Thursday, January 17, 2013
Waziri Simba akabidhi vyerehani kwa wajane
Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Mhe. Sophia Simba
akimsikiliza Gavana wa Lions Ukanda wa Uganda na Tanzania, Joseph
Kiwanuka, wakati alipomtembelea leo ofisini kwake akiwa na ujumbe wa
watu watano.
Waziri Simba akiangalia baadhi ya vyerehani viwili viliyotolewa na Lions kwa ajili ya kuwasaidia wanawake wajane. Vyerehani hivyo ni kati ya 100 vitakavyotolewa na Lions kuwawezesha wanawake kujikimu kimaisha.
Waziri Simba akimkabidhi mmoja wa wafaidi wa vyerehani vilivyotolewa na Lions Bi. Jane Fuiko wakati wa hafla fupi ya kuwakabidhi zilizofanyika leo ofisini kwa Waziri.
Waziri Simba akiangalia baadhi ya vyerehani viwili viliyotolewa na Lions kwa ajili ya kuwasaidia wanawake wajane. Vyerehani hivyo ni kati ya 100 vitakavyotolewa na Lions kuwawezesha wanawake kujikimu kimaisha.
Waziri Simba akimkabidhi mmoja wa wafaidi wa vyerehani vilivyotolewa na Lions Bi. Jane Fuiko wakati wa hafla fupi ya kuwakabidhi zilizofanyika leo ofisini kwa Waziri.
WAFANYAKAZI OFISI YA WAZIRI MKUU WATOA MAONI YA KATIBA MPYA
Mjumbe wa Sekretarieti ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Bi. Hanifa
Masaninga (kushoto) akitoa ufafanuzi kuhusu mfumo uandaaji wa maoni ya
wananchi katika taarifa rasmi (Hansard) kwa wafanyakazi kutoka Ofisi ya
Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)wakiongozwa
na Kaimu Katibu Mkuu, Bw. Jamanne Sagini (wa pili kushoto) wakati
waliotembelea ofisi za Tume hiyo
Mjumbe wa Sekretarieti ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Bi. Nenelwa Mwihambi (kulia) akitoa maelezo kuhusu mfumo wa uchambuzi wa maoni ya wanachi kwa wafanyakazi kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)wakiongozwa na Kaimu Katibu Mkuu, Bw. Jamanne Sagini (Kaunda suti nyeupe) wakati waliotembelea ofisi za Tume hiyo
Mjumbe wa Sekretarieti ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Bi. Nenelwa Mwihambi (kulia) akitoa maelezo kuhusu mfumo wa uchambuzi wa maoni ya wanachi kwa wafanyakazi kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)wakiongozwa na Kaimu Katibu Mkuu, Bw. Jamanne Sagini (Kaunda suti nyeupe) wakati waliotembelea ofisi za Tume hiyo
Wednesday, January 16, 2013
Chadema sasa waanza kulipuana
KATIKA kuonyesha hali si shwari ndani ya Chadema, Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Vijana (Bavicha) wa chama hicho, Juliana Shonza amesema ameamua kumshtaki Mwenyekiti wake, John Heche kwa kumuita kuwa ni msaliti wa chama na kwamba anatumiwa na CCM na kuamua kumfukuza nafasi yake bila kutoa nafasi ya kusikilizwa.
Pia, amemlipua Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk Willibrod Slaa akidai kuwa amefanya ufisadi ndani ya chama kwa kujikopesha Sh140 milioni ambazo hajazilipa hadi sasa.
Mbali na hilo, amemshukia Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe kwa kudai kuwa anatoa kauli za kukurupuka ambazo zinakiyumbisha chama hicho kikuu cha upinzani nchini.
Shonza alitoa kauli hizo jana wakati akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam juu ya tuhuma zilizotolewa na mwenyekiti wa Bavicha na kuhusu kufukuzwa kwake ndani ya chama akiwa na wenzake Mtela Mwampamba na Habibu Mchange.
Pia, amemlipua Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk Willibrod Slaa akidai kuwa amefanya ufisadi ndani ya chama kwa kujikopesha Sh140 milioni ambazo hajazilipa hadi sasa.
Mbali na hilo, amemshukia Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe kwa kudai kuwa anatoa kauli za kukurupuka ambazo zinakiyumbisha chama hicho kikuu cha upinzani nchini.
Shonza alitoa kauli hizo jana wakati akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam juu ya tuhuma zilizotolewa na mwenyekiti wa Bavicha na kuhusu kufukuzwa kwake ndani ya chama akiwa na wenzake Mtela Mwampamba na Habibu Mchange.
