MBUNGE wa Kawe, Halima Mdee amewasilisha hoja binafsi bungeni akiitaka Serikali kusitisha ugawaji wa ardhi hadi tathmini ifanyike, huku akimtuhumu Waziri Mkuu kuwa anashiriki katika kuwakumbatia wawekezaji wanaopora ardhi wananchi.
Mdee amesema kuwa bila kufanya hivyo, ardhi yote ya nchi hii itachukuliwa na wawekezaji huku wananchi wakiachwa masikini.
Akiwasilisha bungeni hoja binafsi kuhusu kusitishwa ugawaji ardhi nchini, Mdee aliitaka Serikali kusitisha ugawaji wa ardhi hadi hapo tathmini ya kina itakapofanyika kujua kiasi cha ardhi kilichopo mikononi mwa wawekezaji.
Vile vile, alitaka tathmini ya kina ifanyike kubaini raia wa kigeni na wa ndani waliojipatia ardhi kinyemela kupitia Serikali za vijiji kinyume na matakwa ya sheria ya ardhi namba 5 ya mwaka 1999.
“Kwa mujibu wa Kanuni namba 54(1), (2) na (3) ya Kanuni za Kudumu za Bunge, Toleo la 2007 naomba kutoa hoja binafsi ya kuitaka Serikali kusitisha ugawaji wa ardhi kwa wawekezaji wa ndani na wa nje mpaka hapo tathmini ya kina itakapofanyika kubaini ni kiwango gani cha ardhi kiko mikononi mwa wawekezaji,” alisema Mdee.
Alisema katika miaka ya hivi karibuni, kutokana mtikisiko wa uchumi duniani, tumeshuhudia wimbi la wawekezaji kutoka nje wakingia nchini kuwekeza katika kilimo kwa maelezo kwamba watasaidia kuinua uzalishaji katika sekta ya kilimo.
Hata hivyo, alisema uwekezaji huo wa wageni katika ardhi umegeuka kuwa shubiri kwa wananchi hususan wakulima wadogo.
Alisema wakulima hao wamekuwa wakiondolewa katika maeneo yao ya asili ili kuwapisha wageni huku wakiachwa katika lindi la umasikini mkubwa.
Mdee alisema ardhi hiyo imekuwa ikichukuliwa na Serikali kuwa haina mwenyewe au haitumiki.
“Hii inatokana na ukweli kwamba kumekuwa na tafsiri ambayo sio sahihi, kwamba ardhi wanayopewa wawekezaji haina wenyewe, haina mtu, haitumiki. Wakati ukweli ni kwamba maeneo mengi kama sio yote yalikuwa yanatumiwa na wakulima wadogo,” alisema.
Mdee alisema wawekezaji wamechukua maeneo makubwa ambayo wameshindwa kuyaendeleza na hata yale ambayo wanayaendeleza ni kwa kiasi kidogo.
Alisema baadhi ya waewekezaji wengine baada ya kumilikishwa ardhi kwa bei ya kutupa wamekuwa wakikaa nayo na baadaye kuiza kwa wawekezaji wengine.
Mdee aliliomba Bunge kukubali Serikali kusitisha ugawaji wa ardhi ili kuangalia wapi ilipokosea kwa manufaa ya nchi.
Mbunge huyo kupitia Chadema, alisema hata wizara ya ardhi na maendeleo ya makazi wakitakiwa leo kutoa taarifa sahihi ya ardhi kiasi gani iko chini ya miliki ya wageni hawana taarifa hizo.
Alisema kutokana na waewekezaji kupewa ardhi bila ya kufuata taratibu, hivi sasa migogoro mingi ya ardhi iliyopo nchini inatokana na wananchi kuporwa ardhi kwa kisingizio cha uwekezaji.
Alitoa mfano wa Kampuni ya Kigoma inayofahamika kama Agrisol na FELISA ambayo imenunua hekari 3,000 katika Kijiji cha Basanza Kata ya Uvinza wilayani ya Uvinza.
Alisema wawekezaji hao ambao wanakingiwa kifua na Waziri Mkuu, wamewakuta wakulima na wafugaji katika maeneo haya.
Alisema mwekezaji kwa kushirikiana na vyombo vya dola aliwatoa kwa nguvu wananchi akitumia askari mgambo kupiga wananchi, kuchoma nyumba, kuharibu mazao na halikadhalika kuwafungulia wananchi mashtaka.
Alitaja maeneo mengine yenye migogoro kuwa ni wananchi na wawekezaji kuwa ni Rufiji, Kilombero, Bagamoyo, Kisarawe, Muheza, Pangani, Katavi ,Meatu, Kinondoni, Njombe na Ngorogoro.
Moto wa hoja hiyo uliwafanya baadhi ya mawaziri kuinuka kuchangia akiwamo, Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi, Profesa Tibaijuka, Waziri Nchi ofisi ya Waziri Mkuu, (Uwekezaji na Uwezeshaji), Mary Nagu na Waziri wa Nchi ofisi ya Rais (Mahusiano), Steven Wassira.
Akichangia hoja hiyo, Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi, Profesa Tibaijuka alikubali kufanya marekebisho katika sheria ya ardhi ili iweze kuwanifaisha watanzania.
Alisema hakubaliani na hoja ya Mbunge Mdee ya kutaka kusitisha utoaji wa ardhi kwa wawekezaji akisema hali hiyo inaweza kuleta matatizo zaidi.
Profesa Tibaijuka alisema ni aibu kwa nchi yenye ardhi kubwa na yenye rutuba kushindwa kujitosheleza kwa chakula.
Hivyo, alisema kuwapa wageni wenye mitaji ardhi kwa ajili ya kilimo kutasaidia kuongezeka kwa uzalishaji wa mazao na hivyo kujitosheleza kwa chakula.
Profesa Tibaijuka alisema ili watanzania waweze kunufaika na uwekezaji mkubwa wa ardhi nchini, Serikali itakuwa inachukua hisa katika mshamaba hayo na kuziuza kwa wananachi.
“Serikali hii haiwezi kukukbali wananchi wake kuporwa ardhi na wawekezaji,” alisema.
Alisema anakubalina kufanyiwa marekebisho sheria hiyo ili iweze kumsiadia mwananchi.
Waziri Nagu, alisema hatuwezi kusitisha uwekezaji kwa wageni kwa sababu itasabisha kurudisha nyuma maendeleo katika sekta ya kilimo.
Chanzo: http://www.mwananchi.co.tz/habari/siasa
Saturday, November 10, 2012
Friday, November 9, 2012
Dk Mwinyi Atembelea Vituo Vya Uchunguzi Na Matibabu Vinavyojengwa Mkoani Dodoma
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Hussein Mwinyi akiwasili katika eneo la Ujenzi wa kituo cha kisasa cha Matibabu mkoani Dodoma.
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Hussein Mwinyi (kulia) akizungumza kabla ya kukagua ujenzi wa Kituo cha Kisasa cha uchunguzi na Matibabu katika Chuo Kikuu cha Dodoma kinachonjengwa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya.
