Wanajeshi saba wamarekani wa kitengo cha Elite akiwemo mmoja wa maafisa wa jeshi aliyehusika na kumkamata na kumuua Osama bin Laden wameadhibiwa kwa madai ya kutoa taarifa za siri za marekani kinyume na sheria.
Kuvunjwa kwa usalama huo kunadaiwa kujiri wakati wanajeshi hao walikuwa wakifanya kazi ya kutoa huduma za ushauri katika kutengeneza mchezo wa video inayoonyesha makabiliano ya kijeshi.
Saba hao walipata barua za nidhamu na kupokea nusu ya mishahara yao kwa kipindi cha miezi miwili .
Idara ya usalama ya marekani bado inachunguza iwapo maafisa zaidi wa kitengo cha Seal walihusika
Chanzo: http://www.bbc.co.uk/swahili/news
Saturday, November 10, 2012
Dk. Shein Afanya Mazungumzo Na Balozi Mdogo Wa India Zanzibar
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein akizungumza na Balozi Mdogo wa India wa Zanzibar, Pawan Kumar alipofika Ikulu Mjini Zanzibar Kujitambulisha kwa Rais.
[Picha na Ramadhan Othman Ikulu]
Hoja Ya Mdee ‘Kaa La Moto’ Kwa Serikali
MBUNGE wa Kawe, Halima Mdee amewasilisha hoja binafsi bungeni akiitaka Serikali kusitisha ugawaji wa ardhi hadi tathmini ifanyike, huku akimtuhumu Waziri Mkuu kuwa anashiriki katika kuwakumbatia wawekezaji wanaopora ardhi wananchi.
Mdee amesema kuwa bila kufanya hivyo, ardhi yote ya nchi hii itachukuliwa na wawekezaji huku wananchi wakiachwa masikini.
Akiwasilisha bungeni hoja binafsi kuhusu kusitishwa ugawaji ardhi nchini, Mdee aliitaka Serikali kusitisha ugawaji wa ardhi hadi hapo tathmini ya kina itakapofanyika kujua kiasi cha ardhi kilichopo mikononi mwa wawekezaji.
Vile vile, alitaka tathmini ya kina ifanyike kubaini raia wa kigeni na wa ndani waliojipatia ardhi kinyemela kupitia Serikali za vijiji kinyume na matakwa ya sheria ya ardhi namba 5 ya mwaka 1999.
“Kwa mujibu wa Kanuni namba 54(1), (2) na (3) ya Kanuni za Kudumu za Bunge, Toleo la 2007 naomba kutoa hoja binafsi ya kuitaka Serikali kusitisha ugawaji wa ardhi kwa wawekezaji wa ndani na wa nje mpaka hapo tathmini ya kina itakapofanyika kubaini ni kiwango gani cha ardhi kiko mikononi mwa wawekezaji,” alisema Mdee.
Alisema katika miaka ya hivi karibuni, kutokana mtikisiko wa uchumi duniani, tumeshuhudia wimbi la wawekezaji kutoka nje wakingia nchini kuwekeza katika kilimo kwa maelezo kwamba watasaidia kuinua uzalishaji katika sekta ya kilimo.
Hata hivyo, alisema uwekezaji huo wa wageni katika ardhi umegeuka kuwa shubiri kwa wananchi hususan wakulima wadogo.
Alisema wakulima hao wamekuwa wakiondolewa katika maeneo yao ya asili ili kuwapisha wageni huku wakiachwa katika lindi la umasikini mkubwa.
Mdee alisema ardhi hiyo imekuwa ikichukuliwa na Serikali kuwa haina mwenyewe au haitumiki.
“Hii inatokana na ukweli kwamba kumekuwa na tafsiri ambayo sio sahihi, kwamba ardhi wanayopewa wawekezaji haina wenyewe, haina mtu, haitumiki. Wakati ukweli ni kwamba maeneo mengi kama sio yote yalikuwa yanatumiwa na wakulima wadogo,” alisema.
Mdee alisema wawekezaji wamechukua maeneo makubwa ambayo wameshindwa kuyaendeleza na hata yale ambayo wanayaendeleza ni kwa kiasi kidogo.
