Thursday, August 16, 2012
KAULI YA KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI KUHUSU MAJINA YA WALIOWEKA FEDHA USWIS.
Kambi rasmi ya upinzani bungeni imesema italazimika kuweka wazi taarifa na majina ya watu wenye umiliki wa fedha katika benki nchini Uswis zinazofikia bilioni 315.5 kama serikali haitatoa hizo taarifa.
Waziri kivuli na msemaji mkuu wa kambi rasmi ya upinzani bungeni Wizara ya fedha na uchumi Zitto Kabwe amesema hizo fedha zililipwa na makampuni ya utafutaji mafuta na gesi kwenye pwani ya mkoa wa Mtwara, kampuni ambazo zilipewa mikataba kati ya mwaka 2004 na 2006.
Nimemkariri Zitto akiongea bungeni kwamba “kambi rasmi ya upinzani bungeni imepata taarifa kuwa mmoja wa viongozi wa juu kabisa wa Tanzania na baadhi ya mawaziri wa serikali ya awamu zilizopita ni miongoni mwa wamiliki wa fedha hizi, sehemu kubwa ya fedha zililipwa na kampuni za utafutaji wa mafuta na gesi katika pwani ya mkoa wa Mtwara zilizopewa mikataba kati ya mwaka 2004 na 2006, kambi rasmi ya upinzani inaitaka serikali kutoa taarifa rasmi ya hatua gani ambayo imechukua mara baada ya kutolewa kwa taarifa kutoka benki ya taifa ya Uswis, tunaitaka serikali kuliambia taifa hatua itakazochukua kurejesha fedha hizi na nyingine zozote zilizofichwa ughaibuni”
Kuhusu ishu ya mjadala kuhusu kampuni ya BAE system ya Uingereza, Mh Zitto amesema “ukilinganisha fedha iliyorejeshwa kama chenchi ya rada na fedha ambayo Tanzania iliilipa benki ya Barclays, je chenchi ya rada ilikua na thamani yoyote kifedha? mjadala wa ununuzi wa rada hauwezi kuisha kwa kufurahia kurejesha chenchi tu, mjadala huu bado mbichi kabisa kwani tunataka ukweli mtupu uelezwe kwa umma na kuona taifa lilipata hasara kiasi gani kwa ufisadi huu wa kimataifa na hatua stahiki za kisheria kuchukuliwa dhidi ya wote walioliingizia taifa hasara”
Baada ya Zitto Kabwe kumaliza kuwasilisha, Mbunge wa Simanjiro (CCM) Christopher Ole Sendeka aliomba mwongozo kwa spika na kusema “tuhuma hii ni kubwa sana nilitaka kuomba mwongozo wako kwamba nani abebe mzigo huu, ni Zitto ataje majina ya wanaohusika au serikali iwataje hao wanaohusika katika utoroshaji wa fedha hizo ambazo zimeenda ughaibuni ili kila mmoja abebe msalaba wake pale itakapothibitika kwamba fedha za wananchi wa Tanzania zimepelekwa nje ya nchi bila kufata taratibu za kisheria”
Waziri kivuli na msemaji mkuu wa kambi rasmi ya upinzani bungeni Wizara ya fedha na uchumi Zitto Kabwe amesema hizo fedha zililipwa na makampuni ya utafutaji mafuta na gesi kwenye pwani ya mkoa wa Mtwara, kampuni ambazo zilipewa mikataba kati ya mwaka 2004 na 2006.
Nimemkariri Zitto akiongea bungeni kwamba “kambi rasmi ya upinzani bungeni imepata taarifa kuwa mmoja wa viongozi wa juu kabisa wa Tanzania na baadhi ya mawaziri wa serikali ya awamu zilizopita ni miongoni mwa wamiliki wa fedha hizi, sehemu kubwa ya fedha zililipwa na kampuni za utafutaji wa mafuta na gesi katika pwani ya mkoa wa Mtwara zilizopewa mikataba kati ya mwaka 2004 na 2006, kambi rasmi ya upinzani inaitaka serikali kutoa taarifa rasmi ya hatua gani ambayo imechukua mara baada ya kutolewa kwa taarifa kutoka benki ya taifa ya Uswis, tunaitaka serikali kuliambia taifa hatua itakazochukua kurejesha fedha hizi na nyingine zozote zilizofichwa ughaibuni”
Kuhusu ishu ya mjadala kuhusu kampuni ya BAE system ya Uingereza, Mh Zitto amesema “ukilinganisha fedha iliyorejeshwa kama chenchi ya rada na fedha ambayo Tanzania iliilipa benki ya Barclays, je chenchi ya rada ilikua na thamani yoyote kifedha? mjadala wa ununuzi wa rada hauwezi kuisha kwa kufurahia kurejesha chenchi tu, mjadala huu bado mbichi kabisa kwani tunataka ukweli mtupu uelezwe kwa umma na kuona taifa lilipata hasara kiasi gani kwa ufisadi huu wa kimataifa na hatua stahiki za kisheria kuchukuliwa dhidi ya wote walioliingizia taifa hasara”
Baada ya Zitto Kabwe kumaliza kuwasilisha, Mbunge wa Simanjiro (CCM) Christopher Ole Sendeka aliomba mwongozo kwa spika na kusema “tuhuma hii ni kubwa sana nilitaka kuomba mwongozo wako kwamba nani abebe mzigo huu, ni Zitto ataje majina ya wanaohusika au serikali iwataje hao wanaohusika katika utoroshaji wa fedha hizo ambazo zimeenda ughaibuni ili kila mmoja abebe msalaba wake pale itakapothibitika kwamba fedha za wananchi wa Tanzania zimepelekwa nje ya nchi bila kufata taratibu za kisheria”
KITU ALICHOKIFANYA RAIS MUSEVEN KWA MGANDA ALIESHINDA OLYMPIC,
Kiprotich ambae ni askari magereza alieshinda kwenye mbio za wanaume jumapili iliyopita ndani ya Olypic 2012, amezawadiwa cheki ya dola za kimarekani elfu 80 ambazo zimetolewa na Rais Yoweri Museveni ambae pia amempandisha cheo mara tisa kwenye kazi yake ya uaskari Magereza.
