Imenukuliwa kutoka kwenye gazeti la Mwananchi, ARUSHA-- Giza limeukumba Mkoa wa Arusha baada ya kutokea vifo vya ghafla vya watu maarufu. Jana Wakili Nyaga Mawalla alifariki baada ya kujirusha kutoka ghorofani akiwa jijini Nairobi, Kenya alikokwenda kwa matibabu.
Habari zilizopatikana zinaeleza kuwa Nyaga alikufa baada ya kujirusha kutoka katika jengo la ghorofa ya hospitali aliyokuwa akitibiwa jijini Nairobi usiku wa kuamkia jana.
Mfanyakazi wa Kampuni ya Mawalla Advocate, John Minja aliliambia gazeti hili kuwa mwili wa marehemu ulitarajiwa kurejeshwa nchini jana.
Friday, March 22, 2013
MAANDAMANO YA CHADEMA KESHO: MBOWE ADAI YAKO PALE PALE NA WATAANDAMANA MBELE YA RAIS WA CHINA
LICHA ya serikali kuyapiga marufuku maandamano yaliyoratibiwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kuishinikiza kumwajibisha Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi na Naibu wake wajiuzulu kutokana na matokeo mabaya ya mtihani wa kidato cha nne 2012, chama hicho kimesema yapo pale pale.
Chama hicho kimewaomba wananchi wote waliochoshwa na kufelishwa kwa watoto wao, kunyimwa elimu bora wajitokeze kuandamana kwa nguvu zote, na wanafunzi wote waliofeli pia wajitokeze kudai elimu bora kwani ni haki yao.
Akizungumza kwa simu na gazeti hili jana na kutoa msimamo huo, Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe alisema “wananchi wajitokeze kwa wingi ili kilio chao kisikike duniani kote.”
Alisisitiza kuwa maandamano hayo yatafanyika mbele ya ugeni wa Rais wa China, Xi Jinping ili kufikisha kilio hicho na kamwe haikubaliani na sababu ya serikali kuyazuia kwa sababu ya ugeni huo.
Chama hicho kimewaomba wananchi wote waliochoshwa na kufelishwa kwa watoto wao, kunyimwa elimu bora wajitokeze kuandamana kwa nguvu zote, na wanafunzi wote waliofeli pia wajitokeze kudai elimu bora kwani ni haki yao.
Akizungumza kwa simu na gazeti hili jana na kutoa msimamo huo, Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe alisema “wananchi wajitokeze kwa wingi ili kilio chao kisikike duniani kote.”
Alisisitiza kuwa maandamano hayo yatafanyika mbele ya ugeni wa Rais wa China, Xi Jinping ili kufikisha kilio hicho na kamwe haikubaliani na sababu ya serikali kuyazuia kwa sababu ya ugeni huo.
RIPOTI YA POLISI: MADAI YA KULAWITIWA KWA WANAFUNZI WA IFM SI YA KWELI
Kamati iliyoundwa kuchunguza vitendo vya udhalilishaji na kuporwa vitu vyao wanavyofanyiwa wanafunzi wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), wanaoishi katika hosteli zilizopo Kigamboni Manispaa ya Temeke imebaini hakuna wanafunzi waliofanyiwa vitendo hivyo.
Kamati hiyo iliyoundwa na Kamanda wa Polisi, Kanda Maalumu ya Polisi jijini Dar es Salaam, Suleiman Kova baada ya kuwahutubia wanafunzi hao katika Viwanja vya Machava, ilijumuisha wanafunzi wanne wa IFM na wakuu wa upelelezi kutoka kanda hiyo .
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kipolisi Temeke, Englebert Kiondo, alisema kamati hiyo ilichunguza kwa kina madai hayo ya wanafunzi, lakini hakuna na hata moja walilobaini kuwa na ukweli .
Kamati hiyo iliyoundwa na Kamanda wa Polisi, Kanda Maalumu ya Polisi jijini Dar es Salaam, Suleiman Kova baada ya kuwahutubia wanafunzi hao katika Viwanja vya Machava, ilijumuisha wanafunzi wanne wa IFM na wakuu wa upelelezi kutoka kanda hiyo .
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kipolisi Temeke, Englebert Kiondo, alisema kamati hiyo ilichunguza kwa kina madai hayo ya wanafunzi, lakini hakuna na hata moja walilobaini kuwa na ukweli .
