Tuesday, July 10, 2012

Rais wa Chama cha Madaktari Afikishwa Mahakamani Leo

Rais wa Chama cha madaktari Tanzania MAT Dr Namala Nkopi hii leo amefikishwa katika mahakama ya hakim kazi kisutu kujibu mashtaka yanayohusiana na mgomo wa madaktari.

Kwa mujibu hakimu anayesikiliza kesi hiyo Faisal Kahama, Dr Mkopi amesomewa mashtaka 2 ambayo ni
1) Kutotii amri ya mahakama ya kutangaza kusitisha mgomo
2) kuhamasisha mgomo

Hata hivyo mshtakiwa amekana mashitaka hayo na kuachiwa kwa dhamana ya watu wawili ambao ni watumishi wa serikali wakiwa na vitambulisho vya kazi na shillingi laki 5 kila mmoja.

Mawakili wa serikali walipinga masharti hayo na kuomba Hakim aongeze masharti ikiwa ni pamoja na Dr Nkopi kusalimisha hati yake ya kusafiria lakini hakim aliyakataa maombi hayo na kusisitiza kuwa maamuzi aliyoyafanya yatabaki kama yalivyo.

No comments: