Katika hali ya kushitua,Mh.Mbowe akiongea na wanachama wa chadema leo Ubungo plaza amemkaanga Zitto kabwe na kudai kuwa chadema haiko tayari kumtimua Lwakatare katika chama hata kama ni gaidi....
"Eti nashangaa kuna watu wanataka CHADEMA kimuache Lwakatare na kumsimamisha uongozi kwa uzushi uliopandikizwa na CCM, Hilo halitafanyika"- alisema Mbowe.
IKUMBUKWE siku chache zilizopita naibu katibu Mkuu wa CHADEMA Mh. Zitto Kabwe alitoa mapendekezo ya kuomba Mshitakiwa mkuu kwenye kesi ya Ugaidi ambaye ni Ndugu Lwakatare aliyekuwa mkuu wa usalama wa chadema awajibike kisiasa...
Kuwajibika kisiasa ni pamoja na kuachia ngazi ya ukurugenzi wa usalama ili kupisha uchunguzi salama na kukiacha chama salama.
Monday, April 15, 2013
Saturday, April 13, 2013
PADRI ALIYEOA KWA SIRI AFUNGWA JELA MIEZI 6
KUSHOTO: Padri William akimbusu mkewe, Beverley. KULIA: Kanisa la Mt. Clara ambamo Padri huyo alibambwa akifanya uchavu wake kwa binti wa miaka 17.
Padri mmoja wa kanisa Katoliki ambaye alifunga ndoa kwa siri amehukumiwa kifungo cha miezi sita jela jana kwa kumsumbua msichana mdogo kwa kile jaji alichoelezea 'uvunjifu mkubwa wa uaminifu'.
William Finnegan, akifahamika kama 'Fadha Bill', alimpapasa binti huyo mwenye miaka 17 chini na kulazimisha kumbusu kwa nguvu katika Kanisa Katoliki la Mt Clara mjini Bradford siku ya Jumapili ya Pasaka mwaka jana.
Jaji Roger Thomas alisema kwamba Padri huyo mwenye miaka 60, alikiri wakati wa kesi hiyo kwamba alifunga ndoa kwa siri miaka 14 iliyopita.
Pia alitumia maneno makali kwa wanaparokia wa Finnegan ambao walikuwa upande wake licha ya mashitaka hayo, akisema: "Pengine baadhi yao wanaweza kuamini kesho jua litachomoza magharibi kesho kama akisema hivyo."
Padri mmoja wa kanisa Katoliki ambaye alifunga ndoa kwa siri amehukumiwa kifungo cha miezi sita jela jana kwa kumsumbua msichana mdogo kwa kile jaji alichoelezea 'uvunjifu mkubwa wa uaminifu'.
William Finnegan, akifahamika kama 'Fadha Bill', alimpapasa binti huyo mwenye miaka 17 chini na kulazimisha kumbusu kwa nguvu katika Kanisa Katoliki la Mt Clara mjini Bradford siku ya Jumapili ya Pasaka mwaka jana.
Jaji Roger Thomas alisema kwamba Padri huyo mwenye miaka 60, alikiri wakati wa kesi hiyo kwamba alifunga ndoa kwa siri miaka 14 iliyopita.
Pia alitumia maneno makali kwa wanaparokia wa Finnegan ambao walikuwa upande wake licha ya mashitaka hayo, akisema: "Pengine baadhi yao wanaweza kuamini kesho jua litachomoza magharibi kesho kama akisema hivyo."
MWENYEKITI WA CHADEMA ATUPWA JELA MWAKA MMOJA KWA WIZI WA MIL. 1.2
Mwenyekiti wa chadema, mtaa wa isamilo kaskazini B wilayani nyamagana Philbert Bulinjiye amehukumiwa kifungo cha mwaka mmoja jela kwa kosa la kujipatia shs milioni 1,250,000 kwa njia ya udanganyifu.
Hukumu hiyo, imetolewa na hakimu Vaineth Mahizi wa mahakama hiyo, kufuatia kesi ya jinai namba 196/2012, iliyofunguliwa na Vedasto Mavubhi ambaye alimtuhumu mwenyekiti huyo kuchukua kwake kiasi hicho cha fedha, kwa ajili ya kumuuzia kiwanja.