Alisema baadhi ya waewekezaji wengine baada ya kumilikishwa ardhi kwa bei ya kutupa wamekuwa wakikaa nayo na baadaye kuiza kwa wawekezaji wengine.
Mdee aliliomba Bunge kukubali Serikali kusitisha ugawaji wa ardhi ili kuangalia wapi ilipokosea kwa manufaa ya nchi.
Mbunge huyo kupitia Chadema, alisema hata wizara ya ardhi na maendeleo ya makazi wakitakiwa leo kutoa taarifa sahihi ya ardhi kiasi gani iko chini ya miliki ya wageni hawana taarifa hizo.
Alisema kutokana na waewekezaji kupewa ardhi bila ya kufuata taratibu, hivi sasa migogoro mingi ya ardhi iliyopo nchini inatokana na wananchi kuporwa ardhi kwa kisingizio cha uwekezaji.
Alitoa mfano wa Kampuni ya Kigoma inayofahamika kama Agrisol na FELISA ambayo imenunua hekari 3,000 katika Kijiji cha Basanza Kata ya Uvinza wilayani ya Uvinza.
Alisema wawekezaji hao ambao wanakingiwa kifua na Waziri Mkuu, wamewakuta wakulima na wafugaji katika maeneo haya.
Alisema mwekezaji kwa kushirikiana na vyombo vya dola aliwatoa kwa nguvu wananchi akitumia askari mgambo kupiga wananchi, kuchoma nyumba, kuharibu mazao na halikadhalika kuwafungulia wananchi mashtaka.
Alitaja maeneo mengine yenye migogoro kuwa ni wananchi na wawekezaji kuwa ni Rufiji, Kilombero, Bagamoyo, Kisarawe, Muheza, Pangani, Katavi ,Meatu, Kinondoni, Njombe na Ngorogoro.
Moto wa hoja hiyo uliwafanya baadhi ya mawaziri kuinuka kuchangia akiwamo, Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi, Profesa Tibaijuka, Waziri Nchi ofisi ya Waziri Mkuu, (Uwekezaji na Uwezeshaji), Mary Nagu na Waziri wa Nchi ofisi ya Rais (Mahusiano), Steven Wassira.
Akichangia hoja hiyo, Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi, Profesa Tibaijuka alikubali kufanya marekebisho katika sheria ya ardhi ili iweze kuwanifaisha watanzania.
Alisema hakubaliani na hoja ya Mbunge Mdee ya kutaka kusitisha utoaji wa ardhi kwa wawekezaji akisema hali hiyo inaweza kuleta matatizo zaidi.
Profesa Tibaijuka alisema ni aibu kwa nchi yenye ardhi kubwa na yenye rutuba kushindwa kujitosheleza kwa chakula.
Hivyo, alisema kuwapa wageni wenye mitaji ardhi kwa ajili ya kilimo kutasaidia kuongezeka kwa uzalishaji wa mazao na hivyo kujitosheleza kwa chakula.
Profesa Tibaijuka alisema ili watanzania waweze kunufaika na uwekezaji mkubwa wa ardhi nchini, Serikali itakuwa inachukua hisa katika mshamaba hayo na kuziuza kwa wananachi.
“Serikali hii haiwezi kukukbali wananchi wake kuporwa ardhi na wawekezaji,” alisema.
Alisema anakubalina kufanyiwa marekebisho sheria hiyo ili iweze kumsiadia mwananchi.
Waziri Nagu, alisema hatuwezi kusitisha uwekezaji kwa wageni kwa sababu itasabisha kurudisha nyuma maendeleo katika sekta ya kilimo.
Chanzo: http://www.mwananchi.co.tz/habari/siasa
Mdee amesema kuwa bila kufanya hivyo, ardhi yote ya nchi hii itachukuliwa na wawekezaji huku wananchi wakiachwa masikini.
Akiwasilisha bungeni hoja binafsi kuhusu kusitishwa ugawaji ardhi nchini, Mdee aliitaka Serikali kusitisha ugawaji wa ardhi hadi hapo tathmini ya kina itakapofanyika kujua kiasi cha ardhi kilichopo mikononi mwa wawekezaji.
