Wednesday, July 4, 2012

HAHAHAHAHAHAHAHAH................ AMKA,TUMERUDI KAZINI


RAIS KIKWETE AREJEA TOKA RWANDA NA BURUNDI

Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete wakiwasili Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam jana jioni
wakitokea Burundi na Rwanda walikohuidhuria sherehe za miaka 50 wa uhuru wa nchi hizo. Anayeongozana nao ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Saidi Mecky Sadik.
Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa na Inspekta Jenerali wa Polisi Afande Saidi Mwema na Mkuu wa Majeshi Jenerali Davies Mwamunyange baada ya kuwasili Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam jana jioni wakitokea Burundi na Rwanda walikohuidhuria sherehe za miaka 50 wa uhuru wa nchi hizo

PICHA NA IKULU

Banda la Wizara ya Fedha, lachukua ushindi wa pili kwenye Maonesho ya Sabasaba

Mchumi Mwandamizi wa Wizara ya Fedha, Idara ya Bajeti, Adam Msumule, akimpatia maelezo mwananchi aliyetembelea banda la wizara ya Fedha, kuhusu bejeti ya nchi, kwenye maonesho ya Biashara ya Kimataifa, viwanja vya J.K. Nyerere, barabara ya Kilwa, Dar es Salaam leo.
Baadhi ya wafanyakazi wa Wizara ya Fedha wanaotoa huduma ya kuwaelimisha wananchi kwenye banda la wizara hiyo, Viwanja vya Maonesho ya Biashara ya Kimataifa, wakipiga picha ya pamoja kwa ajili ya kumbukumbu ya maonesho hayo leo




Wananchi wakiingia kwenye banda la Wizara ya Fedha, leo kujionea na kupata huduma mbalimbali zitolewazo na wizara hiyo.

HIVI UMEMSIKIA KIPA SHABAN KADO ALICHOSEMA KUHUSU KURUDISHWA MTIBWA? UNAYAJUA MAONI YAKE KUHUSU KIPA MPYA YANGA ALIETOKA SIMBA?

                                           Kipa Shaban Kado kushoto mwenye jezi nyeusi
Kwa long time kidogo stori zimekua zikiandikwa kwenye magazeti, Radio na Tv kuhusu kipa wa Yanga Shaban Kado ambae club hiyo imetangaza kumrudisha kucheza kwa mkopo Mtibwa Sugar hivyo ikasajili kipa mwingine mpya ambae ni Bartez kutoka Simba.

Amesema “hizo taarifa nilianza kuzisikia kwenye vyombo vya habari bila mimi mwenyewe kuambiwa na uongozi lakini baadae nikafanya mawasiliano na boss wangu na sasa tuko kwenye mikakati ambayo ikikamilika ndio itajulikana Kado anakwenda wapi, inaweza kuwa sio Mtibwa”

Kuhusu Kurudi Mtibwa Kado amesema “kwa makubaliano ikitokea hivyo ninaweza kurudi kwa sababu ni timu yangu iliyonifanya kila mtu anasikia kuhusu Kado, sitakataa kurudi Mtibwa ila itategemea itahitajika nirudi vipi na kuhusu ishu ya mimi kuondolewa Yanga kuna sababu tu nazifaham ambazo baadae zitakuja kujulikana”

Kuhusu stori za kurudishwa Mtibwa kwa sababu kiwango chake cha uchezaji kimeshuka akiwa Yanga, Kado amesema  “katika mechi zote za Yanga nimepoteza mechi mbili au tatu, sasa utaniambiaje kiwango kimeshuka wakati kupoteza mechi ni kitu cha kawaida tu”

Kado ambae ni mmoja kati  ya wachezaji wa kibongo wanaotumia sana mtandao wa kijamii wa facebook amekubali kuzungumzia ishu za yeye kuhamia kwenye club nyingine ikiwemoa Simba ambayo inadaiwa kumuita kwa ajili ya kumpa mkataba.

