Kutekwa kwa Kibanda si tukio la kihalifu! Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam,Suleimani Kova, amedai kuwa kutekwa na kuumizwa vibaya kwa Mwandishi nguli na Mhariri wa New Habari,Absalom Kibanda, si tukio la kihalifu. Kamanda Kova amedai kuwa tukio hilo limetokana na chuki na kulipiziana visasi Hii ni kwasababu waliomteka na kumshambulia Kibanda hawakuchukua kitu
chochote toka kwake. Alikuwa akizungumza na waandishi wa habari kutoa taarifa za uchunguzi wa awali wa jeshi la polisi juu ya tukiohilo lililotokea jana,
Thursday, March 7, 2013
MAAFANDE WAHUSISHWA NA TUKIO LA UTEKAJI WA MWENYEKITI WA JUKWAA LA WAHARIRI, ABSALOM KIBANDA HII NI KAULI YA ABSALOM KIBANDA BAADA YA KUTEKWA...............
"Baada ya kutoka kwenye gari, nahisi nilikanyaga sehemu mbaya, nikateleza na
kuanguka wakanifuata...niliona kama watu watatu hivi wakaanza kunishambulia.
Sikuwa nafahamu kilichojiri, lakini nilisikia mwingine akimwambia mwenzake
afande 'mshuti... mshuti' huyo alipoelekeza mtutu na kujaribu 'kushuti'
(kupiga risasi) ilikuwa kama vile imegoma.
“Nikiwa bado niko chini, wakanipiga kwa kitu cha ncha kali kwenye jicho la
kushoto, wakaning’oa meno na kucha katika vidole vya mkono wa kulia,
walinipiga sana na nilipata maumivu makali. Baada ya kunipiga na kunijeruhi
waliniburuza hadi bembeni ya nyumba yangu na kunitupa na wakaondoka, baadaye
majirani na wasamaria wema walikuja kuniokoa..."
kuanguka wakanifuata...niliona kama watu watatu hivi wakaanza kunishambulia.
Sikuwa nafahamu kilichojiri, lakini nilisikia mwingine akimwambia mwenzake
afande 'mshuti... mshuti' huyo alipoelekeza mtutu na kujaribu 'kushuti'
(kupiga risasi) ilikuwa kama vile imegoma.
“Nikiwa bado niko chini, wakanipiga kwa kitu cha ncha kali kwenye jicho la
kushoto, wakaning’oa meno na kucha katika vidole vya mkono wa kulia,
walinipiga sana na nilipata maumivu makali. Baada ya kunipiga na kunijeruhi
waliniburuza hadi bembeni ya nyumba yangu na kunitupa na wakaondoka, baadaye
majirani na wasamaria wema walikuja kuniokoa..."
MATOKEO YA UCHAGUZI KENYA: MFUMO WA ELEKRONIKI UMEKWAMA....ZOEZI LINAANZA UPYA
Huku Wakenya wakiendela kusubiri kwa hamu kubwa kumjua mshindi wa kura ya urais kufuatia uchaguzi wa Jumatatu, wasiwasi unaongezeka baada ya kukwama kwa mfumo wa uwasilishaji matokeo kwa njia ya elekroniki.
Kufuatia hitilafu hiyo, Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka ya Kenya (IEBC) imesema kwamba inategemea sasa matokeo yatakayowasilishwa na wasimamizi wa uchaguzi kutoka majimbo yote 290 kote nchini ili kuanza upya shughuli ya kujumlisha kura za urais.
Kufuatia hitilafu hiyo, Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka ya Kenya (IEBC) imesema kwamba inategemea sasa matokeo yatakayowasilishwa na wasimamizi wa uchaguzi kutoka majimbo yote 290 kote nchini ili kuanza upya shughuli ya kujumlisha kura za urais.
