Mhe. Waziri akiwa na Balozi wa tz Berlin Mhe. Ahmada R. Ngemera (kushoto) na Afisa wa Wizara ya mambo ya Nje, Ali Ubwa Mussa
Mhe. Waziri na ujumbe wake wakiwa katika Majadiliano na Uongozi wa Sekta ya Usafiri wa Anga, Germany
Mhe. Waziri akipata maelezo kutoka kwa mtaalamu wa ndege za Airbus,
nchini ujeruman (hayupo pichani) pembeni yake ni Mhe. balozi wa tz
Berlin.
Mhe. Waziri akiwa ndani ya moja ya ndege iliyokuwepo katika maonyesho hayo.
Mhe. Waziri na ujumbe wake wakiwa katika maonyesho ya Sekta ya usafiri wa Anga mjini Berlin.
Naomba nikutumie baadhi ya picha za ziara ya Mhe. Mwakyembe Berlin, Ujerumani. utaandaa maelezo mazuri wewe mwenyewe. Ila kwa ufupi ni kwamba Mhe. Waziri na ujumbe wake wapo Berlin kuanzia trh 15 hadi 19 sept, 2012. moja ya tukio muhimu ni kusainiwa Mkataba wa Ushirikiano wa Usafiri wa Anga (Bilateral Air Services Agreement - BASA) baina ya nchi hizi mbili tarehe 17 Sept. Aidha, leo tarehe 16 sept, Mhe. Waziri na ujumbe wake walitembelea maonyesho ya Kimaitaifa ya sekta ya Usafiri wa Anga yaliofanyika hapa Berlin. Aidha kwa nyakati mbalimbali, Mhe. na ujumbe wake watakutana na wafanyabiasha na wawekezaji mbalimbali hususani katika sekta ya usafiri (Anga, reli na meli).
Baada ya ziara ya hapa ujeruman, ujumbe wa wataalam (tu) aliofatana nao mhe. waziri utaelekea the Hague Uholanzi kwa ajili ya majadiliano mengine kuhusu usafiri wa anga tarehe 19 hadi 21 sept. Mhe waziri hatushiriki. NAOMBA SANA UIREKEBISHE STORI HII KABLA YA KUITOA ILI ITOE UJUMBE MZURI: SASA NAKULETEA MAELEZO YA PICS NLIZOKUTUMIA.
Monday, September 17, 2012
Dk.Titus Kamani Adai Anachafuliwa
MIKAKATI na kampeni za majitaka zenye lengo la kumchafua Mbunge wa Jimbo la Busega mkoani Simiyu, Dk. Titus Kamani, zimeanza kubainika kwa kumhusisha na tena na tuhuma za mauaji.
Dk. Kamani, ambaye ni miongoni mwa wanachama wa CCM waliojitosa kuwania nafasi ya Mwenyekiti wa Mkoa mpya wa Simiyu, ameanza kuchafuliwa akihusishwa na tuhuma za kutaka kumuua aliyekuwa mbunge wa Busega, Dk. Raphael Chegeni.
Hata hivyo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Liberatus Barlow, aliwahi kueleza bayana kuwa wamefanya uchunguzi wa kina na kubaini Dk. Kamani hahusiki na tuhuma hizo na kwamba, waliotuhumiwa wameshafikishwa mahakamani.
“Hatumtafuti Dk Kamani, tukimhitaji tutampata lakini katika uchunguzi wetu tumebaini tuhuma hizo hazimuhusu," alikaririwa Kamanda Barlow baada ya kuibuka kwa uvumi kuwa mbunge huyo alikuwa akisakwa na polisi.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari mjini Dar es Salaam, jana, Dk. Kamani amesema kumekuwepo na kampeni chafu za kuhakikisha jina lake linachafuka ili kudhoofisha harakati zake za kukitumikia Chama.
Amesema kuwa tangu alipojitosa kuwania nafasi hiyo, kumekuwepo na mikakati ya kumchafua inayofanywa na baadhi ya wanasiasa wakiwemo waliopo ndani ya CCM na kwamba, hilo amelibaini na atalifikisha kwenye vikao husika.
Dk. Kamani katika taarifa yake amesema kuwa, mbinu chafu hizo zimekuwa zikisukwa na wanasiasa hao kwa lengo la kumchafua na kumchonganisha na wapigakura wake pamoja na jamii imuone kuwa hafai.
“Makovu na visasi vya kushindwa katika uchaguzi uliopita kamwe havitaiharibu Busega wala kunidhoofisha kuwatumia wananchi wangu. Nafahamu hizi ni mbinu chafu kwa ajili ya kuniharibia katika harakati zangu za kuwania nafasi ndani ya Chama," alisema katika taarifa hiyo.
Tayari watu wanaotuhumiwa kuhusika katika njama za kutaka kumuua Dk. Chegeni
wameshapandishwa kizimbani kujibu mashitaka hayo.
Dk. Kamani, ambaye ni miongoni mwa wanachama wa CCM waliojitosa kuwania nafasi ya Mwenyekiti wa Mkoa mpya wa Simiyu, ameanza kuchafuliwa akihusishwa na tuhuma za kutaka kumuua aliyekuwa mbunge wa Busega, Dk. Raphael Chegeni.