Katika sentensi nyingine Kado amesema mpaka sasa hayuko tayari kuzungumza ni timu gani atakayokwenda kuichezea baada ya Yanga lakini amethibitisha kwamba kuna uwezekano akarudi Mtibwa au timu nyingine yoyote.

 Chanzo: millardayo.com

MKE MJAMZITO WA GAEL GLICHY NDIO HUYU.

Baada ya Mario Balotelli kutangaza kwamba anatarajia kupata mtoto na demu wake Raffaella, leo Gael Glichy amejitokeza mitaani na mkewe wake Charlene Guric ambaye sasa imegundulika ni mjamzito wa miezi minne.

Clichy na mkewe Charlene walionekana wakitembea kwenye maduka ya St.Lopez wakifanya manunuzi ya vitu mbalimbali siku mbili baada ya mchezaji mwenzie wa Manchester City Mario Balotelli na mchumba Modo Raffaella kutangaza kwamba wanatarajia kupata mtoto.

Inaonekana wachezaji wa City wamepania kutengeneza timu nyingine ya watoto wao sasa.

HUYU NDIO MISS DAR INDIAN OCEAN 2012, NA HII NI SEHEMU YA MAGUMU ALIYOYAPITIA.



                                                     Diana Hussein Miss Dar Indian Ocean 2012.
Kuna asilimia kubwa ya mastaa au watu maarufu unaowapenda au kuwafaham kupitia  TV, Magazeti, radio na internet lakini umaarufu walionao haujaja kirahisi.

Stori nyingi sana za mastaa kusikia alikoanzia, na ni mbali wengi sana wametoa jasho debe kufikia walipo mtu kama Sean Kingston ambae aliwahi kuja bongo kwenye KTMA aliwahi kufanya kazi ya kukata nyasi kwenye garden za watasha ili mwisho wa day zipatikane dola kwa ajili ya kula, nakumbuka mwaka jana aliandika kwenye twitter kwamba kazi ya kuwa msimamizi wa garnen aliichukia sana.

Tukirudi home bongo, wako mastaa kibao wameanza kwa kusota sana… au kupitia kwenye mambo magumu ya maisha pia akiwemo binti mrembo ambae juzi juzi ndio alivishwa taji la miss Dar Indian ocean Diana Hussein,  ni mrembo lakini mwenye makovu mengi ya kimaisha yasioyoonekana kwenye ngozi yake nzuri, ameanza kufanya kazi miaka mitatu iliyopita akiwa na umri wa miaka 17 tu kazi ambazo hakuzipenda kabisa lakini alifanya hivyo kwa sababu ya maisha.

Baada ya kukosa ada ya kuendelea na masomo ya sekondari ilibidi Diana aje Dar akitokea Tanga na kuanza kazi yake ya kwanza ya kuajiriwa kwenye duka la dawa, aliifanya hiyo kazi kwa mwaka mmoja na baadae huku akiwa na machungu ya kuisaidia familia yake kiuwezo aliamua kutafuta kibarua kingine na akafanikiwa kuwa mkaribisha wageni kwenye kampuni moja Dar es salaam, kazi zote hizo alizifanya lakini hakuwahi kuzipenda kabisa.

Japo bado hajatimiza ndoto zake lakini amefikia kwenye hatua ya kuridhisha baada ya kuacha kazi za kuajiriwa mwaka huu na kuanzisha biashara yake ya kuuza vitu vya warembo wenzake, kama mikufu, perfume na vingine…. huku mawazo yake yakimpa msukumo wa kufanya vizuri zaidi kwenye mashindano yanayofata ya juu zaidi.

Magazeti Ya Leo Jumatano 4th July 2012


Tuesday, July 3, 2012

Wenyeji 12 Wa Euro 2020

Platini anasema huenda ikawa bora michuano ya Euro 2020 kufanyika katika miji mbalimbali ya Ulaya

Michel Platini, rais wa shirikisho la soka barani Ulaya, UEFA, amesema michuano ya Euro 2020 huenda ikafanyika katika miji mbalimbali mwaka 2020, badala ya kuwa na mji mmoja ambao utakuwa ni mwenyeji.