Hakimu Mahizi katika hukumu yake, alidai ameridhika na ushahidi uliotolewa na upnade wa mlalamikaji, mashahidi pamoja na wazee wa baraza hivyo kumhukumu mwenyekiti kwenda jela.
Alisema mwenyekiti huyo pamoja na Balozi Robert Byagaye wanastahili kutumikia kifungo hicho cha mwaka mmoja jela kutokana na kutiwa hatiani.
"kitendo kilichofanywa na viongozi hawa, kuwaibia raia wanaowaongoza kiutapeli kwa kuwadanganya kuwauzia kiwanja na kisha kutafuta mtu bandia kwa madai kuwa kiwanja hicho kiko katika mtaa wanaouongoza, ni udanganyifu" Alisema hakimu na kuongeza kuwa Mwenyekiti huyo amehukumiwa kifungo hicho ili iwe fundisho kwa viongozi wengine matapeli.
Hukumu hiyo, imetolewa na hakimu Vaineth Mahizi wa mahakama hiyo, kufuatia kesi ya jinai namba 196/2012, iliyofunguliwa na Vedasto Mavubhi ambaye alimtuhumu mwenyekiti huyo kuchukua kwake kiasi hicho cha fedha, kwa ajili ya kumuuzia kiwanja.
Hakimu Mahizi katika hukumu yake, alidai ameridhika na ushahidi uliotolewa na upnade wa mlalamikaji, mashahidi pamoja na wazee wa baraza hivyo kumhukumu mwenyekiti kwenda jela.
Alisema mwenyekiti huyo pamoja na Balozi Robert Byagaye wanastahili kutumikia kifungo hicho cha mwaka mmoja jela kutokana na kutiwa hatiani.
"kitendo kilichofanywa na viongozi hawa, kuwaibia raia wanaowaongoza kiutapeli kwa kuwadanganya kuwauzia kiwanja na kisha kutafuta mtu bandia kwa madai kuwa kiwanja hicho kiko katika mtaa wanaouongoza, ni udanganyifu" Alisema hakimu na kuongeza kuwa Mwenyekiti huyo amehukumiwa kifungo hicho ili iwe fundisho kwa viongozi wengine matapeli.
NYARAKA NZITO ZA CCM ZAVUJA...
Taarifa za ndani kabisa zilizopatikana kutoka kwa Waandishi wa habari,Vyombo vya usalama na ndani ya CCM kwenyewe zinaonyesha sakata la Kuteswa kwa Kibanda na kufunguliwa mashtaka ya ugaidi Mkurugenzi wa usalama wa Chadema ndugu Alfred Lwakatare linachukua sura mpya na mapya yamefichuka kwa ushahidi.
Dennis Msacky ambaye ni mhariri wa Mwananchi aliyehusishwa na kuwa mojawapo wa watu waliopangwa kutekwa,amekua akifanya mawasiliano na Ludovick Joseph Lwezaura kama ifuatavyo
Tarehe 27/12/2012: Dennis Msacky kupitia simu ya mkononi namba 07643310** aliwasiliana kwa simu na Ludovick Joseph kupitia simu namba 07539271** akiwa Tamal hotel,Mwenge jijini dar-Es Salaam. Hii ilikua siku moja kabla ya mkanda wa video uliowekwa youtube kurekodiwa.mkanda ulionyesha kuwa ulirekodiwa kesho yake yaani tarehe 28/12/2013
Dennis Msacky ambaye ni mhariri wa Mwananchi aliyehusishwa na kuwa mojawapo wa watu waliopangwa kutekwa,amekua akifanya mawasiliano na Ludovick Joseph Lwezaura kama ifuatavyo
Tarehe 27/12/2012: Dennis Msacky kupitia simu ya mkononi namba 07643310** aliwasiliana kwa simu na Ludovick Joseph kupitia simu namba 07539271** akiwa Tamal hotel,Mwenge jijini dar-Es Salaam. Hii ilikua siku moja kabla ya mkanda wa video uliowekwa youtube kurekodiwa.mkanda ulionyesha kuwa ulirekodiwa kesho yake yaani tarehe 28/12/2013
MWANAMKE MPUMBAVU HUIVUNJA NDOA YAKE MWENYEWE NA SERIKALI PUMBAVU HUBOMOA NCHI"... MH. SUGU
Wakati akichangia bajeti ya PM, Mh Mbilinyi ametumia lugha kali sana dhini ya serikali na Mwigulu Nchemba akazua ubishi mkubwa kati yake na Speaker..
