Sunday, June 22, 2014

Breaking News, Ajali iliyoua sita leo Dar es salaam.



Watu sita wamefariki papo hapo na wengine 12 kujeruhiwa kufuatia ajali mbaya iliyohusisha magari manne iliyotokea eneo la Makongo karibu na hospitali ya Lugalo Dar es salaam.

Baadhi ya mashahuda wa ajali hii wamesema kuwa imesababishwa na uzembe uliofanywa na dereva wa daladala iliyokuwa ikitoka Tegeta kwa kupita upande usio wake.