Standard Media wameripoti kwamba mzigo ulikua mzito manake watu walipanga foleni kumpokea Stephen huko Entebbe akiwa amebebwa kwenye gari ambalo lilikua na plate namba iliyoandikwa UG GOLD.
Nyumba aliyokua akiishi Stephen.
Watu walikua wengi mpaka waliziba njia ambapo magari yaliyokua kwenye msafara yalikosa pa kupita wakati yakielekea ikulukumpeleka Stephen kunywa chai asubuhi na Rais Museveni.
Baada ya Kiprotich kupewa cheki yake ya dola elfu 80, alimuomba rais Museveni kuwajengea wazazi wake nyumba kaskazini mashariki mwa Uganda ambapo rais Museveni amekubali kujenga hiyo nyumba ya vyumba vitatu.
Kwenye line nyingine ni kwamba rais Museven ameahidi kwamba katika muda ujao, mwanamichezo yoyote wa Uganda atakaeshinda medali ya kimataifa, atakua analipwa shilingi shilingi milioni moja za Uganda kila mwezi.
Wednesday, August 15, 2012
HOTUBA YA WAZIRI KIVULI NA MSEMAJI MKUU WA KAMBI RASMI YA UPINZANI WIZARA YA FEDHA NA UCHUMI NDUGU KABWE ZUBERI ZITTO KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA WIZARA KWA MWAKA WA FEDHA 2012/2013
1.0 UTANGULIZI
Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Kanuni za Bunge kanuni ya 99(7), toleo la mwaka 2007 na kwa niaba ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni,napenda kuwasilisha maoni ya Kambi Rasmi ya Upinzani kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Mafungu ya Wizara ya Fedha – Fungu 50 Wizara ya Fedha, Fungu 21 Hazina, Fungu 22 Deni la Taifa na Fungu 23 Ofisi ya Mhasibu Mkuu wa Serikali. Vile vile Fungu 10 Tume ya Pamoja ya Fedha na Fungu 13 Kitengo cha Udhibiti wa Fedha Haramu na Ufadhili wa Ugaidi.
Mheshimiwa Spika, mafungu yote yaliyo chini ya Wizara ya Fedha yanaomba kuidhinishiwa na Bunge lako tukufu jumla ya shilingi Bilioni 4,208 (trilioni 4.2) ili yaweze kutekeleza majukumu yake. Mafungu haya maombi yake ya Fedha ni sawa na asilimia 28 ya Bajeti nzima ya Serikali ya mwaka wa Fedha 2012/13.
Mheshimiwa Spika, Wizara ya Fedha ndiyo msimamizi mkuu wa Uchumi wa nchi ikitekeleza majukumu mbalimbali ikiwemo, kusimamia ukusanyaji wa mapato ya ndani na ya nje, kusimamia matumizi ya Serikali, kusimamia utendaji wa Taasisi na Mashirika ya Umma, kusimamia manunuzi ya Serikali na Taasisi na Mashirika ya Umma,
kusimamia Deni la Taifa na dhamana za Serikali, kutafuta suluhisho na kusimamia mfumo wa kodi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano na kupambana na Fedha haramu. Sambamba na hayo ni kusimamia na kutekeleza mpango wa kupunguza umasikini nchini kupitia utekelezaji wa MKUKUTA II.
Mheshimiwa Spika, Wizara ya Fedha na mafungu yote yaliyo chini yake ndio moyo wa Serikali na hivyo ni lazima kuitazama Wizara hii kwa jicho kali na kutilia mashaka kila jambo ambalo inalifanya ili kuhakikisha kuwa moyo huu hausimami maana madhara yake ni kwa taifa zima na watu wake. Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kupitia Waziri Kivuli wa Fedha inatekeleza wajibu huu kwa Uzalendo, Uadilifu na kwa misingi ya Uwajibikaji. Tumetekeleza wajibu huu na tunaendelea kuutekeleza bila kujali maneno na kuweka maslahi ya Taifa letu mbele ya kila kitu kingine. Maslahi ya Taifa ni zaidi ya vyama vya siasa, mahala tunapotoka au dini tunazoamini. Maslahi ya Taifa ni kwa ajili ya Watazania na hasa Watanzania milioni 30 (The Bottom 30M) ambao bado wanaishi katika ufukara mkubwa sana wakikosa huduma muhimu za jamii na wanaoishi vijijini ambapo hakuna umeme, barabara hazipitiki na wanahangaika kutwa kutafuta maji safi na salama. Maslahi ya Taifa sio faida ya wachache wenye kuishi mijini au wanasiasa wanaotafuta ushawishi kwa umma bila kujali matakwa ya Umma. Watanzania wanyonge wa vijijini wanajua maslahi yao ni nini. Wanajua kina nani wanapigania maslahi ya Wanyonge.
Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Kanuni za Bunge kanuni ya 99(7), toleo la mwaka 2007 na kwa niaba ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni,napenda kuwasilisha maoni ya Kambi Rasmi ya Upinzani kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Mafungu ya Wizara ya Fedha – Fungu 50 Wizara ya Fedha, Fungu 21 Hazina, Fungu 22 Deni la Taifa na Fungu 23 Ofisi ya Mhasibu Mkuu wa Serikali. Vile vile Fungu 10 Tume ya Pamoja ya Fedha na Fungu 13 Kitengo cha Udhibiti wa Fedha Haramu na Ufadhili wa Ugaidi.
Mheshimiwa Spika, mafungu yote yaliyo chini ya Wizara ya Fedha yanaomba kuidhinishiwa na Bunge lako tukufu jumla ya shilingi Bilioni 4,208 (trilioni 4.2) ili yaweze kutekeleza majukumu yake. Mafungu haya maombi yake ya Fedha ni sawa na asilimia 28 ya Bajeti nzima ya Serikali ya mwaka wa Fedha 2012/13.
