Saturday, June 30, 2012

DEIDRE LORENZ KUITANGAZA TANZANIA

Deidre Lorenz akihojiwa na waandishi wa habari mjini Moshi.…
Deidre Lorenz akimkabidhi picha ya Ground Zero (New York) Rais wa Mt. Kili Marathon 1991, Onesmo Ngowi baada ya kukimbia mbio hizo.

Mcheza sinema maarufu wa Marekani Deidre Lorenz ameahidi kuleta wacheza sinema wenzake na kushiriki kwenye mbio za mwaka kesho za mt. Kilimanjaro Marathon zitakazokuwa zinatimiza miaka 23 tangu zianzishwe mwaka 1991.

Lorenz aliyekimbia mbio za mwaka huu ambazo zilipewa jina la “mbio za kutimiza miaka 50 ya uhuru wa Tanganyika” na Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) amesema kuwa atakuja na timu yake ya wapiga picha ili kupiga picha vivutio kadhaa vya Tanzania ikiwa ni pamoja na mlima Kilimanjaro. Gwiji hili la sinema za Santorini Blue, The Great Fight, Perfect Strangers na nyingine nyingi ameelezea kuipenda sana Tanzania.

“Sikutegemea kuikuta nchi nzuri kama hii” alisema mcheza sinema huyo ambaye ameshawahi kuchaguliwa zaidi ya mara 4 kugombea tuzo maarufu za Oscar. “Sasa nimeamini kuwa mlima Kilimanjaro ni mali ya Tanzania na nitautangaza katika sinema zangu zote”aliendelea kusema Deidre Lorenz.

Mcheza sinema huyu ambaye ameingia kwenye mkataba na kampuni kubwa ya Google hivi karibuni ili kuuza sinema zake katika mtandao aliielezea Tanzania kama nchi nzuri na yenye watu wakarimu sana.

Mbio za Mount Kilimanjaro Marathon zilianzishwa mwaka 1991 na Marie Frances anayetoka katika jiji la matajiri la Bethesda nchini Marekani baada ya kuombwa na balozi wa zamani wa Tanzania nchini Misri. Tangu kuanzishwa kwake mbio hizi zimekuwa zinaleta watalii matajiri katika mji wa Moshi kupanda mlima Kilimanjaro na kukimbia mbio hizi zinazojulikana kama Seven Continental Races.

Hakuna masharti yote ya kukimbia mbio hizi na watanzania wanaoshiriki katika mbio hizi huwa hawatozwi pesa za kiingilio.

Kwa kutambua mchango wake katika uchumi wake Manispaa ya Moshi iliibadilisha jina barabara ya zamani ya Bustani Ale na kuiita Marie Frances Boulevard ili kumuenzi mama huyu aliyejitolea maisha yake kuutangaza mlima Kilimanjaro.

“Kila siku napokea ujumbe kutoka nchi mbalimbali niende huko kuanzisha mbio za marathon lakini kwa sasa basi” alisema mama huyo aliyekuwa mtayarishaji wa vipindi vya televisheni ya ABC kabla ya kunzisha Mt. Kilimanjaro Marathon.

Alisema kuwa mwaka jana yeye na Rais wa klabu ya Mt. Kilimanjaro Marathon Mtanzania Onesmo Ngowi walifanya makubaliano ya Ethiopia Airlines (ET) jijini Addis Ababa kuzifanya mbio hizo kuwa za kimataifa zaidi. “ET walikubali kutoa ufadhili kwetu na pia kugharamia kushiriki kwetu katika mbio za New York Marathon, Boston Marathon na Los Angelos Maratthon ili kuitangaza vyema Tanznaia” alibainisha Frances.

Katika makubaliano hayo, Ngowi na Frances pia wataanzisha mbio za “King Solomon Marathon” zitakazofanyika katika jiji la Addis Ababa nchini Ethiopia.

Deidee Lorenz amefungua pazia kwa watu mashuhuri kushiriki katika mbio za marathon nchini Tanzania na ni jukumu la Watanzania kuchangamkia fursa zinazoletwa na ujio wao.