Utamaduni wa mashindano hayo huwa ni nchi moja, au mbili, kushirikiana katika kuwa mwenyeji, kama ilivyo wakati huu michuano hiyo kufanyika Poland na Ukraine.
Mashindano yajayo yatafanyika nchini Ufaransa, mwaka 2016.

"Euro 2020 inaweza kufanyika popote barani Ulaya," alielezea Platini. "Yanaweza kufanyika katika nchi moja yenye viwanja 12, au kufanyika katika uwanja mmoja katika miji 12 au 13 ya Ulaya."

Platini ameelezea kwamba wazo hilo pia linaweza kuokoa senti katika kuepuka gharama kubwa za ukarabati, na juhudi za kujenga viwanja vipya na kuimarisha viwanja vya ndege.

Uturuki ilitazamiwa na wengi kupata nafasi ya kuandaa mashindano ya mwaka 2020, lakini ombi la nchi hiyo limekumbwa na tatizo, kwa kuwa nchi hiyo pia ina nia ya kuandaa michezo ya Olimpiki mjini Istanbul, mwaka huohuo wa 2020.

Mataifa ya Uskochi, Wales na Jamhuri ya Ireland, rasmi pia yameelezea nia yao ya kuandaa michuano ya 2020.

Platini ametangaza kwamba uamuzi kamili utatangazwa kati ya mwezi Januari hadi Februari mwaka ujao.

Chanzo:BBC

Afisa Mkuu Mtendaji Wa Barclays Ajiuzulu

Afisa mkuu mtendaji wa benki ya Barclays Bob Diamond hatimaye amejiuzulu.Mwenyekiti anayeondoka Marcus Agius, ambaye alitangaza kujiuzulu kwake hiyo jana, sasa atakuwa mwenyekiti wa kudumu wa benki hiyo na ataongoza mikakati ya kumtafuta afisa mkuu mtendaji mpya.Benki ya Barclays, imekumbwa na kashfa ya kuongeza viwango vya riba kinyume cha sheria.
Chanzo:BBC

Mgomo Wa Madaktari: JK Akoleza Moto

Waandishi Wetu
SIKU moja baada ya Rais Jakaya Kikwete kusema daktari anayeona kuwa hawezi kufanya kazi serikalini bila ya kulipwa mshahara wa Sh3.5 milioni aache kazi, viongozi wa dini, wanasiasa, wabunge na wasomi wamemtaka apunguze jazba.Wakizungumza kwa nyakati tofauti jana walisema mgogoro wa madaktari na Serikali bado unajadilika huku Mbunge wa Ubungo (Chadema), John Mnyika akienda mbali zaidi na kusema Serikali iache kisingizio cha Mahakama kulizuia Bunge kujadili mgogoro baina yake na madaktari, wakati yenyewe inajadili na kutoa maelezo.

Juzi, katika hotuba yake ya kila mwisho wa mwezi, Rais Kikwete alisema Serikali haiwezi kuahidi kuwa inao uwezo wa kuwalipa madaktari mshahara huo na posho zote kwani ikifanya hivyo malipo ya daktari anayeanza kazi yatakuwa Sh7.7 milioni kwa mwezi kitu ambacho hakiwezekani.

Jana, wakizungumza kwa nyakati tofauti, wadau hao walisema mgogoro huo kati ya Serikali na madaktari bado unajadilika na kusisitiza kuwa hotuba ya Rais Kikwete haijajibu madai ya madaktari.

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Bashiru Ally alisema ingekuwa jambo jema kama kungekuwa na uwezekano wa mazungumzo kuendelea.

Alisema kauli ya Rais ni upande wa Serikali hivyo, ingekuwa vyema kama madaktari nao wangepata nafasi ya kujieleza.

