vimewasilishwa jana mahakamani hapo.
Habari zimeeleza kuwa moja ya vielelezo hivyo vya Jamhuri ni Mkanda wa video aina ya CD, yenye mahohjiano kati ya mshtakiwa huyo na mtangazaji mmoja nchini.
"Vingine ni maelezo ya mshtakiwa huyo aliyoyatoa polisi wakati alipohojiwa kuhusu tuhuma zinazomkabili, maombi ya hati ya kusafiria (Passport) na maombi ya leseni ya udereva, alisema mmoja wa mawakili hao.
Awali vielelezo hivyo walitakiwa kuviwasilishwa juzi, lakini ilishindikana na badala yake vikawasilishwa jana.
Baada ya vielelezo kesi hiyo itasikilizwa Juni 25 mwaka huu. Lulu anakabiliwa na kesi ya mauaji katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akituhumiwa kumuua msanii mwenzake, Marehemu Steven Kanumba aliyefariki dunia nyumbani kwake Sinza, April 7, 2012.
Hata hivyo umri wake umezua utata baada ya mawakili wake wanaomtetea kudai kuwa bado ni mtoto kwa kuwa ana umri wa miaka 17 na si 18 kama hati ya mashtaka inavyoonyesha.
Hivyo mawakili hao walilazimika kuwasilisha maombi mahakamani kuiomba mahakama iruhusu ufanyike uchunguzi wa umri sahihi wa mshtakiwa huyo na ikiridhika kuwa ni mtoto basi kesi yake iendeshwe kwa misingi ya kesi za watoto wanaokinzana na sheria ili kulinda maslahi yake.
Juni 11, 2012 Mahakama Kuu ilikubali yenyewe kufanya uchunguzi huo kwa lengo la kubaini usahihi wa umri wa mshtakiwa huyo na ikaziagiza na kuzipangia tarehe pande zote katika kesi hiyo kuwasilisha mahakamani hapo vielelezo watakavyovitumia katika hoja zao.
Jopo la mawakili wanaomtetea Lulu likiongozwa na Kennedy Fungamtama Juni 13 waliwasilisha mahakamani hati za viapo vya wazazi wake na vielelezo vingine kikiwemo cheti cha kuzaliwa na cha ubatizo vinavyoonesha kuwa bado ni mtoto.
Lakini taarifa zilizopatikana mahakamani hapo zinaeleza kuwa vielelezo vilivyowasilishwa na Jamhuri vinaonesha kuwa mshtakiwa huyo ni mtu mzima kwa kuwa kwa mujibu wa vielezo hivyo ana umri zaidi ya miaka 18.
Viapo vya wazazi wa mshtakiwa huyo vilivyowasilishwa mahakamani hapo na Makamu wa Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) Peter Kibatala ambaye ni mmoja wa mawakili wanaomtetea Lulu vinaeleza kuwa mshtakiwa huyo ana umri wa miaka 17.
Viapo hivyo ambavyo Gazeti hili limefanikiwa kuviona ni kiapo cha mama yake Lulu Lucresia Augustin Kalugila, mkazi wa Dar eS Salaam na kiapo cha baba mzazi Michael Kimemeta, mkazi wa Moshi.
Viapo vyote vinaeleza kuwa mshtakiwa huyo alizaliwa April 16, 1995 katika kituo cha Afya Muhimbili na kupewa cheti cha kuzaliwa namba B.0318479 cha Julai 23, 2004.
Pia viapo hivyo vinaeleza kuwa baada ya kuzaliwa mshtakiwa, mama yake alimpa jina la Diana Michael Kimemeta, lakini alimpeleka mtoto huyo Moshi mkoani Kilimanjaro kwa ndugu zake, walimpa jina la Elizabeth, jina la bibi yake Elizabeth Shikana
Okwi asaini Orlando Pirates kwa Sh 190m
Emmanuel Okwi.
KLABU ya Orlando Pirates ipo kwenye hatua za mwisho kumsajili kiungo mshambuliaji wa Simba, Emmanuel Okwi, raia wa Uganda.
Okwi anatarajiwa kwenda nchini Afrika Kusini wiki ijayo ili kukamilisha mchakato wa usajili wake ambao utaigharimu Orlando Pirates kiasi cha randi milioni 7 ambazo ni zaidi ya shilingi milioni 190.
Mganda huyo ambaye alichangia kuipa Simba ubingwa wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara msimu uliopita, aliwahi kufanya majaribio klabuni hapo msimu uliopita na alikuwa ameitwa tena kwa ajili ya kukamilisha zoezi hilo kwa mara ya pili.
Gazeti moja la michezo la Afrika Kusini limemnukuu Ofisa Habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga: “Kila kitu kimekamilika lakini kuna vitu vichache ambavyo tunatakiwa kukamilisha kabla hatujamruhusu rasmi Okwi.
“Okwi alikuwa msaada mkubwa kwenye klabu yetu kutwaa ubingwa wa ligi kuu (Bara) msimu uliopita, ulikuwa ni uamuzi mgumu kumruhusu aondoke, lakini tuna furaha na tunamtakia neema huko aendako.”
KLABU ya Orlando Pirates ipo kwenye hatua za mwisho kumsajili kiungo mshambuliaji wa Simba, Emmanuel Okwi, raia wa Uganda.
Okwi anatarajiwa kwenda nchini Afrika Kusini wiki ijayo ili kukamilisha mchakato wa usajili wake ambao utaigharimu Orlando Pirates kiasi cha randi milioni 7 ambazo ni zaidi ya shilingi milioni 190.