JACK CHUZI WA BONGO MOVIE ABADILI DINI NA KUOLEWA....

Katika Hali ya Kushtusha na Kufuraisha....Staa wa Bongo Movie Jack Pentezel amewashtusha wengi baada ya Kuamua kubadili dini kuwa Muislamu kisha kuolewa na Mpenzi wake wa Muda Gadner Dibibi....
wadau wengi na wapenzi wa Bongo Movie wamekuwa wakihoji juu ya Ndoa Hiyo iliofungwa kisiri sana na kwa haraka,Je Ndoa Hiyo Itadumu? Je ni kweli wamehamua kukaa kwenye Maadili ya Ndoa..? au Ni kama Mchezo wa Mjini kubadilishana Dini na kuoana mwishowe ni kuachana....Tusubiri Tuone.....
Mpekuzi inapenda kumtakia Jack Pentezel na Mumewe Gadner Dibibi Baraka Tele,Amani na Upendo utawale kwenye Maisha yao ya Ndoa..
" MIMI NI MTI WENYE MATUNDA MILELE....SIOGOPI KUPIGWA MAWE"... HUU NI UJUMBE WA DIAMOND
MSANII wa muziki wa bongo fleva Diamond Platinam ameendelea kujinadi kupitia mitandao ya kijamiii huku akiteka hisia za mashabiki wake kwa kutuma baadhi ya picha zinazomuonyesha akiwa jukwaani akifanya 'makamuzi' pamoja na kutuma ujumbe wa kujipongeza kwa kazi anayoifanya
Kupitia mtandao wake wa 'Instagram' msanii huyo alituma ujumbe uliosomeka hivi "Mimi ni mti wenye matunda milele siogopi kupigwa mawe"
Ujumbe huo ulionekana kuteka baadhi ya mashabiki wake huku wengine wakituma ujumbe za kumpongeza kwa kuwa na imani hiyo huku akionyesha kutoteteleka kwa jambo lolote linalomkabili ambalo linaonyesha kutaka kumdondosha kimuziki
Maneno ya ujumbe huo pia umeonekana kutumiwa katika nyimbo yake mpya inayojulikana kwa jina la 'Muziki gani' ambayo wameshirikiana na msanii Ney wa Mitego
Kupitia mtandao wake wa 'Instagram' msanii huyo alituma ujumbe uliosomeka hivi "Mimi ni mti wenye matunda milele siogopi kupigwa mawe"
Ujumbe huo ulionekana kuteka baadhi ya mashabiki wake huku wengine wakituma ujumbe za kumpongeza kwa kuwa na imani hiyo huku akionyesha kutoteteleka kwa jambo lolote linalomkabili ambalo linaonyesha kutaka kumdondosha kimuziki
Maneno ya ujumbe huo pia umeonekana kutumiwa katika nyimbo yake mpya inayojulikana kwa jina la 'Muziki gani' ambayo wameshirikiana na msanii Ney wa Mitego
RIPOTI YA GAZETI LA IJUMAA KUHUSU WABUNGE KUTEMBEA NA WANAFUNZI WA CHUO KIKUU CHA DODOMA ( UDOM )
MITANDAO mingi ya kijamii na kurasa binafsi za mawasiliano zinazopatikana ndani ya simu za viganjani kama Instagram, WhatsApp na BBM (Blackberry Messenger) zinazomilikiwa na baadhi ya wasichana wanaosoma Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom) zimejaa mambo ya ngono na kashfa kwa baadhi ya wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Unyemeleaji taarifa uliofanywa na Ijumaa kwa muda mrefu kwenye huduma hizo za mawasiliano ya kisasa umebaini wanafunzi wa kike wamewabatiza jina la ‘mabuzi yao’ baadhi ya wabunge.
Bila kupepesa mitandao hiyo imekuwa pia ikitumiwa na wasichana hao kuuza miili yao huku ufahari kama si ujanja ukiwa ni mtu kujipatia bwana mwenye cheo cha ubunge ambaye anaaminika waleti yake haikaukiwi fedha kutokana na posho za vikao na utumishi wa umma.
Unyemeleaji taarifa uliofanywa na Ijumaa kwa muda mrefu kwenye huduma hizo za mawasiliano ya kisasa umebaini wanafunzi wa kike wamewabatiza jina la ‘mabuzi yao’ baadhi ya wabunge.