Mheshimiwa Spika, Wizara ya Fedha ndiyo msimamizi mkuu wa Uchumi wa nchi ikitekeleza majukumu mbalimbali ikiwemo, kusimamia ukusanyaji wa mapato ya ndani na ya nje, kusimamia matumizi ya Serikali, kusimamia utendaji wa Taasisi na Mashirika ya Umma, kusimamia manunuzi ya Serikali na Taasisi na Mashirika ya Umma,
kusimamia Deni la Taifa na dhamana za Serikali, kutafuta suluhisho na kusimamia mfumo wa kodi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano na kupambana na Fedha haramu. Sambamba na hayo ni kusimamia na kutekeleza mpango wa kupunguza umasikini nchini kupitia utekelezaji wa MKUKUTA II.
Mheshimiwa Spika, Wizara ya Fedha na mafungu yote yaliyo chini yake ndio moyo wa Serikali na hivyo ni lazima kuitazama Wizara hii kwa jicho kali na kutilia mashaka kila jambo ambalo inalifanya ili kuhakikisha kuwa moyo huu hausimami maana madhara yake ni kwa taifa zima na watu wake. Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kupitia Waziri Kivuli wa Fedha inatekeleza wajibu huu kwa Uzalendo, Uadilifu na kwa misingi ya Uwajibikaji. Tumetekeleza wajibu huu na tunaendelea kuutekeleza bila kujali maneno na kuweka maslahi ya Taifa letu mbele ya kila kitu kingine. Maslahi ya Taifa ni zaidi ya vyama vya siasa, mahala tunapotoka au dini tunazoamini. Maslahi ya Taifa ni kwa ajili ya Watazania na hasa Watanzania milioni 30 (The Bottom 30M) ambao bado wanaishi katika ufukara mkubwa sana wakikosa huduma muhimu za jamii na wanaoishi vijijini ambapo hakuna umeme, barabara hazipitiki na wanahangaika kutwa kutafuta maji safi na salama. Maslahi ya Taifa sio faida ya wachache wenye kuishi mijini au wanasiasa wanaotafuta ushawishi kwa umma bila kujali matakwa ya Umma. Watanzania wanyonge wa vijijini wanajua maslahi yao ni nini. Wanajua kina nani wanapigania maslahi ya Wanyonge.
Wanafunzi 20 waliofanya vizuri katika mitihani wa kidato cha sita kwa mwaka 2012
Wanafunzi 20 waliofanya vizuri katika mitihani wa kidato cha sita kwa
mwaka 2012 wakiwa katika picha ya pamoja nje ya ukumbi wa Bunge Jana
mjini Dodoma.
Waziri Mkuu Mizengo Pinda akitoa wosia kwa wanafunzi 20 waliofanya vizuri katika mitihani ya kidato cha sita kwa mwaka 2012 bungeni jana mjini Dodoma. Wanafunzi hao 10 wasichana na 10 wavulana wamepewa cheti , kopyuta ya pakato (laptop) na fedha taslimu shilingi laki mbili kwa kila mmoja.Wanafunzi hao 10 wasichana na 10 wavulana wamepewa cheti na Waziri Mkuu, kopyuta ya pakato (laptop) na fedha taslimu shilingi laki mbili kwa kila mmoja.
WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda amewataka wanafunzi wote nchini kuwa na nidhamu , kujituma na kufuata maelekezo vizuri ya walimu wao na kuepuka makundi mabaya ili kuweza kupata mafanikio katika masomo yao.
Aidha Waziri Mkuu Pinda amewaasa wanafunzi waliofanya vizuri katika mtihani wa kuhitimu kidato cha sita wa mwaka huu kutumia uhuru vizuri watakaoupata kwenye maisha ya vyuo vya elimu ya juu bila kurudi nyuma katika maendeleo ya masomo yao.
Kauli hiyo ilitolewa jana na Waziri Mkuu, Pinda Bungeni mjini Dodoma kabla ya kuwatunuku vyeti vya kuwapongeza wanafunzi hao 19 kati 20 waliofanya vizuri katika mtihani huo,kutoka shule mbalimbali nchini, ambapo mmoja wao, Jamal Juma yuko nje ya nchi.
Wanafunzi hao ambao wote walipata ufaulu wa daraja la kwanza katika mtihani huo, saba kati yao wanatoka katika shule ya wasichana ya Marian, watatu Mzumbe, wawili Fedha na wengine wawili Kibaha. Waliobakia mmoja mmoja anatoka Kilakala, Ufundi Ifunda, Tabora girls, Tabora boys, Minaki na Mpwapwa.
“Mmefanya vizuri. Mnastahili ! Hongereni Sana. Tunataka ufaulu wenu uwe mzuri zaidi kwa vile sasa ninyi mnakweda kujenga weledi. Mnakuwa wataalamu wa fani Fulani. Tumieni muda wenu kujifunza zaidi kutafuta maarifa zaidi na kuvumbua mambo makubwa zaidi yatakayowasaidia ninyi wenywe na jamii kwa ujumla kujiletea maendeleo,” alisema Waziri Mkuu Pinda.
Aliongeza kuwa ni vizuri utaratibu huo wa kuwatambua wanafunzi bora uwe endelevu na ikiwezekana wapatiwe fursa ya kuendelezwa katika vyuo vikuu vya kipekee nje ya nchi hususan kwenye fani zitakazojenga uwezo kwa taifa.
Waziri Mkuu alisema kati ya shule 10 ,ambazo wanafunzi hao wanatoka, wawili ni kutoka shule za kata, ambao ni Ester Marcel toka shule ya sekondari ya wasichana ya Olele Kilimanjaro na Brighton Lema toka shule ya sekondari ya Kitangiri, Mwanza.
“Napenda niwape pongezi za pekee wanafunzi hawa kwa jihudi kubwa walizozionesha. Kufaulu kwao kunadhihirisha kwamba shule hizi za kata tukiweka bidii kwa kuziwezesha zaidi zitafanya vizuri zaidi kama ilivyo katika shule nyingine,” alisisitiza .
Waziri Mkuu pia aliwataka walimu wote nchini kushirikiana na wazazi na serikali kwa pamoja kufundisha watoto kwa bidii ili waweze kufanya vizuri katika masomo yao kama wanafunzi hao waliotunukiwa vyeti hivyo.
Kwa upande wake Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa alisema wanafunzi hao watazawadiwa pakato (laptop) na sh. 200,000, pia kila shule iliyotoa mwanafunzi bora itazawadiwa sh. milioni moja katika hafla maalum itakayofanyika jioni.