Mganda huyo ambaye alichangia kuipa Simba ubingwa wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara msimu uliopita, aliwahi kufanya majaribio klabuni hapo msimu uliopita na alikuwa ameitwa tena kwa ajili ya kukamilisha zoezi hilo kwa mara ya pili.
Gazeti moja la michezo la Afrika Kusini limemnukuu Ofisa Habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga: “Kila kitu kimekamilika lakini kuna vitu vichache ambavyo tunatakiwa kukamilisha kabla hatujamruhusu rasmi Okwi.
“Okwi alikuwa msaada mkubwa kwenye klabu yetu kutwaa ubingwa wa ligi kuu (Bara) msimu uliopita, ulikuwa ni uamuzi mgumu kumruhusu aondoke, lakini tuna furaha na tunamtakia neema huko aendako.”
UNAIJUA NGOZI YAKO NI AINA GANI NA UITUNZAJE?!!
Ni vizuri sana kwako kuweza kujua aina ya ngozi yako maana itasidia wewe uweze kuitunza ngozi yako vizuri.Vile vile itakusaidi katika kujua ni vipozi vya aina gani utumie kutokana na ngozi yako. Hakuna ngozi mbili ambazo zinafanana exactly ila zinatofautiana ambapo inawezekana ngozi yako ikawa ni Ngozi Kavu, Ngozi ya Kawaida, Ngozi ya mafuta na ngozi mchanganyiko yaani combine skin.
ZAIDI INGIA BONGO UREMBO UKAREMBEKE
ZAIDI INGIA BONGO UREMBO UKAREMBEKE
Mrisho Ngassa atua Jangwani
Mrisho Ngassa.
KIUNGO wa Azam FC, Mrisho Ngassa, jana Alhamisi alitua makao makuu ya klabu ya Yanga yaliyopo Jangwani jijini Dar es Salaam na kupokewa kwa shangwe kubwa.
Ngassa ana uwezekano mkubwa wa kuwemo kwenye kikosi cha Yanga kitakachoshiriki michuano ya Kombe la Kagame inayotarajiwa kuanza Julai 14, mwaka huu.
Ngassa aliwasili Jangwani saa 5:07 asubuhi akiwa ndani ya gari lake aina ya Toyota Corona lenye namba za usajili T 508 AUB, ikiwa ni muda mfupi baada ya mazoezi ya timu hiyo kumalizika kwenye Uwanja wa Kaunda, kisha kwenda kuegesha gari lake sehemu maalum inayotumiwa na viongozi na wachezaji wa Yanga pindi wanapowasili klabuni hapo.
Wakati umati wa mashabiki uliokuwa ukishuhudia mazoezi ukijiandaa kuondoka, ghafla ulimuona Ngassa na ndipo ukalizunguka gari lake na kuanza kumshangilia. Kuona hivyo Ngassa alisita kwa muda kutoka kisha kufungua mlango wa gari na kutoka.
Mashabiki hao walimvamia na kumbeba juujuu kwa furaha huku wakiimba kwa kulitaja jina lake ‘Ngassa! Ngassa! Ngassa! Ngassa!’ Lakini baadaye aliwataka wamshushe, mashabiki hao walitii amri hiyo.
Baada ya hapo, alianza kuelekea ndani ya jengo huku akisalimiana na wachezaji wa Yanga waliokuwepo eneo hilo, muda mfupi baadaye Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Yanga, Seif Ahmeid ‘Seif Magari’ alitokea ndani ya jengo hilo na kuingia naye kwenye chumba namba saba.
Baadaye, Ngassa alipandisha ghorofani na kuingia kwenye chumba namba saba ambapo alikuwemo mshambuliaji wa timu hiyo, Jerry Tegete. Mpaka gazeti hili lilipoondoka klabuni hapo 5:45 asubuhi, Ngassa alikuwa hajatoka chumbani humo.
Alipoulizwa kuhusiana na ujio wake Jangwani, Ngassa alisema: “Nimekuja kuonana na Jerry, tulipanga tukutane hapa kwa ajili ya kufanya mazungumzo yetu binafsi, siyo ya mpira.”
Aidha, habari za ndani kutoka kwa mmoja wa viongozi wa klabu hiyo, zimethibitisha kuwa kweli Jangwani wamefanya mazungumzo na Azam, kilichobakia ni makubaliano ya mwisho kabla ya kumtambulisha rasmi Ngassa kuwa mchezaji wa Yanga.
Mpigapicha wa gazeti hili, Richard Bukos, alimpiga picha mchezaji huyo wakati akiwasili klabuni hapo lakini Ngassa na baadhi ya mashabiki walimuomba kufuta picha hizo sababu mambo hayajakamilika na kudai zinaweza kumsababishia matatizo ya uhamisho wake.
Ureno yatua nusu fainali Euro 2012
CRISTIANO Ronaldo jana aliendelea kung’aa baada ya kufanikiwa kuiongoza nchi yake kufuzu hatua ya nusu fainali ya michuano ya Euro 2012 kwa kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Czech.
Ronaldo alifunga bao pekee kwenye mchezo huo baada ya kuiwahi krosi safi iliyopigwa na winga wa Manchester United, Luis Nani katika dakika ya 79.
Katika mchezo huo Czech walionekana kuzidiwa katika dakika zote na walifanikiwa kufika langoni mwa Ureno mara moja tu kipindi cha kwanza.
Ronaldo sasa amefikisha mabao matatu kwenye michuano hiyo baada ya kufanikiwa kufunga mawili kwenye mchezo wa makundi dhidi ya Uholanzi.