Ameanza kwa kusema kuwa "Mwanamke mpumbavu huvunja nyumba yake mwenyewe" na hivyo hivyo serikali pumbavu hubomoa nchi.
Akiwa na jaziba nyingi, Joseph Mbilinyi 'sugu' amemchanachana Mwigulu kuwa ni mpumbavu na kudai kuwa anafanya dili alafu anatumia m-pesa...
Baada ya kumvaa Mwigulu, Sugu alimgeukia waziri wa elimu Mulugo na kudai kuwa ana elimu ya kuungaunga na ni chenga tupu...
Sugu anadai kushangazwa na tabia ya usalama wa taifa kuifuatilia Chadema na kung'oa watu kucha na meno.
Pamoja na kukalishwa mara mbili na spika ili atumie lugha ya staha bado aliendelea
Ameanza kwa kusema kuwa "Mwanamke mpumbavu huvunja nyumba yake mwenyewe" na hivyo hivyo serikali pumbavu hubomoa nchi.
Akiwa na jaziba nyingi, Joseph Mbilinyi 'sugu' amemchanachana Mwigulu kuwa ni mpumbavu na kudai kuwa anafanya dili alafu anatumia m-pesa...
Baada ya kumvaa Mwigulu, Sugu alimgeukia waziri wa elimu Mulugo na kudai kuwa ana elimu ya kuungaunga na ni chenga tupu...
Sugu anadai kushangazwa na tabia ya usalama wa taifa kuifuatilia Chadema na kung'oa watu kucha na meno.
Pamoja na kukalishwa mara mbili na spika ili atumie lugha ya staha bado aliendelea
FASTJET YAKANUSHA KUNYANG'ANYWA LESENI YAKE YA BIASHARA TANZANIA
Kampuni ya ndege ya Fast Jet imezikanusha ripoti kuwa imenyang’anywa leseni yake ya biashara katika nchi kadhaa barani Afrika ikiwemo Tanzania.Kupitia website yake kampuni hiyo imeandika:
Licha ya taarifa za leo kwenye vyombo vya habari, ni biashara kama kawaida hapa fastjet. Madai kuhusu kunyang’anywa leseni ni uongo mtupu. Tunaendelea na safari zetu kutoka Tanzania na tunaendelea kuanzisha safari mpya kama ilivyopangwa.
Hii ni njama/hujuma ‘binafsi’ dhidi ya fstjet katika jaribio wazi lililotengenezwa kuharibu brand na sifa ya Fastjet.Ofisi zetu na matawi yetu bado zipo wazi kwa booking mpya na hakuna refund zozote.
Licha ya taarifa za leo kwenye vyombo vya habari, ni biashara kama kawaida hapa fastjet. Madai kuhusu kunyang’anywa leseni ni uongo mtupu. Tunaendelea na safari zetu kutoka Tanzania na tunaendelea kuanzisha safari mpya kama ilivyopangwa.
Hii ni njama/hujuma ‘binafsi’ dhidi ya fstjet katika jaribio wazi lililotengenezwa kuharibu brand na sifa ya Fastjet.Ofisi zetu na matawi yetu bado zipo wazi kwa booking mpya na hakuna refund zozote.
NAULI MPYA NCHINI SASA NI VURUGU TUPU
Viwango vipya vya nauli za daladala na mabasi yaendayo mikoani zimeanza kutumika jana, huku wananchi wakizipinga wakidai zinawaumiza zaidi kiuchumi.