Wanafunzi hao wanatoka katika mchepuo wa PCM ambao ni 16 na mmojammoja toka mchepuo wa PGM, CBA, ECA na HKL.
Naye Spika wa Bunge la Jamhuri, Anna Makinda aliwataka wanafunzi hao kuwa makini na makundi kwa kuyasilikiza huku wakitumia akili zao huku akitoa changamoto shule nyingine kujitahidi kufanya vizuri.
Picha na Anna Nkinda – Maelezo
Waziri Mkuu Mizengo Pinda akitoa wosia kwa wanafunzi 20 waliofanya vizuri katika mitihani ya kidato cha sita kwa mwaka 2012 bungeni jana mjini Dodoma. Wanafunzi hao 10 wasichana na 10 wavulana wamepewa cheti , kopyuta ya pakato (laptop) na fedha taslimu shilingi laki mbili kwa kila mmoja.Wanafunzi hao 10 wasichana na 10 wavulana wamepewa cheti na Waziri Mkuu, kopyuta ya pakato (laptop) na fedha taslimu shilingi laki mbili kwa kila mmoja.
WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda amewataka wanafunzi wote nchini kuwa na nidhamu , kujituma na kufuata maelekezo vizuri ya walimu wao na kuepuka makundi mabaya ili kuweza kupata mafanikio katika masomo yao.
Aidha Waziri Mkuu Pinda amewaasa wanafunzi waliofanya vizuri katika mtihani wa kuhitimu kidato cha sita wa mwaka huu kutumia uhuru vizuri watakaoupata kwenye maisha ya vyuo vya elimu ya juu bila kurudi nyuma katika maendeleo ya masomo yao.
Kauli hiyo ilitolewa jana na Waziri Mkuu, Pinda Bungeni mjini Dodoma kabla ya kuwatunuku vyeti vya kuwapongeza wanafunzi hao 19 kati 20 waliofanya vizuri katika mtihani huo,kutoka shule mbalimbali nchini, ambapo mmoja wao, Jamal Juma yuko nje ya nchi.
Wanafunzi hao ambao wote walipata ufaulu wa daraja la kwanza katika mtihani huo, saba kati yao wanatoka katika shule ya wasichana ya Marian, watatu Mzumbe, wawili Fedha na wengine wawili Kibaha. Waliobakia mmoja mmoja anatoka Kilakala, Ufundi Ifunda, Tabora girls, Tabora boys, Minaki na Mpwapwa.
“Mmefanya vizuri. Mnastahili ! Hongereni Sana. Tunataka ufaulu wenu uwe mzuri zaidi kwa vile sasa ninyi mnakweda kujenga weledi. Mnakuwa wataalamu wa fani Fulani. Tumieni muda wenu kujifunza zaidi kutafuta maarifa zaidi na kuvumbua mambo makubwa zaidi yatakayowasaidia ninyi wenywe na jamii kwa ujumla kujiletea maendeleo,” alisema Waziri Mkuu Pinda.
Aliongeza kuwa ni vizuri utaratibu huo wa kuwatambua wanafunzi bora uwe endelevu na ikiwezekana wapatiwe fursa ya kuendelezwa katika vyuo vikuu vya kipekee nje ya nchi hususan kwenye fani zitakazojenga uwezo kwa taifa.
Waziri Mkuu alisema kati ya shule 10 ,ambazo wanafunzi hao wanatoka, wawili ni kutoka shule za kata, ambao ni Ester Marcel toka shule ya sekondari ya wasichana ya Olele Kilimanjaro na Brighton Lema toka shule ya sekondari ya Kitangiri, Mwanza.
“Napenda niwape pongezi za pekee wanafunzi hawa kwa jihudi kubwa walizozionesha. Kufaulu kwao kunadhihirisha kwamba shule hizi za kata tukiweka bidii kwa kuziwezesha zaidi zitafanya vizuri zaidi kama ilivyo katika shule nyingine,” alisisitiza .
Waziri Mkuu pia aliwataka walimu wote nchini kushirikiana na wazazi na serikali kwa pamoja kufundisha watoto kwa bidii ili waweze kufanya vizuri katika masomo yao kama wanafunzi hao waliotunukiwa vyeti hivyo.
Kwa upande wake Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa alisema wanafunzi hao watazawadiwa pakato (laptop) na sh. 200,000, pia kila shule iliyotoa mwanafunzi bora itazawadiwa sh. milioni moja katika hafla maalum itakayofanyika jioni.
Wanafunzi hao wanatoka katika mchepuo wa PCM ambao ni 16 na mmojammoja toka mchepuo wa PGM, CBA, ECA na HKL.
Naye Spika wa Bunge la Jamhuri, Anna Makinda aliwataka wanafunzi hao kuwa makini na makundi kwa kuyasilikiza huku wakitumia akili zao huku akitoa changamoto shule nyingine kujitahidi kufanya vizuri.
Picha na Anna Nkinda – Maelezo

Mabaki ya Helikopta mbili za Uganda ambazo ziliripotiwa kutoweka siku ya Jumapili zimepatikana mashambani nchini kenya.
Kanali Cyrus Oguna ambae ni msemaji wa jeshi la Kenya amesema hatma ya watu 14 waliokuwemo ndani ya chombo hicho haijulikani.
Ndege hizo mbili zilikuwa ni sehemu ya vifaa vilivyokuwa vikipelekwa nchini Somalia kuongezea nguvu kikosi cha umoja wa Afrika kilichoko huko.
Helikopta ya tatu ambayo pia ilikuwa katika msafari huo ilitua kwa ghafla katika eneo la mlima Kenya siku ya Jumapili.
Kanali Oguna amesema wote waliokuwa katika helikopta hiyo ya tatu waliokolewa.
Ni helikopta moja peke yake ndio faulu kutua vizuri na kuongeza mafuta katika mji wa Garissa ulioiko kaskzzini mwa Kenya.
Helikopta hizo nne ambazo zimetengezezwa Urusi ziliondoka siku ya Jumapili Uganda zikelekea Somalia kabla ya kukumbwa na mkasa huo.
