Tuesday, December 4, 2012
STORI KUHUSU USHINDI WA KILI STARS DEC 3 2012.
Tanzania Bara (Kilimanjaro Stars) itacheza nusu fainali ya michuano ya Kombe la Chalenji 2012 Alhamisi (Desemba 6 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Mandela ulioko Namboole jijini Kampala, Uganda.
Kilimanjaro Stars ambayo itacheza mechi hiyo na mshindi wa robo fainali ya Desemba 4 kati ya wenyeji Uganda na Ethiopia imeingia hatua hiyo baada ya kuitoa Rwanda Desemba 3 2012.
Mabao ya Amri Kiemba dakika ya 33 na John Bocco dakika ya 53 ndiyo yaliyoifanya Kilimanjaro Stars itinge nusu fainali na kuifungisha virago Rwanda (Amavubi) inayofundishwa na Milutin ‘Micho’ Sredojovic kutoka Serbia.
Vijana wa Kilimanjaro Stars wanaonolewa na Kim Poulsen walitawala pambano hilo, hasa kipindi cha kwanza kwa pasi fupi fupi. Kilimanjaro Stars imefungwa bao moja katika mechi nne ilizocheza tangu michuano hiyo ilipoanza Novemba 24 mwaka huu jijini Kampala.
Kilimanjaro Stars ambayo katika michuano hiyo iliyofanyika Dar es Salaam mwaka jana iliishia hatua ya nusu fainali iliwakilishwa na; Juma Kaseja, Erasto Nyoni, Amir Maftah, Shomari Kapombe, Kelvin Yondani, Amri Kiemba, Salum Abubakar/Athuman Idd, Frank Domayo, Mwinyi Kazimoto, John Bocco na Mrisho Ngasa.
Kwenye line nyingine mwandishi Shaffih Dauda ameandika kuhusu Michuano ya kombe la Uhai kuanza disemba 7 2012 ni kwamba michuano hiyo inayoshirikisha timu za U20 za klabu za Ligi Kuu ya Vodacom inatarajiwa kumalizika Desemba 22 mwaka huu.
Wachezaji watakaoshiriki michuano hiyo ni wale tu ambao usajili wao umefanyika Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na kupata leseni. Hakutakuwa na usajili mwingine wowote mbali na ule uliofanyika sambamba na wa Ligi Kuu.
Taratibu zote za michuano hiyo zitafahamishwa kwa klabu husika ikiwemo ratiba ya michuano hiyo.
Kilimanjaro Stars ambayo itacheza mechi hiyo na mshindi wa robo fainali ya Desemba 4 kati ya wenyeji Uganda na Ethiopia imeingia hatua hiyo baada ya kuitoa Rwanda Desemba 3 2012.
Mabao ya Amri Kiemba dakika ya 33 na John Bocco dakika ya 53 ndiyo yaliyoifanya Kilimanjaro Stars itinge nusu fainali na kuifungisha virago Rwanda (Amavubi) inayofundishwa na Milutin ‘Micho’ Sredojovic kutoka Serbia.
Vijana wa Kilimanjaro Stars wanaonolewa na Kim Poulsen walitawala pambano hilo, hasa kipindi cha kwanza kwa pasi fupi fupi. Kilimanjaro Stars imefungwa bao moja katika mechi nne ilizocheza tangu michuano hiyo ilipoanza Novemba 24 mwaka huu jijini Kampala.
Kilimanjaro Stars ambayo katika michuano hiyo iliyofanyika Dar es Salaam mwaka jana iliishia hatua ya nusu fainali iliwakilishwa na; Juma Kaseja, Erasto Nyoni, Amir Maftah, Shomari Kapombe, Kelvin Yondani, Amri Kiemba, Salum Abubakar/Athuman Idd, Frank Domayo, Mwinyi Kazimoto, John Bocco na Mrisho Ngasa.
Kwenye line nyingine mwandishi Shaffih Dauda ameandika kuhusu Michuano ya kombe la Uhai kuanza disemba 7 2012 ni kwamba michuano hiyo inayoshirikisha timu za U20 za klabu za Ligi Kuu ya Vodacom inatarajiwa kumalizika Desemba 22 mwaka huu.
Wachezaji watakaoshiriki michuano hiyo ni wale tu ambao usajili wao umefanyika Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na kupata leseni. Hakutakuwa na usajili mwingine wowote mbali na ule uliofanyika sambamba na wa Ligi Kuu.
Taratibu zote za michuano hiyo zitafahamishwa kwa klabu husika ikiwemo ratiba ya michuano hiyo.
TAARIFA YA KILICHOENDELEA KUHUSU KESI YA MWIGIZAJI LULU DEC 3 2012.