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Hussein Mwinyi (kushoto) akiwa na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, Dk. Emmanuel Humba baada ya kukagua ujenzi wa Kituo cha Mfano cha Uchunguzi na Matibabu katika Hospitali ya Mkoa wa Dodoma kinachojengwa na Mfuko huo.
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Hussein Mwinyi (kulia) akizungumza kabla ya kukagua ujenzi wa Kituo cha Kisasa cha uchunguzi na Matibabu katika Chuo Kikuu cha Dodoma kinachonjengwa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya.
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Hussein Mwinyi (kushoto) akiwa na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, Dk. Emmanuel Humba baada ya kukagua ujenzi wa Kituo cha Mfano cha Uchunguzi na Matibabu katika Hospitali ya Mkoa wa Dodoma kinachojengwa na Mfuko huo.
TAARIFA KWA UMMAUzinduzi Wa Shindano La Kusaka Mabingwa Wa Kero Kwa Wateja
Uzinduzi wa Shindano la Kusaka Mabingwa wa Kero kwa Wateja
Jumuiya ya watumiaji wa huduma mbalimbali nchini kupitia mitandao ya kijamii ya Facebook na Twitter imezindua rasmi shindano la kusaka kampuni zinazotoa huduma na bidhaa mbovu kwa wateja nchini Tanzania.
Jumuiya hiyo inawajumuisha watu wa kada mbalimbali wakiwemo wanasheria, wanaharakati, waandishi wa habari, viongozi wa kisiasa, wafanyabiashara na wateja wa huduma na bidhaa mbalimbali nchini Tanzania.
Lengo la jumuiya hiyo ni kushinikiza wafanyabiashara nchini kutoa huduma na bidhaa bora kwa wateja na kuwakumbusha umuhimu wa wateja. Kauli mbiu ya wanajumuiya hao ni Mteja ni Mfalme.
Katika wiki ya kwanza tangu jumuiya hiyo kuzinduliwa jumla ya makampuni 21 yameingizwa katika shindano hilo kwa wateja wao kuwasilisha malalamiko yao. Kwa taarifa zaidi kuhusu ni fuatilia akaunti ya Twitter @hudumambayatz au kundi la Facebook linalojulikana kama HUDUMA BONGO.
Ili kuweza kupiga kura yako unahitajika kuwa na akaunti hai (yenye mawasiliano mara kwa mara) katika mtandao wa Twitter au Facebook na kujiunga na jumuiya hiyo. Mara tu utakapowasilisha kero yako utaifanya kampuni unayoilalamikia kuingia katika mchuano mkali wa kumsaka bingwa wa huduma mbovu kwa wateja nchini.
Huduma Bongo inatoa wito kwa makampuni yote kuboresha huduma na bidhaa zao ili kuweza kuwapatia wateja kilicho bora zaidi katika soko hili la ushindani.
Imetolewa na Mshauri wa Habari wa Huduma Bongo - hudumabongo@gmail.com
Novemba 9, 2012
Jumuiya ya watumiaji wa huduma mbalimbali nchini kupitia mitandao ya kijamii ya Facebook na Twitter imezindua rasmi shindano la kusaka kampuni zinazotoa huduma na bidhaa mbovu kwa wateja nchini Tanzania.
Jumuiya hiyo inawajumuisha watu wa kada mbalimbali wakiwemo wanasheria, wanaharakati, waandishi wa habari, viongozi wa kisiasa, wafanyabiashara na wateja wa huduma na bidhaa mbalimbali nchini Tanzania.
Lengo la jumuiya hiyo ni kushinikiza wafanyabiashara nchini kutoa huduma na bidhaa bora kwa wateja na kuwakumbusha umuhimu wa wateja. Kauli mbiu ya wanajumuiya hao ni Mteja ni Mfalme.
Katika wiki ya kwanza tangu jumuiya hiyo kuzinduliwa jumla ya makampuni 21 yameingizwa katika shindano hilo kwa wateja wao kuwasilisha malalamiko yao. Kwa taarifa zaidi kuhusu ni fuatilia akaunti ya Twitter @hudumambayatz au kundi la Facebook linalojulikana kama HUDUMA BONGO.
Ili kuweza kupiga kura yako unahitajika kuwa na akaunti hai (yenye mawasiliano mara kwa mara) katika mtandao wa Twitter au Facebook na kujiunga na jumuiya hiyo. Mara tu utakapowasilisha kero yako utaifanya kampuni unayoilalamikia kuingia katika mchuano mkali wa kumsaka bingwa wa huduma mbovu kwa wateja nchini.
Huduma Bongo inatoa wito kwa makampuni yote kuboresha huduma na bidhaa zao ili kuweza kuwapatia wateja kilicho bora zaidi katika soko hili la ushindani.
Imetolewa na Mshauri wa Habari wa Huduma Bongo - hudumabongo@gmail.com
Novemba 9, 2012
Akamatwa Na Sehemu Za Siri Za Mpwa Wake A. Kusini
Mwanamume mmoja nchini Afrika Kusini amekamatwa baada ya kupatikana akiwa na sehemu za siri kwenye pochi lake ambazo zinaaminika kuwa za mpwa wake ambaye hajulikani aliko.
Msemaji wa polisi, aliambia BBC kuwa babada ya kukamatwa kwake , mwanaume huyo aliwapeleka maafisa wa polisi kwenye msitu katika mkoa wa Eastern Cape, ambako mwili uliokatwakatwa ulipatikana.
Kichwa cha msichana huyo pamoja na miguu yake ilikuwa imekatwa na zilipatikana karibu na kiwiliwili chake. Mtu huyo mwenye umri wa miaka 42, anatarajiwa kufikishwa mahakamani kwa kosa la mauaji.
Mmwanaume huyo alishtakiwa baada ya kushukiwa kuhusika na kutoweka kwa msichana huyo mwenye umri wa miaka 18, aliyepotoea katika mji wa Ngcobo siku ya Jumapili.
Msemaji wa polisi, Mzukisi Fatyela alisema kuwa sehemu hizo za siri, zilipatikana ndani ya pochi lake. Alisema sababu ya kuuawa kwa msichana huyo haijulikani na kwamba uchunguzi unafanyika.
Alipoulizwa ikiwa mauaji hayo yanahusishwa na waganga ambapo sehemu za mwili wa watu hutumiwa kwenye madawa yao, bwana Fatyela alisema kuwa hawezi kubaini hilo kwa sasa. Kumekuwa na visa vingi vya kuuza sehemu za siri za watu katika sehemu nyingi za Afrika kwa sababu sawa na hizo.
Afrika Mashariki imeshuhudia visa vingi vya kuuawa kwa watu wenye ulemavu wa ngozi au maalbino, huku sehemu za miili yao zikikatwa kwa sababu za kishirikina. Mwanaume huyo anatarajiwa kufikishwa mahakamani leo.
BBC-SWAHILI
Msemaji wa polisi, aliambia BBC kuwa babada ya kukamatwa kwake , mwanaume huyo aliwapeleka maafisa wa polisi kwenye msitu katika mkoa wa Eastern Cape, ambako mwili uliokatwakatwa ulipatikana.
