Tuesday, February 19, 2013

"SINA KINYONGO JUU YA PENZI LA DIAMOND NA PENNY"...JOKATE

BAADA ya Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ kupata demu mpya, Penniel Mungilwa ‘Penny’, Jokate Mwegelo ametoa baraka zake kwa jamaa huyo aliyewahi kudaiwa kuwa mpenzi wake akisema haoni tatizo wawili hao kuwa pamoja kama kweli wamependana na kuridhiana.

Akizungumza katika mahojiano maalum alipobanwa kuhusiana na uhusiano wa wapenzi hao huku ikifahamika kuwa Penny alikuwa shosti wake, Jokate ambaye ni Miss Tanzania namba 2, 2006/07 alisema kwamba yeye na mrembo huyo walikuwa washikaji tu na wala hawakuwa na urafiki wa karibu kama baadhi ya watu wanavyoamini.

Jokate ambaye pia ni mtangazaji wa Runinga ya Channel O alifunguka kuwa anawatakia kila la heri na baraka zote Diamond na Penny katika uhusiano wao mpya wa kimapenzi endapo tu watakuwa wamependana na kuridhiana kwa dhati.

“Japokuwa sipendi kumuongelea Diamond lakini ukweli sioni tatizo kwa wao kupendana, mimi naona poa tu,” alifunguka Jokate ambaye pia ni bonge la mwigizaji.

Kabla ya kutoka kimapenzi na Penny ambaye naye ni mtangazaji wa Runinga ya DTV, Diamond aliwahi kuviteka vyombo vya habari akiripotiwa kuwa na Jokate, kabla ya mambo kwenda mrama.
tagazo

"SIPO TAYARI KUKUTANA NA LULU MICHAEL KUTOKANA NA UNYAMA ALIOUFANYA KWA KANUMBA"...MAYA

STAA wa filamu za Kibongo, Mayasa Mrisho ‘Maya’ amefunguka kuwa tangu Elizabeth Michael ‘Lulu’ atolewe gerezani kwa dhamana, moyo wake unakuwa mzito kukutana naye.

Akipiga stori na mwandishi wetu, Maya aliweka plain kuwa kila anapofikiria ukaribu aliokuwa nao na marehemu Steven Kanumba, moyo wake unakuwa mzito kumuona Lulu ambaye alikuwa mpenzi wa marehemu.

“Mh! Kukutana na Lulu ni ngumu sana, sijui hata najisikiaje? Moyo unakuwa mzito sana kukutana naye na sijui kwa nini,” alisema Maya.

Baba Mtakatifu aanza wiki ya kufunga na kutoonekana hadharani.

Baba Mtakatifu Benedict wa 16 ameanza wiki yake ya mafungo ya kiroho ambapo atakuwa haonekani hadharani kwa wiki nzima ikiwa ni mwanzo wa safari yake ya kuelekea kuachia rasmi uongozi wa kanisa Katoliki na kusema kuwa ana matumaini ibada zake zitakuwa na mafanikio.

 Baba mtakatatifu atabakia Vatican na baadhi ya wasaidizi wake wa karibu kwa ajili ya ibada za awali za sikukuu ya Pasaka na atapata mapumziko mafupi kila siku kwa ajili ya kuonana na katibu wake Georg Gaenswein, ili kuyashughulikia masuala ya dharura ya kanisa.

 Baada ya wiki nzima ya ibada, Baba Mtakatifu atakutana na rais wa Italia, Giorgio Napolitano, tarehe 23 Februari kushiriki ibada ya Jumapili yake ya mwisho ifikapo tarehe 24 mwezi huu na kuzungumza hadharani kwa mara ya mwisho mbele ya waumini wapatao 10,000.

Kiongozi huyo wa kanisa Katoliki duniani ataachia uongozi rasmi tarehe 28 mwezi huu na inasemakana kuwa Waziri wa Utamaduni wa Vatican Kadinali Gianfranco Ravasi ndiye anayeonekana mtu mwenye nafasi kubwa ya kuchukua nafasi yake kwa muda mfupi au mrefu.

KAULI ZA SERIKALI YA ZNZ NA MAASKOFU WAKUU KATOLIKI KUHUSU MAUAJI YA PADRE.

 Baada ya kifo cha Padre Evarist Mushi ambae alifariki kwa kupigwa risasi Zanzibar jumapili iliyopita, kanisa Katoliki limewataka waumini wa kanisa hilo na Watanzania wengine kuwa watulivu na kufanya maombi ya amani katika kipindi hiki.

Askofu mkuu wa kanisa hilo Tanzania Muadhama Polycarp Cardinal Pengo amesema kifo cha Padre Mushi ni pigo kwa kanisa na Taifa na ni ishara ya kutoweka kwa amani hivyo hilo swala linatakiwa kufanyiwa kazi kabla ya madhara kuzidi, kwa sababu ukikosekana usalama kwa imani moja, kesho na kesho kutwa haijulikani ni imani gani ikashambuliwa.

Namkariri akisema “vyombo vya usalama vinatakiwa viwe makini, mimi sio mtaalamu wa usalama lakini naona ni jambo ambalo lingeweza kuzuilika na lisitokee kama watu wangesoma ishara za nyakati, wale wanaohusika wazuie kisitokee chochote… kuendeleza moyo wa kisasi hakutasaidia chochote na badala yake kutaleta madhara zaidi”

Magazeti ya leo Jumanne ya 19th February 2013





Saturday, February 9, 2013

Tanzania yashiriki utalii hispania

 Ujumbe wa Tanzania ukiwa katika picha ya pamoja na Youssou Ndour Waziri wa Utalii na Utamaduni nchini Senegal  ambaye pia ni mwanamuziki maarufu duniani wakati alipotembelea banda la Tanzania katika maonyesho hayo , Youssou Ndour amewahi kufanya ziara ya kimuziki mara tatu nchini Tanzania kabla ya kuteuliwa kuwa Waziri wa Utalii na Utamaduni nchini mwake.

