Monday, March 25, 2013

WEMA SEPETU AJITOLEA KUTOA MILIONI 13 KUMUOKOA KAJALA ALIEHUKUMIWA MIAKA MITANO ....

Leo imesomwa hukumu ya kesi iliyokuwa inamkabili mcheza filamu za Kitanzania anayefahamika kwa jina la 'Kajala Masanja' na mumewe mbele ya Hakimu 'Sundi Fimbo' kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es salaam.

 Katika hukumu hiyo 'Kajala'  amehukumiwa kwenda jela miaka mitano au kulipa faini ya shilingi milioni 13 na mumewe kwenda jela miaka saba au kulipa faini ya shilingi milioni 200.

Kajala alikuwa anakabiliwa na kesi ya kuuza nyumba iliyowekwa kizuizini na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) baada ya mumewe 'Faraji Agustino' kukumbwa na makosa ya kutakatisha fedha haramu.

Hata hivyo baada ya hukumu hiyo kutolea mahakamani hapa, mwanadada mwenye michejo mingi hapa Bongo anayefahamika kwa jina la Wema Sepetu' aliweza kujitolea yeye mwenyewe kiasi cha Tsh. milioni 13 kutoka mfukoni mwake kwa ajili ya kumlipia msanii mwenzake wa filamu 'Kajala' asiweze kutumikia adhabu ya kifungo hicho cha miaka 5 jela.

 Hii ni mara ya pili kwa msanii 'Wema Sepetu' kujitolea kiasi kikubwa cha fedha kusaidia msanii mwenzake.!

BREAKING NEWS: MSANII KAJALA MASANJA AHUKUMIWA MIAKA 5, MUMEWE MIAKA 7

Habari  njema kwa mashabiki wa muigizaji Kajala Masanja ambaye leo hukumu yake imesomwa katika mahakama ya hakimu mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam.

Katika hukumu hiyo Kajala amehukumiwa kwenda jela miaka mitano au kulipa faini ya shilingi milioni 13 na mumewe kwenda jela miaka saba au kulipa faini ya shilingi milioni 200. Taarifa kutoka mahakamani zinadai kuwa wasanii wa bongomovie wanachanga fedha hizo ili wazilipe na tayari inasemekana Wema Sepetu amezitoa fedha hizo zote kutoka mfukoni mwake.

Mrembo huyo na mumewe Faraja Chambo walikuwa wakikabiliwa na makosa matatu ambayo ni pamoja na kula njama ambapo washtakiwa wote kwa pamoja walitenda kosa kwa kuhamisha umiliki wa nyumba iliyopo Kunduchi Salasala jijini Dar es Salaam.

Shtaka la pili ni ni kwamba Aprili 14 mwaka 2010 waliamisha isivyo halali umiliki wa nyumba hiyo kinyume na kifungu cha 34(2)A(3) cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa ya mwaka 2007. Shitaka la tatu ni la kutakatisha fedha ambalo walilitenda Aprili 14 mwaka 2010 huku wakijua ni kinyume cha sheria.

AFYA YA KIBANDA YAANZA KUIMARIKA NA AMEWEZA KUSIMAMA

 Hope all is well.
Salamu nyingi saaana toka JBG!
I could not resist! Yes I cried! But Absalom is the same person I knew last two months! Amesimama! Mungu ni Mwema!!!
Anaomba watanzania wamwombee na amesema anaendelea vizuri kwa sasa…
Cheers,
Hoyce Temu.

KAULI YA RAIS KIKWETE KUHUSU UCHAWI KWENYE SOKA LA BONGO

Moja kati ya kauli ambazo zimeingia kwenye headlines za michezo kwa wiki iliyokwisha ni kauli ya President Jakaya Kikwete, kauli kuhusu ushirikina kwenye soka la bongo aliyoitoa wakati akizindua uwanja mpya wa club ya soka ya Azam Chamazi Dar es salaam.