Katika historia ya Ureno haijawahi kutwaa ubingwa huu zaidi ya kufika hatua ya nusu fainali mara mbili mwaka 1984 na 2000.
Kutokana na ushindi huo, Ureno inasubiri kukutana na mshindi wa mechi kati ya Ufaransa dhidi ya Hispania katika nusu fainali ya kwanza mnamo Juni 27, 2012.
Ronaldo alifunga bao pekee kwenye mchezo huo baada ya kuiwahi krosi safi iliyopigwa na winga wa Manchester United, Luis Nani katika dakika ya 79.
Katika mchezo huo Czech walionekana kuzidiwa katika dakika zote na walifanikiwa kufika langoni mwa Ureno mara moja tu kipindi cha kwanza.
Ronaldo sasa amefikisha mabao matatu kwenye michuano hiyo baada ya kufanikiwa kufunga mawili kwenye mchezo wa makundi dhidi ya Uholanzi.
Katika historia ya Ureno haijawahi kutwaa ubingwa huu zaidi ya kufika hatua ya nusu fainali mara mbili mwaka 1984 na 2000.
Kutokana na ushindi huo, Ureno inasubiri kukutana na mshindi wa mechi kati ya Ufaransa dhidi ya Hispania katika nusu fainali ya kwanza mnamo Juni 27, 2012.
Thursday, June 21, 2012
DOGO JANJA ANARUDI DAR KESHO, YOTE MENGINE ALIYOYASEMA NDIO HAYA.
Exclusive na AMPLIFAYA Janja ambae amemaliza wiki moja toka arudi kwao Arusha, amesema “namshukuru Mungu amesikia kilio changu na nakuja kucheki mikataba ya kujiunga na kundi la WATANASHATI kwa Ostaz Juma na kama nitaridhika na mikataba nitajiunga nao, nimekaa na wazazi wameniambia zile zilikua hasira tu nirudi Dar es salaam kusoma na kufanya muziki kweli nikakaa nikajifikiria nikaona ni sawa”
Janja mwenye umri wa miaka 16 kwenye sentensi nyingine amesema “Ostaz kaniambia atanisomesha shule ambayo nitakua nasoma napelekwa na kurudishwa nyumbani na gari nitakua sina mawazo, kama mashabiki wangu mnanipenda njooni mnipokee Airport ijumaa nitatua na ndege pale”
KWA MASHABIKI WOTE WA MAREHEMU KANUMBA.
Wakati huu ambapo maonyesho ya sabasaba yanakaribia kuanza Dar es salaam familia yake imeamua kuchukua banda maalum kwenye viwanja vya saba saba kwa ajili tu ya kuendelea kumuenzi Marehemu Kanumba.
Seth ambae ni Mdogo wake waliekua wakiishi pamoja Sinza Dar es salaam amesema ni banda la Kanumba litakalokua na Nguo zenye alama alizokua anazitumia Kanumba ikiwa ni pamoja na jina na ujumbe, kutakua na picha zilizo kwenye frame za Kanumba zinazomuonyesha toka akiwa utotoni, pia vikombe, kanga, bazee na vitu vingine vingi vyenye alama na picha za Kanumba.
Taswira Za Mheshimiwa Godbless Lema Akiung'uruma Kwenye Mkutano Wa Hadhara Wa CHADEMA Manzese Jijini Dar es Salaam
Aliyekua Mbunge wa Arusha Mjini(CHADEMA)Mheshimiwa Godbles Lema Akiunguruma kwenye mkutano wa hadhara Manzese jijini Dar es SalaamMwenyekiti wa Umoja wa Baraza la Vijana wa CHADEMA John Henche(kushoto)akifwatilia kwa makini mkutano wa Chadema.
Sehemu ya Umati Mkubwa wa Wananchi waliojitokeza kwenye mkutano wa hadhara wa chadema
Omotola Kuizindua Supa Star ya Wema Sepetu Jumapili Giraffe Hotel
Ni onyesho maalum la familia
MKALI wa filamu nchini Nigeria na Afrika, Omotola Jalade atazindua filamu ya Wema Sepetu Jumapili hii katika Ukumbi wa Hoteli ya Girafee Ocean View, iliyopo Mbezi Beach.
Filamu hiyo iitwayo Super Star imechezwa na Wema, ikionyesha maisha ya mtu maarufu na changamoto anazozipata ikiwemo kuandikwa mambo mbalimbali ikiwemo taarifa za vyombo vya habari.
Katika uzinduzi huo, bendi kutoka Tanzania House Of Talent (THT) watatoa burudani, kabla ya mashabiki kupata nafasi ya kupiga picha na msanii huyo.
Omotola, ambaye ni mke wa rubani Kapteni Matthew Ekeinde, ambao walifunga ndoa yao angani kwenye ndege atatoa nafasi ya kupiga picha na watu kadhaa.
Katika uzinduzi huo, pamoja na burudani ya muziki, mashabiki watakaofika hapo, watapata pia fursa ya kuiona filamu ya Super Star katika viwanja hivyo vya hoteli hiyo iliyoko ufukweni.
Omotola ambaye yuko kwenye ndoa kwa miaka 16 akiwa na watoto wanne, ana jumla ya albamu mbili za muziki.
Msanii huyo ambaye mwaka jana alitangaza kuachana na kucheza filamu kutokana na kuandikwa vibaya, anatarajiwa kuwa kivutio kikubwa kwenye uzinduzi huo ambao kiingilio kitakuwa Sh 30, 000 kwa wakubwa na watoto 10,000. USIKOSE.