Imetumwa na:

Grace Soka

Afisa Uhusiano

MT. KILIMANJARO MARATHON 1991

Friday, June 29, 2012

OMOTOLA AONDOKA WEMA AMZAWADIA MAPAMBO YA ASILI

 Mwigizaji Omotola Jalade wa pili kushoto akikabidhiwa zawadi na za khanga, shanga na viatu Wema Sepetu wakati akiondoka kuelekea Nigeria jana usiku. Wanaoshuhudia ni Mkurugenzi wa Kampuni ya One Touch Solutions, Petter Mwendapole ambao waliratibu ziara ya msanii huyo. Mwingine wa msanii Snura.


Omotola akijaribu bangili za kimasai alizopewa kama zawadi
Mwigizaji Wema Sepetu akimvalisha Khanga Omotola Jalade muda mfupi kabla ya hajandoka nchini kuelekea Nigeria.


 MWIGIZAJI  maarufu kutoka Nigeria Omotola Jalade Ekeinde aliondoka nchini jana usiku na kuahidi kusaidia soko la filamu nchini liweze kufikia ngazi za kimataifa.

Akizungumza na Mkurugenzi wa kampuni ya One Touch Solutions, Petter Mwendapole iliyoratibu ziara yake pamoja na mwigizaji Wema Sepetu aliyekuwa mwenyeji wake, Omotola alisema Tanzania ina kila sababu ya kuwika kimataifa katika filamu.

“Kwa Afrika Tanzania inaweza kuwa namba moja kama Nigeria, mna hali ya hewa nzuri, vivutio vya utalii na pia mna waigizaji ambao wana vipaji, hii inaweza kuwapeleka mbali yapo mambo madogo ya kurekebisha,” amesema.

Alisema kwa kuanzia atafanya kazi kwa karibu na Wema Sepetu ambaye ndiye alikuwa mwenyeji wake na kuhakikisha anafikia mafanikio ya juu katika tasnia hiyo kwa kimataifa.

Omotola mama wa watoto watatu, alisema kwa Nigeria yeye anafahamika kama Super Star hiyo alipoambiwa anakuja kuzindua filamu ya jina hilo alijiona kuwa ni muhisika wa moja kwa moja.
Tangu kuwasili kwake nchini vyombo mbalimbali vya habari vya Nigeria vimekuwa vikatangaza na kuzipa taarifa za uzinduzi wa filamu ya super star nafasi kubwa.

Akiwa nchini alitembelea kituo cha watoto yatima kinachohudumiwa na Tanzania Mitindo House, kabla ya kula chakula cha mchana na watoto hao nyumbani kwa Wema na jioni yake kuzindua filamu katika hoteli ya Giraffe. Pia alitembelea jengo la Quality Plaza ambapo alikwenda kuangalia sinema.

Wakati akiondoka, Omotola alikabidhiwa Khanga, viatu vya kimasai na shanga. Mbali na Wafanyakazi wa One Touch na Endless Fame na Image Professional mwigizaji mwingine maarufu nchini na Mkurugenzi wa 5 Effect, Gabriel Mtitu alikuwepo uwanjani hapo kumsindikiza na walizungumza mambo kadhaa.

HIVI KWELI KUNA MTU “ANASTAHILI” KITENDO HIKI?

Soma hii habari kuhusu kauli ya Mbunge wa Korogwe Vijijini,Steven Ngonyani(Maji Marefu) na kujiuliza hivi baadhi ya hawa watu tunaowaita wawakilishi wetu huwa wanaropoka tu au wakiwa kule Bungeni wanasema kile ambacho wananchi wao wamewatuma au kile ambacho wanaamini kabisa kitasaidia wananchi wa jimbo wanaloliwakilisha?

Hivi kweli katika dunia ya leo ambapo wote tunaongelea habari za ukomeshwaji wa mateso(torture) dhidi ya binadamu, yupo Mbunge ambaye anaweza kusimama na kusema kipigo kama alichokipata Dr.Steven Ulimboka alistahili? Yaani kwa mwakilishi huyu,case closed,justice has been served! Mbaya zaidi Mbunge huyu hakutolewa Bungeni!

    "Mbunge wa Jimbo la Korogwe Vijijini, Steven Ngonyani maarufu kwa jina la Profesa Maji Marefu (pichani), leo amesema bungeni kuwa kipigo alichopata Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari, Dk. Steven Ulimboka, kinastahili ili naye apate machungu wanayopata wagonjwa wengine mahospitalini.