Namkariri akisema “najua mtapata tabu sana mkiwaleta hapa watasema kiwanja hiki kina namna, yote ni ushirikina tu…. ni wale ambao hawataki kuwekeza kwenye maendeleo ya mchezo, wanataka kuwekeza kwenye mambo ya kipuuzi… we tangu lini uchawi ukacheza mpira? ingekua uchawi unacheza mpira Afrika ingekua ina kombe la dunia na hatunyang’anywi, nyie hamjajua kwamba jambo hili la kipuuzi? mnawekeza pesa nyingi kwenye kamati ya ufundi hakuna chochote, haiwafikishi kokote”

Rais aliongeza  kwa  kusema “wekeza kwa kocha mzuri, vifaa vizuri, mafunzo mazuri, wachezaji walale mahali pazuri, Uwanja wa Azam Complex ni mzuri na wa kisasa, kuna sehemu ya mazoezi, vijana wanalala sehemu nzuri… ndio maana naamini nyinyi hakuna sababu ya kutofanikiwa"

" RAY AFUNGUKA KUHUSU SAKATA LA FILAMU YAKE YA "SISTER MARRY" ILIYODAIWA KUFUNGIWA

Mwigizaji mahiri wa Bongo Movies Vicent Kigosi maarufu kama Ray amewatoa hofu mashabiki wake kuhusu filamu yake ya ‘Sister Mary’ kuwa haijafungiwa japo kuna baadhi ya sehemu wameambiwa wazifanyie marekebisho na baadaye itakuja kutoka.

Ray amekuwa akilalamikia wahakiki wa kazi za wasanii kutowatendea haki pale wanapowapelekea kazi ambazo zinawagusa wahakiki na kushindwa kuzitendea maamuzi yalio sahihi.

“Kuna udhaifu mkubwa katika kuhakiki kazi ya mwisho ya msanii kwa kuwa wanaohakiki mara nyingi hawapendi filamu inayowagusa na kuwakosoa,” amesema Ray.

Sister Mary ilidaiwa kuwa inalidhalilisha kanisa katoliki na hivyo mapadre kutaka ipigwe marufuku.

Friday, March 22, 2013

WAKILI MAWALA NYAGA AJIUA KWA KUJITUPA TOKA JUU YA GHOROF

Imenukuliwa kutoka kwenye gazeti la Mwananchi, ARUSHA-- Giza limeukumba Mkoa wa Arusha baada ya kutokea vifo vya ghafla vya watu maarufu. Jana Wakili Nyaga Mawalla alifariki baada ya kujirusha kutoka ghorofani akiwa jijini Nairobi, Kenya alikokwenda kwa matibabu.

Habari zilizopatikana zinaeleza kuwa Nyaga alikufa baada ya kujirusha kutoka katika jengo la ghorofa ya hospitali aliyokuwa akitibiwa jijini Nairobi usiku wa kuamkia jana.

Mfanyakazi wa Kampuni ya Mawalla Advocate, John Minja aliliambia gazeti hili kuwa mwili wa marehemu ulitarajiwa kurejeshwa nchini jana.

MAANDAMANO YA CHADEMA KESHO: MBOWE ADAI YAKO PALE PALE NA WATAANDAMANA MBELE YA RAIS WA CHINA

 LICHA ya serikali kuyapiga marufuku maandamano yaliyoratibiwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kuishinikiza kumwajibisha Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi na Naibu wake wajiuzulu kutokana na matokeo mabaya ya mtihani wa kidato cha nne 2012, chama hicho kimesema yapo pale pale.
Chama hicho kimewaomba wananchi wote waliochoshwa na kufelishwa kwa watoto wao, kunyimwa elimu bora wajitokeze kuandamana kwa nguvu zote, na wanafunzi wote waliofeli pia wajitokeze kudai elimu bora kwani ni haki yao.

Akizungumza kwa simu na gazeti hili jana na kutoa msimamo huo, Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe alisema “wananchi wajitokeze kwa wingi ili kilio chao kisikike duniani kote.”

Alisisitiza kuwa maandamano hayo yatafanyika mbele ya ugeni wa Rais wa China, Xi Jinping ili kufikisha kilio hicho na kamwe haikubaliani na sababu ya serikali kuyazuia kwa sababu ya ugeni huo.

RIPOTI YA POLISI: MADAI YA KULAWITIWA KWA WANAFUNZI WA IFM SI YA KWELI

 Kamati iliyoundwa kuchunguza vitendo vya udhalilishaji na kuporwa vitu vyao  wanavyofanyiwa wanafunzi  wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), wanaoishi  katika hosteli zilizopo Kigamboni Manispaa ya Temeke imebaini hakuna wanafunzi waliofanyiwa vitendo hivyo.