Kesi ya mauaji ya marehemu Steven Kanumba inayomkabili movie star wa Tanzania Elizabeth Michael (Lulu) imeendelea kutajwa katika mahakama ya Hakimu mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam huku suala la umri wa mshitakiwa huyo likiendelea kuwekwa kiporo.
Mbele ya hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama ya Hakimu mkazi Kisutu AUGUSTINA MMBANDO, Wakili wa Serikali KENNETH SEKWAO amesema upelelezi bado haujakamilika na kwa sasa ipo katika hatua ya kutajwa.
Mapema baada ya LULU kufunguliwa mashitaka ya mauaji ya msanii mwenzake STEVEN KANUMBA April mwaka huu, mawakili wanaomtetea waliwasilisha hoja ya kupinga umri wa mshitakiwa huyo na kutaka achukuliwe kama mkosaji mtoto kutokana na umri wake kuwa chini ya miaka 18 hali iliyolazimu suala hilo kupelekwa Mahakama Kuu ya Tanzania iliyoamua kulirejesha jambo hilo kwenye mahakama ya Kisutu.
Pamoja na kurejeshwa kwa suala hilo katika mahakama ya Hakimu mkazi Kisutu kumekuwa na ukimya wa muda sasa, kesi ya LULU imeahirishwa mpaka Disemba 17 mwaka huu ambapo itakwenda kwaajili ya kutajwa.
Mbele ya hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama ya Hakimu mkazi Kisutu AUGUSTINA MMBANDO, Wakili wa Serikali KENNETH SEKWAO amesema upelelezi bado haujakamilika na kwa sasa ipo katika hatua ya kutajwa.
Mapema baada ya LULU kufunguliwa mashitaka ya mauaji ya msanii mwenzake STEVEN KANUMBA April mwaka huu, mawakili wanaomtetea waliwasilisha hoja ya kupinga umri wa mshitakiwa huyo na kutaka achukuliwe kama mkosaji mtoto kutokana na umri wake kuwa chini ya miaka 18 hali iliyolazimu suala hilo kupelekwa Mahakama Kuu ya Tanzania iliyoamua kulirejesha jambo hilo kwenye mahakama ya Kisutu.
Pamoja na kurejeshwa kwa suala hilo katika mahakama ya Hakimu mkazi Kisutu kumekuwa na ukimya wa muda sasa, kesi ya LULU imeahirishwa mpaka Disemba 17 mwaka huu ambapo itakwenda kwaajili ya kutajwa.
Friday, November 30, 2012
Basata Yatoa Salaam Za Rambirambi Kufatia Vifo Vya Wasanii..!
Yah: Salaam za Rambirambi
Baraza la Sanaa la Taifa limepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za misiba ya wasanii watatu wa tasnia ya filamu na muziki nchini.
“ Baraza limestushwa na kuhuzunishwa sana kutokana na taarifa ya vifo hivi vya wasanii hawa John Mganga, Mlopelo na Hussein Mkeity a.k.a Sharo Milionea ambao mchango wao unahitajika sana katika tasnia ya sanaa, pengo waliloliacha ni kubwa kwani ubunifu wao bado unahitajika katika tasnia hii.” Baraza linatoa pole kwa familia za marehemu na wasanii wote nchini, aidha linawatakia moyo wa subira katika wakati huu wa majonzi ya kuondokewa na wapendwa wetu.
Tunaomba mwenyezi Mungu azipumzishe mahala pema peponi roho za marehemu. Baraza liko pamoja na familia za marehemu katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo, tutambue kuwa haya ni mapenzi ya Mungu.
Imetolewa na
Ghonche materego
Katibu Mtendaji
Baraza la Sanaa la taifa.
Reactions::
Baraza la Sanaa la Taifa limepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za misiba ya wasanii watatu wa tasnia ya filamu na muziki nchini.
“ Baraza limestushwa na kuhuzunishwa sana kutokana na taarifa ya vifo hivi vya wasanii hawa John Mganga, Mlopelo na Hussein Mkeity a.k.a Sharo Milionea ambao mchango wao unahitajika sana katika tasnia ya sanaa, pengo waliloliacha ni kubwa kwani ubunifu wao bado unahitajika katika tasnia hii.” Baraza linatoa pole kwa familia za marehemu na wasanii wote nchini, aidha linawatakia moyo wa subira katika wakati huu wa majonzi ya kuondokewa na wapendwa wetu.
Tunaomba mwenyezi Mungu azipumzishe mahala pema peponi roho za marehemu. Baraza liko pamoja na familia za marehemu katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo, tutambue kuwa haya ni mapenzi ya Mungu.
Imetolewa na
Ghonche materego
Katibu Mtendaji
Baraza la Sanaa la taifa.