    Profesa Maji Marefu aliitoa kauli hiyo wakati akichangia hoja katika bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Bungeni Dodoma.

    Kauli hiyo ilisababisha tafrani kidogo bungeni, ambapo  Spika wa Bunge, Mhe. Anne Makinda  alilazimika kuingilia kati kumzuia Profesa Maji Marefu asiendelee kutoa kauli hiyo kwani jambo la madaktari bado liko mahakamani."

Chazo: blog ya Michuzi

MADAKTARI 72 WATIMULIWA KAZI MKOANI MBEYA


Mwenyekiti wa Bodi na Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Norman Sigara akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake kuhusu kufukuzwa kazi kwa madaktari hao.
                      Mkurugenzi wa Hospitali ya Rufaa jijini Mbeya, Dk E. Sankey akimsikiliza kwa makini  Kaimu  Mkuu wa Mkoa wa Mbeya.

BODI ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mbeya, imewasimamisha kazi madaktari 72 kwa kosa la kutoingia kazini kwa siku tano jambo ambalo ni kinyume cha makubaliano ya mkataba.

Imeelezwa kuwa madaktari hao ambao 54 ni wale wa mafunzo ambao waliingia mkataba wa miaka miwili na hospitali ya Rufaa na madaktari 18 ni wale walioajiriwa na Wizara ya

Akizungumza na waandishi wa habari, Mwenyekiti wa Bodi Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Norman Sigara, alisema kitendo cha madaktari kutoripoti kazini kwa siku tano ni ukiukwaji wa kanuni za utumisha wa umma toleo la 2009 kifungu namba F.16-F17 na F. 27.

"Hivyo kupitia kanuni hiyo madaktari hao wamesimamishwa kazi na kurudishwa kwa mwajiri wao ambaye ni Katibu Mkuu Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kwa hatua zaidi za kinidhamu,"alisema Sigara.

Kwa mujibu wa Mwenyekiti huyo wa Bodi, imeelezwa kuwa siku ya tarehe 23/6/2012 wafanyakazi 15 waliokuwa zamu(Intern Doctors 12 na Registrars3) hawakufika kazini na tarehe 24/6/2012 wafanyakazi 19(Intern doctors 15 na Registrars 4) hawakufika kazini.

Alisema, kuanzia tarehe 25/6/2012 hadi leo imethibitika kuwa Interns doctor 54 na Registrars 18 hawakufika kazini hadi leo tarehe 28/6/2012 ambapo tarehe 25/6/2012 bodi ya hospitali ilifanya kikao cha dharura kujadili hali ya utendaji kazi na utoaji huduma hospitalini na kutoa uamuzi.

Sigara, aliyataja maamuzi hayo kuwa ni Mwenyekiti wa Bodi akutane na madaktari ambao hawakufika kazini ili awasikilize sababu za kutofika na kujadili namna ya kumaliza matatizo hayo jambo ambalo madaktari hao waligoma.

Alisema, baada ya madaktari hao kukaidi ombi hilo, Bodi ya hospitali ili waandikia barua za kujieleza kwanini wasichukuliwe hatua za kinidhamu kwa kuvunja mkataba walioingia na hospitali na pia kukiuka kanuni za kudumu za utumishi wa umma nalo walilikaidi

"Iwapo madaktari ambao hawakuripoti au kueleza sababu za kuridhisha ifikapo tarehe 28/6/2012. Kwa kuzingatia kanuni za utumishi wa Umma, madaktari hao watasimamishwa kazi na kurudishwa kwa mwajiri wao ambaye ni Katibu Mkuu Wizara ya Afya na Ustawi wa jamii,"alisema.

Aidha, alisema kuwa kwa ujumala madaktari hao waligomea barua zote mbili yaani ya kuitwa kwenye kikao pamoja na ile ya kuwataka kujieleza hivyo Bodi imechukua hatua za kisheria za kuwafukuza kazi.

Hata hivyo Mwenyekiti huyo wa bodi, alisema kuwa tayari hospitali ya Rufaa kwa ushirikiano wa Mkurugenzi wa Jiji la Mbeya, madaktari watano wamepatikana ili kusaidia huduma kwa hospitali hiyo.

CHANZO: http://mbeyayetu.blogspot.com/

HIVI ULISIKIA ALICHOSEMA WAZIRI MKUU JANA BUNGENI? KUHUSU KUJIUZULU NA MGOMO WA MADAKTARI? CHOTE KIKO HAPA..