Masalia ya helikopta hizo mbili ambazo awali ziliripotiwa kutoweka zilionekana juu ya mlima Kenya na maafisa wa Shirika la Wanyama pori, limeripoti gazeti la Daily Nation la Kenya.
Msemaji wa jeshi Kanali Oguna ameimbia BBC kwamba kikosi cha jeshi la Kenya linaelekea katika eneo hilo la Mlima Kenya , ambao ndio mlima wapili kwa urefu ,afrika.
Afisa huyo amefafanua kwamba moja ya helikopta hizo imeharibika kabisa ilhali ya pili imeharibika kiasi.
Helikpta hizo zilikuwa zinaelekea nchini Somalia kuongezea nguvu vikosi vya Umoja wa Afrika ambavyo vinajitayarisha kuvamia mji wa Kismayo na kuwafurusha wapiganaji wa Al Shabaab toka mji huo ambyo ndio ngome yao kuu.
Chanzo: http://www.bbc.co.uk/swahili
Polisi: Tuko Tayari Kumlinda Ulimboka
HOFU YATANDA NYUMBANI KWAKE, MILANGO YATIWA KUFULI
JESHI la Polisi limesema liko tayari kumlinda kiongozi wa Jumuiya ya Madaktari Tanzania, Dk Steven Ulimboka iwapo atahitaji ulinzi huo.Kauli hiyo imekuja siku mbili tangu daktari huyo wa magonjwa ya binadamu arejee nchini, huku usiri ukiwa umetawala taarifa zake kutokana na kutokuwapo kwa ndugu, jamaa au rafiki aliyekuwa tayari kusema chochote kumhusu.
“Nitachoweza kusema ni kwamba nashukuru mwanangu amerejea salama, lakini siwezi kusema chochote kuhusu mambo yanayomuhusu yeye,” alisema baba mzazi wa Dk Ulimboka, Mzee Mwaitenda.
Tofauti na juzi ambapo nyumbani kwake kulikuwa na watu kadhaa akiwamo Mweitenda, jana mageti yote ya nyumba hiyo iliyoko eneo la Kibangu, Manispaa ya Kinondoni, Dar es Salaam, yalifungwa na hapakuwa na mtu yeyote ndani.
Katikati ya hofu hiyo ya usalama, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Charles Kenyela alisema Jeshi lake haliwezi kutoa ulinzi kwa Dk Ulimboka bila yeye mwenyewe kuomba.
"Kwanza walishaamua (madaktari) kuchagua ulinzi, sisi tufanyeje? Atakapoona kuna ulazima atatujulisha," alisema Kenyela na kuongeza;
"Hatuwezi kupeleka askari bila kuombwa. Ukipeleka halafu akasema hawahitaji, itakuwa embarrasing (fedheha) sana. Sisi tunajua amerudi na tunamtakia heri aendelee vizuri, apone na aungane na wenzake,"
Kamanda Kenyela alifafanua kuwa nyumbani kwa mtu ni eneo la faragha ambalo polisi hawawezi kwenda bila kuombwa na kufanya hivyo, ni kitu kisichokubalika.
"Mimi kama kamanda sijapokea ombi lolote kutoka kwa Ulimboka wala kusikia tishio lolote dhidi ya usalama wake. Akiona kuna haja ya kulindwa, aseme tutakwenda," alisema.
Awali Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleman Kova alisema hawezi kuzungumzia ulinzi wa Dk Ulimboka kwa sababu tayari madaktari waliomba ulinzi UN.
UN wagoma kuongea
Msemaji wa Mwakilishi Mkazi wa UN nchini, Hoyce Temu hakutaka kueleza endapo taasisi hiyo ya kimataifa ilikubali ombi hilo au la akisema, suala la ulinzi halipaswi kuwekwa hadharani.
Alifafanua kuwa iwapo suala hilo litawekwa hadharani ni sawa na kuwapa nafasi maadui kujua namna mipango ya ulinzi ilivyopangwa.
"Suala la security (usalama) kama lilivyo si suala la kuwekwa wazi kwa public (umma)," alisema Temu.
Mwanzoni mwa Julai mwaka huu, Chama cha Madaktari Tanzania (MAT) kiliomba ulinzi kutoka ofisi za Umoja wa Mataifa (UN) jijini Dar es Salaam kikieleza kuwa hakina imani na polisi.
Chama hicho kiliomba ulinzi huo baada ya kuwapo na madai kwamba kuna kikundi cha watu kimekusudia kumuua Dk Ulimboka wakati akiwa kwenye matibabu nchini Afrika Kusini.
Katibu Mkuu wa MAT, Dk Rodrick Kabangila alipoulizwa endapo UN ilikubali kutoa ulinzi kwa Dk Ulimboka alijibu "haikuwa lazima kwa UN kutujibu."
Aliongeza, "Sisi tuliwasilisha barua, tukitoa malalamiko yetu, namna gani watafanya kazi ya ulinzi siyo lazima watujibu, wao wanataratibu zao za kufanya kazi."
Daktari wake anena
Profesa Joseph Kahamba alisema hajaonana na Dk Ulimboka tangu arejee nchini Jumapili ila anaamini anaendelea vizuri.Alipoulizwa imekuaje hajaonana na mgonjwa wake wakati yeye ndiye aliyemwandikia rufaa ya kutibiwa nje ya nchi alisema, "Siyo ajabu".
Alisema siyo lazima daktari aliyemwandikia mgonjwa rufaa ya kwenda kutibiwa nje ya nchi kuwasiliana naye anaporudi kwa kuwa hili linategemea hali aliyonayo mgonjwa husika.
"Hapa kuna mambo mawili; kuna kurudi akitakiwa tena kulazwa na kurudi kwa maana ya kupona," alieleza Profesa Kahamba baada ya kuulizwa kama ni lazima daktari aliyetoa rufaa awasiliane na mgonjwa baada ya kurudi kwenye matibabu.
Aliendelea "Angerudi (Dk Ulimboka) kwa state (hali) ya kulazwa, lazima angefikia kwangu nimwone, lakini kama amepona, anaweza kwenda kusalimia ndugu na kunywa bia kwanza halafu baada ya siku, wiki au mwezi akaja nikaonana naye."