Kamati hiyo iliyoundwa na Kamanda wa Polisi, Kanda Maalumu ya Polisi jijini Dar es Salaam, Suleiman Kova baada ya kuwahutubia wanafunzi hao katika Viwanja vya Machava, ilijumuisha wanafunzi wanne wa IFM na wakuu wa upelelezi kutoka kanda hiyo .
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kipolisi Temeke, Englebert Kiondo, alisema kamati hiyo ilichunguza kwa kina madai hayo ya wanafunzi, lakini hakuna na hata moja walilobaini kuwa na ukweli .

JACK CHUZI WA BONGO MOVIE ABADILI DINI NA KUOLEWA....


 
 Katika Hali ya Kushtusha na Kufuraisha....Staa wa Bongo Movie Jack Pentezel amewashtusha wengi baada ya Kuamua kubadili dini kuwa Muislamu kisha kuolewa na Mpenzi wake wa Muda Gadner Dibibi....

wadau wengi na wapenzi wa Bongo Movie wamekuwa wakihoji juu ya Ndoa Hiyo iliofungwa kisiri sana na kwa haraka,Je Ndoa Hiyo Itadumu? Je ni kweli wamehamua kukaa kwenye Maadili ya Ndoa..? au Ni kama Mchezo wa Mjini kubadilishana Dini na kuoana mwishowe ni kuachana....Tusubiri Tuone.....

Mpekuzi  inapenda kumtakia Jack Pentezel na Mumewe Gadner Dibibi Baraka Tele,Amani na Upendo utawale kwenye Maisha yao ya Ndoa..

" MIMI NI MTI WENYE MATUNDA MILELE....SIOGOPI KUPIGWA MAWE"... HUU NI UJUMBE WA DIAMOND

MSANII wa muziki wa bongo fleva Diamond Platinam ameendelea kujinadi kupitia mitandao ya kijamiii huku akiteka hisia za mashabiki wake kwa kutuma baadhi ya picha zinazomuonyesha akiwa jukwaani akifanya 'makamuzi' pamoja na kutuma ujumbe wa kujipongeza kwa kazi anayoifanya

Kupitia mtandao wake wa 'Instagram' msanii huyo alituma ujumbe uliosomeka hivi "Mimi ni mti wenye matunda milele siogopi kupigwa mawe"

Ujumbe huo ulionekana kuteka baadhi ya mashabiki wake huku wengine wakituma ujumbe za kumpongeza kwa kuwa na imani hiyo huku akionyesha kutoteteleka kwa jambo lolote linalomkabili ambalo linaonyesha kutaka kumdondosha kimuziki

Maneno ya ujumbe huo pia umeonekana kutumiwa katika nyimbo yake mpya inayojulikana kwa jina la 'Muziki gani' ambayo wameshirikiana na msanii Ney wa Mitego

RIPOTI YA GAZETI LA IJUMAA KUHUSU WABUNGE KUTEMBEA NA WANAFUNZI WA CHUO KIKUU CHA DODOMA ( UDOM )

 MITANDAO mingi ya kijamii na kurasa binafsi za mawasiliano zinazopatikana ndani ya simu za viganjani kama Instagram, WhatsApp na BBM (Blackberry Messenger) zinazomilikiwa na baadhi ya wasichana wanaosoma Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom) zimejaa mambo ya ngono na kashfa kwa baadhi ya wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Unyemeleaji taarifa uliofanywa na Ijumaa kwa muda mrefu kwenye huduma hizo za mawasiliano ya kisasa  umebaini wanafunzi wa kike wamewabatiza jina la ‘mabuzi yao’ baadhi ya wabunge.

Bila kupepesa mitandao hiyo imekuwa pia ikitumiwa na wasichana hao kuuza miili yao huku ufahari kama si ujanja ukiwa ni mtu kujipatia bwana mwenye cheo cha ubunge ambaye anaaminika waleti yake haikaukiwi fedha kutokana na posho za vikao na utumishi wa umma.

MAHAKAMA KUU YAITISHA MAFAILI YA KESI YA LWAKATARE

Dar es Salaam. Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, imeiamuru Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu iwasilishe majalada ya kesi ya ugaidi inayomuhusu Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chadema, Wilfred Lwakatare na mwenzake katika kesi hiyo, Ludovick Joseph.