MKALI wa filamu nchini Nigeria na Afrika, Omotola Jalade atazindua filamu ya Wema Sepetu Jumapili hii katika Ukumbi wa Hoteli ya Girafee Ocean View, iliyopo Mbezi Beach.
Filamu hiyo iitwayo Super Star imechezwa na Wema, ikionyesha maisha ya mtu maarufu na changamoto anazozipata ikiwemo kuandikwa mambo mbalimbali ikiwemo taarifa za vyombo vya habari.
Katika uzinduzi huo, bendi kutoka Tanzania House Of Talent (THT) watatoa burudani, kabla ya mashabiki kupata nafasi ya kupiga picha na msanii huyo.
Omotola, ambaye ni mke wa rubani Kapteni Matthew Ekeinde, ambao walifunga ndoa yao angani kwenye ndege atatoa nafasi ya kupiga picha na watu kadhaa.
Katika uzinduzi huo, pamoja na burudani ya muziki, mashabiki watakaofika hapo, watapata pia fursa ya kuiona filamu ya Super Star katika viwanja hivyo vya hoteli hiyo iliyoko ufukweni.
Omotola ambaye yuko kwenye ndoa kwa miaka 16 akiwa na watoto wanne, ana jumla ya albamu mbili za muziki.
Msanii huyo ambaye mwaka jana alitangaza kuachana na kucheza filamu kutokana na kuandikwa vibaya, anatarajiwa kuwa kivutio kikubwa kwenye uzinduzi huo ambao kiingilio kitakuwa Sh 30, 000 kwa wakubwa na watoto 10,000. USIKOSE.
Wednesday, June 20, 2012
Tuesday, June 19, 2012
HOTUBA YA MWENYEKITI WA TUME YA MABADILIKO YA KATIBA
HOTUBA YA MWENYEKITI WA TUME YA MABADILIKO YA KATIBA
MHE. JOSEPH WARIOBA KATIKA MKUTANO WA WAANDISHI WA
HABARI TAREHE 19 JUNI, 2012 KATIKA UKUMBI WA
KARIMJEE, DAR ES SALAAM
Ndugu Wanahabari,
Nianze kwa kuwashukuru kwa kuitikia mwaliko wetu. Tume ya Mabadiliko ya Katiba ilianza kazi mwanzoni mwa Mwezi Mei, 2012 na kipindi hiki tumekitumia kwa maandalizi na sasa tuko tayari kuanza awamu ya kwanza ya kazi yetu, yaani kukusanya na kuratibu maoni ya wananchi. Baada ya hapo itafuata awamu ya pili ya kuandaa taarifa, mapendekezo na Rasimu ya Katiba Mpya. Baadaye Tume itakutana na Mabaraza ya Katiba na mwisho Rasimu ya Katiba itafikishwa kwenye Bunge Maalum.
Kabla ya kuanza mchakato wa kushauriana na wananchi, ikiwa ni pamoja na safari za mikoani, tumeona ni muhimu na busara kukutana na nyinyi kwanza. Vyombo vya habari ni wadau wakubwa katika mchakato huu. Tume inaamini kwamba vyombo vya habari vina nafasi kubwa sana katika kufanikisha mchakato mzima hasa katika kutangaza maoni ya wananchi ili, licha ya kukusanya maoni tu, mchakato uwasaidie wananchi kubadilishana mawazo kuhusu aina ya Taifa wanalolitaka na aina ya Katiba wanayoitaka.
Ndugu Wanahabari,
Pamoja nami leo Wajumbe wote wa Tume, ikiwa ni pamoja na Makamu Mwenyekiti - Jaji Augustino Ramadhani, Katibu na Naibu Katibu.
Jukumu tulilokabidhiwa ni kubwa na muhimu kwa Watanzania, hivyo basi matayarisho tuliyokuwa tunayafanya yalikuwa na lengo la kuhakikisha mchakato mzima unakwenda kama ilivyokusudiwa.
Katika maandalizi yetu, tulitambua umuhimu wa elimu kwa umma kuhusu mambo yatakayozingatiwa katika Katiba. Ni wazi kuwa wananchi hawawezi kutoa maoni yao kwa ukamilifu bila ya kuwa na elimu ya kutosha. Kwa hiyo, kwa kuzingatia umuhimu huo, Tume imetumia muda mwingi kupata na kuandaa nyaraka muhimu kwa ajili ya kuwapatia wananchi elimu ya kutosha.
Tume imepata nakala elfu mia tano za Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya 1977, nakala elfu kumi za Katiba ya Zanzibar ya 1984 na nakala elfu mia tano za Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Sura ya 83. Kwa kutambua kwamba nyaraka hizi hazitoshi, na hata kama zikipatikana kwa wingi ni vigumu kwa wananchi kuzisoma na kuzielewa kwa urahisi, Tume imeandaa nyaraka ambazo ni rahisi kuzisoma na kuzielewa.
Nyaraka hizo ni Katiba ya Jamhuri ya 1977, Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Sura ya 83, kwa lugha nyepesi, Hadidu za Rejea, Program ya Elimu kwa Umma na Utekelezaji wa Kazi za Tume. Nyaraka hizi tumeanza kuzisambaza na leo, tunawakabidhi nyinyi nyaraka zote ili msaidie kuzitangaza na kuelemisha wananchi. Aidha, Tume imeandaa vipeperushi kuhusu kazi za Tume ya Mabadiliko ya Katiba na Maswali Yanayoulizwa Mara kwa Mara.