Kichwa cha msichana huyo pamoja na miguu yake ilikuwa imekatwa na zilipatikana karibu na kiwiliwili chake. Mtu huyo mwenye umri wa miaka 42, anatarajiwa kufikishwa mahakamani kwa kosa la mauaji.
Mmwanaume huyo alishtakiwa baada ya kushukiwa kuhusika na kutoweka kwa msichana huyo mwenye umri wa miaka 18, aliyepotoea katika mji wa Ngcobo siku ya Jumapili.
Msemaji wa polisi, Mzukisi Fatyela alisema kuwa sehemu hizo za siri, zilipatikana ndani ya pochi lake. Alisema sababu ya kuuawa kwa msichana huyo haijulikani na kwamba uchunguzi unafanyika.
Alipoulizwa ikiwa mauaji hayo yanahusishwa na waganga ambapo sehemu za mwili wa watu hutumiwa kwenye madawa yao, bwana Fatyela alisema kuwa hawezi kubaini hilo kwa sasa. Kumekuwa na visa vingi vya kuuza sehemu za siri za watu katika sehemu nyingi za Afrika kwa sababu sawa na hizo.
Afrika Mashariki imeshuhudia visa vingi vya kuuawa kwa watu wenye ulemavu wa ngozi au maalbino, huku sehemu za miili yao zikikatwa kwa sababu za kishirikina. Mwanaume huyo anatarajiwa kufikishwa mahakamani leo.
BBC-SWAHILI
Uongozi Wa Sauti Za Busara Wakana Kumdhulumu Bi Kidude
Mkurugenzi wa Sauti za Busara ZanzibarYussuf Mahmoud amesema kutokana na malalamiko yanayotolewa na familia ya Bi Fatma Baraka Khamisi (Bi Kidude) wameamua kuzikabidhi fedha za msanii huyo mkongwe alizokuwa akizihifadhi ili kuepusha migogoro zaidi.
Ameyasema hayo katika Ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo huko Kikwajuni wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kufuatia malamiko ya baadhi ya wanafamilia wa Bi Kidude wanaodai kwamba mzazi wao anaibiwa fedha zake na viongozi wa Sauti za Busara.
Mkurugenzi huyo amesema lengo la Sauti za Busara ni kuwasaidia wasanii wa Zanzibar na Afrika kwa jumla katika kuwatangaza na kuwatafutia maslahi ndani na nje ya nchi na sio kuwadhulumu kipato chao.
Amesema baada ya juhudi kubwa walizofanya kuanzia mwaka 2005 walipoanza kumsaidia Bi Kidude ikiwa ni pamoja na kumuwezesha kupata tunzo ya Womex, wamefanikiwa kukusanya shilingi milioni 36 zilizotokana na maonyesho mbali mbali yaliyosimamiwa na Sauti za busara, mauzo ya CD na mahojiano aliyofanya na vyombo vya Habari.
Ameongeza kuwa fedha hizo amekuwa akizutumia mwenyewe, kusimamia kuitengeneza nyumba yake na wamekuwa wakizitumia kwa matibabu yake anapoumwa na hivi sasa fedha zilizobakia ni shilling Millioni tatu laki sita na elfu nne (3,604,000) ambazo zimo mikononi mwake na hivyo alitaka fedha hizo azikabidhi kwa mtu wa familia ambae Bi Kidude ataridhia mwenyewe.
Hata hivyo shughuli ya kukabidhi fedha hizo kwa wanafamilia ilishindikana kutokana na wanafamilia kukataa kuhudhuria katika kikao hicho cha leo.
Mkuu wa miradi wa Sauti za Busara Janny Ramadhani amedai kuwa chanzo cha mzozo ni pale Bi Kidude alipomtambulisha mwanafamilia Baraka Abdalla kuwa ndie atakuwa dhamana wa kumchukulia fedha za kila wiki shilingi 50,000 ambazo walikubaliana lakini baadhi ya wiki kijana huyo alikuwa hazipeleki kwa Bi Kidude.
Amesema familia ya Bi Kidude imechangia kwa kiasi kikubwa katika kumuangusha mzazi wao licha ya juhudi walizokuwa wakizichukua katika kumtangaza na kumpatia safari za mara kwa mara nje na ndani ya nchi.
Viongozi hao wa Sauti za Busra wamewataka wasanii wote nchini wawe pamoja na kujenga moyo wa kushirikiana na kusaidiana ili waweze kukuza vipaji vyao na kuinua sanaa zao na kufikia maendeleo waliyokusudia.
Na: Ramadhan Ali na Mwanaisha Mohamed-Maelezo Zanzibar 09/11/2012
IMETOLEWA NA IDARA YA HABARI MAELEZO ZANZIBAR 9/11/2011
Ameyasema hayo katika Ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo huko Kikwajuni wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kufuatia malamiko ya baadhi ya wanafamilia wa Bi Kidude wanaodai kwamba mzazi wao anaibiwa fedha zake na viongozi wa Sauti za Busara.
Mkurugenzi huyo amesema lengo la Sauti za Busara ni kuwasaidia wasanii wa Zanzibar na Afrika kwa jumla katika kuwatangaza na kuwatafutia maslahi ndani na nje ya nchi na sio kuwadhulumu kipato chao.
Amesema baada ya juhudi kubwa walizofanya kuanzia mwaka 2005 walipoanza kumsaidia Bi Kidude ikiwa ni pamoja na kumuwezesha kupata tunzo ya Womex, wamefanikiwa kukusanya shilingi milioni 36 zilizotokana na maonyesho mbali mbali yaliyosimamiwa na Sauti za busara, mauzo ya CD na mahojiano aliyofanya na vyombo vya Habari.
Ameongeza kuwa fedha hizo amekuwa akizutumia mwenyewe, kusimamia kuitengeneza nyumba yake na wamekuwa wakizitumia kwa matibabu yake anapoumwa na hivi sasa fedha zilizobakia ni shilling Millioni tatu laki sita na elfu nne (3,604,000) ambazo zimo mikononi mwake na hivyo alitaka fedha hizo azikabidhi kwa mtu wa familia ambae Bi Kidude ataridhia mwenyewe.
Hata hivyo shughuli ya kukabidhi fedha hizo kwa wanafamilia ilishindikana kutokana na wanafamilia kukataa kuhudhuria katika kikao hicho cha leo.
Mkuu wa miradi wa Sauti za Busara Janny Ramadhani amedai kuwa chanzo cha mzozo ni pale Bi Kidude alipomtambulisha mwanafamilia Baraka Abdalla kuwa ndie atakuwa dhamana wa kumchukulia fedha za kila wiki shilingi 50,000 ambazo walikubaliana lakini baadhi ya wiki kijana huyo alikuwa hazipeleki kwa Bi Kidude.
Amesema familia ya Bi Kidude imechangia kwa kiasi kikubwa katika kumuangusha mzazi wao licha ya juhudi walizokuwa wakizichukua katika kumtangaza na kumpatia safari za mara kwa mara nje na ndani ya nchi.