Jana ndio siku ambayo waziri mkuu Mizengo Pinda aliahidi kutoa jibu la serikali bungeni kuhusu itakachofanya kuhusu mgomo wa Madaktari.

Kuhusu kujiuzulu kutokana na mgomo wa sasa likiwa ni swali kutoka kwa mbunge Tundu Lisu wa Singida Mashariki amesema “yako mazingira unaweza ukawajibika kwa njia hiyo lakini sio lazima yakawa yoote na mimi sioni kama hili ni moja ya maeneo ambayo unaweza ukasema kistahiki hivi unaweza kufikia hatua hiyo, ninachokubali tu ni kwamba tatizo hili ni kweli ni la muda mrefu na nimefanya kila njia kujaribu kulitatua kwa kiasi kikubwa sana, inabidi tukubali kwamba bado lina changamoto nyingi kwa sababu ya mambo mengi tu ambayo yameingiliana na mgogoro wenyewe”

Freeman Mbowe kiongozi wa kambi ya Upinzani bungeni alisimama na kumuuliza Waziri Mkuu kwamba “ulitoa kauli ambayo kama mzazi au kama baba imetia hofu kubwa sana katika taifa pale ulipokua unazungumzia mgomo wa Madaktari na hatimae ukasema na LITAKALOKUWA NA LIWE, vilevile zilipatikana taarifa nyingine kwamba rais wa Madaktari ametekwa juzi usiku, ameteswa, kavunjwa meno, kango’lewa kucha.. unalieleza nini taifa kuhusu kauli yako ya LITAKALOKUA NA LIWE? na serikali inafanya nini cha ziada?

Hili ndio jibu alilotoa Waziri mkuu kwa Freeman Mbowe: “Kwanza nikiri kwamba ni kweli nilitamka hivyo jana lakini kilichokua kinanisumbua kichwani ni kwa sababu nilijua jambo hili liko mbele ya mahakama kuu, kuhusu yaliyompata Dr Ulimboka naonyesha masikitiko yangu juu ya jambo hili na ninamtakia kila la kheri na apone haraka”

Kuhusu alichoahidi kukiongea leo kuhusu Mgomo unaoendelea Waziri Mkuu amesema “tumezungumza na vyombo mbalimbali ili tuone katika mazingira tuliyonayo ni namna gani tutawahudumia wagonjwa, tumewaomba wenzetu wa LUGALO tutumie hospitali ile kuhakikisha wagonjwa hawakosi hiyo huduma, hata hospitali zake nyingine ndogo zote tumeamue tuzitumie kwa njia hiyo, lakini pia tumeona ni vizuri kama kutakua na madaktari wengine waliostaafu na wengine waliopo wizarani pale wote tumeomba sasa watafutiwe njia mbalimbali ili warudi waweze kutoa hiyo huduma kwa Watanzania”

MAGAZETI YA LEO IJUMAA JUNE 29


RIPOTI KAMILI

     Dk Ulimboka akiendelea kupata matibabu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kitengo cha mifupa (MOI)  kwenye chumba cha wagonjwa mahututi (ICU).

   NYUMA ya kipigo alichopewa kiongozi wa madaktari ambao wako kwenye mgomo nchi nzima, Dk. Steven Ulimboka kuna siri nzito, Ijumaa lina ripoti kamili.

  Gazeti hili lilinyetishiwa mkanda mzima na mtu aliyekuwa na Dk. Ulimboka (jina tunalo ambaye naye ni daktari) usiku wa kuamkia Jumatano wiki hii kwenye Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni jijini Dar es Salaam.

   MUVI LA MATESO LAANZA
Jamaa huyo alidai kuwa, wakiwa viwanjani hapo wakipooza koo, walifika watu watano waliojitambulisha kuwa ni askari wakiwa na silaha ambapo walidai kuwa walimfuata Dk. Ulimboka na kumwambia anatakiwa Kituo cha Polisi Kati (Central).

  Ilidaiwa kuwa Dk. Ulimboka alishurutishwa kupanda kwenye gari leusi ambalo halikuwa na namba za usajili na kuondoka eneo hilo huku akiacha gumzo kuwa Central anapelekwa kwa ishu gani.
Ikadaiwa kuwa baada ya Dk. Ulimboka kuchukuliwa, marafiki zake walitoka spidi kuelekea Central kujua kulikoni na pia kumwekea dhamana.