Profesa Kahamba alieleza "Tangu Ulimboka arudi sijaonana naye zaidi ya kufanya mawasiliano na wenzake kwenye simu ila amepona kwa kuwa hajarudi kwangu."
MAT: Mwacheni apumzike
MAT kimewataka waandishi wa habari kutoendelea kumfuatilia Dk Ulimboka ambaye ni kiongozi wa jumuiya hiyo kwa kile walichoeeleza anatakiwa kupata fursa ya kupumzika.Makamu wa Rais wa MAT, Dk Prinus Saidia alipotakiwa kueleza ni lini atajitokeza hadharani kufuta kiu ya Watanzania kuhusu kilichomsibu, alisema:“Yeye mwenyewe ametuomba tumwache apumuzike kwa muda na sisi tumeona hili ni sahihi. Tumemwacha kwanza hadi hapo atakapotuambia kuwa yuko tayari kuungana nasi.”
Dk Saidia alisema madaktari kwa umoja wao wamefurahi kuona Dk Ulimboka amerejea akiwa mzima na kwamba hilo ndilo jambo bora zaidi kuliko kitu kingine chochote kwa sasa.
“Tunamshukuru Mungu Dk Ulimboka amerudi akiwa mzima, hili ndilo lilikuwa la msingi. Hata hivyo, suala liko wazi mgogoro baina yetu (madaktari) na Serikali haujafikia mwafaka. Inatakiwa pande zote zikae na kukubaliana na si upande mmoja kutumia nguvu,” alisema Dk Saidia.
Katika hatua nyingine habari kutoka ndani ya MAT zinasema viongozi wake wamekuwa wakifanya vikao vya ndani tangu juzi kujadili mambo mbalimbali likiwamo la kuandaa mazingira yatakayomwezesha Dk Ulimboka kuzungumza hadharani.
“Kuna vikao vinaendelea tangu jana (juzi), viongozi wanakutana kujadili mambo mbalimbali likiwamo namna Dk Ulimboka atakavyopata fursa ya kuzungumza,” kilisema chanzo hicho.
Dk Ulimboka alitekwa, kuteswa na kutupwa kwenye Msitu wa Pande nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam usiku wa kuamkia Juni 26 mwaka huu.
Chanzo: http://www.mwananchi.co.tz
Tuesday, August 14, 2012
PICHA MBALIMBALI KATIKA HARAMBEE WA M4C YA CHADEMA JIJINI DAR ZILIPATIKANA JUMLA YA TSH MILIONI 323
Mshehereshaji Bi. Rose akiendesha shughuli yenyewe.
Mwenyekiti wa hakati za Movement for Change - M4C iliyo chini ya CHADEMA Bw. Alex Mayunga akiongea machache.
Wanakamati wa hakati za Movement for Change - M4C iliyo chini ya CHADEMA wakiwa mbele ya wageni wakati mwenyekiti wao Bw. Alex Mayunga akiwatambulisha.
Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe akiingia ukumbini huku akiwa ameambatana na viongozi wenzake.
Wapambe wakiwa katika picha ya pamoja na wageni waalikwa.
Mweka hazina wa hakati za Movement for Change - M4C iliyo chini ya CHADEMA akiongea machache.
Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe akimtambulisha kwa wanaharakati Mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nasari wakati wa ufunguzi wa harambee ya Movement for Change - M4C iliyopo chini ya CHADEMA. Jumla ya shilingi Milioni 323 zimepatikana katika harambee hiyo ambapo katika hizo pesa taslimu ni shilingi milioni 70 na ahadi ni milioni 253. Hafla hiyo ya kuchangia ilifanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar.
Mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nasari
Mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nasari huku pembeni yake akiwepo Mbunge mstaafu wa Jimbo la Arusha Godbless Lema.
Mbunge mstaafu wa Jimbo la Arusha Godbless Lema.
Wanakamati wa hakati za Movement for Change - M4C iliyo chini ya CHADEMA wakiwa mbele ya wageni wakati mwenyekiti wao Bw. Alex Mayunga akiwatambulisha.
Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe akiingia ukumbini huku akiwa ameambatana na viongozi wenzake.
Wapambe wakiwa katika picha ya pamoja na wageni waalikwa.
Mweka hazina wa hakati za Movement for Change - M4C iliyo chini ya CHADEMA akiongea machache.
Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe akimtambulisha kwa wanaharakati Mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nasari wakati wa ufunguzi wa harambee ya Movement for Change - M4C iliyopo chini ya CHADEMA. Jumla ya shilingi Milioni 323 zimepatikana katika harambee hiyo ambapo katika hizo pesa taslimu ni shilingi milioni 70 na ahadi ni milioni 253. Hafla hiyo ya kuchangia ilifanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar.
Mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nasari
Mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nasari huku pembeni yake akiwepo Mbunge mstaafu wa Jimbo la Arusha Godbless Lema.
Mbunge mstaafu wa Jimbo la Arusha Godbless Lema.
Serikali kujenga hospitali teule Himo
Naibu Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Aggrey Mwanri
SERIKALI imetenga kiasi sh. milioni 400 katika kipindi cha mwaka wa fedha 2012/2013 kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali teule ya Wilaya kwenye Mji wa Himo.
Kauli hiyo imetolewa jana mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Aggrey Mwanri wakati akijibu swali la Mbunge wa Jimbo la Vunjo(TLP) Augustine Mrema lililouliza kuwa utekelezaji wa hospitali hiyo imefiki hutua gani? Na ni lini hospitali hiyo itakamilika.
Akijibu swali hilo Naibu Waziri huyo alisema Serikali kwa kutambua umuhimu wa mradi huo imetenga fedha hizo mbazo zitatumika kuanza ujenzi wa hospitali hiyo. Hivyo zabuni zilitangazwa na kufunguliwa Julai 18, mwaka huu na mchakato wa kumpta mkandrasi mpya unaendelea.
Naibu Waziri huyo aliongeza kuwa ni kusudio la seriklai kukamilisha ujenzi wa hospitali hii haraka iwezekanvyo ili kuwaondolea usumbufu wanananchi wa Vunjo.