Bila kupepesa mitandao hiyo imekuwa pia ikitumiwa na wasichana hao kuuza miili yao huku ufahari kama si ujanja ukiwa ni mtu kujipatia bwana mwenye cheo cha ubunge ambaye anaaminika waleti yake haikaukiwi fedha kutokana na posho za vikao na utumishi wa umma.
MAHAKAMA KUU YAITISHA MAFAILI YA KESI YA LWAKATARE
Dar es Salaam. Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, imeiamuru Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu iwasilishe majalada ya kesi ya ugaidi inayomuhusu Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chadema, Wilfred Lwakatare na mwenzake katika kesi hiyo, Ludovick Joseph.
Hati ya kuitisha majalada hayo ilitolewa jana alasiri na Msajili wa Mahakama Kuu, baada ya mawakili wanaomtetea Lwakatare kuwasilisha maombi ya marejeo ya mwenendo wa kesi hiyo, iliyofunguliwa katika Mahakama ya Kisutu.
Hati ya kuitisha majalada hayo ilitolewa jana alasiri na Msajili wa Mahakama Kuu, baada ya mawakili wanaomtetea Lwakatare kuwasilisha maombi ya marejeo ya mwenendo wa kesi hiyo, iliyofunguliwa katika Mahakama ya Kisutu.
"NAWASHANGAA WANAOPOTEZA MUDA KUYAFUATILIA MAISHA YANGU"....WEMA SEPETU
Msanii anayetafuta mafanikio kwa kasi, Wema Sepetu amesema kuwa haoni sababu ya watu kutishiana maisha hasa kwa kipindi hiki ambacho maisha yapo juu.
Wema alisema hayo kufuatia hivi karibuni kutishiwa maisha na watu asiowafahamu na kulazimika kuongeza ulinzi nyumbani kwake na kila anapokuwa anatoka.
Alisema maisha ni magumu na kila mmoja anatakiwa afanye kazi kwa bidii ili kufikia malengo, badala yake watu wanaanza kutishiana maisha.
"Nawashangaa watu wanaoendelea kuwafuatafuata wengine wanapata wapi ujasiri huo na hali ya maisha ilivyo ngumu na kuhitaji muda mwingi wa kufanya kazi ili kujikwamua,"alishangaa Wema.
Aidha, aliongeza kuwa hana adui wala mtu ambaye anamdai au kitu kama hicho hivyo watu wanaomtumia mesaji za vitisho anahisi wana chuki binafsi na si kingine.
Wema alisema hayo kufuatia hivi karibuni kutishiwa maisha na watu asiowafahamu na kulazimika kuongeza ulinzi nyumbani kwake na kila anapokuwa anatoka.
Alisema maisha ni magumu na kila mmoja anatakiwa afanye kazi kwa bidii ili kufikia malengo, badala yake watu wanaanza kutishiana maisha.
"Nawashangaa watu wanaoendelea kuwafuatafuata wengine wanapata wapi ujasiri huo na hali ya maisha ilivyo ngumu na kuhitaji muda mwingi wa kufanya kazi ili kujikwamua,"alishangaa Wema.
Aidha, aliongeza kuwa hana adui wala mtu ambaye anamdai au kitu kama hicho hivyo watu wanaomtumia mesaji za vitisho anahisi wana chuki binafsi na si kingine.
Thursday, March 21, 2013
Meneja Fastjet akamatwa
Wafanyakazi wa shirika la ndege, Fast Jet
Meneja wa wahudumu wa ndege za kampuni ya ndege ya Fastjet, Emma Donavan, amekamatwa na polisi, kuwekwa mahabusu na kuhojiwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam kwa tuhuma za kumtolea lugha ya matusi mmoja wa wafanyakazi wa kampuni hiyo.
Polisi walimshikilia na kumhoji Donavan kwa takribani saa tisa kuhusiana na tuhuma za kumtolea lugha ya matusi mfanyakazi huyo raia wa Tanzania.
Kamanda wa Polisi wa Viwanja vya Ndege, Deusdedit Kato, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba meneja huyo alikamatwa jana saa 2:00 asubuhi kwa tuhuma za kumtukana mfanyakazi mwenzake, Samson Isembe, ambaye ni Ofisa Mwendeshaji wa kampuni hiyo.