  Jamaa huyo alidai kuwa marafiki zake walipofika Central hawakumkuta na wala hakukuwa na dalili za Dk. Ulimboka kufikishwa mahali hapo.

  Aliendelea kudai kuwa walianza kufanya mawasiliano usiku huo ili kujua rafiki yao alipelekwa wapi lakini jitihada hizo hazikuzaa matunda.

  SIMU HAIPATIKANI
Alidai wakiwa Central, askari mmoja aliwataka kutulia hadi asubuhi wangepata taarifa kamili kwani kwa wakati huo hata simu yake ilikuwa haipatikani.

  Jamaa huyo alidai kuwa saa 12:00 asubuhi alipokea simu kutoka kwa msamaria mwema aliyekuwa maeneo ya Mabwepande nje kidogo ya Jiji la Dar akamwambia kuna mtu amemkuta akiwa taabani ambaye alimtajia namba kwa shida ili aipige na kutoa taarifa ya hali yake.

  “Alisema alimtajia namba tu na hakumsesha tena,” alisema rafiki huyo wa Dk. Ulimboka.
Alidai kuwa baada ya kujulishwa habari hiyo alitaka aende mwenyewe lakini alipoomba ushauri watu walimsihi asiende peke yake.

  Jamaa huyo alisema alitafuta watu akaenda nao na walipofika huko walimkuta Dk. Ulimboka aliyechukuliwa akiwa mzima hajitambui na hakuwa na uwezo wa kuzungumza.

  Alisema kuwa baada ya kumuona mwenzao alivyochakazwa, wakamchukua na kumpeleka kwenye Kituo cha Polisi cha Bunju ambapo yule msamaria mwema alitoa maelezo jinsi alivyomkuta.

  Rafiki huyo wa Dk. Ulimboka alidai kuwa, katika maelezo ya yule msamaria mwema alisema kuwa alishtuka alipomkuta akiwa porini na hali mbaya huku akiwa amefungwa kitambaa cheusi usoni na kutapakaa madonda mabichi mwili mzima.

  Baada ya kuchukuliwa maelezo walipatiwa PF-3 ambapo walifanya jitihada za kumkimbiza katika Hospitali ya Muhimbili kwa kutumia ambulance ya AAR, alipofikishwa tu madaktari wenzake walianza kumpa matibabu ya hali ya juu ili kunusuru uhai wake huku mgomo wao ukiendelea.

 MTU ALA KIPIGO
Wakati anafikishwa Muhimbili tayari wanaharakati mbalimbali walishajitokeza ili kumpokea lakini mara baada ya kufikisha mtu mmoja aliyesadikiwa kuwa ‘njagu’ aliingia chooni na akasikika akizungumza na simu.

Ilidaiwa kuwa katika mazungumzo yake alisikika akisema kumbe jamaa hajafa, jambo lililoibua hisia kwamba alijua kilichoendelea.
Ilisemekana kuwa watu waliomsikia wakamchomoa na kumpa kipigo cha mbwa mwizi hadi Radio Call inayotumiwa na polisi ikamchomoka kwenye suruali kabla ya askari waliokuwa doria kumwokoa na kuondoka naye.

KOVA ATHIBITISHA
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova alithibitisha kutokea kwa tukio hilo linalodaiwa kuwa la utekaji na kuongeza kuwa uchunguzi unafanyika na sheria itachukua mkondo wake dhidi ya wahusika.

Wananchi waishauri serikali
Wakiongea na Ijumaa mara baada ya tukio hilo kutokea, baadhi ya wananchi wameitaka serikali kuhakikisha uchunguzi wa kina na wa haraka unafanyika na ripoti yake kuwekwa hadharani ili kuondoa utata uliotawala.

Imeandaliwa na Haruni Sanchawa, Issa Mnally na Makongoro Oging.

Kikazi Zaidi Jamani

Anatisha Wema Sepetu


Tuesday, June 26, 2012

HII NDIO KAULI YA RAFAEL VAN DER VAART MPAKA SASA.

Rafael van der Vaart amesisitiza kwamba hakuna mawasiliano yoyote yanayofanyika kati yake na club ya Hamburg japo bado kuna fununu kwamba club hiyo ina mpango wa kumpa mkataba mpya.