Vile vile, alitaka tathmini ya kina ifanyike kubaini raia wa kigeni na wa ndani waliojipatia ardhi kinyemela kupitia Serikali za vijiji kinyume na matakwa ya sheria ya ardhi namba 5 ya mwaka 1999.
“Kwa mujibu wa Kanuni namba 54(1), (2) na (3) ya Kanuni za Kudumu za Bunge, Toleo la 2007 naomba kutoa hoja binafsi ya kuitaka Serikali kusitisha ugawaji wa ardhi kwa wawekezaji wa ndani na wa nje mpaka hapo tathmini ya kina itakapofanyika kubaini ni kiwango gani cha ardhi kiko mikononi mwa wawekezaji,” alisema Mdee.
Alisema katika miaka ya hivi karibuni, kutokana mtikisiko wa uchumi duniani, tumeshuhudia wimbi la wawekezaji kutoka nje wakingia nchini kuwekeza katika kilimo kwa maelezo kwamba watasaidia kuinua uzalishaji katika sekta ya kilimo.
Hata hivyo, alisema uwekezaji huo wa wageni katika ardhi umegeuka kuwa shubiri kwa wananchi hususan wakulima wadogo.
Alisema wakulima hao wamekuwa wakiondolewa katika maeneo yao ya asili ili kuwapisha wageni huku wakiachwa katika lindi la umasikini mkubwa.
Mdee alisema ardhi hiyo imekuwa ikichukuliwa na Serikali kuwa haina mwenyewe au haitumiki.
“Hii inatokana na ukweli kwamba kumekuwa na tafsiri ambayo sio sahihi, kwamba ardhi wanayopewa wawekezaji haina wenyewe, haina mtu, haitumiki. Wakati ukweli ni kwamba maeneo mengi kama sio yote yalikuwa yanatumiwa na wakulima wadogo,” alisema.
Mdee alisema wawekezaji wamechukua maeneo makubwa ambayo wameshindwa kuyaendeleza na hata yale ambayo wanayaendeleza ni kwa kiasi kidogo.
Alisema baadhi ya waewekezaji wengine baada ya kumilikishwa ardhi kwa bei ya kutupa wamekuwa wakikaa nayo na baadaye kuiza kwa wawekezaji wengine.
Mdee aliliomba Bunge kukubali Serikali kusitisha ugawaji wa ardhi ili kuangalia wapi ilipokosea kwa manufaa ya nchi.
Mbunge huyo kupitia Chadema, alisema hata wizara ya ardhi na maendeleo ya makazi wakitakiwa leo kutoa taarifa sahihi ya ardhi kiasi gani iko chini ya miliki ya wageni hawana taarifa hizo.
Alisema kutokana na waewekezaji kupewa ardhi bila ya kufuata taratibu, hivi sasa migogoro mingi ya ardhi iliyopo nchini inatokana na wananchi kuporwa ardhi kwa kisingizio cha uwekezaji.
Alitoa mfano wa Kampuni ya Kigoma inayofahamika kama Agrisol na FELISA ambayo imenunua hekari 3,000 katika Kijiji cha Basanza Kata ya Uvinza wilayani ya Uvinza.
Alisema wawekezaji hao ambao wanakingiwa kifua na Waziri Mkuu, wamewakuta wakulima na wafugaji katika maeneo haya.
Alisema mwekezaji kwa kushirikiana na vyombo vya dola aliwatoa kwa nguvu wananchi akitumia askari mgambo kupiga wananchi, kuchoma nyumba, kuharibu mazao na halikadhalika kuwafungulia wananchi mashtaka.
Alitaja maeneo mengine yenye migogoro kuwa ni wananchi na wawekezaji kuwa ni Rufiji, Kilombero, Bagamoyo, Kisarawe, Muheza, Pangani, Katavi ,Meatu, Kinondoni, Njombe na Ngorogoro.
Moto wa hoja hiyo uliwafanya baadhi ya mawaziri kuinuka kuchangia akiwamo, Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi, Profesa Tibaijuka, Waziri Nchi ofisi ya Waziri Mkuu, (Uwekezaji na Uwezeshaji), Mary Nagu na Waziri wa Nchi ofisi ya Rais (Mahusiano), Steven Wassira.