Bus la champion lamgonga mtembea kwa miguu na kusababisha kifo
YAH: TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA DODOMA KWA VYOMBO VYA
HABARI TAREHE 15/01/2013
Mtu mmoja amefariki Dunia Mkoani Dodoma katika tukio la ajali ya gari kumgonga mtembea kwa miguu na kusababisha kifo.
Tukio hilo limetokea tarehe 14/01/2013 majira ya saa 09:30 alasiri katika kijiji cha Kelema Wilaya ya Chemba barabara ya DODOMA -KONDOA baada ya gari lenye namba za usajili T. 769 BNP aina ya Scania Bus mali ya Kampuni ya Champion likendeshwa na dereva aliyefahamika kwa jina la George s/o Maiko Kwayu likitokea Dodoma kuelekea Kondoa kumgonga mtembea kwa miguu na kumsababishia kifo chake papo hapo.
HABARI TAREHE 15/01/2013
Mtu mmoja amefariki Dunia Mkoani Dodoma katika tukio la ajali ya gari kumgonga mtembea kwa miguu na kusababisha kifo.
Tukio hilo limetokea tarehe 14/01/2013 majira ya saa 09:30 alasiri katika kijiji cha Kelema Wilaya ya Chemba barabara ya DODOMA -KONDOA baada ya gari lenye namba za usajili T. 769 BNP aina ya Scania Bus mali ya Kampuni ya Champion likendeshwa na dereva aliyefahamika kwa jina la George s/o Maiko Kwayu likitokea Dodoma kuelekea Kondoa kumgonga mtembea kwa miguu na kumsababishia kifo chake papo hapo.
MKE WA RAIS MAMA SALMA KIKWETE AWAFANYIA SHERRY PARTY WENZA WA MABALOZI
Mama salma akisoma hotuba
Wake wa Mabalozi katika hafla hiyokatika viwanja vya Ikulu
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiongea kwenye hafla maalumu ya kuwakaribisha wake wa Balozi nchini kwa mwaka mpya 2013, Hafla hiyo imefanyika katika viwanja vya Ikulu jijini Dar- es Salaam , Jan 15,2013,
JK: Uvumilivu sasa basi
SERIKALI imesema haitavumilia kwa namna yeyote ile vurugu za kidini, kikanda na ukabila ambazo baadhi yake zilitaka kulitia doa taifa mwaka jana. Pia imesisitiza kwamba haitawavumilia wanasiasa wanaotumia rasilimali za taifa kujitafutia umaarufu kwa gharama za kuligawa taifa.
Akizungumza na mabalozi kwa nyakati tofauti Ikulu, Dar es Salaam; kwanza katika sherehe ya kuukaribisha Mwaka Mpya iliyofanyika juzi na alipokuwa akiagana na Balozi wa Uingereza nchini, Dianne Corner jana, Rais Jakaya Kikwete alisema vurugu zilizotaka kujitokeza mwaka jana zinatosha.
“Serikali haitavumilia vurugu wala ukabila kwa namna yoyote ile…. Mwaka 2012 vurugu zenye sura ya kidini zilianza kujitokeza ila sasa nasema kwamba hatutazivumilia kwa namna yeyote ile, inatosha,” alisema Rais Kikwete.
Akizungumza na mabalozi kwa nyakati tofauti Ikulu, Dar es Salaam; kwanza katika sherehe ya kuukaribisha Mwaka Mpya iliyofanyika juzi na alipokuwa akiagana na Balozi wa Uingereza nchini, Dianne Corner jana, Rais Jakaya Kikwete alisema vurugu zilizotaka kujitokeza mwaka jana zinatosha.
“Serikali haitavumilia vurugu wala ukabila kwa namna yoyote ile…. Mwaka 2012 vurugu zenye sura ya kidini zilianza kujitokeza ila sasa nasema kwamba hatutazivumilia kwa namna yeyote ile, inatosha,” alisema Rais Kikwete.
MZEE MKAPA NA MZEE MSUYA WATOA MAONI LEO
Rais Mstaafu Mhe. Benjamin Mkapa (kulia) akiongea na Wajumbe wa Tume ya
Mabadiliko ya Katiba Jaji Mkuu Mstaafu Augustino Ramadhani (katikati) na
Dkt. Salim Ahmed Salim. Wajumbe wa Tume walikutana na Rais huyo Mstaafu
leo (Jumatano, Jan 16, 2013) jijini Dar es Salaam ili kupata maoni na
uzoefu wake katika uandishi wa Katiba Mpya.