Aidha Naibu Waziri huyo aliongeza kuwa Serikali iliamua kujenga hospitali ya Wilaya kwa kutenga fedha za ujenzi wa hospitali ya Himo katika mwaka wa fedha 2008/2009 kiasi cha sh. milioni 175. Fedha hizi zilikusudiwa kutumika katika ujenzi swa jingo la wagonjwa wan je (OPD) na kwa sasa jengo hilo, limekamilika na linatumika.
Aliongeza kuwa katika kipindi cha mwaka 2009/2010 Serikali ilitenga kiasi cha shilingi milioni 300, ambapo sh. milioni 200 zilitolewa na kupitia Mpango wa Ruzuku wa Serikali za Mitaa (LGDG) na sh. milioni 100 kupitia Mpango wa Maendeleo wa Afya Msingi (MMAM) kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya uchunguzi(X-ray), utawala, huduma ya mama na mtoto, vyoo, na uzio wa eneo la hospitali hiyo.
Alisema kazi hiyo alipewa mkandarasi Edcat International ConstructionLtd. Hivyo wakti utekelezaji ilidhihirika kuwa mknadarasi huyo alifanya kazi chini ya kiwango na halimashauri iliamua kuvunja mkataba wa kuzingatia kanuni na makubaliano
Katika swali lake la nyongeza Mrema aliuliza kuwa ni hatua gani zitachukuliwa dhidi ya mkandarasi huyo, ikiwemo miradi mingine iliyochini nya kiwango.
Akijibu swali hilo Naibu Waziri huyo alisema hatua iliyochukua ni kumsimamisha na pia watafanya tathimini ya fedha zilizotumika ili kungalia thamani yake, pia watatembelea miradi mingine na iliyochini ya kiwango ili kuwezackuchukua hatua.
Wakati huo huo, Serikali imepanga kununua gari la zimamoto kwa ajili ya kutoa huduma hiyo kwa majengo yenye urefu wa kufikia ghorofa 37, ambao ndio urefu wa mwisho wa gari hilo duniani katika kipindi cha mwaka wa fedha 2013/2014.
Taarifa hiyo imetolewa Agosti 13, 2012 bungeni Dodoma na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Pereira Silima wakati akijibu swali la Mbunge wa Mji Mkongwe, Muhammad Ibrahim Sanya (CUF) akitaka kujua ujenzi wa majengo mapya sasa unafikia ghorofa 20 unazidi kuongezeka ilhali hakuna vifaa vya kuweza kuzima moto kulingana na ujenzi huo.
Chanzo: www.thehabari.com
SERIKALI imetenga kiasi sh. milioni 400 katika kipindi cha mwaka wa fedha 2012/2013 kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali teule ya Wilaya kwenye Mji wa Himo.
Kauli hiyo imetolewa jana mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Aggrey Mwanri wakati akijibu swali la Mbunge wa Jimbo la Vunjo(TLP) Augustine Mrema lililouliza kuwa utekelezaji wa hospitali hiyo imefiki hutua gani? Na ni lini hospitali hiyo itakamilika.
Akijibu swali hilo Naibu Waziri huyo alisema Serikali kwa kutambua umuhimu wa mradi huo imetenga fedha hizo mbazo zitatumika kuanza ujenzi wa hospitali hiyo. Hivyo zabuni zilitangazwa na kufunguliwa Julai 18, mwaka huu na mchakato wa kumpta mkandrasi mpya unaendelea.
Naibu Waziri huyo aliongeza kuwa ni kusudio la seriklai kukamilisha ujenzi wa hospitali hii haraka iwezekanvyo ili kuwaondolea usumbufu wanananchi wa Vunjo.
Aidha Naibu Waziri huyo aliongeza kuwa Serikali iliamua kujenga hospitali ya Wilaya kwa kutenga fedha za ujenzi wa hospitali ya Himo katika mwaka wa fedha 2008/2009 kiasi cha sh. milioni 175. Fedha hizi zilikusudiwa kutumika katika ujenzi swa jingo la wagonjwa wan je (OPD) na kwa sasa jengo hilo, limekamilika na linatumika.
Aliongeza kuwa katika kipindi cha mwaka 2009/2010 Serikali ilitenga kiasi cha shilingi milioni 300, ambapo sh. milioni 200 zilitolewa na kupitia Mpango wa Ruzuku wa Serikali za Mitaa (LGDG) na sh. milioni 100 kupitia Mpango wa Maendeleo wa Afya Msingi (MMAM) kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya uchunguzi(X-ray), utawala, huduma ya mama na mtoto, vyoo, na uzio wa eneo la hospitali hiyo.
Alisema kazi hiyo alipewa mkandarasi Edcat International ConstructionLtd. Hivyo wakti utekelezaji ilidhihirika kuwa mknadarasi huyo alifanya kazi chini ya kiwango na halimashauri iliamua kuvunja mkataba wa kuzingatia kanuni na makubaliano
Katika swali lake la nyongeza Mrema aliuliza kuwa ni hatua gani zitachukuliwa dhidi ya mkandarasi huyo, ikiwemo miradi mingine iliyochini nya kiwango.
Akijibu swali hilo Naibu Waziri huyo alisema hatua iliyochukua ni kumsimamisha na pia watafanya tathimini ya fedha zilizotumika ili kungalia thamani yake, pia watatembelea miradi mingine na iliyochini ya kiwango ili kuwezackuchukua hatua.
Wakati huo huo, Serikali imepanga kununua gari la zimamoto kwa ajili ya kutoa huduma hiyo kwa majengo yenye urefu wa kufikia ghorofa 37, ambao ndio urefu wa mwisho wa gari hilo duniani katika kipindi cha mwaka wa fedha 2013/2014.
Taarifa hiyo imetolewa Agosti 13, 2012 bungeni Dodoma na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Pereira Silima wakati akijibu swali la Mbunge wa Mji Mkongwe, Muhammad Ibrahim Sanya (CUF) akitaka kujua ujenzi wa majengo mapya sasa unafikia ghorofa 20 unazidi kuongezeka ilhali hakuna vifaa vya kuweza kuzima moto kulingana na ujenzi huo.
