Monday, August 27, 2012

MATOKEO NA WAFUNGAJI WA MECHI ZOTE ZA PREMIER LEAGUE, PRIMERA DIVISION NA BUNDESLIGA AUG 26 2012 CHEK HAPA.





Magazeti ya Leo Jumatatu 27th August 2012



















Morogoro: Viongozi wa CHADEMA wakamatwa na polisi, vurugu zaibuka!

                 Askari waliokuwa katika eneo la tukio kabla ya kuanza kwa maandamano hayo

                     Gari la chadema lililokuwa likiongoza maandamano hayo
                Mmoja wa kiongozi wa chadema akiwa amekamatwa akiwa ndani ya gari la polisi
Wafuasi wa chadema wakiwa na maandamao hayo mjini morogoro

                      Mwanachama wa Chadema Aliyepingwa Risasi Na kupotesa Maisha
            Moshi wa mabomu yaliolipuliwa kutawanya maandamano ya chadema leo mjini morogoro

Habari kutoka Morogoro zimetufikia hivi punde kutoka chanzo cha uhakika nguvu ya umma imeshinda watu wanaendelea na maandamano baada ya Mabomu kushindwa kutawanya watu. Hali ni tete polisi wamelegea mabomu yamewaishia watu wanasonga mbele

Ni kweli. Polisi wamevuruga maandamano yaliyokuwa yafanyike kwenda eneo la mkutano, Uwanja wa Ndege, hapa Morogoro Mjini. Wamedhalilisha viongozi waliowakamata na sasa wameanza kuomba samahani, yaishe.

Kamanda wa Polisi Morogoro, Shilogile (mnaojua alihamishwa Dar es Salaam kuja hapa...) amevunja makubaliano yaliyofanyika mara mbili ya kuruhusu maandamano. Tunajua wapo wanasiasa hapa Morogoro ambao hawataki meseji ifike leo kwa wakazi wa Morogoro Mjini.

Inajulikana namna ambavyo CCM wamekuwa shaken big time na operesheni iliyokuwa na mafanikio huko vijijini, itawaumiza zaidi ikifanikiwa hapa mjini. Kwa hiyo lengo hapa si kuvuruga tu maandamano, bali ni kuvuruga mkutano, ili hatimaye watu waogope kuja mkutanoni, ujumbe usifike. Hawatafanikiwa kwa hilo, maana wananchi sasa wanazidi kujikusanya, maeneo kama ya Masika, kwenda eneo la mikutano, kwa maandamano.

Polisi wanachafua mji sasa, polisi wanawapitisha wana-Morogoro kwenye tanuru ambalo watu wa Mwanza, Mbeya, Arusha, Moshi, Musoma, Tarime, Ruaha na kwingineko kwingi, walipita/kupitishwa ili kuwa hapo walipo wakiwa na imani isiyoyumba katika mapambano haya ya kudai na kuwaandaa Watanzania kwa mabadiliko makubwa ya kimfumo na kiutawala. Chuma hakiwezi kuwa chuma mpaka kipite kwenye tanuru, lakini why doing it unnecessary?

Tutawapatia more updates on the issue?

Sunday, August 26, 2012

BINADAMU WA KWANZA KUFIKA MWEZINI AFARIKI DUNIA AKIWA NA MIAKA 82

                                                                       Neil Amstrong
Buzz Aldrin yeye alikuwa wa pili kukanyaga mwezini nyuma ya Neil japo wote walikuwa katika mission moja hiyo ya Apollo 11.
Neil Amstrong alikanyaga kwa mara ya kwanza mwezini yeye akiwa wa kwanza July 20 1969
Alama hiyo ya mguu inaonyesha jinsi gani mwezini ni kama ardhi  laini sana kama poda hivi.
Mission hiyo ya Apollo 11 ilifanyika mwaka 1969 na yeye akiwa kiongozi wa msafara wa watu watatu kuelekea mwezini.
Neil Amstrong kushoto na mwenzake Buzz Aldrin kushoto wakiwa tayari mwezini na kuweka bendera ya Marekani.Walikaa mwezini kwa masaa matatu tu.
 Ilikuwa  july 6 1969 wakijiandaa kuondoka huku wakipunga kuaga na yeye mbele kabisa kuingia kwenye van iliyowapeleka kwenye rocket tayari kuanza safari kuelekea mwezini.
Neil Amstrong amefariki dunia baada ya kutokea complications akifanyiwa oparation ya moyo .Neil Amstrong amefariki akiwa na miaka 82.Dunia itamkumbika kwa rekodi yake ya kihistoria ya kuwa binadamu wa kwanza kuingia na kukanyaga mwezini.
                                                       Akiwa na Presedent Obama 2009.

Matukio ya CHADEMA-M4C Houston







                                                          Mh. Mbowe akiwasili
                                                            Wadau waliohudhuria
                                                                 Wadau wakipata picha