Ndugu Wanahabari,
Hivi karibuni Tume itaanza safari za mikoani. Tume imejigawa katika makundi saba na kila kundi litafanya safari nne mikoani kati ya sasa na mwisho wa mwaka. Kila kundi litafanya kazi katika mkoa kwa wastani wa mwezi mmoja isipokuwa kwenye mikoa iliyo midogo kwa eneo, ambapo Tume itatumia muda mfupi. Tutaanza na mikoa minane ambayo ni Dodoma, Kagera, Kusini Pemba, Kusini Unguja, Manyara, Pwani, Shinyanga na Tanga.
Tunaomba wananchi wajitokeze kwa wingi na kutoa maoni yao kwa uhuru, uwazi, bila ya hofu yoyote na kwa utulivu. Tunaomba wananchi wawe wavumilivu na watoe maoni bila jazba au kubeza. Tunaomba wananchi wawe wavumilivu sana kusikiliza mawazo ya wengine hata kama hawakubaliani na mawazo hayo.
Lengo letu kama Tume, ni kuhakikisha kuwa Watanzania kwa jumla wanatoa maoni yao. Tungependa sana kama ingeliwezekana, kila Mtanzania apate fursa ya kutoa maoni yake. Lakini, ukizingatia ukubwa wa nchi yetu na mazingira halisi, ni wazi haitawezekana kuonana na kila mtu. Pamoja na hivyo, ni kusudio letu kufanya kila linalowezekana kupata mawazo ambayo yataonyesha matakwa, mategemeo na mahitaji ya Watanzania wote. Katika upeo huo, basi tutafanya kila jitihada kwa njia mbali mbali kujaribu kuhakikisha kwamba maoni ya Watanzania kwa ujumla yanawasilishwa na kufanyiwa kazi vilivyo.
Pamoja na mikutano mbali mbali itakayofanyika katika mikoa yote, tutakuwa na mfumo wa kupokea maoni ya Watanzania wa kutoka pande zote za ndani ya nchi na nje ya nchi kupitia simu, barua pepe, mitandao ya kijamii kama facebook, twitter na blogu na tovuti na pia kwa njia ya posta. Tunaomba wananchi wajitahidi kutoa hoja badala ya malalamiko peke yake. Mapendekezo ya mambo ya kuingia kwenye Katiba yatasaidia sana badala ya malalamiko tu.
Tume, kwa kiwango fulani imeanza kuratibu maoni ya wananchi yanayotolewa kwa njia mbali mbali. Mwelekeo wa kubaini maeneo ya kufanyia kazi unaanza kuonekana, hasa kuhusu taasisi za dola kama vile Serikali na vyombo vyake vyote na madaraka ya viongozi na taasisi mbali mbali. Tume inaomba maeneo mengine muhimu nayo yapewe uzito, hasa maeneo yaliyo katika Sura ya Kwanza ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977. Sehemu hiyo ndiyo moyo wa Katiba. Yapo maeneo manne muhimu ambayo Tume ingependa kupata maoni ya wananchi.
Eneo la Kwanza, linahusu misingi ya Taifa. Misingi ndiyo nguzo ya utamaduni wa nchi na wananchi wake; misingi ndiyo nguzo ya nidhamu ya nchi na wananchi wake; misingi ndiyo nguzo ya maadili ya nchi na wananchi wake. Katiba yetu imetaja misingi mikuu kuwa ni uhuru, haki, udugu, amani, demokrasia na Serikali kutofungamana na dini yoyote ingawa wananchi wana uhuru wa kuabudu. Misingi hii ndiyo nguzo ya mshikamano na utulivu wa wananchi. Baadhi ya watu wanasema ama misingi hii haitoshi au imetelekezwa. Wengine wanasema inatosha. Tume ingependa kupata maoni ya wananchi kuhusu eneo hili.
Eneo la Pili, ni kuhusu mamlaka ya wananchi. Katiba ya sasa inaeleza kwamba wananchi ndio msingi wa mamlaka yote na msukumo mkubwa wa mchakato huu wa kupata Katiba Mpya ni matakwa ya kuwawezesha wananchi kutunga Katiba yao. Lakini kuna watu wanasema mamlaka ya wananchi hayakufafanuliwa, wanasema mamlaka ya taasisi za dola kama vile Serikali, Bunge, Mahakama, Tume mbali mbali za kikatiba, na hata Vyama vya Siasa, yamefafanuliwa. Lakini mamlaka ya wananchi hayakufafanuliwa na wala hakuna utaratibu wa kuyatumia madaraka hayo. Wanasema wananchi wanatumiwa tu kisiasa wakati mamlaka yao yote yameporwa. Wengine wanasema mamlaka hayo yapo isipokuwa wananchi wameyakasimu kwa taasisi mbali mbali. Tume ingependa kupata maoni ya wananchi kuhusu eneo hili.
Eneo la Tatu, ni malengo muhimu na misingi ya mwelekeo wa shughuli za Serikali. Malengo hayo yameelezwa vizuri sana katika Ibara ya 9 ya Katiba. Baadhi yake ni:-
Malengo haya ndiyo ndoto (vision) ya wananchi. Malengo haya ndiyo yanajumuisha matumaini ya Watanzania kuhusu aina ya Tanzania wanayoitaka. Mgawanyo wa madaraka kwa mamlaka mbali mbali za dola unakusudiwa kuhakikisha kwamba malengo haya yanafikiwa.