Chanzo: www.thehabari.com
Bodi ya Mikopo, TCU yawaengua 3074 walioomba
BODI ya Mikopo ya Elimu ya Juu nchini pamoja na Tume ya Vyuo Vikuu nchini (TCU) imewaengua zaidi ya wanafunzi 3074 walioomba vyuo na mikopo ya elimu ya juu kwa mwaka 2012/13.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na taasisi hizo kupitia mitandao yao (website) mwezi huu (Agosti 10 na 12, 2012) zaidi ya wanafunzi 3074 wameenguliwa katika maombi yao kwa kuwa na dosari mbalimbali.
Taarifa hiyo imeeleza kuwa Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HESLB) pekee imeorodhesha zaidi ya wanafunzi 2,649 ambao imebaini kuwa na mapungufu kadhaa katika maombi yao ya kupewa mikopo ya vyuo.
Miongoni mwa makosa ama dosari ambazo bodi imezibaini kwa walioenguliwa kwa sasa ni pamoja kukosekana kwa vyeti vya kuzaliwa kwa muombaji, sahihi ya mdhamini/muombaji, kukosekana kwa picha ndogo ya muombaji/mdhamini, kukosekana kwa sahihi za viongozi wa Serikali za mitaa/vijiji kwa waombaji na nyaraka nyingine muhimu kwa waombaji.
Kwa upande wake TCU imewaengua jumla ya waombaji 425 kwa dosari na makosa mbalimbali, ambayo imeyabainisha katika taarifa yake.
Miongoni mwa dosari ambazo zimetajwa na TCU kwa wanafunzi hao ni pamoja na baadhi yao kukosea namba za vyeti vya masomo kwa vidato vya nne na tano (O’ level na A’ level Index number), miaka ya kumaliza masomo (year of completion), mawasiliano sahihi kwa muombaji (Contact information e.g. Mobile phone number, email address and postal address) pamoja na uchaguzi wa masomo (Programme selected).
Waweza kuingia katika linki hii hapo chini na kuona majina ya waliobainika kuwa na dosari anuai katika maombi yao kwa TCU http://www.tcu.go.tz/uploads/file/LIST%20OF%20APPLICANTS%20FOR%202012-2013%20ADMISSIONS%20WITH%20MISSING%20INFORMATION.pdf
Pia waweza kutembelea linki zifuatazo na kushuhudia majina ya waliobainika kuwa na dosari hizo katika maombi yao kwa bodi ya mikopo;- http://www.heslb.go.tz/index.php?option=com_content&view=article&id=365&Itemid=66 http://www.heslb.go.tz/index.php?option=com_content&view=article&id=366&Itemid=67 http://www.heslb.go.tz/index.php?option=com_content&view=article&id=367&Itemid=68
post graduate;- http://www.heslb.go.tz/index.php?option=com_content&view=article&id=363&Itemid=65
Hata hivyo taasisi hizo mbili zimetoa muda kwa walioenguliwa sasa kutokana na dosari hizo kurekebisha na kutuma tena maombi yao kupitia mitandao kwa mujibu wa maelekezo waliyotoa. Kwa taarifa zaidi pia waweza kutembelea mitandao ya www.heslb.go.tz na www.tcu.go.tz
Habari hii imeandaliwa na mtandao wa Thehabari.com (www.thehabari.com)
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na taasisi hizo kupitia mitandao yao (website) mwezi huu (Agosti 10 na 12, 2012) zaidi ya wanafunzi 3074 wameenguliwa katika maombi yao kwa kuwa na dosari mbalimbali.
Taarifa hiyo imeeleza kuwa Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HESLB) pekee imeorodhesha zaidi ya wanafunzi 2,649 ambao imebaini kuwa na mapungufu kadhaa katika maombi yao ya kupewa mikopo ya vyuo.
Miongoni mwa makosa ama dosari ambazo bodi imezibaini kwa walioenguliwa kwa sasa ni pamoja kukosekana kwa vyeti vya kuzaliwa kwa muombaji, sahihi ya mdhamini/muombaji, kukosekana kwa picha ndogo ya muombaji/mdhamini, kukosekana kwa sahihi za viongozi wa Serikali za mitaa/vijiji kwa waombaji na nyaraka nyingine muhimu kwa waombaji.
Kwa upande wake TCU imewaengua jumla ya waombaji 425 kwa dosari na makosa mbalimbali, ambayo imeyabainisha katika taarifa yake.
Miongoni mwa dosari ambazo zimetajwa na TCU kwa wanafunzi hao ni pamoja na baadhi yao kukosea namba za vyeti vya masomo kwa vidato vya nne na tano (O’ level na A’ level Index number), miaka ya kumaliza masomo (year of completion), mawasiliano sahihi kwa muombaji (Contact information e.g. Mobile phone number, email address and postal address) pamoja na uchaguzi wa masomo (Programme selected).
Waweza kuingia katika linki hii hapo chini na kuona majina ya waliobainika kuwa na dosari anuai katika maombi yao kwa TCU http://www.tcu.go.tz/uploads/file/LIST%20OF%20APPLICANTS%20FOR%202012-2013%20ADMISSIONS%20WITH%20MISSING%20INFORMATION.pdf
Pia waweza kutembelea linki zifuatazo na kushuhudia majina ya waliobainika kuwa na dosari hizo katika maombi yao kwa bodi ya mikopo;- http://www.heslb.go.tz/index.php?option=com_content&view=article&id=365&Itemid=66 http://www.heslb.go.tz/index.php?option=com_content&view=article&id=366&Itemid=67 http://www.heslb.go.tz/index.php?option=com_content&view=article&id=367&Itemid=68
post graduate;- http://www.heslb.go.tz/index.php?option=com_content&view=article&id=363&Itemid=65
Hata hivyo taasisi hizo mbili zimetoa muda kwa walioenguliwa sasa kutokana na dosari hizo kurekebisha na kutuma tena maombi yao kupitia mitandao kwa mujibu wa maelekezo waliyotoa. Kwa taarifa zaidi pia waweza kutembelea mitandao ya www.heslb.go.tz na www.tcu.go.tz
Habari hii imeandaliwa na mtandao wa Thehabari.com (www.thehabari.com)
Subscribe to:
Posts (Atom)










