Akichangia hoja hiyo, Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi, Profesa Tibaijuka alikubali kufanya marekebisho katika sheria ya ardhi ili iweze kuwanifaisha watanzania.
Alisema hakubaliani na hoja ya Mbunge Mdee ya kutaka kusitisha utoaji wa ardhi kwa wawekezaji akisema hali hiyo inaweza kuleta matatizo zaidi.
Profesa Tibaijuka alisema ni aibu kwa nchi yenye ardhi kubwa na yenye rutuba kushindwa kujitosheleza kwa chakula.
Hivyo, alisema kuwapa wageni wenye mitaji ardhi kwa ajili ya kilimo kutasaidia kuongezeka kwa uzalishaji wa mazao na hivyo kujitosheleza kwa chakula.
Profesa Tibaijuka alisema ili watanzania waweze kunufaika na uwekezaji mkubwa wa ardhi nchini, Serikali itakuwa inachukua hisa katika mshamaba hayo na kuziuza kwa wananachi.
“Serikali hii haiwezi kukukbali wananchi wake kuporwa ardhi na wawekezaji,” alisema.
Alisema anakubalina kufanyiwa marekebisho sheria hiyo ili iweze kumsiadia mwananchi.
Waziri Nagu, alisema hatuwezi kusitisha uwekezaji kwa wageni kwa sababu itasabisha kurudisha nyuma maendeleo katika sekta ya kilimo.
Chanzo: http://www.mwananchi.co.tz/habari/siasa
Friday, November 9, 2012
Dk Mwinyi Atembelea Vituo Vya Uchunguzi Na Matibabu Vinavyojengwa Mkoani Dodoma
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Hussein Mwinyi akiwasili katika eneo la Ujenzi wa kituo cha kisasa cha Matibabu mkoani Dodoma.
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Hussein Mwinyi (kulia) akizungumza kabla ya kukagua ujenzi wa Kituo cha Kisasa cha uchunguzi na Matibabu katika Chuo Kikuu cha Dodoma kinachonjengwa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya.
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Hussein Mwinyi (kushoto) akiwa na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, Dk. Emmanuel Humba baada ya kukagua ujenzi wa Kituo cha Mfano cha Uchunguzi na Matibabu katika Hospitali ya Mkoa wa Dodoma kinachojengwa na Mfuko huo.
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Hussein Mwinyi (kulia) akizungumza kabla ya kukagua ujenzi wa Kituo cha Kisasa cha uchunguzi na Matibabu katika Chuo Kikuu cha Dodoma kinachonjengwa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya.
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Hussein Mwinyi (kushoto) akiwa na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, Dk. Emmanuel Humba baada ya kukagua ujenzi wa Kituo cha Mfano cha Uchunguzi na Matibabu katika Hospitali ya Mkoa wa Dodoma kinachojengwa na Mfuko huo.
TAARIFA KWA UMMAUzinduzi Wa Shindano La Kusaka Mabingwa Wa Kero Kwa Wateja
Uzinduzi wa Shindano la Kusaka Mabingwa wa Kero kwa Wateja
Jumuiya ya watumiaji wa huduma mbalimbali nchini kupitia mitandao ya kijamii ya Facebook na Twitter imezindua rasmi shindano la kusaka kampuni zinazotoa huduma na bidhaa mbovu kwa wateja nchini Tanzania.
Jumuiya hiyo inawajumuisha watu wa kada mbalimbali wakiwemo wanasheria, wanaharakati, waandishi wa habari, viongozi wa kisiasa, wafanyabiashara na wateja wa huduma na bidhaa mbalimbali nchini Tanzania.
Lengo la jumuiya hiyo ni kushinikiza wafanyabiashara nchini kutoa huduma na bidhaa bora kwa wateja na kuwakumbusha umuhimu wa wateja. Kauli mbiu ya wanajumuiya hao ni Mteja ni Mfalme.
Katika wiki ya kwanza tangu jumuiya hiyo kuzinduliwa jumla ya makampuni 21 yameingizwa katika shindano hilo kwa wateja wao kuwasilisha malalamiko yao. Kwa taarifa zaidi kuhusu ni fuatilia akaunti ya Twitter @hudumambayatz au kundi la Facebook linalojulikana kama HUDUMA BONGO.