Wanasiasa
Mbunge wa Kasulu Mjini (NCCR-Mageuzi), Moses Machali alimtaka Rais apunguze hasira na kuitaka Serikali ikubali kurudi katika meza ya mazungumzo hata kama ndiyo iliyokuwa ya kwanza kuwapeleka mahakamani madaktari waliogoma.

Alisema kama Serikali haiwezi kulipa kiwango cha mshahara kilichopendekezwa na madaktari, irudi katika meza ya mazungumzo ili kutafuta suluhu ya mgomo huo unaowaumiza zaidi wananchi.

“Warudi kwenye meza ya majadiliano siyo kila mmoja kusema la kwake na kuacha mgomo kuendelea huku, watu wakiteseka hospitalini bila msaada wowote,’’ alisema Machali.

Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Julius Mtatiro alisema Serikali haipaswi kuwafukuza madaktari kwa kuwa imetumia gharama kubwa kuwasomesha.

“Ikiwafukuza madaktari italazimika kuwaleta walio nje ya nchi ambao ni gharama kubwa… Serikali itatue mgogoro huu,” alisema.

Mbunge wa Ubungo (Chadema), John Mnyika alisema Serikali iache kutumia kisingizio cha Mahakama kulizuia Bunge kujadili mgogoro wa madaktari wakati yenyewe ikitoa ufafanuzi.

“Uamuzi wa Serikali kutoa kauli kupitia hotuba ya Rais una mwelekeo wa kukwepa wabunge kujadili hotuba husika ambayo awali, ilielezwa kuwa ingetolewa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda bungeni. Inawanyima haki wabunge wasitimize wajibu wa kikatiba wa Ibara 63 (2) wa kuisimamia Serikali kwa niaba ya wananchi,” alisema Mnyika.

Mnyika alisema, kwa kuwa Bunge litajadili mapitio ya utekelezaji wa Bajeti ya Ofisi ya Rais kwa mwaka wa fedha 2011/2012 na makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2012/2013 kuanzia leo, ni muhimu wabunge wakajadili pia masuala ambayo Rais ameyaeleza kwa taifa na kutimiza wajibu wa kikatiba.

“Hotuba ya Rais imeendeleza kauli za upande mmoja ambazo zimekuwa zikitolewa na Serikali kuhusu mgogoro huo bila taifa kupewa fursa ya kupata maelezo na vielelezo vya upande wa pili, hivyo Serikali imetoa kauli yake hadharani badala ya bungeni au mahakamani.

Viongozi wa dini

Mchungaji wa Kanisa la Maombezi (GRC) Ubungo Kibangu, Anthony Lusekelo alisema madaktari hao wanatakiwa kurudi kazini kwa kuwa tayari Serikali imeshasema kuwa haina fedha za kuwalipa na kuongeza kuwa hata kama wana madai yao, wadai wakiwa kazini.

“Asilimia kubwa ya madaktari wamesomeshwa na Serikali… Serikali hiyohiyo inawaeleza kuwa haina fedha za kuwalipa kama wanavyotaka, binafsi nawaomba tu warudi kazini kwa kuwa mgomo wao unawaathiri zaidi wananchi kuliko hata hao viongozi wa Serikali.

“Tunajua tulikotoka ila hatujui tunakokwenda, kama ni kuboreshwa kwa sekta nzima ya afya, Serikali imesema itatekeleza hilo, haiwezi kuyatekeleza kwa siku moja, haya mambo yanajadilika.

Alisema kama Serikali itakuwa na makosa yake, itayajibu mbele za Mungu... “Madaktari watekeleze wajibu wa kazi yao kwa uwezo wa Serikali iliyopo madarakani.”

Askofu Msaidizi wa Jimbo Katoliki la Kagera, Dk Methodius Kilaini alisema kanisa hilo haliwezi kuunga mkono mgomo huo.

Alisema pamoja na kuwa madaktari wana madai yao, jukumu lao kubwa ni kufuata maadili ya kazi yao ambayo hayawaruhusu kugoma.