Rais Mstaafu Mhe. Benjamin Mkapa akiwa na wageni wake
Rais Mstaafu Mhe. Benjamin Mkapa akiwa na wageni wake
JK: AZINDUA AWAMU YA KWANZA YA JENGO JIPYA LA HOSPITALI YA SHREE HINDU MANDAL JIJINI DAR ES SALAAM
Rais Dk. Jakaya Mrisho Kikwete akiwasha mshumaa kama ishara ya uzinduzi wa Awamu ya Kwanza ya jengo jipya na Awamu ya pili ya Hospitali ya Shree Hindu Mandal ya jijini Dar es salaam leo katika Mtaa wa Nyanza, ambapo huduma hiyo itapunguza msongamano wa wagonjwa katika hospitali jijini na kuongeza wigo wa utoaji huduma n kuongeza vitanda vya kulaza wagonjwa, Hospitali ya Shree Hindu Mandalilianzishwa mwaka 1931 ikianza na Zahanati anayeshuhudiatukio hilowa pili katikati ni Mwenyekiti wa hospitali hiyo Bw Ramesh Patel.
Rais Jakaya Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Uongozi , Madaktari , Wauguzi pamoja na wafanyakazi wa hospitali ya Shree Hindu Mandal mara baada ya kuzindua rasmi leo
Rais Dk. Jakaya Kikwete akikata utepe wakati wa uzinduzi wa hoapitali hiyo uliofanyika leo jijini Dar es salaam.
Rais Jakaya Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Uongozi , Madaktari , Wauguzi pamoja na wafanyakazi wa hospitali ya Shree Hindu Mandal mara baada ya kuzindua rasmi leo
Rais Dk. Jakaya Kikwete akikata utepe wakati wa uzinduzi wa hoapitali hiyo uliofanyika leo jijini Dar es salaam.
Manumba mahututi, alazwa Aga Khan
Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai wa Jeshi la Polisi (DCI), Kamishna Robert Manumba
HALI ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai wa Jeshi la Polisi (DCI), Kamishna Robert Manumba ni mbaya na amelazwa katika Chumba cha Wagonjwa Mahututi (ICU), Hospitali ya Aga Khan, Dar es Salaam.Habari zilizopatikana jana zilieleza kuwa Manumba amelazwa hospitalini hapo baada ya kusumbuliwa na maradhi kadhaa, ikiwamo figo.
Taarifa za ndani kutoka Jeshi la Polisi zilisema jana kuwa tangu juzi, Manumba alikuwa hajitambui baada ya kuugua malaria ghafla na hali hiyo ilisababisha pia figo zake zote mbili kushindwa kufanya kazi.
“Alitakiwa kupelekwa nje ya nchi kwa matibabu, lakini ilishindikana kwa sababu hajitambui, wakajaribu kumzindua, ikashindikana,” kilieleza chanzo hicho cha habari ndani ya jeshi hilo.
HALI ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai wa Jeshi la Polisi (DCI), Kamishna Robert Manumba ni mbaya na amelazwa katika Chumba cha Wagonjwa Mahututi (ICU), Hospitali ya Aga Khan, Dar es Salaam.Habari zilizopatikana jana zilieleza kuwa Manumba amelazwa hospitalini hapo baada ya kusumbuliwa na maradhi kadhaa, ikiwamo figo.
Taarifa za ndani kutoka Jeshi la Polisi zilisema jana kuwa tangu juzi, Manumba alikuwa hajitambui baada ya kuugua malaria ghafla na hali hiyo ilisababisha pia figo zake zote mbili kushindwa kufanya kazi.
“Alitakiwa kupelekwa nje ya nchi kwa matibabu, lakini ilishindikana kwa sababu hajitambui, wakajaribu kumzindua, ikashindikana,” kilieleza chanzo hicho cha habari ndani ya jeshi hilo.
Monday, January 14, 2013
RAIS KIKWETE KATIKA UFUNGUZI WA SKULI YA MLIMANI MATEMWE
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Jakaya Mrisho Kikwete amewataka wazee wa matemwe kuitumia fursa waliyopata ya kujengewa Skuli ya kisasa katika kijiji hicho kwa kuwasimamia vijana wao kupata elimu.
Rais Kikwete ameeleza hayo katika ufunguzi wa skuli mpya ya Mlimani Matmwe ambayo ni miongoni mwa skuli 19 zilizomo kwenye mradi wa Uimarishaji wa Elimu ya lazima Zanzibar (ZABEID) ikiwa ni miongoni mwa maadhimisho ya miaka 49 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Amesema wazazi wanapaswa kuwa karibu zaidi katika maendeleo ya elimu ya watoto wao kwa kuwapatia mahitaji yao ya lazima na hata kujinyima katika baadhi ya mambo na kuwapa ushauri wa mara kwa mara.