Baadhi ya watu wanasema kuwa malengo haya yanatosha ila hayatekelezwi kwa ukamilifu. Wengine wanasema kuwa hayatoshi katika zama hizi. Tume ingependa kupata maoni ya wananchi kuhusu malengo muhimu ya Taifa. Tume itapenda kufahamu ndoto za wananchi kuhusu rasilimali za Taifa na jinsi ya kuzilinda, kuziendeleza na kuzitumia kwa ajili ya maendeleo ya wananchi.
Tume ingependa kusikia ndoto za wakulima, wafanyakazi, wafugaji, wavuvi, wafanya biashara wakubwa na wadogo, wanaume, wanawake, wazee, vijana, walemavu na kadhalika.
Eneo la Nne, ni haki za binadamu na wajibu kwa jamii. Sehemu ya Tatu ya Sura ya Kwanza ya Katiba ina orodha ndefu ya haki na wajibu muhimu kwa raia. Baadhi ya watu wanasema haki hizi hazitoshi. Wengine wanasema haki za mtu binafsi zinadhulumu haki za jamii na wengine wanasema haki za binadamu zinaminywa au hazitekelezwi kwa ukamilifu au zinavunjwa. Tume inapenda kupata maoni ya wananchi.
Ndugu Wanahabari,
Awamu ya Pili ya uratibu na ukusanyaji wa maoni ya wananchi itafanyika kupitia Mabaraza ya Katiba. Wakati huo, Tume itawaomba wananchi watoe maoni yao kuhusu Rasimu ya Katiba. Kupitia kwenu, naomba wananchi kufika kwa wingi katika mikutano ya ukusanyaji wa maoni katika awamu zote mbili. Nawaomba wananchi kutoa mawazo yao kwa uwazi na bila ya hofu yoyote. Tume itafanya kazi zake kwa uhuru, uwazi na tunawahakikishia kwamba maoni yote yatakayotolewa na wananchi, taasisi, asasi za kiraia na makundi mengine yote yataheshimiwa na kufanyiwa kazi ipasavyo.
Ndugu Wanahabari,
Nimalizie kwa kurudia tena kwamba jukumu la vyombo vya habari ni kubwa katika kufanikisha kupatikana kwa Katiba Mpya. Pamoja na mambo mengine, wananchi wa sehemu moja ya nchi watafahamu maoni ya wenzao katika sehemu nyingine ya nchi. Naomba mlikubali jukumu hili ili kusaidia nchi ipate Katiba Mpya iliyo nzuri.
Nawashukuru.
TOA MAONI, TUPATE KATIBA MPYA
MHE. JOSEPH WARIOBA KATIKA MKUTANO WA WAANDISHI WA
HABARI TAREHE 19 JUNI, 2012 KATIKA UKUMBI WA
KARIMJEE, DAR ES SALAAM
Ndugu Wanahabari,
Nianze kwa kuwashukuru kwa kuitikia mwaliko wetu. Tume ya Mabadiliko ya Katiba ilianza kazi mwanzoni mwa Mwezi Mei, 2012 na kipindi hiki tumekitumia kwa maandalizi na sasa tuko tayari kuanza awamu ya kwanza ya kazi yetu, yaani kukusanya na kuratibu maoni ya wananchi. Baada ya hapo itafuata awamu ya pili ya kuandaa taarifa, mapendekezo na Rasimu ya Katiba Mpya. Baadaye Tume itakutana na Mabaraza ya Katiba na mwisho Rasimu ya Katiba itafikishwa kwenye Bunge Maalum.
Kabla ya kuanza mchakato wa kushauriana na wananchi, ikiwa ni pamoja na safari za mikoani, tumeona ni muhimu na busara kukutana na nyinyi kwanza. Vyombo vya habari ni wadau wakubwa katika mchakato huu. Tume inaamini kwamba vyombo vya habari vina nafasi kubwa sana katika kufanikisha mchakato mzima hasa katika kutangaza maoni ya wananchi ili, licha ya kukusanya maoni tu, mchakato uwasaidie wananchi kubadilishana mawazo kuhusu aina ya Taifa wanalolitaka na aina ya Katiba wanayoitaka.
Ndugu Wanahabari,
Pamoja nami leo Wajumbe wote wa Tume, ikiwa ni pamoja na Makamu Mwenyekiti - Jaji Augustino Ramadhani, Katibu na Naibu Katibu.
Jukumu tulilokabidhiwa ni kubwa na muhimu kwa Watanzania, hivyo basi matayarisho tuliyokuwa tunayafanya yalikuwa na lengo la kuhakikisha mchakato mzima unakwenda kama ilivyokusudiwa.
Katika maandalizi yetu, tulitambua umuhimu wa elimu kwa umma kuhusu mambo yatakayozingatiwa katika Katiba. Ni wazi kuwa wananchi hawawezi kutoa maoni yao kwa ukamilifu bila ya kuwa na elimu ya kutosha. Kwa hiyo, kwa kuzingatia umuhimu huo, Tume imetumia muda mwingi kupata na kuandaa nyaraka muhimu kwa ajili ya kuwapatia wananchi elimu ya kutosha.
Tume imepata nakala elfu mia tano za Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya 1977, nakala elfu kumi za Katiba ya Zanzibar ya 1984 na nakala elfu mia tano za Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Sura ya 83. Kwa kutambua kwamba nyaraka hizi hazitoshi, na hata kama zikipatikana kwa wingi ni vigumu kwa wananchi kuzisoma na kuzielewa kwa urahisi, Tume imeandaa nyaraka ambazo ni rahisi kuzisoma na kuzielewa.