Reactions::
ACHA KUJIKATISHA TAMAA, UNA THAMANI KUBWA KWENYE MAPENZI!
NI Ijumaa nyingine tena tunakutana katika Let’s Talk About Love, lengo likiwa ni lilelile; kupeana elimu zaidi juu ya mambo ya uhusiano na mapenzi. Sina shaka marafiki zangu wote mtakuwa wazima wa afya njema.Kuna baadhi ya wanawake au wanaume wanakaa kipindi kirefu bila ya kutamkiwa kuwa wanapendwa, kutokana na hali hiyo wanakuwa wapweke na wakati mwingine kufikiria kuwa wao ni wabaya na wasiostahili kabisa kuwa na wapenzi.
Wengine huanza kujiona hawafai kutokana na sababu ambazo wenyewe wanaziweka ambazo kwa kiasi kikubwa huwa za kujikosoa.
Wakati mwingine huanza kufikiria kuwa huenda kwa sababu yupo katika hali fulani ndiyo maana hapati mtu wa kumpenda na fikra nyingine mbaya juu yake ambazo huwa ni za kujikatisha tamaa.
Tambua kitu kimoja, kuna wasichana warembo na wavulana watanashati wengi ambao hawajapata pumziko la kweli katika mioyo yao kwa muda mrefu sasa, wamekuwa wakitafuta watu wenye mapenzi ya dhati kwa muda mrefu bila mafanikio na sasa wamekata tamaa ya kupata wapenzi wa kweli na badala yake wamegeuka vyombo vya starehe.
Wavulana watanashati au wasichana warembo mara nyingi watu wa upande wa pili huwatamani zaidi kuliko kuwa na mapenzi ya kweli, kwa maana hiyo baada ya kushiriki naye ngono mara kadhaa huamua kuachana naye na kumuacha muhusika akiwa na sononeko katika moyo wake.
Watu wa aina hii huachwa na dhiki ya moyo na wakati mwingine hukata tamaa na kuamua kutokuwa na uhusiano mwingine kabisa na wapenzi wapya. Jaribu kufikiri kama kuna mtu wa aina hii ambaye amekuwa akitoneshwa mara kadhaa na wapenzi na wewe ambaye una miezi karibu sita sasa hujapata akupendaye nani mwenye matatizo zaidi? Nadhani jibu yakinifu utakuwa nalo.
Inawezekana wewe ni mmoja kati ya hao ambao wana sononeko la moyo kwa kutopata faraja ya kweli kwa wapenzi wao. Hakika hizi ni mada mbili tofauti lakini leo nitaanza na hili la kutopata mpenzi kwa muda mrefu na sasa umekata tamaa ya kupedwa, kuoa au kuolewa katika siku zote za maisha yako.
Wakati mwingine inawezekana hujafahamu chanzo cha wewe kutopata mpenzi, lakini kuna mambo mengi ya kuzingatia ili uweze kupata mpenzi na hivyo kuepuka upweke katika moyo wako.
JAMBO LA KWANZA
Jiulize mwenyewe, unajijali? Inawezekana ukawa na maswali lukuki kutokana na ninavyouliza swali hilo? Nataka utambue kitu kimoja, kuwa kuna baadhi ya watu hawajipendi! Hivi unadhani kama wewe mwenyewe hujipendi, hujithamini nani atakupenda?
Ninaposema ujipende namaanisha ujipe upendo ule wa kawaida wewe mwenyewe kabla ya kuhitaji upendo wa mtu mwingine. Mwingine anaweza akawa anavaa nguo chafu, hapigi pasi, nywele zipo timtim nani atakupenda kwa muonekano huo?
Hakuna anayependa kuwa na mtu ambaye hana desturi ya usafi kwanza hata kama ni mzuri kiasi gani unapokuwa upo rafu hakuna mtu atakayeusumbua moyo wake kuanza eti kukufikiria wewe usiyejipenda.
Siyo lazima wakati wote uwe ‘smart’, kwa kuwa inawezekana wengine wanafanya kazi ngumu ambazo mazingira yake lazima anakuwa mchafu, lakini baada ya kazi unapaswa kuwa msafi kabisa mbele za watu.
Upande wa wasichana siyo lazima uweke nywele zako dawa au usuke rasta wakati vitu hivyo huna uwezo navyo, unaweza ukasuka nywele zako vizuri au wakati mwingine ukanyoa mtindo mzuri unaokubalika ambao hautakutafsirisha vibaya kwa jamii.
Anza kujipenda kabla ya kuhitaji upendo kutoka kwa mtu mwingine, hiyo itakusaidia kuwa na mvuto na mwonekano mzuri kiasi cha kuweza kumpagawisha mtu mwingine kuanza kuhisi cheche za moto wa mapenzi katika moyo wake.