Katibu Mkuu wa Makanisa ya Kipentekoste Tanzania, Askofu David Mwasota alisema madaktari wanatakiwa kutenganisha siasa na maadili ya kazi yao.

“Hata kama Serikali ina makosa yake lakini, wao kuendelea kugoma si jambo zuri kwa jamii na hata mbele za Mungu, watumie njia nyingine kudai madai yao, lakini waendelee kutoa huduma. Madaktari ni watu muhimu, kurudisha viungo vya binadamu katika hali ya kawaida si kazi ndogo, warudi kazini kuokoa mamia ya Watanzania maskini.”

Katibu wa Baraza Kuu la Waislamu wa Tanzania (Bakwata), Mkoa wa Arusha Abdulkarim Jonjo alisema ipo haja kwa Serikali kukaa meza moja na madaktari hao.

Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Mjini Kati, Thomas Laizer alisema mgogoro wa madaktari umalizwe kwa mazungumzo.

Alisema Serikali inapaswa kuwa wazi inapozungumza na madaktari kwa kueleza ni mambo gani yanawezekana na kwa muda gani ili, kuondoa migogoro.

Akizungumza juzi katika ibada maalumu katika kanisa la KKKT Kimandolu, alisema ili kuondoa hisia kuwa Serikali inahusika na tukio la kutekwa Dk Ulimboka ni lazima iundwe tume huru.

“Nadhani ili kuondoa haya maneno ambayo si jambo dogo, Serikali inapaswa kuunda tume huru kuchunguza tukio hili, kwani inawezekana waliohusika ni watu wengine tu wenye nia mbaya na Serikali lakini ili ukweli ujulikane ni muhimu kuwepo tume huru,” alisema Askofu Laizer.

Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhaj Mussa Salum aliwataka madaktari kutii agizo lililotolewa na Mahakama kwa kurudi kazini.

“Rais ameshaeleza wazi kwamba Serikali haina fedha za kuwalipa kama wanavyotaka, warudi tu kazini na kuweka masilahi ya Watanzania mbele na kuacha kutanguliza masilahi binafsi,” alisema Sheikh Salum.

Wanaharakati

Mkurungezi Mtendaji wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Dk Hellen Kijo-Bisimba alisema hotuba hiyo ya Rais haina jipya zaidi ya kurudia maelezo yake ya awali alipokutana na Wazee wa Mkoa wa Dar es Salaam.

“Nilitarajia kuwa hotuba itakuwa tofauti lakini sivyo. Amerudia maelezo yaleyale aliyoyasema Machi 12 (mwaka huu) alipokutana na wazee katika Ukumbi wa Diamond Jubilee,” alisema Bisimba.

Wakili Peter Jonathan alisema kama kweli Serikali inataka kurudisha imani kwa Watanzania kuhusu tukio la Dk Ulimboka ni lazima ijisafishe kwa kuunda tume huru nje ya Serikali.

“Watafute hata Jaji mstaafu, si lazima atoke Tanzania kuongoza tume huru ikibidi tuchukue hata nje ya nchi ili wakitoa taarifa iweze kuaminiwa na jamii na hiyo ndiyo dhana sahihi ya utawala bora,” alisema.

Mjumbe wa Chama cha Watabibu wa Tiba Asili (ATME), Boniventure Mwalongo ameitaka Serikali kuacha kutumia nguvu kushughulikia madai ya madaktari badala yake ipanue wigo wa majadiliano ili kutatua tatizo hilo.

“Nimesikiliza hotuba ya Rais lakini, haijaonyesha kama kuna jawabu la mgomo hivyo wapanue wigo wa majadiliano ili kumaliza mgogoro huu,” alisema Mwalongo.