Viongozi hao wa Sauti za Busra wamewataka wasanii wote nchini wawe pamoja na kujenga moyo wa kushirikiana na kusaidiana ili waweze kukuza vipaji vyao na kuinua sanaa zao na kufikia maendeleo waliyokusudia.
Na: Ramadhan Ali na Mwanaisha Mohamed-Maelezo Zanzibar 09/11/2012
IMETOLEWA NA IDARA YA HABARI MAELEZO ZANZIBAR 9/11/2011
Taarifa Kwa Vyombo Vya Habari...!
SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania limeteua wadau 10 kwa ajili ya kusaidia timu ya taifa ya vijana walio na umri chini ya miaka 17, Serengeti Boys itakayopambana na Congo (Brazaville) katika mechi ya raundi ya tatu ya michuano ya awali ya Mataifa ya Afrika.Uteuzi huo umefanywa na Rais wa TFF, Leodegar Tenga baada ya Kamati ya Vijana ya TFF kufanya kikao chake kujadili kwa umakini ushiriki wa timu hiyo na kupeleka mapendekezo yake kwa rais huyo wa shirikisho.
Kutokana na umuhimu wa mechi hiyo itakayoamua timu itakayofuzu kucheza fainali za Mataifa ya Afrika, TFF imeona umuhimu wa kuwa na kamati ambayo itakuwa na majukumu mawili makubwa ambayo ni:
1. Kuhamasisha vijana waone umuhimu na kuwa na ari ya kushinda mechi hiyo
2. Kuhamasisha umma uone umuhimu wa mechi hiyo na hivyo kuisaidia iweze kufuzu.
Walioteuliwa kuunda kamati hiyo ni:
1. Ridhiwani Kikwete Mwenyekiti
2. Ahmed Seif (Magari) Mjumbe
3. Nassoro Bin Slum Mjumbe
4. Henry Tandau Katibu
5. Ahmed Mgoyi Mjumbe
6. Aboubakar Bakhresa Mjumbe
7. Angetile Osiah Mjumbe
8. Kassim Dewji Mjumbe
9. Abdallah Bin Kleb Mjumbe
10. Salim Said Mjumbe
Baada ya kuvuka raundi mbili za kwanza bila ya kucheza mechi kutokana na wapinzani wake kujitoa, timu ya Serengeti Boys inahitaji kufanya kila iwezalo kuweza kuiondoa Congo kwenye mashindano hayo na kuweka rekodi ya kufuzu kucheza fainali hizo za Afrika ambazo pia zitatoa wawakilishi wa Afrika kwenye mashindano ya Kombe la Dunia.
Mechi za kwanza za raundi ya tatu zitachezwa kati ya Novemba 16 na 18, 2012 na mechi za marudiano zitachezwa kuanzia Novemba 30, 2012 hadi Desemba 2, 2012
*Kuhusu suala la Azam FC kuwasimamisha wachezaji watatu kwa tuhuma za kuhusika kuhujumu timu, tayari TFF imepokea barua hiyo ya Novemba 8, 2012 na inalishughulikia na kulifuatilia kwa makini.
*TFF inapenda kukipongeza Chama cha Mpira wa Miguu cha Mkoa wa Mwanza kwa kufanya uchaguzi wake kwa amani na kufanikiwa kupata viongozi wapya watakaokuwa chini ya uenyekiti wa Jackson Songora.
Rais wa TFF amewapongeza viongozi waliorekjea madarakani na viongozi wapya akieleza magtumaini yake kuwa kamati mpya ya Utendaji ya MRFA itaelekeza nguvu zake katika kuendeleza mikakati iliyokuwepo ya kuinua kiwango cha mpira wa miguu na kubuni mikakati mingine kwenye mkoa huo na Tanzania kwa ujumla ikishirikiana na TFF.
*Ligi Kuu ya Vodacom inatazamiwa kuendelea kesho kwenye viwanja tofauti
1. Simba v Toto Africans Uwanja wa Taifa
2. T. Prisons v JKT Ruvu Sokoine
3. Kagera Sugar v Polisi Moro Kaitaba
4. African Lyon v Mtibwa Sugar Azam Complex
5. Oljoro JKT v Ruvu Shooting Sheikh Amri Abeid
6. Mgambo JKT v Azam FC Mkwakwani
Jumapili
1. Coastal Union v Young Africans Mkwakwani
Thursday, November 8, 2012
Ikulu: Hatuwezi Kumzuia Lissu Kumshtaki Rais
SIKU moja baada ya Mnadhimu wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Tundu Lissu kusema atawasilisha hoja ya kumshtaki Rais Jakaya Kikwete iwapo atashindwa kuwaondoa kazini majaji wasio na sifa aliowateua, Ikulu imemwambia aendelee na mchakato wake.
Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Salva Rweyemamu alisema jana kuwa hakuna anayemzuia Lissu kushtaki kama anaona kuna sababu za kufanya hivyo.“Lissu ni Mbunge na ana haki zake za msingi na kama amefikia hatua hiyo anaweza kufanya hivyo... hakuna mtu ambaye anaweza kumkataza. Nani mwenye uwezo wa kuingilia uhuru wa mtu?”
Akizungumza na waandishi wa habari katika Ofisi za Bunge jana, Lissu alisema amechukua uamuzi huo baada ya kuona Bunge limeikalia ripoti ya Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge iliyomhoji kuhusu kauli yake ya kuwatuhumu majaji kuwa baadhi yao hawana sifa.
Alisema ameamua kuchukua hatua hiyo baada ya kuona Rais Kikwete ambaye ana mamlaka ya kuteua majaji, ameshindwa kuwaondoa kazini majaji hao wasiokuwa na sifa.
Lissu alisema atawasilisha hoja yake hiyo kwa kutumia Kanuni ya Bunge sehemu ya 11, Ibara ya 121, 122, 123, 124, 125 na 126 na pia kwa kutumia Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ibara ya 146 A. Sehemu ya 11 ya Kanuni ya Bunge, Ibara ya 121 inaeleza kuwa mbunge yeyote anaweza kuwasilisha kwa Spika taarifa ya hoja ya kumshtaki Rais kwa madhumuni ya kumuondoa Rais madarakani kupitia azimio la Bunge kwa mujibu wa Ibara ya 46 A ya Katiba ikiwa inadaiwa kwamba Rais; ametenda vitendo ambavyo kwa ujumla vinavunja katiba au sheria ya maadili ya viongozi wa umma.
Lissu alisema atakusanya saini za wabunge kuunga mkono hoja yake ambayo ni asilimia 20 kwa mujibu wa Kanuni za Bunge. Wabunge wote kikatiba ni 357. Julai 13, mwaka huu wakati akitoa maoni ya kambi ya upinzani katika Wizara ya Katiba na Sheria bungeni, Lissu alisema uteuzi wa majaji umegubikwa na ukiukwaji wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano.
Alisema baadhi ya majaji walioteuliwa hawana sifa, uwezo na kwamba hawakufaa kufanya kazi hiyo. Kauli hiyo ilisababisha Bunge kuiagiza Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge inayoongozwa na Mbunge wa Mlalo (CCM), Hassan Ngwilizi kumhoji ili athibitishe kauli yake.