Meneja wa wahudumu wa ndege za kampuni ya ndege ya Fastjet, Emma Donavan, amekamatwa na polisi, kuwekwa mahabusu na kuhojiwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam kwa tuhuma za kumtolea lugha ya matusi mmoja wa wafanyakazi wa kampuni hiyo.
Polisi walimshikilia na kumhoji Donavan kwa takribani saa tisa kuhusiana na tuhuma za kumtolea lugha ya matusi mfanyakazi huyo raia wa Tanzania.
Kamanda wa Polisi wa Viwanja vya Ndege, Deusdedit Kato, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba meneja huyo alikamatwa jana saa 2:00 asubuhi kwa tuhuma za kumtukana mfanyakazi mwenzake, Samson Isembe, ambaye ni Ofisa Mwendeshaji wa kampuni hiyo.
Nyerere, Karume watajwa kesi ya wafuasi wa Ponda
Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere
Shahidi wa utetezi na Mwanzilishi wa Baraza la Misikiti Tanganyika, Bilali Waikela (87), amedai mahakamani katika kesi inayomkabili Sheikh Issa Ponda na wenzake 49, kwamba Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere na Rais wa kwanza wa Zanzibar, Shekhe Abeid Karume, walivunja Umoja wa Waislamu wa Afrika Mashiriki.
Waikela alidai kuwa umoja huo ulianzishwa kwa lengo la kuwatetea na kuwasaidia Waislamu na kwamba Tanzania ilipata kiwanja cha Chang’ombe Marcas kutoka kwa aliyekuwa Rais wa Misri.
Waikela ambaye ni shahidi wa 48 wa upande wa utetezi katika kesi hiyo alidai kuwa, umoja huo ulifutwa baada ya Karume kudanganywa kuwa wana mpango wa kufanya mapinduzi na kuwarudisha Waarabu Zanzibar.
“Mwalimu Nyerere ndiye aliyemtuma Karume afanye hivyo na mwaka 1964 nilifungwa baada ya kukataa kupokea Shilingi 40,000 ili nikubali kuvunja umoja huo, na Kassim bin Juma, Adam Simba na Salehe Masasi waliotumiwa kuhamasisha watu kuvunja umoja huo,” alidai.
Alidai kuwa ofisi za umoja huo zilifungwa hadi mwaka 1968 lilipoundwa Baraza la Waislamu Tanzania (Bakwata) na kukabidhiwa ofisi pamoja na mali zote kikiwamo kiwanja cha Chang’ombe markazi kilichokuwa kimejengwa shule ya Waislamu.
CHANZO: NIPASHE
Shahidi wa utetezi na Mwanzilishi wa Baraza la Misikiti Tanganyika, Bilali Waikela (87), amedai mahakamani katika kesi inayomkabili Sheikh Issa Ponda na wenzake 49, kwamba Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere na Rais wa kwanza wa Zanzibar, Shekhe Abeid Karume, walivunja Umoja wa Waislamu wa Afrika Mashiriki.
Waikela alidai kuwa umoja huo ulianzishwa kwa lengo la kuwatetea na kuwasaidia Waislamu na kwamba Tanzania ilipata kiwanja cha Chang’ombe Marcas kutoka kwa aliyekuwa Rais wa Misri.
Waikela ambaye ni shahidi wa 48 wa upande wa utetezi katika kesi hiyo alidai kuwa, umoja huo ulifutwa baada ya Karume kudanganywa kuwa wana mpango wa kufanya mapinduzi na kuwarudisha Waarabu Zanzibar.
“Mwalimu Nyerere ndiye aliyemtuma Karume afanye hivyo na mwaka 1964 nilifungwa baada ya kukataa kupokea Shilingi 40,000 ili nikubali kuvunja umoja huo, na Kassim bin Juma, Adam Simba na Salehe Masasi waliotumiwa kuhamasisha watu kuvunja umoja huo,” alidai.
Alidai kuwa ofisi za umoja huo zilifungwa hadi mwaka 1968 lilipoundwa Baraza la Waislamu Tanzania (Bakwata) na kukabidhiwa ofisi pamoja na mali zote kikiwamo kiwanja cha Chang’ombe markazi kilichokuwa kimejengwa shule ya Waislamu.
CHANZO: NIPASHE
Gakondo wadhamiria kuupa nguvu muziki wa asili
Katika kuhakikisha wanalinda asili ya nchi yao wasanii nguli nane wa muziki wa asili nchini Rwanda wameungana na kufanya kazi pamoja kwa lengo la kulinda na kuheshimu kazi yao hiyo.