Habari hii imeandikwa na Fidelis Butahe,
Nora Damian, Bakari Kiango, Freddy Azzah, Daniel Mwingira, Dar; Daniel Mjema, Moshi; Mussa Juma, Arusha na Frederick Katulanda, Mwanza.
Chanzo:  http://www.mwananchi.co.tz


Dk. Mtaki: Usagaji Ni Starehe Kama Zingine ; Asema Ikizidishwa Inaharibu Saikolojia Ya Mchezaji

Dk. Magreth Mtaki.
GUMZO juu ya wachezaji wa timu ya taifa ya wanawake ya Twiga Stars kufanya vitendo vya kustareheshana, limetetewa na baadhi ya wataalam kuwa ni tendo linaloweza kufanyika kama lilivyo tendo lingine.

Mjadala ulizuka wiki mbili zilizopita juu ya kufanya vibaya kwa Twiga Stars kwa kufungwa jumla ya mabao 3-1 na Ethiopia katika mechi za kuwania kucheza Fainali za Afrika zitakazofanyika Equatorial Guinea baadaye Novemba.


Mkwasa alisema kuwa kufanya vibaya kwa timu hiyo kumechangiwa kwa kiasi kikubwa na baadhi ya wachezaji wa timu hiyo kuendekeza vitendo vya kusagana, lakini akasema kuwa waliokuwa wakifanya 'hayo mambo' (bila kuwataja) walitimuliwa.

Lakini vitendo hivyo vimetajwa kushamiri hasa katika timu zinazojumuisha wanawake ama wasichana wengi kwani kila mmoja anakuwa na tabia na mihemko yake kiasi cha kuwaathiri wengine.

Spoti Mikiki ilifanya mahojiano na Dk. Magreth Mtaki, daktari wa michezo wa siku nyingi kutoka Kurugenzi ya Michezo ambaye anasema kuwa kusagana (lesbianism) ni kama starehe nyingine ambayo watu wa jinsi mbalimbali wanafanya.

Anasema kuwa tatizo linakuja kuwa ni suala linalohusisha wasichana ama kinamama ndiyo maana linaleta mshangao, lakini hakuna tofauti na matendo mengine ama kustareheshana kwa watu wawili.

Dk. Mtaki ambaye pia ni Makamu wa Chama cha Soka ya wanawake Tanzania, TWFA, anasema kuwa kitendo cha kusagana, kwa upande mwingine kina athari kubwa kwenye timu kwani endapo kitafanywa kwa kuzidisha, inamaliza nguvu mchezaji.

"Hata ingekuwa wewe na mke wako, una mechi ya kimataifa ama ligi, halafu ukafanya tendo la ndoa kupitiliza, ni wazi itapunguza uwezo wako uwanjani, basi hata hawa wanaosagana, wakizidisha, lazima uwezo utapungua.

"Kingine ambacho naweza kusema, lakini sasa hii ni kwa mchezaji mwenyewe...hali hii itamfanya hatokuwa na hamu ya mwanaume akiamini kuwa mwanamke mwenzake anakata kiu.
Chanzo:  http://www.mwananchi.co.tz

Nimeipenda Hii


Magazeti ya leo Jumanne


Diwani wa Kata ya Makongo (Chadema), Deusdedit Jacob Mtiro.

                                Diwani wa Kata ya Makongo (Chadema), Deusdedit Jacob Mtiro.

ILIKUWA kama sinema pale Diwani wa Kata ya Makongo (Chadema), Deusdedit Jacob Mtiro alipoongoza kundi la vijana waponda kokoto kubomoa sehemu ya nyumba ya Katibu wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), Kata ya Makongo, Judith Lungato Stambuli Ijumaa iliyopita nyumbani kwake Mlalakua, Mwenge jijini Dar es Salaam.

Katika tafrani hiyo kiongozi huyo licha ya kuvunjiwa sehemu ya nyumba yake na kuchaniwa gauni na mtandio, habari za kipolisi zinasema Diwani Mtiro anatuhumiwa kwenda na wahuni kwa kiongozi huyo ambapo alipigwa na kusababisha mali zake kadhaa kuibiwa kutokana na vurugu kubwa iliyozuka.