Alisema wakati akihojiwa na kamati hiyo, pamoja na nyaraka nyingine, aliwasilisha nakala ya ripoti ya kikosi kazi kilichoundwa mwaka 2008 na aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Johnson Mwanyika na aliyekuwa Katibu Mkuu Kiongozi, Philemon Luhanjo kuchunguza uteuzi wa majaji nchini.
Alisema ripoti ya kikosi kazi hicho kilibaini kuwapo majaji ambao hawana sifa ya kufanya kazi hiyo, lakini Rais Kikwete ameshindwa kuwaondoa kazini. Lissu ambaye pia ni Mbunge wa Singida Mashariki kwa tiketi ya Chadema, alisema hali ya Mahakama ni mbaya, kwani kuna majaji wawili ambao waliwahi kukamatwa kwa rushwa wakiwa mawakili, lakini wakateuliwa kufanya kazi hiyo.
Alisema baadhi ya majaji hawana uwezo hata wa kuandika hukumu kutokana na kutojua vyema lugha ya Kiingereza ambayo ndiyo inayotumika katika Mahakama Kuu na Mahakama ya Rufani.
Alisema ili mtu aweze kuchaguliwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu lazima awe na elimu ya shahada ya kwanza ya sheria, awe ametumikia miaka 10 mahakamani na anayechaguliwa kuwa jaji wa Mahakama ya Rufani lazima awe ametumikia miaka 15 mahakamani.
Mbali ya kueleza hayo, Lissu alisema kwamba alitoa pia katika kamati hiyo, ushahidi unaoonyesha kuwa kuna jaji mmoja wa Mahakama Kuu ambaye hawezi hata kuandika sentensi moja ya Kiingereza ilinyooka... “Kama jaji hawezi kuandika hata sentensi moja ya Kiingereza ilinyooka, tunaweza vipi kuwa na Mahakama inayotenda haki?”
Alisema kuna jaji mwingine ambaye ameongezewa mkataba wa kufanya kazi mara ya tatu kitu ambacho ni kinyume cha sheria. Alisema kwa mujibu wa Tume ya Mahakama, hakuna jaji ambaye anaweza kufanya kazi kwa mkataba kwa vipindi vitatu.
Kama Lissu atachukua hatua hiyo, itakuwa ni mara ya pili kwa mbunge kuwasilisha bungeni hoja ya kutaka kumwajibisha kiongozi wa juu serikalini. Mara ya kwanza alikuwa Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe katika Bunge lililopita alipokusanya saini za wabunge kutaka kupiga kura ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akitaka awawajibishe baadhi ya mawaziri waliokuwa wametajwa kuhusika katika matumizi mabaya ya madaraka katika Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).
Hata hivyo, Rais Kikwete alifanya mabadiliko makubwa katika Baraza lake la Mawaziri hivyo kuzima hoja hiyo ya Zitto.
Chanzo: http://www.mwananchi.co.tz/habari
Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Salva Rweyemamu alisema jana kuwa hakuna anayemzuia Lissu kushtaki kama anaona kuna sababu za kufanya hivyo.“Lissu ni Mbunge na ana haki zake za msingi na kama amefikia hatua hiyo anaweza kufanya hivyo... hakuna mtu ambaye anaweza kumkataza. Nani mwenye uwezo wa kuingilia uhuru wa mtu?”
Akizungumza na waandishi wa habari katika Ofisi za Bunge jana, Lissu alisema amechukua uamuzi huo baada ya kuona Bunge limeikalia ripoti ya Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge iliyomhoji kuhusu kauli yake ya kuwatuhumu majaji kuwa baadhi yao hawana sifa.
Alisema ameamua kuchukua hatua hiyo baada ya kuona Rais Kikwete ambaye ana mamlaka ya kuteua majaji, ameshindwa kuwaondoa kazini majaji hao wasiokuwa na sifa.
Lissu alisema atawasilisha hoja yake hiyo kwa kutumia Kanuni ya Bunge sehemu ya 11, Ibara ya 121, 122, 123, 124, 125 na 126 na pia kwa kutumia Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ibara ya 146 A. Sehemu ya 11 ya Kanuni ya Bunge, Ibara ya 121 inaeleza kuwa mbunge yeyote anaweza kuwasilisha kwa Spika taarifa ya hoja ya kumshtaki Rais kwa madhumuni ya kumuondoa Rais madarakani kupitia azimio la Bunge kwa mujibu wa Ibara ya 46 A ya Katiba ikiwa inadaiwa kwamba Rais; ametenda vitendo ambavyo kwa ujumla vinavunja katiba au sheria ya maadili ya viongozi wa umma.
Lissu alisema atakusanya saini za wabunge kuunga mkono hoja yake ambayo ni asilimia 20 kwa mujibu wa Kanuni za Bunge. Wabunge wote kikatiba ni 357. Julai 13, mwaka huu wakati akitoa maoni ya kambi ya upinzani katika Wizara ya Katiba na Sheria bungeni, Lissu alisema uteuzi wa majaji umegubikwa na ukiukwaji wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano.
Alisema baadhi ya majaji walioteuliwa hawana sifa, uwezo na kwamba hawakufaa kufanya kazi hiyo. Kauli hiyo ilisababisha Bunge kuiagiza Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge inayoongozwa na Mbunge wa Mlalo (CCM), Hassan Ngwilizi kumhoji ili athibitishe kauli yake.
Alisema wakati akihojiwa na kamati hiyo, pamoja na nyaraka nyingine, aliwasilisha nakala ya ripoti ya kikosi kazi kilichoundwa mwaka 2008 na aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Johnson Mwanyika na aliyekuwa Katibu Mkuu Kiongozi, Philemon Luhanjo kuchunguza uteuzi wa majaji nchini.
Alisema ripoti ya kikosi kazi hicho kilibaini kuwapo majaji ambao hawana sifa ya kufanya kazi hiyo, lakini Rais Kikwete ameshindwa kuwaondoa kazini. Lissu ambaye pia ni Mbunge wa Singida Mashariki kwa tiketi ya Chadema, alisema hali ya Mahakama ni mbaya, kwani kuna majaji wawili ambao waliwahi kukamatwa kwa rushwa wakiwa mawakili, lakini wakateuliwa kufanya kazi hiyo.
Alisema baadhi ya majaji hawana uwezo hata wa kuandika hukumu kutokana na kutojua vyema lugha ya Kiingereza ambayo ndiyo inayotumika katika Mahakama Kuu na Mahakama ya Rufani.
Alisema ili mtu aweze kuchaguliwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu lazima awe na elimu ya shahada ya kwanza ya sheria, awe ametumikia miaka 10 mahakamani na anayechaguliwa kuwa jaji wa Mahakama ya Rufani lazima awe ametumikia miaka 15 mahakamani.
Mbali ya kueleza hayo, Lissu alisema kwamba alitoa pia katika kamati hiyo, ushahidi unaoonyesha kuwa kuna jaji mmoja wa Mahakama Kuu ambaye hawezi hata kuandika sentensi moja ya Kiingereza ilinyooka... “Kama jaji hawezi kuandika hata sentensi moja ya Kiingereza ilinyooka, tunaweza vipi kuwa na Mahakama inayotenda haki?”