BARUA YA MWANAFUNZI ALIEMALIZA FORM 4 2012 KWA WIZARA YA ELIMU
Pliz my name is MKUWA RAJAB I am finish fom for. Ze everybody is to say we get za divishen 0, My part I am saying not I am not get divshen 0. I am vere vere intelijens, but pipoz don’t like me.
I have experience in singing bongoflava, so pipoz are jelas, the have put ...majik so I get diveshen 0. But I am clever becoz ask me forekzampo, what is fomula for water? Ze fomula for water iz Hech to O.
Now why you give me dishen 0? Ok ask me anadha forekzampo what iz President of America? Ze president of America iz Obama. Ze gavament shud change my marks to dishen 2, because the youth are ze future of my country.
If we get divishen 0 zen all the future is divishen 0. So giv us more maks becoz of ze future. Pliz mzee put on ze yua fb wall so ze Plezident will see.......
Kwa hisani ya James Pricenton Brighton
I have experience in singing bongoflava, so pipoz are jelas, the have put ...majik so I get diveshen 0. But I am clever becoz ask me forekzampo, what is fomula for water? Ze fomula for water iz Hech to O.
Now why you give me dishen 0? Ok ask me anadha forekzampo what iz President of America? Ze president of America iz Obama. Ze gavament shud change my marks to dishen 2, because the youth are ze future of my country.
If we get divishen 0 zen all the future is divishen 0. So giv us more maks becoz of ze future. Pliz mzee put on ze yua fb wall so ze Plezident will see.......
Kwa hisani ya James Pricenton Brighton
TFF YASALIMU AMRI YA SERIKALI...UCHAGUZI UTARUDIWA UPYA
Serikali imelitaka Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), kuandaa upya mchakato wa uchaguzi wake mkuu uliolalamikiwa na wadau mbalimbali wa soka nchini, kiasi cha wengine kufungua kesi mahakamani kuupinga.
TFF imeshitakiwa mahakama za Mwanza na Tanga, baada ya baadhi waliokuwa wagombea wa nafasi mbalimba kuenguliwa kwenda kortini kupinga kufanyika uchaguzi huo mpaka kesi zao za msingi zitakaposilizwa.
Kabla ya mchakato huo, TFF pia imetakiwa kuitisha Mkutano Mkuu wa marekebisho ya katiba kabla ya Aprili 15, na baada ya hapo kuitisha pia Mkutano wa Uchaguzi kabla ya Mei 25 mwaka huu.
TFF imeshitakiwa mahakama za Mwanza na Tanga, baada ya baadhi waliokuwa wagombea wa nafasi mbalimba kuenguliwa kwenda kortini kupinga kufanyika uchaguzi huo mpaka kesi zao za msingi zitakaposilizwa.
Kabla ya mchakato huo, TFF pia imetakiwa kuitisha Mkutano Mkuu wa marekebisho ya katiba kabla ya Aprili 15, na baada ya hapo kuitisha pia Mkutano wa Uchaguzi kabla ya Mei 25 mwaka huu.
MATOKEO YA UCHAGUZI WA URAIS KENYA KWA MUDA HUU
Hadi kufikia muda huu, Kenyatta anaonekana kuongoza kinyang'anyiro hicho.Matokeo kamili yanatariwa kutangazwa kesho.
Wakati huo huo tume ya uchaguzi nchini humo (IEBC) ilikiri kuwa mitambo yake ya kuhesabu kura kwa njia ya kisasa ilishindwa kuhimili vishindo vya zoezi hilo na kulazimika kuhamia kwenye mfumo wa zamani (manual) wa kuhesabu kura.
Wakati huo huo tume ya uchaguzi nchini humo (IEBC) ilikiri kuwa mitambo yake ya kuhesabu kura kwa njia ya kisasa ilishindwa kuhimili vishindo vya zoezi hilo na kulazimika kuhamia kwenye mfumo wa zamani (manual) wa kuhesabu kura.