Hati ya kuitisha majalada hayo ilitolewa jana alasiri na Msajili wa Mahakama Kuu, baada ya mawakili wanaomtetea Lwakatare kuwasilisha maombi ya marejeo ya mwenendo wa kesi hiyo, iliyofunguliwa katika Mahakama ya Kisutu.

"NAWASHANGAA WANAOPOTEZA MUDA KUYAFUATILIA MAISHA YANGU"....WEMA SEPETU

Msanii anayetafuta mafanikio kwa kasi, Wema  Sepetu amesema kuwa haoni sababu ya watu kutishiana maisha hasa kwa kipindi hiki ambacho maisha yapo juu.

Wema alisema hayo kufuatia hivi karibuni  kutishiwa maisha na watu asiowafahamu na  kulazimika kuongeza ulinzi nyumbani kwake na  kila anapokuwa anatoka.

Alisema maisha ni magumu na kila mmoja  anatakiwa afanye kazi kwa bidii ili kufikia  malengo, badala yake watu wanaanza kutishiana  maisha.

"Nawashangaa watu wanaoendelea kuwafuatafuata  wengine wanapata wapi ujasiri huo na hali ya  maisha ilivyo ngumu na kuhitaji muda mwingi wa  kufanya kazi ili kujikwamua,"alishangaa Wema.

Aidha, aliongeza kuwa hana adui wala mtu ambaye  anamdai au kitu kama hicho hivyo watu  wanaomtumia mesaji za vitisho anahisi wana chuki  binafsi na si kingine.

Thursday, March 21, 2013

Meneja Fastjet akamatwa

                                           Wafanyakazi wa shirika la ndege, Fast Jet
Meneja wa wahudumu wa ndege za kampuni ya ndege ya Fastjet, Emma Donavan, amekamatwa na polisi, kuwekwa mahabusu na kuhojiwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam kwa tuhuma za kumtolea lugha ya matusi mmoja wa wafanyakazi wa kampuni hiyo.

Polisi walimshikilia na kumhoji Donavan kwa takribani saa tisa kuhusiana na tuhuma za kumtolea lugha ya matusi mfanyakazi huyo raia wa Tanzania.

Kamanda wa Polisi wa Viwanja vya Ndege, Deusdedit Kato, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba meneja huyo alikamatwa jana saa 2:00 asubuhi kwa tuhuma za kumtukana mfanyakazi mwenzake, Samson Isembe, ambaye ni Ofisa Mwendeshaji wa kampuni hiyo.

Nyerere, Karume watajwa kesi ya wafuasi wa Ponda

                                          Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere
Shahidi wa utetezi  na Mwanzilishi wa Baraza la Misikiti Tanganyika, Bilali Waikela (87), amedai mahakamani katika kesi inayomkabili Sheikh Issa Ponda na wenzake 49, kwamba  Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere na Rais wa kwanza wa Zanzibar, Shekhe Abeid Karume, walivunja Umoja wa Waislamu wa Afrika Mashiriki.

Waikela alidai kuwa umoja huo ulianzishwa kwa lengo la kuwatetea na kuwasaidia Waislamu na kwamba Tanzania ilipata kiwanja cha Chang’ombe Marcas kutoka kwa aliyekuwa Rais wa Misri.

Waikela ambaye ni shahidi wa 48 wa upande wa utetezi katika kesi hiyo alidai kuwa, umoja huo ulifutwa baada ya Karume kudanganywa kuwa wana mpango wa kufanya mapinduzi na kuwarudisha Waarabu Zanzibar.

“Mwalimu Nyerere ndiye aliyemtuma Karume afanye hivyo na mwaka 1964 nilifungwa baada ya kukataa kupokea Shilingi 40,000 ili nikubali kuvunja umoja huo, na  Kassim bin Juma, Adam Simba na Salehe Masasi waliotumiwa kuhamasisha watu kuvunja umoja huo,” alidai.

Alidai kuwa ofisi za umoja huo zilifungwa hadi mwaka 1968 lilipoundwa Baraza la Waislamu Tanzania (Bakwata) na kukabidhiwa ofisi pamoja na mali zote kikiwamo kiwanja cha Chang’ombe markazi kilichokuwa kimejengwa shule ya Waislamu.

CHANZO: NIPASHE