Alisema kuna jaji mwingine ambaye ameongezewa mkataba wa kufanya kazi mara ya tatu kitu ambacho ni kinyume cha sheria. Alisema kwa mujibu wa Tume ya Mahakama, hakuna jaji ambaye anaweza kufanya kazi kwa mkataba kwa vipindi vitatu.
Kama Lissu atachukua hatua hiyo, itakuwa ni mara ya pili kwa mbunge kuwasilisha bungeni hoja ya kutaka kumwajibisha kiongozi wa juu serikalini. Mara ya kwanza alikuwa Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe katika Bunge lililopita alipokusanya saini za wabunge kutaka kupiga kura ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akitaka awawajibishe baadhi ya mawaziri waliokuwa wametajwa kuhusika katika matumizi mabaya ya madaraka katika Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).
Hata hivyo, Rais Kikwete alifanya mabadiliko makubwa katika Baraza lake la Mawaziri hivyo kuzima hoja hiyo ya Zitto.
Chanzo: http://www.mwananchi.co.tz/habari
Viongozi Uamsho Wakosa Dhamana Tena
Na Maelezo Zanzibar 08/11/2012
Kesi inayomkabili Shekh Farid Hadi Ahmed na wenzake sita wa Jumuiya ya UAMSHO na Mihadhara ya Kiislam imeakhirishwa leo hadi terehe 20 mwezi huu.
Akitoa maamuzi hayo Mrajisi wa Mahakama kuu Zanzibar iliyopo Vuga George Kazi amesema kuwa uamuzi huo umetokana na kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika.
Kwa upande wa Wanasheria wa watuhumiwa walielezea juu ya haki ya washitakiwa wao kupatiwa dhamana lakini dhamana hiyo hawakupatiwa na kurejeshwa Rumande hadi tarehe 20 mwezi huu.
Washitakiwa hao ni Farid Had Ahmed (41) wa mkazi wa Mbuyuni, Mselem Ali Mselem(52)wa Kwamtipura, Mussa Juma Issa (37) wa Makadara, Azan Khalid Hamdan (43) wa Mfenesini, Suleiman Juma Suleiman (66) wa Makadara,Khamis Ali Suleiman (59) anayeishi Mwanakwerekwe pamoja na Hassan Bakar Suleiman (39) mkaazi wa Tomondo.
Watuhumiwa wote walishitakiwa kwa kosa la uchochezi wa kufanya fujo kinyume na kifungu cha 45 (a) (b) cha sheria namba 6/2004 sheria za Zanzibar.
Ilifahamishwa kuwa Agosti 17 mwaka huu majira ya saa 11:00 za jioni huko Magogoni Msumbiji Wilaya ya Magharibi Unguja, wakiwa ni Wahadhiri kutoka Jumuiya ya UAMSHO na Mihadhara ya Kiisalam, walitoa matamko ya uchochezi yanayoashiria uvunjaji wa Amani na kusababisha fujo,maafa mbalimbali na mtafaruku kwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
IMETOLEWA NA MAELEZO ZANZIBAR
Kesi inayomkabili Shekh Farid Hadi Ahmed na wenzake sita wa Jumuiya ya UAMSHO na Mihadhara ya Kiislam imeakhirishwa leo hadi terehe 20 mwezi huu.
Akitoa maamuzi hayo Mrajisi wa Mahakama kuu Zanzibar iliyopo Vuga George Kazi amesema kuwa uamuzi huo umetokana na kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika.
Kwa upande wa Wanasheria wa watuhumiwa walielezea juu ya haki ya washitakiwa wao kupatiwa dhamana lakini dhamana hiyo hawakupatiwa na kurejeshwa Rumande hadi tarehe 20 mwezi huu.
Washitakiwa hao ni Farid Had Ahmed (41) wa mkazi wa Mbuyuni, Mselem Ali Mselem(52)wa Kwamtipura, Mussa Juma Issa (37) wa Makadara, Azan Khalid Hamdan (43) wa Mfenesini, Suleiman Juma Suleiman (66) wa Makadara,Khamis Ali Suleiman (59) anayeishi Mwanakwerekwe pamoja na Hassan Bakar Suleiman (39) mkaazi wa Tomondo.
Watuhumiwa wote walishitakiwa kwa kosa la uchochezi wa kufanya fujo kinyume na kifungu cha 45 (a) (b) cha sheria namba 6/2004 sheria za Zanzibar.
Ilifahamishwa kuwa Agosti 17 mwaka huu majira ya saa 11:00 za jioni huko Magogoni Msumbiji Wilaya ya Magharibi Unguja, wakiwa ni Wahadhiri kutoka Jumuiya ya UAMSHO na Mihadhara ya Kiisalam, walitoa matamko ya uchochezi yanayoashiria uvunjaji wa Amani na kusababisha fujo,maafa mbalimbali na mtafaruku kwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
IMETOLEWA NA MAELEZO ZANZIBAR
JK: Azindua Ujenzi Wa Bomba La Gesi Asilia Kutoka Mtwara-Dar es salaam
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na ujumbe wa kampuni inayojenga bomba
la gesi asilia kutoka Mtwata hadi Dar es salaam, Benki ya Exim ya China
na viongozi waandamizi wa serikali alipowakaribisha Ikulu kwa mazungumzo
baada ya uzinduzi rasmi wa ujenzi wa bomba hilo maeneo ya Kinyerezi
jijini Dar es salaam
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Makamu wa Rais Dkt Mohamed Ghalib Bilali na viongozi wengine wakimsikiliza Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo miundombinu ya bomba la gesi asilia toka Mtwara hadi Dar es salaam leo Novemba 8, 2012 maeneno ya Kinyerezi njijini Dar es salaam. Nyuma yake ni Makamu wa Rais Dkt Mohamed Ghalib Bilali.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akizindua rasmi ujenzi wa bomba la gesi asilia toka Mtwara hadi Dar es salaam leo Novemba 8, 2012 maeneno ya Kinyerezi njijini Dar es salaam. Nyuma yake ni Makamu wa Rais Dkt Mohamed Ghalib Bilali.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Makamu wa Rais Dkt Mohamed Ghalib Bilali na viongozi wengine wakimsikiliza Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo miundombinu ya bomba la gesi asilia toka Mtwara hadi Dar es salaam leo Novemba 8, 2012 maeneno ya Kinyerezi njijini Dar es salaam. Nyuma yake ni Makamu wa Rais Dkt Mohamed Ghalib Bilali.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akizindua rasmi ujenzi wa bomba la gesi asilia toka Mtwara hadi Dar es salaam leo Novemba 8, 2012 maeneno ya Kinyerezi njijini Dar es salaam. Nyuma yake ni Makamu wa Rais Dkt Mohamed Ghalib Bilali.
Mashirika 64 Yaliyobinafsishwa Hayafanyi Kazi
Ndugu zangu,
Mara nyingi Watanzania wamekuwa wakipigia kelele kuhusu suala la ubinafsishaji lililoanza mwanzoni mwa miaka ya 1990 kwamba halikwenda sawa.