Ili kuweza kupiga kura yako unahitajika kuwa na akaunti hai (yenye mawasiliano mara kwa mara) katika mtandao wa Twitter au Facebook na kujiunga na jumuiya hiyo. Mara tu utakapowasilisha kero yako utaifanya kampuni unayoilalamikia kuingia katika mchuano mkali wa kumsaka bingwa wa huduma mbovu kwa wateja nchini.
Huduma Bongo inatoa wito kwa makampuni yote kuboresha huduma na bidhaa zao ili kuweza kuwapatia wateja kilicho bora zaidi katika soko hili la ushindani.
Imetolewa na Mshauri wa Habari wa Huduma Bongo - hudumabongo@gmail.com
Novemba 9, 2012
Jumuiya ya watumiaji wa huduma mbalimbali nchini kupitia mitandao ya kijamii ya Facebook na Twitter imezindua rasmi shindano la kusaka kampuni zinazotoa huduma na bidhaa mbovu kwa wateja nchini Tanzania.
Jumuiya hiyo inawajumuisha watu wa kada mbalimbali wakiwemo wanasheria, wanaharakati, waandishi wa habari, viongozi wa kisiasa, wafanyabiashara na wateja wa huduma na bidhaa mbalimbali nchini Tanzania.
Lengo la jumuiya hiyo ni kushinikiza wafanyabiashara nchini kutoa huduma na bidhaa bora kwa wateja na kuwakumbusha umuhimu wa wateja. Kauli mbiu ya wanajumuiya hao ni Mteja ni Mfalme.
Katika wiki ya kwanza tangu jumuiya hiyo kuzinduliwa jumla ya makampuni 21 yameingizwa katika shindano hilo kwa wateja wao kuwasilisha malalamiko yao. Kwa taarifa zaidi kuhusu ni fuatilia akaunti ya Twitter @hudumambayatz au kundi la Facebook linalojulikana kama HUDUMA BONGO.
Ili kuweza kupiga kura yako unahitajika kuwa na akaunti hai (yenye mawasiliano mara kwa mara) katika mtandao wa Twitter au Facebook na kujiunga na jumuiya hiyo. Mara tu utakapowasilisha kero yako utaifanya kampuni unayoilalamikia kuingia katika mchuano mkali wa kumsaka bingwa wa huduma mbovu kwa wateja nchini.
Huduma Bongo inatoa wito kwa makampuni yote kuboresha huduma na bidhaa zao ili kuweza kuwapatia wateja kilicho bora zaidi katika soko hili la ushindani.
Imetolewa na Mshauri wa Habari wa Huduma Bongo - hudumabongo@gmail.com
Novemba 9, 2012
Akamatwa Na Sehemu Za Siri Za Mpwa Wake A. Kusini
Mwanamume mmoja nchini Afrika Kusini amekamatwa baada ya kupatikana akiwa na sehemu za siri kwenye pochi lake ambazo zinaaminika kuwa za mpwa wake ambaye hajulikani aliko.
Msemaji wa polisi, aliambia BBC kuwa babada ya kukamatwa kwake , mwanaume huyo aliwapeleka maafisa wa polisi kwenye msitu katika mkoa wa Eastern Cape, ambako mwili uliokatwakatwa ulipatikana.
Kichwa cha msichana huyo pamoja na miguu yake ilikuwa imekatwa na zilipatikana karibu na kiwiliwili chake. Mtu huyo mwenye umri wa miaka 42, anatarajiwa kufikishwa mahakamani kwa kosa la mauaji.
Mmwanaume huyo alishtakiwa baada ya kushukiwa kuhusika na kutoweka kwa msichana huyo mwenye umri wa miaka 18, aliyepotoea katika mji wa Ngcobo siku ya Jumapili.
Msemaji wa polisi, Mzukisi Fatyela alisema kuwa sehemu hizo za siri, zilipatikana ndani ya pochi lake. Alisema sababu ya kuuawa kwa msichana huyo haijulikani na kwamba uchunguzi unafanyika.