Nyaraka hizo ni Katiba ya Jamhuri ya 1977, Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Sura ya 83, kwa lugha nyepesi, Hadidu za Rejea, Program ya Elimu kwa Umma na Utekelezaji wa Kazi za Tume. Nyaraka hizi tumeanza kuzisambaza na leo, tunawakabidhi nyinyi nyaraka zote ili msaidie kuzitangaza na kuelemisha wananchi. Aidha, Tume imeandaa vipeperushi kuhusu kazi za Tume ya Mabadiliko ya Katiba na Maswali Yanayoulizwa Mara kwa Mara.
Ndugu Wanahabari,
Hivi karibuni Tume itaanza safari za mikoani. Tume imejigawa katika makundi saba na kila kundi litafanya safari nne mikoani kati ya sasa na mwisho wa mwaka. Kila kundi litafanya kazi katika mkoa kwa wastani wa mwezi mmoja isipokuwa kwenye mikoa iliyo midogo kwa eneo, ambapo Tume itatumia muda mfupi. Tutaanza na mikoa minane ambayo ni Dodoma, Kagera, Kusini Pemba, Kusini Unguja, Manyara, Pwani, Shinyanga na Tanga.
Tunaomba wananchi wajitokeze kwa wingi na kutoa maoni yao kwa uhuru, uwazi, bila ya hofu yoyote na kwa utulivu. Tunaomba wananchi wawe wavumilivu na watoe maoni bila jazba au kubeza. Tunaomba wananchi wawe wavumilivu sana kusikiliza mawazo ya wengine hata kama hawakubaliani na mawazo hayo.
Lengo letu kama Tume, ni kuhakikisha kuwa Watanzania kwa jumla wanatoa maoni yao. Tungependa sana kama ingeliwezekana, kila Mtanzania apate fursa ya kutoa maoni yake. Lakini, ukizingatia ukubwa wa nchi yetu na mazingira halisi, ni wazi haitawezekana kuonana na kila mtu. Pamoja na hivyo, ni kusudio letu kufanya kila linalowezekana kupata mawazo ambayo yataonyesha matakwa, mategemeo na mahitaji ya Watanzania wote. Katika upeo huo, basi tutafanya kila jitihada kwa njia mbali mbali kujaribu kuhakikisha kwamba maoni ya Watanzania kwa ujumla yanawasilishwa na kufanyiwa kazi vilivyo.
Pamoja na mikutano mbali mbali itakayofanyika katika mikoa yote, tutakuwa na mfumo wa kupokea maoni ya Watanzania wa kutoka pande zote za ndani ya nchi na nje ya nchi kupitia simu, barua pepe, mitandao ya kijamii kama facebook, twitter na blogu na tovuti na pia kwa njia ya posta. Tunaomba wananchi wajitahidi kutoa hoja badala ya malalamiko peke yake. Mapendekezo ya mambo ya kuingia kwenye Katiba yatasaidia sana badala ya malalamiko tu.
Tume, kwa kiwango fulani imeanza kuratibu maoni ya wananchi yanayotolewa kwa njia mbali mbali. Mwelekeo wa kubaini maeneo ya kufanyia kazi unaanza kuonekana, hasa kuhusu taasisi za dola kama vile Serikali na vyombo vyake vyote na madaraka ya viongozi na taasisi mbali mbali. Tume inaomba maeneo mengine muhimu nayo yapewe uzito, hasa maeneo yaliyo katika Sura ya Kwanza ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977. Sehemu hiyo ndiyo moyo wa Katiba. Yapo maeneo manne muhimu ambayo Tume ingependa kupata maoni ya wananchi.
Eneo la Kwanza, linahusu misingi ya Taifa. Misingi ndiyo nguzo ya utamaduni wa nchi na wananchi wake; misingi ndiyo nguzo ya nidhamu ya nchi na wananchi wake; misingi ndiyo nguzo ya maadili ya nchi na wananchi wake. Katiba yetu imetaja misingi mikuu kuwa ni uhuru, haki, udugu, amani, demokrasia na Serikali kutofungamana na dini yoyote ingawa wananchi wana uhuru wa kuabudu. Misingi hii ndiyo nguzo ya mshikamano na utulivu wa wananchi. Baadhi ya watu wanasema ama misingi hii haitoshi au imetelekezwa. Wengine wanasema inatosha. Tume ingependa kupata maoni ya wananchi kuhusu eneo hili.
Eneo la Pili, ni kuhusu mamlaka ya wananchi. Katiba ya sasa inaeleza kwamba wananchi ndio msingi wa mamlaka yote na msukumo mkubwa wa mchakato huu wa kupata Katiba Mpya ni matakwa ya kuwawezesha wananchi kutunga Katiba yao. Lakini kuna watu wanasema mamlaka ya wananchi hayakufafanuliwa, wanasema mamlaka ya taasisi za dola kama vile Serikali, Bunge, Mahakama, Tume mbali mbali za kikatiba, na hata Vyama vya Siasa, yamefafanuliwa. Lakini mamlaka ya wananchi hayakufafanuliwa na wala hakuna utaratibu wa kuyatumia madaraka hayo. Wanasema wananchi wanatumiwa tu kisiasa wakati mamlaka yao yote yameporwa. Wengine wanasema mamlaka hayo yapo isipokuwa wananchi wameyakasimu kwa taasisi mbali mbali. Tume ingependa kupata maoni ya wananchi kuhusu eneo hili.