Wakati baadhi wakilalamikia kupanda kwa nauli za dalala katika maeneo yao, baadhi ya wafanyakazi wa mabasi yaendayo mikoani wameendelea kutoza nauli ya zamani.
Zoezi la kupandisha nauli nchini lililoanza jana limewagawanya wamiliki wa magari na kufanya baadhi ya safari za mikoani kupandisha nauli, huku nyingine zikiendelea kuwa kama zamani wakati nauli za daladala Dar es salaam zikipanda kama ilivyoagizwa.
Hatua hiyo ya kupandisha nauli ilizua tafrani baina ya makondakta na abiria waliokuwa wakisafiri katika safari mbalimbali ndani ya jiji, hususan wale waliokuwa hawajui kuwa jana ndiyo siku ambapo nauli zilitakiwa kupanda.
Wakati baadhi wakilalamikia kupanda kwa nauli za dalala katika maeneo yao, baadhi ya wafanyakazi wa mabasi yaendayo mikoani wameendelea kutoza nauli ya zamani.
Zoezi la kupandisha nauli nchini lililoanza jana limewagawanya wamiliki wa magari na kufanya baadhi ya safari za mikoani kupandisha nauli, huku nyingine zikiendelea kuwa kama zamani wakati nauli za daladala Dar es salaam zikipanda kama ilivyoagizwa.
Hatua hiyo ya kupandisha nauli ilizua tafrani baina ya makondakta na abiria waliokuwa wakisafiri katika safari mbalimbali ndani ya jiji, hususan wale waliokuwa hawajui kuwa jana ndiyo siku ambapo nauli zilitakiwa kupanda.
KITENDO CHA KUWANYANG'ANYA ARDHI WANANCHI WA LOLIONDO CHAMCHANGANYA RAIS KIKWETE
Sakata la mgogoro unaorindima kwa sasa kuhusu unyang'anywaji wa Ardhi ya Loliondo kwa lengo la kumpa mwekezaji wa kiarabu umemvuruga sana Rais Kikwete na kusita kujitokeza hadharani kulitolea kauli.
Hapo awali Kupitia kikao cha baraza la mawaziri iliamriwa kuwa WAKAZI WA LOLIONDO WANYANG'ANYWE ENEO HILO na kumtuma Waziri wa Maliasili na Utalii Hamisi Kagasheki kwenda kulisimamia kwa nguvu zote....
Hapo awali Kupitia kikao cha baraza la mawaziri iliamriwa kuwa WAKAZI WA LOLIONDO WANYANG'ANYWE ENEO HILO na kumtuma Waziri wa Maliasili na Utalii Hamisi Kagasheki kwenda kulisimamia kwa nguvu zote....
HUU NDO UFISADI MKUBWA WA JOHN CHEYO CHINI YA "KOFIA YA BUNGE"
John Momose Cheyo mwanasiasa wa siku nyingi ametumia cheo chake cha Uenyekiti wa Kamati ya PAC, kujinufaisha kupitia kampuni ya mdogo wake anayejulikana kwa jina la Sylvester Maghembe Cheyo ambaye anamiliki kampuni inayoitwa ATLAS PLUMBERS AND BUILDERS LTD.
Kwa kipindi ambacho Mheshimiwa Cheyo amekuwa Mwenyekiti wa Kamati hii ya Bunge kampuni ya ATLAS Plumbers amd Builders imepata miradi ifuatayo katika mashirika ya Serikali ambayo yapo chini ya Kamati iliyokuwa inaoongozwa na Bwana Mapesa.
Kwa kipindi ambacho Mheshimiwa Cheyo amekuwa Mwenyekiti wa Kamati hii ya Bunge kampuni ya ATLAS Plumbers amd Builders imepata miradi ifuatayo katika mashirika ya Serikali ambayo yapo chini ya Kamati iliyokuwa inaoongozwa na Bwana Mapesa.
Friday, April 12, 2013
RIPOTI KUHUSU WATOTO WA NELSON MANDELA KUGOMBANIA MALI
Zenani ndio huyu wa nyumba ya Mzee Mandela, hawa wengine ni wajukuu na vitukuu wa Mandela.