Alipoulizwa ikiwa mauaji hayo yanahusishwa na waganga ambapo sehemu za mwili wa watu hutumiwa kwenye madawa yao, bwana Fatyela alisema kuwa hawezi kubaini hilo kwa sasa. Kumekuwa na visa vingi vya kuuza sehemu za siri za watu katika sehemu nyingi za Afrika kwa sababu sawa na hizo.
Afrika Mashariki imeshuhudia visa vingi vya kuuawa kwa watu wenye ulemavu wa ngozi au maalbino, huku sehemu za miili yao zikikatwa kwa sababu za kishirikina. Mwanaume huyo anatarajiwa kufikishwa mahakamani leo.
BBC-SWAHILI
Msemaji wa polisi, aliambia BBC kuwa babada ya kukamatwa kwake , mwanaume huyo aliwapeleka maafisa wa polisi kwenye msitu katika mkoa wa Eastern Cape, ambako mwili uliokatwakatwa ulipatikana.
Kichwa cha msichana huyo pamoja na miguu yake ilikuwa imekatwa na zilipatikana karibu na kiwiliwili chake. Mtu huyo mwenye umri wa miaka 42, anatarajiwa kufikishwa mahakamani kwa kosa la mauaji.
Mmwanaume huyo alishtakiwa baada ya kushukiwa kuhusika na kutoweka kwa msichana huyo mwenye umri wa miaka 18, aliyepotoea katika mji wa Ngcobo siku ya Jumapili.
Msemaji wa polisi, Mzukisi Fatyela alisema kuwa sehemu hizo za siri, zilipatikana ndani ya pochi lake. Alisema sababu ya kuuawa kwa msichana huyo haijulikani na kwamba uchunguzi unafanyika.
Alipoulizwa ikiwa mauaji hayo yanahusishwa na waganga ambapo sehemu za mwili wa watu hutumiwa kwenye madawa yao, bwana Fatyela alisema kuwa hawezi kubaini hilo kwa sasa. Kumekuwa na visa vingi vya kuuza sehemu za siri za watu katika sehemu nyingi za Afrika kwa sababu sawa na hizo.
Afrika Mashariki imeshuhudia visa vingi vya kuuawa kwa watu wenye ulemavu wa ngozi au maalbino, huku sehemu za miili yao zikikatwa kwa sababu za kishirikina. Mwanaume huyo anatarajiwa kufikishwa mahakamani leo.
BBC-SWAHILI
Uongozi Wa Sauti Za Busara Wakana Kumdhulumu Bi Kidude
Mkurugenzi wa Sauti za Busara ZanzibarYussuf Mahmoud amesema kutokana na malalamiko yanayotolewa na familia ya Bi Fatma Baraka Khamisi (Bi Kidude) wameamua kuzikabidhi fedha za msanii huyo mkongwe alizokuwa akizihifadhi ili kuepusha migogoro zaidi.
Ameyasema hayo katika Ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo huko Kikwajuni wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kufuatia malamiko ya baadhi ya wanafamilia wa Bi Kidude wanaodai kwamba mzazi wao anaibiwa fedha zake na viongozi wa Sauti za Busara.
Mkurugenzi huyo amesema lengo la Sauti za Busara ni kuwasaidia wasanii wa Zanzibar na Afrika kwa jumla katika kuwatangaza na kuwatafutia maslahi ndani na nje ya nchi na sio kuwadhulumu kipato chao.
Amesema baada ya juhudi kubwa walizofanya kuanzia mwaka 2005 walipoanza kumsaidia Bi Kidude ikiwa ni pamoja na kumuwezesha kupata tunzo ya Womex, wamefanikiwa kukusanya shilingi milioni 36 zilizotokana na maonyesho mbali mbali yaliyosimamiwa na Sauti za busara, mauzo ya CD na mahojiano aliyofanya na vyombo vya Habari.
Ameongeza kuwa fedha hizo amekuwa akizutumia mwenyewe, kusimamia kuitengeneza nyumba yake na wamekuwa wakizitumia kwa matibabu yake anapoumwa na hivi sasa fedha zilizobakia ni shilling Millioni tatu laki sita na elfu nne (3,604,000) ambazo zimo mikononi mwake na hivyo alitaka fedha hizo azikabidhi kwa mtu wa familia ambae Bi Kidude ataridhia mwenyewe.