Wasanii hao wameungana na kujipa jina la ‘Gakondo’ambapo mwanamuziki nguli wa muziki huo nchini humo, Intore Massamba ndiye aliyetoa wazo hilo badala ya kuimba msanii mmoja mmoja.
Kundi hilo lina wasanii mahiri wa muziki huo, Jules Sentore, Daniel Ngarukiye, Michel Ngabo, Manu-teta Kamaliza and Didier Bass-tamfun.
Akizungumza kwenye umoja huo, Massamba alisema kufanya kazi pamoja ni vizuri lakini kwa muziki wa asili ni bora wakafanya pamoja ili kuunusuru muziki huo na kuufanya uwe imara ndani ya jamii.
Alisema wanachofanya kwa sasa baada ya muungano huo ni kuandaa nyimbo ambazo watazirekodi kabla ya kuziingiza sokoni”tunataka kuhakikisha tunaufanya muziki wa asili wa Rwanda uchezwe sehemu mbali mbali Barani Afrika na nje ya Afrika.
Chanzo: Mwananchi
Wasanii hao wameungana na kujipa jina la ‘Gakondo’ambapo mwanamuziki nguli wa muziki huo nchini humo, Intore Massamba ndiye aliyetoa wazo hilo badala ya kuimba msanii mmoja mmoja.
Kundi hilo lina wasanii mahiri wa muziki huo, Jules Sentore, Daniel Ngarukiye, Michel Ngabo, Manu-teta Kamaliza and Didier Bass-tamfun.
Akizungumza kwenye umoja huo, Massamba alisema kufanya kazi pamoja ni vizuri lakini kwa muziki wa asili ni bora wakafanya pamoja ili kuunusuru muziki huo na kuufanya uwe imara ndani ya jamii.
Alisema wanachofanya kwa sasa baada ya muungano huo ni kuandaa nyimbo ambazo watazirekodi kabla ya kuziingiza sokoni”tunataka kuhakikisha tunaufanya muziki wa asili wa Rwanda uchezwe sehemu mbali mbali Barani Afrika na nje ya Afrika.
Chanzo: Mwananchi
WAFUASI 52 WA PONDA WAHUKUMIWA KIFUNGO CHA MWAKA MMOJA JELA
Washitakiwa 52 kati ya 54 katika kesi ya kula njama na kufanya maandamano isivyo halali wamehukumiwa kwenda jela kila mmoja baada ya kukutwa na makosa matatu huku mmoja akiachiwa huru baada ya kukutwa hana hatia na mwingine kufariki dunia kabla ya hukumu iliyotolewa leo na hakimu Sundi Fimbo wa Mahakama ya Hamimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam.
Washtakiwa hao walidaiwa kutenda kosa Februari 15 mwaka huu.
Baada ya pande zote kusikilizwa na washtakiwa kutoa hoja za utetezi, hatimaye hakimu Fimbo alitoa hukumu hiyo leo ambapo aliwatia hatiani washtakiwa 52 kwa makosa matatu kati ya manne na kila mmoja akamhukumu kwenda jela mwaka mmoja kwa kila kosa.
Washtakiwa hao walidaiwa kutenda kosa Februari 15 mwaka huu.
Baada ya pande zote kusikilizwa na washtakiwa kutoa hoja za utetezi, hatimaye hakimu Fimbo alitoa hukumu hiyo leo ambapo aliwatia hatiani washtakiwa 52 kwa makosa matatu kati ya manne na kila mmoja akamhukumu kwenda jela mwaka mmoja kwa kila kosa.
Wednesday, March 20, 2013
RAIS KIKWETE AHANI MSIBA WA TRAFIKI ALIYEGONGWA MAENEO YA BAMAGA
Taarifa tulizozipata zinaeleza kuwa yule dereva aliyemgonga askari polisi wa usalama barabarani WP 2493 CPL-Elikiza Lokisa Nko na kutokomea, amekamatwa juzi usiku masaa kadhaa baada ya kupoteza uhai wa askari huyo maeneo ya Bamaga mapema jana mchana.
Kwa Mujibu wa Mkuu wa Kikosi cha Polisi cha Usalama barabarani nchini, Kamanda Mohamed Mpinga alisema jana kuwa gari lilohusika kwenye ajali hiyo aina ya Landlover Discovery rangi nyeusi limepatikana likiwa limefichwa maeneo ya Tabata dampo jijini Dar.