BBC wameandika kwamba watoto wa Rais mstaafu wa Afrika Kusini Nelson Mandela Makaziwe na Zenani Mandela, wameamua kuchukua hatua za kuwaondoa wasaidizi watatu kutoka katika makampuni anayoyamiliki wakidai kuwa watatu hao hawana haki ya kuwa kwenye bodi mbili za kampuni hiyo ambazo ni za thamani ya dola milioni 1.1
Kesi hiyo inakuja wakati kuna wasiwasi kuhusu afya ya Mandela mwenye umri wa miaka 94 ambae aliondoka hospitali baada ya kutibiwa mapafu akiwa tayari kalazwa hospitali mara nne katika kipindi cha miaka miwili.
BBC wameandika kwamba watoto wa Rais mstaafu wa Afrika Kusini Nelson Mandela Makaziwe na Zenani Mandela, wameamua kuchukua hatua za kuwaondoa wasaidizi watatu kutoka katika makampuni anayoyamiliki wakidai kuwa watatu hao hawana haki ya kuwa kwenye bodi mbili za kampuni hiyo ambazo ni za thamani ya dola milioni 1.1
Kesi hiyo inakuja wakati kuna wasiwasi kuhusu afya ya Mandela mwenye umri wa miaka 94 ambae aliondoka hospitali baada ya kutibiwa mapafu akiwa tayari kalazwa hospitali mara nne katika kipindi cha miaka miwili.
WEMA WEPETU AMFIKISHA POLISI MAMA YAKE BAADA YA KUMFANYIA VURUGU NYUMBANI
NI kivumbi! Kuna madai kwamba, staa wa Bongo asiyechuja, Wema Sepetu amemfikisha mama yake, Miriam Sepetu kwenye Kituo cha Polisi Kijitonyama ‘Mabatini’, Dar kwa madai ya kwenda nyumbani kwake na kufanya vurugu zilizosababisha kuharibika kwa samani mbalimbali...
Kwa mujibu wa chanzo chetu, ishu hiyo ilijiri usiku wa kuamkia Jumatano iliyopita, nyumbani kwa Wema, Kijitonyama, jijini Dar.
Mbali na mama mtu, wengine waliofikishwa kituoni hapo ni dada mkubwa wa Wema aitwaye Nuru na kijana aliyefahamika kwa jina moja la Bestizo ambaye inasemekana ni mshirika mkubwa wa Diamond kwenye masuala ya mtandao wa msanii huyo.
“Wema alikuwa nyumbani kwake usiku huo, watuhumiwa hao wakamzukia na kuanza kumchapa makofi ya ‘kelbu’ ambapo katika mshikemshike huo, baadhi ya vitu vilivunjika na kumtia hasara staa huyo,” kilisema chanzo.
Haikujulikana mara moja ni kitu gani kilisababisha mama mzazi huyo, dada mtu na kijana asiyekuwa ndugu kwenda kwa Wema na kutenda kosa hilo.
Wema alikwenda polisi na kuandikisha maelezo ambayo yameingizwa kwenye jalada lenye kumbukumbu; KJN/RB/2755/2013 SHAMBULIO, KUHARIBU MALI.
Kwa mujibu wa chanzo chetu, ishu hiyo ilijiri usiku wa kuamkia Jumatano iliyopita, nyumbani kwa Wema, Kijitonyama, jijini Dar.
Mbali na mama mtu, wengine waliofikishwa kituoni hapo ni dada mkubwa wa Wema aitwaye Nuru na kijana aliyefahamika kwa jina moja la Bestizo ambaye inasemekana ni mshirika mkubwa wa Diamond kwenye masuala ya mtandao wa msanii huyo.
“Wema alikuwa nyumbani kwake usiku huo, watuhumiwa hao wakamzukia na kuanza kumchapa makofi ya ‘kelbu’ ambapo katika mshikemshike huo, baadhi ya vitu vilivunjika na kumtia hasara staa huyo,” kilisema chanzo.
Haikujulikana mara moja ni kitu gani kilisababisha mama mzazi huyo, dada mtu na kijana asiyekuwa ndugu kwenda kwa Wema na kutenda kosa hilo.