Kwamba, pamoja na shinikizo la Benki ya Dunia na IMF kutekeleza Sera ya Ubinafsishaji kwa mashirika yaliyokuwa mzigo kwa serikali, lakini viongozi wetu waliyabinafsishaji hata yale yaliyokuwa na uwezo wa kujiendesha, mengi wakajiuzia wao.
Sasa inasikitisha tunapoasikia leo kwamba, mashirika 64 kati ya yaliyobinafsishwa mpaka sasa hayafanyi kazi tena.
Tujiulize, mashirika hayo ni yetu hasa; kabla ya kubinafsishwa hali ilikuwaje; sasa yamebinafsishwa kwa akina nani; na kwa nini mpaka sasa serikali inawaangalia tu wawekezaji hao ambao wameshindwa kutekeleza masharti ya mkataba?
Ikumbukwe kwamba, mpaka yanabinafsishwa, kulikuwa na wafanyakazi, ambao walikuwa na familia zilizotegemea kazi wanazofanya kwenye mashirika hayo, na kubinafsishwa kwa mashirika maana yake kumewafanya wengi wakose kazi, wengine wamepoteza maisha kutokana na ugumu wa maisha kwani kiinua mgongo walicholipwa hakikutosha.
Tuijadili zaidi, lakini isome pia hapa...wp-content/uploads/2012/11/Janet-Mbene.jpg
Kutoka kwa: Mbega Mnyama,
Mara nyingi Watanzania wamekuwa wakipigia kelele kuhusu suala la ubinafsishaji lililoanza mwanzoni mwa miaka ya 1990 kwamba halikwenda sawa.
Kwamba, pamoja na shinikizo la Benki ya Dunia na IMF kutekeleza Sera ya Ubinafsishaji kwa mashirika yaliyokuwa mzigo kwa serikali, lakini viongozi wetu waliyabinafsishaji hata yale yaliyokuwa na uwezo wa kujiendesha, mengi wakajiuzia wao.
Sasa inasikitisha tunapoasikia leo kwamba, mashirika 64 kati ya yaliyobinafsishwa mpaka sasa hayafanyi kazi tena.
Tujiulize, mashirika hayo ni yetu hasa; kabla ya kubinafsishwa hali ilikuwaje; sasa yamebinafsishwa kwa akina nani; na kwa nini mpaka sasa serikali inawaangalia tu wawekezaji hao ambao wameshindwa kutekeleza masharti ya mkataba?
Ikumbukwe kwamba, mpaka yanabinafsishwa, kulikuwa na wafanyakazi, ambao walikuwa na familia zilizotegemea kazi wanazofanya kwenye mashirika hayo, na kubinafsishwa kwa mashirika maana yake kumewafanya wengi wakose kazi, wengine wamepoteza maisha kutokana na ugumu wa maisha kwani kiinua mgongo walicholipwa hakikutosha.
Tuijadili zaidi, lakini isome pia hapa...wp-content/uploads/2012/11/Janet-Mbene.jpg
Kutoka kwa: Mbega Mnyama,
Obama Tears Up While Addressing Campaign Staff
Before heading back to the White House on Wednesday, President Obama made a stop at campaign headquarters in Chicago to address his campaign staff after Tuesday night's big victory.
The president gave an emotional thanks to the staff, tearing up as he expressed his gratitude for their support and dedication to the reelection effort.
"I'm really proud of all of you," Obama said. "What you guys accomplished will go on in the annals of history."
Source: http://www.huffingtonpost.com
The president gave an emotional thanks to the staff, tearing up as he expressed his gratitude for their support and dedication to the reelection effort.
"I'm really proud of all of you," Obama said. "What you guys accomplished will go on in the annals of history."
Source: http://www.huffingtonpost.com
kesi ya lema yahairishwa tena
RUFAA ya aliyekuwa Mbunge wa Arusha Mjini kupitia Chadema, Godbless Lema imeponea chupuchupu kutupiliwa mbali baada ya Mahakama ya Rufani, kukubali hoja moja ya pingamizi la makada wa CCM dhidi ya rufaa hiyo.
Mahakama hiyo ilikubali hoja ya wajibu rufaa kuwa rufaa hiyo ilikuwa na dosari kutokana na tofauti ya vifungu vya sheria vilivyotumika katika hukumu iliyomvua ubunge na vilivyotumika katika hati ya kukaza hukumu, iliyowasilishwa mahakamani sambamba na rufaa hiyo.
Hata hivyo, kilichomwokoa Lema ni kifungu cha 111 cha Kanuni za Mahakama, ambapo mahakama hiyo ilisema kuwa chini ya kanuni hiyo dosari hizo zinaweza kurekebishwa.
Chini ya kanuni hiyo, Mahakama ya Rufani ilimwamuru Lema kupitia kwa mawakili wake, Tundu Lissu na Method Kimomogoro, kufanya marekebisho ya dosari hizo zilizobainika na kisha kuwasilisha upya rufaa yake ndani ya siku 14 kutoka jana.
Lema alivuliwa wadhifa huo na Mahakama Kuu Kanda ya Arusha, Aprili 5, 2012 kutokana na kesi iliyofunguliwa na wanachama watatu wa CCM, Mussa Mkanga, Happy Kivuyo na Agnes Mollel, wakipinga ushindi wake katika Uchaguzi Mkuu mwaka 2010.
Lakini baadaye alikata rufaa Mahakama ya Rufani, kupitia kwa wakili wake, Method Kimomogoro kupinga hukumu ya Mahakama Kuu, huku akitoa hoja 18 za kupinga hukumu hiyo.
Tarehe ambayo rufaa hiyo ilipangwa kusikilizwa na jopo la majaji watatu Mahakama ya Rufani; Salum Massati, Natalia Kimaro na Jaji Mkuu, Mohamed Othman Chande (kiongozi wa jopo), wakili wa wajibu rufaa, Alute Mughwai, aliweka pingamizi la awali.
Katika pingamizi hilo,wakili Mghwai aliiomba Mahakama hiyo iitupilie mbali rufaa hiyo, akidai kuwa ina kasoro za kisheria na za kikanuni huku akibainisha hoja tatu za kuunga mkono pingamizi hilo.
Hoja hizo za pingamizi la awali zilikuwa ni pamoja na kuchanganywa au kutofautiana kwa vifungu vya Sheria ya Uchaguzi ya Mwaka 2010, kati ya hukumu iliyomvua ubunge na hati ya kukaza hukumu hiyo.
Pia hoja nyingine ni kwamba hati ya kukaza hukumu hiyo haikuwa na mhuri wa Jaji aliyeitoa wala tarehe ambayo hati hiyo ya kukaza hukumu ilitolewa.
Hoja ya tatu ilikuwa ni mtindo wa kuandika hati ya kukaza hukumu, kwa kutokuandika maneno, “imetolewa kwa mkono wangu na mhuri wa mahakama.”