Nina mengi ya kuzungumza nanyi kuhusu mada hii,lakini kutokana na changamoto ya nafasi finyu, vuta subira hadi wiki ijayo tutaendelea, USIKOSE! kusoma globalpublishers
UVUMI KIFO CHA RAY C
WAKATI msanii Hussein Ramadhan Mkieti ‘Sharo Milionea’ akizikwa kijijini kwao, Muheza, Tanga Jumatano iliyopita, uvumi mkubwa umelitikisa Jiji la Dar es Salaam kuwa, mwanamuziki wa Kizazi Kipya, Rehema Chalamila ‘Ray C’ naye ameaga dunia ghafla.
Uvumi huo ulizagaa kwa kasi kuanzia saa kumi na mbili jioni kupitia mitandao ya kijamii na ujumbe mfupi wa maneno (SMS) kupitia simu za mkononi huku wengine wakidai ni ‘komfemdi’.
Baadhi ya watu walianza kuamini uzushi huo na kujiuliza kulikoni katika burudani Bongo kuwapoteza mastaa wao mfululizo.
“Juzi tu Mlopelo, halafu John Maganga, jana (Jumatatu) Sharo Milionea. Leo tena Ray C, kuna nini kwa mastaa wetu?” alihoji mmoja wa watu waliotumiwa ujumbe huo huku akishika kichwa kuonesha hali ya majonzi.
Hata hivyo, hadi kufikia saa 4 usiku, mama mzazi wa Ray C, Margaret Mtweve alijitokeza hadharani kupitia Radio Clouds FM na kukanusha vikali taarifa hizo huku akisema:
“Mwanangu ni mzima, tena anaendelea vizuri kwa sasa. Hao wanaoneza uzushi huo washindwe kwa jina la Yesu.”
Awali, mchana wa siku
hiyo, zilienea tetesi eti msanii nyota wa sinema Bongo, Juma Sadiki Kilowoko ‘Sajuki’ naye amefariki dunia wakari si kweli.
Watu waliozungumza na gazeti hili jana walionesha wasiwasi wao mkubwa juu ya ufahamu wa baadhi ya Watanzania ambao wamekuwa na tabia ya kueneza uvumi mara kwa mara kwamba mtu f’lani, hasa maarufu amefariki dunia.
“Nahisi kuna Watanzania si wazima vichwani kwani sasa imekuwa fasheni. Mtu anaamua tu, anaandika ujumbe kwenye simu kwamba staa f’lani amefariki dunia wakati si kweli,” alisema Hamad Hussein, mkazi wa Magomeni-Kagera, Dar.
Uvumi huo ulizagaa kwa kasi kuanzia saa kumi na mbili jioni kupitia mitandao ya kijamii na ujumbe mfupi wa maneno (SMS) kupitia simu za mkononi huku wengine wakidai ni ‘komfemdi’.
Baadhi ya watu walianza kuamini uzushi huo na kujiuliza kulikoni katika burudani Bongo kuwapoteza mastaa wao mfululizo.
“Juzi tu Mlopelo, halafu John Maganga, jana (Jumatatu) Sharo Milionea. Leo tena Ray C, kuna nini kwa mastaa wetu?” alihoji mmoja wa watu waliotumiwa ujumbe huo huku akishika kichwa kuonesha hali ya majonzi.
Hata hivyo, hadi kufikia saa 4 usiku, mama mzazi wa Ray C, Margaret Mtweve alijitokeza hadharani kupitia Radio Clouds FM na kukanusha vikali taarifa hizo huku akisema:
“Mwanangu ni mzima, tena anaendelea vizuri kwa sasa. Hao wanaoneza uzushi huo washindwe kwa jina la Yesu.”
Awali, mchana wa siku
hiyo, zilienea tetesi eti msanii nyota wa sinema Bongo, Juma Sadiki Kilowoko ‘Sajuki’ naye amefariki dunia wakari si kweli.
Watu waliozungumza na gazeti hili jana walionesha wasiwasi wao mkubwa juu ya ufahamu wa baadhi ya Watanzania ambao wamekuwa na tabia ya kueneza uvumi mara kwa mara kwamba mtu f’lani, hasa maarufu amefariki dunia.
“Nahisi kuna Watanzania si wazima vichwani kwani sasa imekuwa fasheni. Mtu anaamua tu, anaandika ujumbe kwenye simu kwamba staa f’lani amefariki dunia wakati si kweli,” alisema Hamad Hussein, mkazi wa Magomeni-Kagera, Dar.
Subscribe to:
Posts (Atom)























.png)


