The Dutch midfielder bado ananyenyekewa na mashabiki kutokana na kazi nzuri aliyoifanya kwa miaka mitatu ambapo kwa mujibu wa skysports, Hamburg-based billionaire Klaus-Michael Kuehne yuko tayari kuisaidia club kumpa gamba jipya Tottenham playmaker Van der Vaart.

KAMA WEWE NI FAN WA ARSENAL HII INAKUHUSU.


Club ya Arsenal imethibitisha kwamba imemdaka na kumpa mkataba striker wa Ufaransa Olivier Giroud.

Giroud mwenye miaka 25 toka aingie kwenye hii dunia amejiunga kutokea Montpellier kwa mkataba mrefu na Arsenal.

Jamaa ameifungia Montpellier magoli 33 kwa miaka miwili aliyoitumikia, kwa timu yake ya taifa ameifungia goli moja toka aanze kuichezea 2011.

OMOTOLA JALADE @GIRAFFE KUZINDUA FILAMU YA SUPERSTAR

 WEMA SEPETU SAMBAMBA NA OMOTOLA JALADE MSANII ALIYEMLETA TOKA NIGERIA KUSHUHUDIA UZINDUZI WA FILAMU YAKE YA SUPERSTAR KATIKA HOTEL YA GIRRAFE JIJINI

DK SLAA AALIKWA KUWA MMOJA WA WANAJOPO WANNE WATAKAOJADILI MADA ISEMAYO “DEMOKRASIA SHINIKIZONI (DEMOCRACY UNDER PRESSURE)” NCHINI UJERUMANI

Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dkt. Willibrod Peter Slaa.

KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dkt. Willibrod Peter Slaa amealikwa kuwa mmoja wa wanajopo (panelists) wanne, kutoka Mabara ya Afrika, Asia, Amerika Kusini na Ulaya, watakaojadili mada isemayo “Demokrasia Shinikizoni (democracy under pressure)” nchini Ujerumani.

Katibu Mkuu Dkt. Slaa ambaye amesafiri jana jioni kuelekea Ujerumani, atakuwa pamoja na wanajopo wenzake wengine ambao ni Prof. Dr. Kyaw Yin Hlaing (Academic Director Myanmar Egress; kutoka Rangum/Myanmar), Dkt. Aliaksandr Milinkiewitsch (Chairman, Movement for Freedom; kutoka Minsk/ Belarus), Gavana Henrique Capriles Radonski (Leader of the Opposition Movement Mesa de la Unidad Democratica; kutoka Carcas/ Venezuela).

Mjadala wa mada hiyo ya Demokrasia Shinikizoni, itakuwa ni sehemu ya sherehe za miaka 50 za Siku ya Shirika la Konrad-Adenauer-Stiftung (KAS Day) katika mahusiano yake ya kimataifa na wadau wake mbalimbali kutoka nchi 80 duniani.

Mwenyekiti wa wanajopo katika kuendesha mjadala huo ni Christoph Lanz (Director of Global Content; Deutsche Welle, Berlin/ Germany)

Sherehe hizo pia zitahudhuriwa na Kansela wa Ujerumani, Dr. Angela Merkel, Rais Mstaafu wa Chile, Seneta Eduardo Frei Ruiz-Tangle na Rais Mstaafu wa Bunge la Ulaya ambaye pia ni Mwenyekiti wa KAS, Dr. Hans-Gert Pottering.

Shirika la KAS linatimiza miaka 50 tangu lilipoanza rasmi kujihusisha na ukuzaji wa demokrasia, uhuru, amani maendeleo na haki. Kwa muda wote huo limekuwa likifanya kazi na wadau katika nchi mbalimbali duniani kutimiza malengo hayo tajwa.

Mpaka sasa KAS ina ofisi 80 sehemu mbalimbali duniani (pamoja na Tanzania), ikishirikiana na wadau wake katika kuendesha miradi inayohusiana na malengo hayo katika nchi 120.
Katika kusherehekea Jubilee ya Miaka 50 ya Siku ya KAS itakayofanyika Juni 27, 2012, shirika hilo limeamua kukutana na wadau na marafiki zake ambao pia wamekuwa wakitoa mchango mkubwa katika utendaji kazi wa KAS katika shughuli za kupigania demokrasia na maendeleo kwa ajili ya manufaa ya wananchi wa nchi husika.