Hata hivyo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Liberatus Barlow, aliwahi kueleza bayana kuwa wamefanya uchunguzi wa kina na kubaini Dk. Kamani hahusiki na tuhuma hizo na kwamba, waliotuhumiwa wameshafikishwa mahakamani.
“Hatumtafuti Dk Kamani, tukimhitaji tutampata lakini katika uchunguzi wetu tumebaini tuhuma hizo hazimuhusu," alikaririwa Kamanda Barlow baada ya kuibuka kwa uvumi kuwa mbunge huyo alikuwa akisakwa na polisi.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari mjini Dar es Salaam, jana, Dk. Kamani amesema kumekuwepo na kampeni chafu za kuhakikisha jina lake linachafuka ili kudhoofisha harakati zake za kukitumikia Chama.
Amesema kuwa tangu alipojitosa kuwania nafasi hiyo, kumekuwepo na mikakati ya kumchafua inayofanywa na baadhi ya wanasiasa wakiwemo waliopo ndani ya CCM na kwamba, hilo amelibaini na atalifikisha kwenye vikao husika.
Dk. Kamani katika taarifa yake amesema kuwa, mbinu chafu hizo zimekuwa zikisukwa na wanasiasa hao kwa lengo la kumchafua na kumchonganisha na wapigakura wake pamoja na jamii imuone kuwa hafai.
“Makovu na visasi vya kushindwa katika uchaguzi uliopita kamwe havitaiharibu Busega wala kunidhoofisha kuwatumia wananchi wangu. Nafahamu hizi ni mbinu chafu kwa ajili ya kuniharibia katika harakati zangu za kuwania nafasi ndani ya Chama," alisema katika taarifa hiyo.
Tayari watu wanaotuhumiwa kuhusika katika njama za kutaka kumuua Dk. Chegeni
wameshapandishwa kizimbani kujibu mashitaka hayo.
Saturday, September 15, 2012
Inaijua asili yako tanzania asilialive inakuletea utamaduni mwa mwaafrika halisi
Hawa ni akina mama ambao ni majirani wa wasandawe yaani wagogo mkoani dodoma unajua hilo
Je watanzania tuna vazi la kitanazania ili tuweze kujivunia mimi na wewe. Kama una picha yako ya mavazi ya kabila yako tutumie tanzania asilialive ipo kwa ajili yako tuma kwa email, Asilialive@yahoo.com
TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2012 LARINDIMA UWANJA WA JAMHURI MJINI DODOMA USIKU HUU
Mkuu wa mkoa wa Dodoma Dkt. Rehema Nchimbi akitangaza namba ya mshindi wa bahati nasibu ya gari aina ya Toyota Virtz aliyejishindia gari hilo katika droo ya tamasha la Serengeti Fiesta 2012 mkoani Dodoma kwenye tamasha la lililofanyika katika uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma usiku huu, aliyeshika kompyuta ni Meneja masoko wa kampuni ya Push Mobile Rugambo Rodney, kulia ni Mkuu wa wilaya ya Dodoma Lephy Gembe na wa pili kutoka kulia ni mwakilishi wa bodi ya michezo ya kubahatisha Bw. Humud.
Katika tamasha hilo wasanii mbalimbali wanatumbuiza katika tamasha hilo kubwa baada ya matamasha mengine kama hayo katika mikoa ya Kilimanjaro, Tanga, Mwanza, Shinyanga, Mara, Tabora, Singida na sasa mkoani Dodoma.
![]() |
| Waigizaji wa filamu wakielezea uwezo wao katika kusakata muziki kutopka kulia ni Jacob Steven JB, Wema Sepetu, na Aunt Ezekikel. |
![]() |
| Aunt Ezekiel akimwaga mauno yake lanini mbewle ya mashabiki |
![]() |
| Raymond Kigosi Ray akifanya vitu vyake katika kusakata mayenu. |
![]() |
| Wema Sepetu akinyonga viuono mbele ya mashabiki wa tamasha la Serengeti Fiesta uuwanja wa mjini Jamhuri Dodoma |

Rachel na mmoja wa wanenguaji wake jukwaani.
![]() |
| Rachel akifanya vitu vyake jukwaani |
Msanii w a muziki wa kizazi kipya Bongofleva Ommy Dimpoz akifanya vitu vyake kwenye Tamasha la Serengeti Fiesta 2012 katika uwanja wa Jamhuri Mjini Dodoma
Msanii Richa Mavoko akionyesha uwezo wake jukwaani katika tamasha la Serengeti Fiesta linalofanyika musiku huu kwenye uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma.
Richa Mavoko akiwaimbisha mashabiki wake
Mtangazaji wa kituo cha rediao cha Clouds FM Gea Habib akiwa pamoja na wadau wengine wa fiesta kwenye uwanja wa jamhuri usiku huu katika tamasha la Serengeti Fiesta 2012.
Mashabiki wakiwashangilia
Msanii Diana kutoka THT akiimba katika tamasha hilo usiku huu kwenye uwanja wa Jamhuri.
Subscribe to:
Posts (Atom)





























































