Thursday, September 27, 2012

Ushirikiano wa pamoja unahitajika ili kumuinua mwanamke na mtoto wa kike


Mshikamano  wa pamoja unahitajika baina ya nchi zilizoendelea na zinazoendelea ili kuhakikisha kuwa mtoto wa kike ambaye hajapata nafasi ya kwenda shule anapata elimu, kuwainua wanawake kiuchumi na kupunguza vifo vya kinamama wajawazito na watoto vinavyotokana na tatizo la uzazi na  ugonjwa wa kansa.

 Hayo yamesemwa  jana na Mke wa rais Mama Salma Kikwete wakati akichangia mada  kwenye mkutano wa The RAND African First Ladies Initiative uliofanyika makao Makuu ya Taasisi ya Ford mjini New York nchini Marekani.
Mama Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) alisema kuwa taasisi mbalimbali za Kiserikali na zisizo za kiserikali zinafanya jitihada kubwa ya kuhakikisha kuwa zinawasaidia wanawake wanaokabiliwa na changamoto mbalimbali za maisha  tatizo  lililopo ni upungufu wa rasilimai fedha za kuweza kukabiliana  na changamoto hizo  hivyo basi ushirikiano wa pamoja unahitajika ili kuweza kufanikisha malengo hayo.

  Aliendelea kusema kuwa watoto wa kike wakipata elimu ya kutosha watakuwa na silaha muhimu katika maisha yao ya kuweza  kupambana na matatizo mbalimbali  ikiwa ni pamoja na maradhi, ujinga na umaskini  kwani elimu ni nguzo muhimu katika maendeleo ya taifa lolote Duniani bila ya watu kuwa na  na elimu nchi haiwezi kuendelea.

Magazeti Ya Leo Alhamisi 27th September 2012


fujo zatokea mjini arusha wafanya biashara ndogondogo na mapolisi

Mji wa arusha umechafuka ghafla baada ya wafanyabiashara ndogo ndogo mjini hapa kuvamia eneo lililouzwa na aliyekuwa meya miaka ya nyuma. Eneo hilo liko karibu na soko la kilombero. Hali hiyo imekuja baada wa manispaa ya arusha kukamata bidhaa za wafanyabiashara hao ambapo eneo walilokuwa wamepangiwa kuwa dogo kuliko wafanyabiashara hao. angalia picha yaliyojiri
           Wafanyabiashara wakiondoa mabati yaliyokuwa yamezungushiwa eneo hili lililokuwa limeuzwa


                                             Magari ya FFU yakiwa yamepaki pembeni
                                             Askari wakiwa pembeni wakiangalia
                                       Hii ndio hali Halisi ilivyokuwa leo mjini arusha