“Fursa waliyopata vijana wenu hivi sasa ilikosekana hapa Matemwe kwa miaka mingi kabla ya Mapinduzi ya Zanzibar, hivyo mchango wenu ni muhimu katika kujenga maisha bora ya baadae ya watoto wenu”, amesema Dk. Kikwete
Rais Kikwete ameeleza hayo katika ufunguzi wa skuli mpya ya Mlimani Matmwe ambayo ni miongoni mwa skuli 19 zilizomo kwenye mradi wa Uimarishaji wa Elimu ya lazima Zanzibar (ZABEID) ikiwa ni miongoni mwa maadhimisho ya miaka 49 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Amesema wazazi wanapaswa kuwa karibu zaidi katika maendeleo ya elimu ya watoto wao kwa kuwapatia mahitaji yao ya lazima na hata kujinyima katika baadhi ya mambo na kuwapa ushauri wa mara kwa mara.
“Fursa waliyopata vijana wenu hivi sasa ilikosekana hapa Matemwe kwa miaka mingi kabla ya Mapinduzi ya Zanzibar, hivyo mchango wenu ni muhimu katika kujenga maisha bora ya baadae ya watoto wenu”, amesema Dk. Kikwete
Sunday, January 13, 2013
BONDIA MTANZANIA THOMAS MSALI ALIVYOMKOROGA BERNARD MACKOLIECH WA KENYA
Bondia Mtanzania Thomas Mashali kushoto akiwa amemgalagaza bondiaBernad
Mackoliech na kwenda chini akimsubili ili amwendelezee kipondo wakati wa
mchezo wao wa kugombania ubingwa wa Afrika Mashariki uliofanyika katika
ukumbi wa Friends Conner, Manzese jijini Dar es Salaam na Mashali
kuibuka na ushindi wa K,O katika raundi ya sita
Bondia Bernad Mackoliech wa kenya na Mtanzania Thomas Mashali wakioneshana ufundi wa kutupiana makonde wakati wa mchezo wao wa ubingwa wa Afrika Mashariki Mashali alishinda kwa K,O raundi ya sita
Baadhi ya mashabiki waliojitokeza katika mpambano huo wa ubingwa wa Afrika Mashariki
Refarii Mark Hatia akimwesabia Bondia Bernad Mackoliech huku akimuamuluThomas Mashalikwenda katika kona nyeupe baada ya kumtwanga konde zito lililomsababisha kulamba sakafu wakati wa mpambano wao wa ubingwa wa Afrika Mashariki
Kamanda wa polisi mkoa wa Kipolisi wa kinondoni Charles Kenyela akimvisha ubingwa wa Afrika Mashariki bondia Thomas Mashali baada ya kumpiga Bernad Mackoliech wa Kenya kwa K,O Raundi ya 6
Refarii Mark Hatia akimwesabia Bondia Bernad Mackoliech huku akimuamuluThomas Mashalikwenda katika kona nyeupe baada ya kumtwanga konde zito lililomsababisha kulamba sakafu wakati wa mpambano wao wa ubingwa wa Afrika Mashariki. Picha zote na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Bernad Mackoliech wa kenya na Mtanzania Thomas Mashali wakioneshana ufundi wa kutupiana makonde wakati wa mchezo wao wa ubingwa wa Afrika Mashariki Mashali alishinda kwa K,O raundi ya sita
Baadhi ya mashabiki waliojitokeza katika mpambano huo wa ubingwa wa Afrika Mashariki
Refarii Mark Hatia akimwesabia Bondia Bernad Mackoliech huku akimuamuluThomas Mashalikwenda katika kona nyeupe baada ya kumtwanga konde zito lililomsababisha kulamba sakafu wakati wa mpambano wao wa ubingwa wa Afrika Mashariki
Kamanda wa polisi mkoa wa Kipolisi wa kinondoni Charles Kenyela akimvisha ubingwa wa Afrika Mashariki bondia Thomas Mashali baada ya kumpiga Bernad Mackoliech wa Kenya kwa K,O Raundi ya 6
Refarii Mark Hatia akimwesabia Bondia Bernad Mackoliech huku akimuamuluThomas Mashalikwenda katika kona nyeupe baada ya kumtwanga konde zito lililomsababisha kulamba sakafu wakati wa mpambano wao wa ubingwa wa Afrika Mashariki. Picha zote na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Subscribe to:
Posts (Atom)













