MWENYEKITI WA JUKWAA LA WAHARIRI "ABSALOM KIBANDA" APELEKWA AFRIKA KUSINI KWA MATIBABU
Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahahariri na Mhariri Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya New Habari 2006 Ltd,Absalon Kibanda akipakiwa kwenye ndege ya Kampuni ya Flightlink tayari kwa safari ya kwenda nchini Afrika Kusini kwa Matibabu baada ya kuvamiwa na watu wasiojulikana na kujeruhiwa vibaya,alipokuwa akirudi nyumbani kwake Mbezi Beach jijini Dar es Salaam.
Wednesday, March 6, 2013
MATUMAINI AIOMBA SERIKALI IMSAIDIE MATIBABU....
KOMEDIANI maarufu Bongo, Tumaini Mwakibibi ‘Matumaini’ ameiomba serikali imsaidie kupata matibabu ili aweze kupona maradhi ya figo na ini yanayomkabili.
Akizungumza na mwandishi wetu jijini Dar es Salaam alisema: “Hali yangu bado si nzuri ingawa natumia dawa lakini sijapata tiba sawasawa. Sina fedha na familia yangu kwa sasa imeishiwa kwa sababu magonjwa yanayonisumbua ni makubwa na yanahitaji fedha nyingi.
“Naiomba serikali kupitia Wizara ya Habari, Vijana Utamaduni na Michezo isikie kilio changu. Hali yangu si nzuri, nahitaji msaada ili kuokoa maisha yangu. Nina imani nikipata tiba kamili nitapona na kurejea tena jukwaani.”
Akizungumza na mwandishi wetu jijini Dar es Salaam alisema: “Hali yangu bado si nzuri ingawa natumia dawa lakini sijapata tiba sawasawa. Sina fedha na familia yangu kwa sasa imeishiwa kwa sababu magonjwa yanayonisumbua ni makubwa na yanahitaji fedha nyingi.
“Naiomba serikali kupitia Wizara ya Habari, Vijana Utamaduni na Michezo isikie kilio changu. Hali yangu si nzuri, nahitaji msaada ili kuokoa maisha yangu. Nina imani nikipata tiba kamili nitapona na kurejea tena jukwaani.”
Umoja wa Mataifa walaani vitendo vya kushambuliwa albino nchini Tanzania
Umoja wa mataifa umelaani vikali vitendo vya kushambuliwa kikatili walemavu wa ngozi, albino nchini Tanzania kutokana na imani za kishirikina.
“Ninalaani vikali mauaji na mashambulio haya ambayo yamefanyika katika mazingira ya kutisha na ambayo yamehusishwa kukata viungo vya watu wakiwemi watoto wakati wakiwa hai,” alisema jana kamishna mkuu wa haki za binadamu wa umoja wa Navi Pillay.
“Ninalaani vikali mauaji na mashambulio haya ambayo yamefanyika katika mazingira ya kutisha na ambayo yamehusishwa kukata viungo vya watu wakiwemi watoto wakati wakiwa hai,” alisema jana kamishna mkuu wa haki za binadamu wa umoja wa Navi Pillay.
JAMES MBATIA AJITOA TUME YA KUCHUNGUZA UBOVU WA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE
Mwenyekiti wa Chama cha NCCR-Mageuzi, James Mbatia amejitoa kwenye Tume ya serikali kuchunguza chanzo cha kushuka kwa kiwango cha kustisha cha matokeo ya kidato cha nne, iliyoundwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.
Mbatia ambaye ametajwa kuwa mmoja wa wajumbe wa tume hiyo yenye wajumbe 15, alisema kamwe hatoweza kufanya kazi yake kwa uhuru kwa sababu ni Mbunge wa kuteuliwa, kamati hiyo imeundwa na serikali hivyo lazima kutakuwa na mgongano wa maslahi.
Hatua hiyo imekuja siku tatu baada ya chama hicho kumwandikia barua Rais Jakaya Kikwete, kikimuomba aunde tume ya kudumu ya elimu nchini.