Kupatikana kwa gari hilo kumekuja baada ya Polisi kufuatilia na kujua mmiliki wa gari hilo kuwa ni kanisa la TAG chini ya Mchungaji Wambura, ambaye kwa ushirikiano alioutoa dereva aliyetambuliwa kama Jackson Stephen, alijulikana na hatimaye kupatikana
Kamanda Mpiga alitoa taarifa hiyo mbele ya Rais Jakaya Mrisho Kikwete jana jioni nyumbani kwa Marehemu hukoUnunio kiasi cha kilomita 25 hivi Kaskazini mwa jiji la Dar.
Rais Kikwete pamoja na uongozi wa juu wa jeshi la polisi walifika kuhani msiba huo nyumbani kwa marehemu ambaye ameacha Mume na watoto watatu. Mume wa marehemu pia ni askari polisi.
Kwa Mujibu wa Mkuu wa Kikosi cha Polisi cha Usalama barabarani nchini, Kamanda Mohamed Mpinga alisema jana kuwa gari lilohusika kwenye ajali hiyo aina ya Landlover Discovery rangi nyeusi limepatikana likiwa limefichwa maeneo ya Tabata dampo jijini Dar.
Kupatikana kwa gari hilo kumekuja baada ya Polisi kufuatilia na kujua mmiliki wa gari hilo kuwa ni kanisa la TAG chini ya Mchungaji Wambura, ambaye kwa ushirikiano alioutoa dereva aliyetambuliwa kama Jackson Stephen, alijulikana na hatimaye kupatikana
Kamanda Mpiga alitoa taarifa hiyo mbele ya Rais Jakaya Mrisho Kikwete jana jioni nyumbani kwa Marehemu hukoUnunio kiasi cha kilomita 25 hivi Kaskazini mwa jiji la Dar.
Rais Kikwete pamoja na uongozi wa juu wa jeshi la polisi walifika kuhani msiba huo nyumbani kwa marehemu ambaye ameacha Mume na watoto watatu. Mume wa marehemu pia ni askari polisi.
NANCY SUMARI AZINDUA KITABU CHA WATOTO NYOTA YAKO
Miss World Africa 2005, Nancy Sumari leo amezindua kitabu chake cha watoto kiitwacho Nyota Yako. Uzinduzi huo umefanyika jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na watu mbalimbali maarufu wakiwemo mamiss Tanzania wa zamani, Jacqueline Ntuyabaliwe na Faraja Nyalandu.
Nancy Sumari akizungumza kwenye uzinduzi huoNancy Sumari akizungumza kwenye uzinduzi huo
Wengine ni pamoja DAKTARI Bingwa wa magonjwa ya watoto na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Hubert Kairuki, Profesa Esther Mwaikambo, Jokate Mwegelo, Shaa, Ally Remtullah. Fina Mango na wanafunzi mbalimbali.
Akizungumzia jambo lililomsukuma kuandi ka kitabu hicho, Nancy alisema:
Vilinisukuma vitu vingi, kwanza nafasi ya mwanamke kwenye jamii yetu, umuhimu wake, sababu ya kumuenzi na kumsherehekea na kutambua michango yetu, mwanamke mdogo, msichana mdogo, mama zetu, bibi zetu. Kuna kila sababu ya sisi kuangaliana na kutambuana na pia kufananisha.
Nancy Sumari akizungumza kwenye uzinduzi huoNancy Sumari akizungumza kwenye uzinduzi huo
Wengine ni pamoja DAKTARI Bingwa wa magonjwa ya watoto na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Hubert Kairuki, Profesa Esther Mwaikambo, Jokate Mwegelo, Shaa, Ally Remtullah. Fina Mango na wanafunzi mbalimbali.
Akizungumzia jambo lililomsukuma kuandi ka kitabu hicho, Nancy alisema:
Vilinisukuma vitu vingi, kwanza nafasi ya mwanamke kwenye jamii yetu, umuhimu wake, sababu ya kumuenzi na kumsherehekea na kutambua michango yetu, mwanamke mdogo, msichana mdogo, mama zetu, bibi zetu. Kuna kila sababu ya sisi kuangaliana na kutambuana na pia kufananisha.
Subscribe to:
Posts (Atom)











(1).jpg)