Habari ambazo polisi wanazo ni kwamba mali alizoibiwa kiongozi huyo ni simu aina ya Blackberry yenye thamani ya shilingi 350,000, nguo aina ya dera na vitenge vyenye thamani kubwa, saa ya mkononi na nondo kadhaa zilizokuwa kwenye nyumba ya mama huyo.

Mwandishi wetu aliambiwa na kiongozi mmoja wa polisi kuwa tayari Diwani Mtiro amefunguliwa jalada Kituo cha Polisi Chuo Kikuu cha Mlimani lenye namba UD/RB/4045/2012 (Shambulio la mwili).

Akizungumza na mwandishi wetu, Bi Stambuli alisema sehemu iliyosababisha ashambuliwe hakujenga hivi karibuni bali imejengwa miaka zaidi ya miwili iliyopita na wala haikuwa na usumbufu wowote kwa raia.

“Mwenyekiti wa serikali ya mtaa wangu aliwahi kusuluhisha suala hili baada ya watu wenye roho mbaya kuvunja, wakaamriwa wajenge, tukiwa polisi alikiri kufanya kosa na wakaamua kunijengea kwa gharama zao, nilishangaa kuona Diwani Mtiro anakuja na kunibomolea tena bila hata notisi, ” alisema katibu huyo.

Baadhi ya wananchi wa Mlalakua akiwemo mzee Kariakoo, walisema kitendo alichofanyiwa mwanamke huyo ni cha kinyama na siasa imeingizwa, “Hakuna sehemu ilikuwa nadhifu kama hii kwani mvua ikinyesha watu walikuwa hawakanyagi tope.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, ACP Charles Kenyela alipopigiwa simu alisema hajapata taarifa ya tukio hilo na akaahidi kufuatilia.

Imeandaliwa Na Haruni Sanchawa.

Mwanamke azikwa akiwa hai Mbeya


                   Baadhi ya wananchi wa Kijiji cha Malamba, Wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya.

KUMEZUKA vitendo vya unyama mkoani Mbeya vya kuzika watu wanaotuhumiwa kuwa ni washirikina wakiwa hai ambapo hivi karibuni watu wawili akiwemo mwanamke mmoja wamefanyiwa unyama huo.
Mwanamke aliyezikwa akiwa hai kwa tuhuma za kujihusisha na ushirikina ni Rozina Mwadala (60) ambapo tukio hilo lilitokea Juni 2, mwaka huu.

Mwanamke huyo alichukuliwa hatua hiyo baada ya kifo cha mmoja wa ndugu yake ambaye alifariki muda mchache baada ya kulalamika kuwa alikuwa akiumwa sikio na kichwa. Hata hivyo, hakukuwa na mtu yeyote aliyekuwa tayari kuhojiwa na mwandishi wetu kwa hofu ya kukamatwa na polisi.

Kufuatia vitendo hivyo kushika kasi mkoani Mbeya, Mwenyekiti wa Muungano wa Jamii Tanzania (Mujata), Chifu Soja Masoko, amewaonya wananchi wa Kijiji cha Malamba, Wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya kuacha mara moja tabia za kujichukulia sheria mikononi alipokuwa akiwahutubia katika mkutano wa hadhara Juni 15, mwaka huu.

“Hasara yake mnaona. Sasa kufuatia kitendo hicho cha kikatili baadhi ya wananchi wamehama kijijini hapa kukwepa mkono wa sheria na shughuli za kiuchumi zimezorota,” alisema.

Mbali na mwanamke huyo kuzikwa hai, hivi karibuni mwanaume mmoja, Nyerere Kombwee naye alizikwa hai baada ya kutokea kifo cha mdogo wake kisha yeye kutohudhuria msibani ndipo wananchi wakamsaka na walipompata wakampiga na yeye akatoa vitisho kuwa damu yake isingeweza kwenda bure ndipo wakaamua kumzika akiwa hai.