Eneo la Tatu, ni malengo muhimu na misingi ya mwelekeo wa shughuli za Serikali. Malengo hayo yameelezwa vizuri sana katika Ibara ya 9 ya Katiba. Baadhi yake ni:-
- Kwamba utu na haki nyinginezo zote za binadamu zinaheshimiwa na kuthaminiwa;
- Kwamba shughuli za Serikali zinatekelezwa kwa njia ambazo zitahakikisha kwamba utajiri wa Taifa unaendelezwa, unahifadhiwa na unatumiwa kwa manufaa ya wananchi wote kwa jumla na pia kuzuia mtu kumnyonya mtu mwingine;
- Kwamba mtu mwenye uwezo wa kufanya kazi anafanya kazi;
- Kwamba aina zote za dhuluma, vitisho, ubaguzi, rushwa, uonevu au upendeleo zinaondolewa nchini.
- Kwamba matumizi ya utajiri wa Taifa yanatilia mkazo maendeleo ya wananchi na hasa zaidi yanaelekezwa kwenye jitihada za kuondosha umaskini, ujinga na maradhi;
- Kwamba shughuli za uchumi haziendeshwi kwa njia zinazoweza kusababisha ulimbikizaji wa mali au njia kuu za uchumi katika mamlaka ya watu wachache binafsi.
Malengo haya ndiyo ndoto (vision) ya wananchi. Malengo haya ndiyo yanajumuisha matumaini ya Watanzania kuhusu aina ya Tanzania wanayoitaka. Mgawanyo wa madaraka kwa mamlaka mbali mbali za dola unakusudiwa kuhakikisha kwamba malengo haya yanafikiwa.
Baadhi ya watu wanasema kuwa malengo haya yanatosha ila hayatekelezwi kwa ukamilifu. Wengine wanasema kuwa hayatoshi katika zama hizi. Tume ingependa kupata maoni ya wananchi kuhusu malengo muhimu ya Taifa. Tume itapenda kufahamu ndoto za wananchi kuhusu rasilimali za Taifa na jinsi ya kuzilinda, kuziendeleza na kuzitumia kwa ajili ya maendeleo ya wananchi.
Tume ingependa kusikia ndoto za wakulima, wafanyakazi, wafugaji, wavuvi, wafanya biashara wakubwa na wadogo, wanaume, wanawake, wazee, vijana, walemavu na kadhalika.
Eneo la Nne, ni haki za binadamu na wajibu kwa jamii. Sehemu ya Tatu ya Sura ya Kwanza ya Katiba ina orodha ndefu ya haki na wajibu muhimu kwa raia. Baadhi ya watu wanasema haki hizi hazitoshi. Wengine wanasema haki za mtu binafsi zinadhulumu haki za jamii na wengine wanasema haki za binadamu zinaminywa au hazitekelezwi kwa ukamilifu au zinavunjwa. Tume inapenda kupata maoni ya wananchi.
Ndugu Wanahabari,
Awamu ya Pili ya uratibu na ukusanyaji wa maoni ya wananchi itafanyika kupitia Mabaraza ya Katiba. Wakati huo, Tume itawaomba wananchi watoe maoni yao kuhusu Rasimu ya Katiba. Kupitia kwenu, naomba wananchi kufika kwa wingi katika mikutano ya ukusanyaji wa maoni katika awamu zote mbili. Nawaomba wananchi kutoa mawazo yao kwa uwazi na bila ya hofu yoyote. Tume itafanya kazi zake kwa uhuru, uwazi na tunawahakikishia kwamba maoni yote yatakayotolewa na wananchi, taasisi, asasi za kiraia na makundi mengine yote yataheshimiwa na kufanyiwa kazi ipasavyo.
Ndugu Wanahabari,
Nimalizie kwa kurudia tena kwamba jukumu la vyombo vya habari ni kubwa katika kufanikisha kupatikana kwa Katiba Mpya. Pamoja na mambo mengine, wananchi wa sehemu moja ya nchi watafahamu maoni ya wenzao katika sehemu nyingine ya nchi. Naomba mlikubali jukumu hili ili kusaidia nchi ipate Katiba Mpya iliyo nzuri.
Nawashukuru.
TOA MAONI, TUPATE KATIBA MPYA
JOHN MNYIKA: Msimamo wangu wa sasa juu ya Kauli yangu bungeni!
Nitatoa tamko la kina baadae kuhusu kilichotokea lakini kwa ufupi ubovu wa bajeti hii ni matokeo ya udhaifu wa Rais Kikwete, yeye ndiye aliyesaini Mpango wa Taifa wa miaka mitano kama Kiongozi Mkuu wa Nchi tena kwa wino mwekundu kama Amiri Jeshi Mkuu.
Na yeye ndiye Mwenyekiti wa baraza la mawaziri, bajeti hii iliyoacha kuzingatia mpango wa Taifa imepita kwenye baraza alilloliongoza, pia kushindwa kutekelezwa kwa bajeti iliyopita ni matokeo pia ya udhaifu wa taasisi ya Urais.
Pia kwa mujibu wa Katiba Rais ndiye ambaye anapeleka bajeti bungeni, Waziri mwenye dhamana anapeleka tu kwa niaba.
Rais amepewa mamlaka makubwa juu ya bajeti ibara ya 99 imeweka mipaka kuhusu mambo ambayo bunge lina mamlaka nayo huku ibara ya 90 inasema bunge likikataa bajeti rais ana mamlaka ya kuvunja bunge.
Hivyo Rais Kikwete anapaswa kuagiza Waziri wa Fedha bajeti iondolewe irudi kwenye baraza la mawaziri ikafanyiwe marekebisho!
John Mnyika
19 Juni 2012
Subscribe to:
Posts (Atom)

