Hata hivyo shughuli ya kukabidhi fedha hizo kwa wanafamilia ilishindikana kutokana na wanafamilia kukataa kuhudhuria katika kikao hicho cha leo.
Mkuu wa miradi wa Sauti za Busara Janny Ramadhani amedai kuwa chanzo cha mzozo ni pale Bi Kidude alipomtambulisha mwanafamilia Baraka Abdalla kuwa ndie atakuwa dhamana wa kumchukulia fedha za kila wiki shilingi 50,000 ambazo walikubaliana lakini baadhi ya wiki kijana huyo alikuwa hazipeleki kwa Bi Kidude.
Amesema familia ya Bi Kidude imechangia kwa kiasi kikubwa katika kumuangusha mzazi wao licha ya juhudi walizokuwa wakizichukua katika kumtangaza na kumpatia safari za mara kwa mara nje na ndani ya nchi.
Viongozi hao wa Sauti za Busra wamewataka wasanii wote nchini wawe pamoja na kujenga moyo wa kushirikiana na kusaidiana ili waweze kukuza vipaji vyao na kuinua sanaa zao na kufikia maendeleo waliyokusudia.
Na: Ramadhan Ali na Mwanaisha Mohamed-Maelezo Zanzibar 09/11/2012
IMETOLEWA NA IDARA YA HABARI MAELEZO ZANZIBAR 9/11/2011
Ameyasema hayo katika Ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo huko Kikwajuni wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kufuatia malamiko ya baadhi ya wanafamilia wa Bi Kidude wanaodai kwamba mzazi wao anaibiwa fedha zake na viongozi wa Sauti za Busara.
Mkurugenzi huyo amesema lengo la Sauti za Busara ni kuwasaidia wasanii wa Zanzibar na Afrika kwa jumla katika kuwatangaza na kuwatafutia maslahi ndani na nje ya nchi na sio kuwadhulumu kipato chao.
Amesema baada ya juhudi kubwa walizofanya kuanzia mwaka 2005 walipoanza kumsaidia Bi Kidude ikiwa ni pamoja na kumuwezesha kupata tunzo ya Womex, wamefanikiwa kukusanya shilingi milioni 36 zilizotokana na maonyesho mbali mbali yaliyosimamiwa na Sauti za busara, mauzo ya CD na mahojiano aliyofanya na vyombo vya Habari.
Ameongeza kuwa fedha hizo amekuwa akizutumia mwenyewe, kusimamia kuitengeneza nyumba yake na wamekuwa wakizitumia kwa matibabu yake anapoumwa na hivi sasa fedha zilizobakia ni shilling Millioni tatu laki sita na elfu nne (3,604,000) ambazo zimo mikononi mwake na hivyo alitaka fedha hizo azikabidhi kwa mtu wa familia ambae Bi Kidude ataridhia mwenyewe.
Hata hivyo shughuli ya kukabidhi fedha hizo kwa wanafamilia ilishindikana kutokana na wanafamilia kukataa kuhudhuria katika kikao hicho cha leo.
Mkuu wa miradi wa Sauti za Busara Janny Ramadhani amedai kuwa chanzo cha mzozo ni pale Bi Kidude alipomtambulisha mwanafamilia Baraka Abdalla kuwa ndie atakuwa dhamana wa kumchukulia fedha za kila wiki shilingi 50,000 ambazo walikubaliana lakini baadhi ya wiki kijana huyo alikuwa hazipeleki kwa Bi Kidude.
Amesema familia ya Bi Kidude imechangia kwa kiasi kikubwa katika kumuangusha mzazi wao licha ya juhudi walizokuwa wakizichukua katika kumtangaza na kumpatia safari za mara kwa mara nje na ndani ya nchi.
Viongozi hao wa Sauti za Busra wamewataka wasanii wote nchini wawe pamoja na kujenga moyo wa kushirikiana na kusaidiana ili waweze kukuza vipaji vyao na kuinua sanaa zao na kufikia maendeleo waliyokusudia.