Katika mada ya “Demokrasia Shinikizoni”, wanajopo watajadili changamoto zinazowakabili watetezi wa demokrasia katika tawala mbalimbali zinazotumia njia dhalimu zinazobana upanukaji wa demokakrasia ambayo ni msingi muhimu wa maendeleo ya watu.

Imetolewa Juni 25, 2012, Dar es Salaam na;
Tumaini Makene
Afisa Habari, CHADEMA 

FUMANIZI KATILI

Mwanafunzi, Fikiri Mtasimwa (20) akiwa wodini kwenye Hospitali ya Mkoa wa Geita alikolazwa akitibu majeraha baada ya kukatwa mapanga.
  Kiganja cha Fikiri Mtasimwa kilichokatwa kwa panga.

 Mwanadada Machiwa Ramadhan (21) akiwa amelazwa katika Kituo cha Afya cha Miono baada ya kujeruhiwa katika fumanizi.

WIKI iliyopita watu wa familia mbili tofauti walijikuta wakijiingiza katika matatizo makubwa baada ya kutokea walichodai fumanizi ambapo binti mmoja na mwanaume walijikuta wakijeruhiwa baada ya kukatwa na wanaodai waliowafumania.

Waliopata majeraha ni mvulana wa Geita na msichana wa Miono, Bagamoyo.

BINTI MIAKA 21
Tukio la kwanza lilimpata binti wa miaka 21, Machiwa Ramadhan mkazi wa Kijiji cha Mandela, Wilaya ya Bagamoyo, mkoani Pwani ambaye sasa amelazwa katika Kituo cha Afya cha Miono baada ya kujeruhiwa katika fumanizi.

Vyanzo vyetu vya habari vilidai kwamba mwanadada huyo alijeruhiwa Alhamisi ya wiki iliyopita saa 3.00 usiku kwa baba yake mdogo aliyetambulika kwa jina la Mwinyijuma Paulo baada ya kukutwa na mume wa mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina la mama Hema wakiwa gizani huku wakizungumza kwa sauti za kimahaba.

Habari zaidi zilidai kwamba mwanaume huyo aliyejulikana kwa jina la Walter Emili maarufu kwa jina la Kojoka aliyekutwa na Machiwa, baada ya kufumwa alitimua mbio huku mwanamke huyo akishambuliwa hadi kupasuliwa shavuni na kitu chenye ncha kali na kushonwa nyuzi 12 katika Kituo cha Afya cha Miono.

Taarifa hizo ziliendelea kudai kwamba mke wa Emili alipata taarifa kwa marafiki zake kwamba Machiwa yupo na mumewe hivyo aliwafuma wakiwa pamoja ndipo alipoamua kumpiga mgoni wake.
Mwandishi wa habari hii alienda hadi Kituo cha Afya Miono na kumkuta Machiwa akiwa amelazwa na alipoulizwa kulikoni, alisema kuwa amejeruhiwa na mama Hema.

Machiwa alikataa katakata kwamba alifumaniwa na huyo mwanaume akadai kuwa huyo mwanamke alimvamia njiani wakati akitoka katika biashara zake karibu na nyumbani kwa baba yake mdogo.

“Aliponijeruhi niliamua kwenda kwa dada yangu aitwaye Tatu Ramadhan ambaye alinipeleka kwa mwenyekiti wao wa Kitongoji cha Chemichemi na akatuandikia barua ya kwenda Kituo cha Polisi Wami tulikopata PF 3 kwa ajili ya kutibiwa,” alisema.

Aliendelea kusema kwamba alifika katika Kituo cha Afya Miono akashonwa nyuzi 12 na hadi sasa bado amelazwa.

Kwa upande wake Paulo ambaye ni baba mdogo wa Machiwa alipoulizwa juu ya tukio hilo alisema kwamba yeye ni kipofu bali alikuja kupata taarifa za tukio hilo baadaye.

Mama Hema ambaye ni mtuhumiwa hakupatikana kwa kile kilichoelezwa kuwa bado anashikiliwa na polisi kutokana na hali ya Machiwa kuwa mbaya huku mumewe akiwa hajulikani alipo.

Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Mandela, Andrew Semiono alipoulizwa na gazeti hili kuhusu tukio hilo, alisema uchunguzi unaonesha kuwa fumanizi hilo lina mazingira ya ukweli kutokana na kwamba hata Machiwa alipokuwa anashambuliwa hakupiga kelele kuhitaji msaada.

Naye Afisa Mtendaji wa Kata ya Mandela, Wema Ali Nzenzi alikiri kutokea kwa tukio hilo na kudai kuwa wivu wa kimapenzi umesababisha yote hayo na kwamba mama Hema alikuwa akimtafuta mgoni wake siku nyingi.

“Siku hiyo mama Hema aliposikia kuwa mumewe yupo na Machiwa alichukua tochi na kuwavizia hatimaye kuwafumania na kufanya alichofanya,” alisema Nzenzi.

MWANAUME AKATWA MKONO
Naye Victor Bariety wa Geita anaripoti kuwa mwanafunzi wa kidato cha tatu katika Shule ya Sekondari ya Nyakamwaga wilayani hapa, amenusurika kifo baada ya kudaiwa kufumaniwa na mke wa mtu japokuwa mwenyewe amekanusha.

Kijana huyo alijeruhiwa kwa mapanga sehemu mbalimbali za mwili wake na kukatwa kiganja cha mkono wa kushoto na mwanaume mmoja aliyedai kuwa anatembea na mke wake na siku ya tukio alionekana akiwa na mke wa mwanaume huyo.

Akisimulia mkasa huo akiwa wodini kwenye Hospitali ya Mkoa wa Geita alikolazwa akitibu majeraha, mwanafunzi huyo Fikiri Mtasimwa (20), mkazi wa Kijiji cha Gengetano, Kata ya Nyakamwaga mkoani hapa alidai kuwa alikutwa na balaa hilo usiku wa Juni 17, mwaka huu wakati akinywa uji kwenye kijiwe chao.

Alidai mwanaume huyo anayemfahamu kwa jina la baba Neema alimvamia kwenye kijiwe hicho kinachomilikiwa na binti aliyemtaja kwa jina moja la Mektirida na kuanza kumshambulia kwa mapanga sehemu za kichwani, mgongoni na begani kabla ya kumkata mapanga katika mkono wake wa kushoto na kusababisha kiganja cha mkono huo kunyofoka akimtuhumu kutembea na mkewe aliyemtaja kwa jina la mama Neema.

“Wakati nakunywa uji nilimuona baba Neema akichomoa panga kiunoni mwake na kuanza kunikata kwa kunilenga shingoni, nilikwepa lakini bahati mbaya lilitua kisogoni na kunijeruhi ndipo nilipoamua kukimbia lakini sikufika mbali kwani nilidondoka, akanifuata na kunikata panga jingine la pili kichwani.

“Nilinyanyuka tena na kukimbia huku damu zikivuja...nikadondoka tena, akanikata begani.
“Inavyoonekana alikuwa na lengo la kuniua kwani alianza kunikata mkono wangu wa kushoto mara kadhaa na kiganja changu kikadondoka ndipo rafiki yangu aitwaye Fikiri William ninayesoma naye kidato cha tatu, alipofika kunisaidia na njemba hilo likatoweka na kwenda kusikojulikana nami nikapoteza fahamu,” alisema Mtasimwa.

Alisema alijikuta yupo hospitali akiwa hana kiganja na kufafanua:
“Siku moja kabla ya tukio nilikutana na baba Neema na kumsalimia lakini akaniambia kuwa mimi nina dharau sana wala hahitaji salamu yangu na akanitishia kuwa maisha yangu yapo hatarini, aliondoka bila kunieleza sababu.”

MGANGA MKUU
Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali hiyo, Dk. Ndallo Ndallo alithibitisha kuwepo kwa majeruhi huyo katika hospitali hiyo na kuongeza kuwa hali yake ni mbaya kutokana na majeraha aliyoyapata sehemu mbalimbali za mwili.

KAMANDA WA POLISI
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita Kamishna Msaidizi wa Polisi, Leonard Paulo alithibitisha kuwepo kwa tukio hilo na kuongeza kuwa juhudi za kumsaka mtuhumiwa huyo zinaendelea. Picha Hisani Ya Global Publishers.

Angalia,Tafakari na Toa Maoni Yako