Wema alikwenda polisi na kuandikisha maelezo ambayo yameingizwa kwenye jalada lenye kumbukumbu; KJN/RB/2755/2013 SHAMBULIO, KUHARIBU MALI.
TATIZO LA ELIMU TANZANIA SIYO VIBOKO.....BORESHENI MIUNDO MBINU KWANZA BADALA YA KUFIKIRIA KUTEMBEZA VIBOKO
Taifa liko katika wakati mgumu juu mustakabali wa sekta ya elimu kutokana na changamoto mbalimbali zinazoikabili. Kuna mengi yanazungumzwa, yamependekezwa na mengine bado yanaendelea kutolewa juu ya njia sahihi ya kukoa elimu ya watu wa taifa hili.
Kuna hoja zinatolewa kwamba sekta ya elimu imeachwa kuporomoka hadi kufikia hali mbaya ya sasa kutokana na kuminywa kwa bajeti ya sekta hiyo, matokeo yake ni janga la kufeli kwa wananfunzi wengi katika mitihani yao kama ilivyodhihirika kwa wanafunzi wa kidato cha nne waliomaliza elimu ya sekondari mwaka jana kwa zaidi ya asilimia 60 kupata daraja sifuri.
Kuna hoja zinatolewa kwamba sekta ya elimu imeachwa kuporomoka hadi kufikia hali mbaya ya sasa kutokana na kuminywa kwa bajeti ya sekta hiyo, matokeo yake ni janga la kufeli kwa wananfunzi wengi katika mitihani yao kama ilivyodhihirika kwa wanafunzi wa kidato cha nne waliomaliza elimu ya sekondari mwaka jana kwa zaidi ya asilimia 60 kupata daraja sifuri.
HAKUNA SHERIA INAYOMLAZIMISHA MTU KUPIMA UKIMWI ILI AFUNGE NDOA AU APATIWE AJIRA
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo wa Kwanza wa Rais, Fatma Abdul habib Fereji
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imesema suala la kupima Ukimwi ni la hiari kwa hivyo hakuna mwananchi wala mgeni atakayelazimishwa kufanya hivyo endapo akitaka kufunga ndoa au akipatiwa ajira.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo wa Kwanza wa Rais, Fatma Abdul habib Fereji aliwaambia wajumbe wa baraza la wawakilishi jana wakati akijibu swali la nyongeza la Mwakilishi wa Jimbo la Mtambwe ( CUF) Salim Abdalla Hamad aliyetaka kujuwa kwa nini Serikali isipime afya za wananchi kwa lazima kujuwa kama wapo salama na ugonjwa wa Ukimwi.Fereji alisema Zazibar hakuna sheria inayoilazimisha Serikali kuwapima wananchi afya zao kwa lazima kuhusu ugonjwa wa Ukimwi na kwa kuwa hilo ni suali la mtu binafsi serikali yake ni kutoa elimu na kuwahamasisha wapime afya zao lakini sio kuwalazimisha.
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imesema suala la kupima Ukimwi ni la hiari kwa hivyo hakuna mwananchi wala mgeni atakayelazimishwa kufanya hivyo endapo akitaka kufunga ndoa au akipatiwa ajira.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo wa Kwanza wa Rais, Fatma Abdul habib Fereji aliwaambia wajumbe wa baraza la wawakilishi jana wakati akijibu swali la nyongeza la Mwakilishi wa Jimbo la Mtambwe ( CUF) Salim Abdalla Hamad aliyetaka kujuwa kwa nini Serikali isipime afya za wananchi kwa lazima kujuwa kama wapo salama na ugonjwa wa Ukimwi.Fereji alisema Zazibar hakuna sheria inayoilazimisha Serikali kuwapima wananchi afya zao kwa lazima kuhusu ugonjwa wa Ukimwi na kwa kuwa hilo ni suali la mtu binafsi serikali yake ni kutoa elimu na kuwahamasisha wapime afya zao lakini sio kuwalazimisha.
Subscribe to:
Posts (Atom)
