Na: Ramadhan Ali na Mwanaisha Mohamed-Maelezo Zanzibar 09/11/2012
IMETOLEWA NA IDARA YA HABARI MAELEZO ZANZIBAR 9/11/2011
Taarifa Kwa Vyombo Vya Habari...!
SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania limeteua wadau 10 kwa ajili ya kusaidia timu ya taifa ya vijana walio na umri chini ya miaka 17, Serengeti Boys itakayopambana na Congo (Brazaville) katika mechi ya raundi ya tatu ya michuano ya awali ya Mataifa ya Afrika.Uteuzi huo umefanywa na Rais wa TFF, Leodegar Tenga baada ya Kamati ya Vijana ya TFF kufanya kikao chake kujadili kwa umakini ushiriki wa timu hiyo na kupeleka mapendekezo yake kwa rais huyo wa shirikisho.
Kutokana na umuhimu wa mechi hiyo itakayoamua timu itakayofuzu kucheza fainali za Mataifa ya Afrika, TFF imeona umuhimu wa kuwa na kamati ambayo itakuwa na majukumu mawili makubwa ambayo ni:
1. Kuhamasisha vijana waone umuhimu na kuwa na ari ya kushinda mechi hiyo
2. Kuhamasisha umma uone umuhimu wa mechi hiyo na hivyo kuisaidia iweze kufuzu.
Walioteuliwa kuunda kamati hiyo ni:
1. Ridhiwani Kikwete Mwenyekiti
2. Ahmed Seif (Magari) Mjumbe
3. Nassoro Bin Slum Mjumbe
4. Henry Tandau Katibu
5. Ahmed Mgoyi Mjumbe
6. Aboubakar Bakhresa Mjumbe
7. Angetile Osiah Mjumbe
8. Kassim Dewji Mjumbe
9. Abdallah Bin Kleb Mjumbe
10. Salim Said Mjumbe
Baada ya kuvuka raundi mbili za kwanza bila ya kucheza mechi kutokana na wapinzani wake kujitoa, timu ya Serengeti Boys inahitaji kufanya kila iwezalo kuweza kuiondoa Congo kwenye mashindano hayo na kuweka rekodi ya kufuzu kucheza fainali hizo za Afrika ambazo pia zitatoa wawakilishi wa Afrika kwenye mashindano ya Kombe la Dunia.
Mechi za kwanza za raundi ya tatu zitachezwa kati ya Novemba 16 na 18, 2012 na mechi za marudiano zitachezwa kuanzia Novemba 30, 2012 hadi Desemba 2, 2012
*Kuhusu suala la Azam FC kuwasimamisha wachezaji watatu kwa tuhuma za kuhusika kuhujumu timu, tayari TFF imepokea barua hiyo ya Novemba 8, 2012 na inalishughulikia na kulifuatilia kwa makini.
*TFF inapenda kukipongeza Chama cha Mpira wa Miguu cha Mkoa wa Mwanza kwa kufanya uchaguzi wake kwa amani na kufanikiwa kupata viongozi wapya watakaokuwa chini ya uenyekiti wa Jackson Songora.
Rais wa TFF amewapongeza viongozi waliorekjea madarakani na viongozi wapya akieleza magtumaini yake kuwa kamati mpya ya Utendaji ya MRFA itaelekeza nguvu zake katika kuendeleza mikakati iliyokuwepo ya kuinua kiwango cha mpira wa miguu na kubuni mikakati mingine kwenye mkoa huo na Tanzania kwa ujumla ikishirikiana na TFF.
*Ligi Kuu ya Vodacom inatazamiwa kuendelea kesho kwenye viwanja tofauti
1. Simba v Toto Africans Uwanja wa Taifa
2. T. Prisons v JKT Ruvu Sokoine
3. Kagera Sugar v Polisi Moro Kaitaba
4. African Lyon v Mtibwa Sugar Azam Complex
5. Oljoro JKT v Ruvu Shooting Sheikh Amri Abeid
6. Mgambo JKT v Azam FC Mkwakwani
Jumapili
1. Coastal Union v Young Africans Mkwakwani
Subscribe to:
Posts (Atom)
























.jpg)




