Miss Utalii Tanzania 2013 kutembelea Hifadhi za Taifa na vivutio vya utalii





    Miss Utalii Tanzania 2012/13 wiki ijayo wataanza ziara ndefu ya kutembelea Hifadhi za Taifa na vivutio vya utalii katika mikoa ya Dar es salaam,Morogoro,Mtwara,Lindi na Pwani. Vivutio hivyo ni pamoja na Hifadhi za Taifa za Mikumi, Udizungwa, Saadani, Selous, pia maeneo ya kihistoria ya Bagamoyo, Amboni, Kijiji cha makumbusho,Makumbusho ya Taifa, Pugu sekondari,maeneo mengine ni ufukwe wa kigamboni, soko la kimataifa la Magogoni, Uwanja wa Taifa, uwanja wa ndege wa  J.K.Nyerere Air Port, Soko la Kariakoo, Mashule ya sekondari na msingi, pia watatembelea manispaa za Ilala, Temeke na Kinondoni ambapo watakutana na viongozi wakuu wa wilaya, mikoa, na wabunge katika majimbo ya mikoa hiyo.

JK atua msumbiji Jana

 Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya nchi jumuiya ya Maendeleo ya Uchumi Kusini Mwa Afrika SADC Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akikagua gwaride la heshima muda mfupi baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Maputo.Rais Kikwete yupo nchini Msumbiji kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi za SADC

MAgazeti ya leo Jumamosi ya 9th February 2013




YALIYOJIRI BUNGENI

 Mh Kigwangalla alimalizia kwa kusema “naomba atumie uungwana yeye mwenyewe kusimama katika bunge hili.. aidha kuwaomba radhi Watanzania kwa kudanganya ama kutimiza wajibu aliousema hapa yeye mwenyewe wa kujiuzulu, uongo aliousema ni mkubwa sana.. naomba nitoe hoja kwamba Mh Mbatia aadhibiwe kwa mujibu wa kanuni ya 63, asihudhurie vikao visivyozidi 20 na aombe radhi kwa maandishi kwa Watanzania kwa kusema uongo bungeni”

Friday, February 8, 2013

MSIKUBALI KUDANGANYWA ANGALIENI MAFANIKIO YENU- PALANGYO

WANACHAMA wa Chama cha Mapinduzi wilaya ya Meru,mkoani Arusha,wameshauriwa kutokukubali kudanganywa na Vyama vya kisiasa ambavyo vinaeneza Propaganda chafu  kuwa hakuna kilichofanyika tangia Uhuru,badala yake wachukie siasa zinazosababisha uvunjifu wa amani

KAMPUNI YA NDEGE YA fastjet YAKANUSHA UVUMI KUWA IMEFUTIWA LESENI YA BIASHARA

Jean Uku Meneja Masoko na Mauzo wa Kampuni ya ndege ya Fastjet akizungumza na waandishi wa habari kwenye hoteli ya Hyyat Regency Dar es salaam kukanusha uvumi wa habari zinazosema kampuni hiyo imenyang’anywa leseni ya kufanya biashari nchini Tanzania, Kushoto ni Givaldine Dawe Meneja Utawala.

Pamoja na habari zilizoandikwa na kusemwa kwenye vyombo vya habari leo, biashara ndani ya kampuni ya fastjet inaendelea kama kawaida. Madai yanayotukabili ya kunyang’anywa leseni hayana ukweli wowote. Tunaendelea kufanya kazi na ndege zetu nchini Tanzania kama kawaida na bado tunazidi kuzindua vituo vipya kama ilivyopangwa. Huu ni uzushi wa baadhi ya watu au kampuni zenye chuki dhidi ya kampuni ya fastjet, kusudi lao ni kudhoofisha uaminifu na kuharibu sifa ya jina la biashara na bidhaa zetu za fastjet.

Ofisi zetu na vituo vyetu vya kuuzia tiketi bado viko wazi kwa ajili ya bookings na Kwa tiketi zilizolipiwa pesa haitarudishwa.

TAMKO RASMI BAADA YA MASAA MACHACHE

MAGUNIA MENGINE 97 YA BANGI YAKAMATWA NA JESHI LA POLISI ARUSHA

 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi wa Polisi Liberatus Sabas akiwaonyesha waandishi wa habari madawa ya kulevya aina ya bangi ambayo yalikuwa kwenye magunia 97 yaliyokamatwa na askari wa jeshi hilo katika eneo la Usa river wilayani Arumeru (Picha na Rashid Nchimbi wa Jeshi la Polisi)

HIVI NDIVYO MATUMAINI ALIVYOPOKELEWA JIJINI DAR

    Matumaini (katikati) akisaidiwa na wasanii wenzake muda mfupi baada ya kutua.
   Matumaini (kulia) akiwa na Bi. Mwenda (wa pili kushoto) na anayefuata (kushoto) ni msanii mwenzake Kiwewe wakisubiri gari la kumpeleka hospitali.
                                     Bi. Mwenda akiwa amembeba Matumaini mgongoni.

Yaliyojiri Magazetini Leo Ijumaa ya 8th February 2013