Hata hivyo, katika uamuzi wake jana, Mahakama ya Rufani ilikubaliana na hoja moja ya pingamizi hilo, kuwa tofauti au kuchanganywa kwa vifungu hivyo vya sheria ni dosari ambayo inaifanya hati hiyo isiwe halali na ikatupilia mbali hoja nyingine mbili kuwa hazina msingi.
Uamuzi huo ulioandikwa na Jaji Nathalie Kimaro kwa niaba ya jopo hilo, ulisomwa na Naibu Msajili wa Mahakama ya Rufani, Zahra Maruma.
Mahakama hiyo ilikubali hoja ya wajibu rufaa kuwa rufaa hiyo ilikuwa na dosari kutokana na tofauti ya vifungu vya sheria vilivyotumika katika hukumu iliyomvua ubunge na vilivyotumika katika hati ya kukaza hukumu, iliyowasilishwa mahakamani sambamba na rufaa hiyo.
Hata hivyo, kilichomwokoa Lema ni kifungu cha 111 cha Kanuni za Mahakama, ambapo mahakama hiyo ilisema kuwa chini ya kanuni hiyo dosari hizo zinaweza kurekebishwa.
Chini ya kanuni hiyo, Mahakama ya Rufani ilimwamuru Lema kupitia kwa mawakili wake, Tundu Lissu na Method Kimomogoro, kufanya marekebisho ya dosari hizo zilizobainika na kisha kuwasilisha upya rufaa yake ndani ya siku 14 kutoka jana.
Lema alivuliwa wadhifa huo na Mahakama Kuu Kanda ya Arusha, Aprili 5, 2012 kutokana na kesi iliyofunguliwa na wanachama watatu wa CCM, Mussa Mkanga, Happy Kivuyo na Agnes Mollel, wakipinga ushindi wake katika Uchaguzi Mkuu mwaka 2010.
Lakini baadaye alikata rufaa Mahakama ya Rufani, kupitia kwa wakili wake, Method Kimomogoro kupinga hukumu ya Mahakama Kuu, huku akitoa hoja 18 za kupinga hukumu hiyo.
Tarehe ambayo rufaa hiyo ilipangwa kusikilizwa na jopo la majaji watatu Mahakama ya Rufani; Salum Massati, Natalia Kimaro na Jaji Mkuu, Mohamed Othman Chande (kiongozi wa jopo), wakili wa wajibu rufaa, Alute Mughwai, aliweka pingamizi la awali.
Katika pingamizi hilo,wakili Mghwai aliiomba Mahakama hiyo iitupilie mbali rufaa hiyo, akidai kuwa ina kasoro za kisheria na za kikanuni huku akibainisha hoja tatu za kuunga mkono pingamizi hilo.
Hoja hizo za pingamizi la awali zilikuwa ni pamoja na kuchanganywa au kutofautiana kwa vifungu vya Sheria ya Uchaguzi ya Mwaka 2010, kati ya hukumu iliyomvua ubunge na hati ya kukaza hukumu hiyo.
Pia hoja nyingine ni kwamba hati ya kukaza hukumu hiyo haikuwa na mhuri wa Jaji aliyeitoa wala tarehe ambayo hati hiyo ya kukaza hukumu ilitolewa.
Hoja ya tatu ilikuwa ni mtindo wa kuandika hati ya kukaza hukumu, kwa kutokuandika maneno, “imetolewa kwa mkono wangu na mhuri wa mahakama.”
Hata hivyo, katika uamuzi wake jana, Mahakama ya Rufani ilikubaliana na hoja moja ya pingamizi hilo, kuwa tofauti au kuchanganywa kwa vifungu hivyo vya sheria ni dosari ambayo inaifanya hati hiyo isiwe halali na ikatupilia mbali hoja nyingine mbili kuwa hazina msingi.
Uamuzi huo ulioandikwa na Jaji Nathalie Kimaro kwa niaba ya jopo hilo, ulisomwa na Naibu Msajili wa Mahakama ya Rufani, Zahra Maruma.
DIRECTOR WA FILAMU ILIYOKASHIFU UISLAMU AHUKUMIWA.
The man behind an anti-Muslim film that led to violence in the Middle East has been sentenced to one year in prison.
Mark Basseley Youssef, 55, was sentenced on Wednesday for violating probation stemming from a 2010 bank fraud conviction.
US District Court Judge Christina Snyder handed down the sentence after Youssef admitted four of eight alleged violations including obtaining a fraudulent California driver’s licence.
Youssef served most of a 21-month prison term in the bank fraud case. Federal authorities wanted Youssef to serve two years for the violations.
After he was released from prison, Youssef was barred from using computers or the Internet for five years without approval from his probation officer.
None of the violations had to do with the content of “Innocence of Muslims,” a film that depicts Mohammad as a religious fraud, pedophile and a womaniser.
The movie sparked violence in Libya and other parts of the Middle East, killing dozens. Enraged Muslims had demanded severe punishment for him, with a Pakistani cabinet minister even offering $100,000 to anyone who kills him.
Federal authorities have said they believe Youssef is responsible for the film, but they have not said whether he was the person who posted it online.
He also was not supposed to use any name other than his true legal name without the prior written approval of his probation officer.
At least three names have been associated with Youssef since the film trailer surfaced – Sam Bacile, Nakoula Basseley Nakoula and Youssef. Bacile was the name attached to the YouTube account that posted the video.
Court documents show Youssef legally changed his name from Nakoula in 2002, though when he was tried, he identified himself as Nakoula. He wanted the name change because he believed Nakoula sounded like a girl’s name, according to court documents.
Mark Basseley Youssef, 55, was sentenced on Wednesday for violating probation stemming from a 2010 bank fraud conviction.
US District Court Judge Christina Snyder handed down the sentence after Youssef admitted four of eight alleged violations including obtaining a fraudulent California driver’s licence.
Youssef served most of a 21-month prison term in the bank fraud case. Federal authorities wanted Youssef to serve two years for the violations.
After he was released from prison, Youssef was barred from using computers or the Internet for five years without approval from his probation officer.
None of the violations had to do with the content of “Innocence of Muslims,” a film that depicts Mohammad as a religious fraud, pedophile and a womaniser.
The movie sparked violence in Libya and other parts of the Middle East, killing dozens. Enraged Muslims had demanded severe punishment for him, with a Pakistani cabinet minister even offering $100,000 to anyone who kills him.
Federal authorities have said they believe Youssef is responsible for the film, but they have not said whether he was the person who posted it online.
He also was not supposed to use any name other than his true legal name without the prior written approval of his probation officer.
At least three names have been associated with Youssef since the film trailer surfaced – Sam Bacile, Nakoula Basseley Nakoula and Youssef. Bacile was the name attached to the YouTube account that posted the video.
Court documents show Youssef legally changed his name from Nakoula in 2002, though when he was tried, he identified himself as Nakoula. He wanted the name change because he believed Nakoula sounded like a girl’s name, according to court documents.
Subscribe to:
Posts (Atom)

.jpg)























.jpg)
.jpg)
.jpg)






