MHARIRI MKUU NA MWENYEKITI WA JUKWAA LA WAHARIRI ABSALOM KIBANDA AVAMIWA USIKU WA MANANE NA KUJERUHIWA VIBAYA
Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya New Habari wachapishaji wa magazeti ya Mtanzania, Dimba, Bingwa na Dimba, Absalom Kibanda amevamiwa na watu wasiojulikana akiwa ndani ya gari lake wakati akiingia nyumbani kwake Mbezi nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.
Kibanda alivamia majira ya saa sita usiku wa kumkia leo, akitokea kwenye majukumu yake ya kila siku. Inadaiwa kuwa alichomolewa kwene gari, akapigwa na vitu vyenye ncha kali kichwani, ametobolewa jicho lake la kushoto pamoja na kunyofolewa kucha na baadhi ya vidole na hatimaye kutupwa umbali kidogo ya nyumbani kwake.
Kibanda alivamia majira ya saa sita usiku wa kumkia leo, akitokea kwenye majukumu yake ya kila siku. Inadaiwa kuwa alichomolewa kwene gari, akapigwa na vitu vyenye ncha kali kichwani, ametobolewa jicho lake la kushoto pamoja na kunyofolewa kucha na baadhi ya vidole na hatimaye kutupwa umbali kidogo ya nyumbani kwake.
HUYU NDO MWANAMKE ANAYEOLEWA NA 2FACE WIKI HII
Blogger maarufu wa Nigeria Linda Ikeji ameripoti kwamba staa wa muziki 2Face Idibia anatarajia kufunga ndoa ya kimila ijumaa hii tarehe 8 March 2013 na party nyingine ya harusi itafanyika Dubai.
VURUGU ZA IFUNDA SECONDARY:..MKUU WA SHULE ANUSURIKA KUUAWA.KISA NI "BARAGHASIA" DARASANI WANAFUNZI wa Shule ya Sekondari ya Ufundi Ifunda, iliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Vijijini, jana walifanya vurugu kubwa shuleni hapo na kutaka kumuua Mkuu wa shule hiyo, Bw. Shaaban Nsute. Katika vurugu hizo ambazo zilianza juzi jioni hadi saa tano usiku, wanafunzi hao ambao walivalia kininja na kuficha sura zao wakiwa na visu mkononi, walivunja vioo vya madirisha shuleni hapo. Wanafunzi hao wanadaiwa kumfuata Bw. Nsute nyumbani kwake lakini alikimbia na kwenda kujificha kwenye shamba la mahindi ambapo wanafunzi hao walimpiga mlinzi wa shule Bw. Yasini Luhala kwa mawe akiwa katika ofisi yake. Akizungumza na Majira jana, Bw. Nsute alisema chanzo cha vurugu hizo ambazo zilidhibitiwa na Jeshi la Polisi ni baada ya mwanafunzi mmoja shuleni hapo kuvaa kofia zinazotumiwa na Waislam (baraghashia). Alisema mlinzi wa shule hiyo, Bw. Luhala alimnyang'anya kofia hiyo ili asiingie nayo darasani kwa sababu si sare ya shule lakini mwanafunzi huyo alichukua uamuzi wa kwenda kuwaita wenzake na kufanya vurugu. Aliongeza kuwa, kutokana na vurugu hizo zaidi ya wanafunzi 30 wamefukuzwa shule na kuwataja baadhi yao kuwa ni Sadi Mwamed, Jamal Hashim na Athuman Ibrahim wanosoma kidato cha tano. Wengine ni Abdulazizi Hussein na Ally Abdallah wanaosoma kidato cha nne. Mwanafunzi aliyenyang'anywa kofia alidai Waislamu katika shule hii wanatengwa, kunyanyaswa na kuzuiwa wasifanye mambo yanayoendana na dini yao. Hawa wanafunzi walikuja nyumbani kwangu usiku na kugonga mlango, nilitoka mlango wa nyuma nikakimbia kwenye shamba la mahindi, mke wangu alifungua mlango na kuwaambia sipona alipowahoji wakamwambia walikuwa wakinihitaji ili niende nao Msikitini kuna kazi muhimu, Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wilayani humo ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya hiyo, Dk Letisia Warioba, alisema tukio hilo limemsikitisha sana. Alilipongeza Jeshi la Polisi kwa kufika mapema eneo la tukio, kutuliza vurugu na kuimarisha ulinzi shuleni hapo hadi asubuhi na kuwataka wanafunzi waliobaki, waendelee na masko kwa kuzingatia taratibu za shule.
WANAFUNZI wa Shule ya Sekondari ya Ufundi Ifunda, iliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Vijijini, jana walifanya vurugu kubwa shuleni hapo na kutaka kumuua Mkuu wa shule hiyo, Bw. Shaaban Nsute.
Katika vurugu hizo ambazo zilianza juzi jioni hadi saa tano usiku, wanafunzi hao ambao walivalia kininja na kuficha sura zao wakiwa na visu mkononi, walivunja vioo vya madirisha shuleni hapo.
Wanafunzi hao wanadaiwa kumfuata Bw. Nsute nyumbani kwake lakini alikimbia na kwenda kujificha kwenye shamba la mahindi ambapo wanafunzi hao walimpiga mlinzi wa shule Bw. Yasini Luhala kwa mawe akiwa katika ofisi yake.
Akizungumza na Majira jana, Bw. Nsute alisema chanzo cha vurugu hizo ambazo zilidhibitiwa na Jeshi la Polisi ni baada ya mwanafunzi mmoja shuleni hapo kuvaa kofia zinazotumiwa na Waislam (baraghashia).
Katika vurugu hizo ambazo zilianza juzi jioni hadi saa tano usiku, wanafunzi hao ambao walivalia kininja na kuficha sura zao wakiwa na visu mkononi, walivunja vioo vya madirisha shuleni hapo.
Wanafunzi hao wanadaiwa kumfuata Bw. Nsute nyumbani kwake lakini alikimbia na kwenda kujificha kwenye shamba la mahindi ambapo wanafunzi hao walimpiga mlinzi wa shule Bw. Yasini Luhala kwa mawe akiwa katika ofisi yake.
Akizungumza na Majira jana, Bw. Nsute alisema chanzo cha vurugu hizo ambazo zilidhibitiwa na Jeshi la Polisi ni baada ya mwanafunzi mmoja shuleni hapo kuvaa kofia zinazotumiwa na Waislam (baraghashia).
MAPENZI YA FACEBOOK: BIBI WA MIAKA 67 AUAWA NA MPENZI WAKE WA MIAKA 28 SIKU MOJA BAADA YA KUKUTANA LIVE...
Polisi wa Afrika Kusini bado wanaendelea kuchunguza tukio la kutisha linalodaiwa kufanywa na kijana wa Kinigeria mwenye umri wa miaka 28 ambae anatuhumiwa kumuua bibi wa kizungu mwenye umri wa miaka 67 huko Johannesburg.
Bibi kizee Jette Jacobs ambae ni raia wa Australia alisafiri mpaka Johannesburg kwa lengo la kufunga ndoa na mwanaume anayempenda lakini siku mbili baada ya kukutana na mwanaume huyo, bibi huyo amekutwa amefariki kwenye mazingira ya kutatanisha kwenye jiji hilo lililo kwenye list ya majiji hatari kwa uhalifu duniani.
Bibi kizee Jette Jacobs ambae ni raia wa Australia alisafiri mpaka Johannesburg kwa lengo la kufunga ndoa na mwanaume anayempenda lakini siku mbili baada ya kukutana na mwanaume huyo, bibi huyo amekutwa amefariki kwenye mazingira ya kutatanisha kwenye jiji hilo lililo kwenye list ya majiji hatari kwa uhalifu duniani.
Subscribe to:
Posts (Atom)















