Friday, July 13, 2012

Rais Jakaya Mrisho Kikwete Akishiriki kikao Maalumu.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akishiriki katika kikao maalumu cha maandalizi ya mkutano wa Commonwealth Partnership for Technology Management (CPTM) kwenye makao makuu ya CPTM inayojiandaa kwa mkutano wake mkuu wa Global 2012 International Smart Partneship Dialogue unaotarajiwa kufanyika mwezi Mei Mwakani jijini Dar es salaam.

Netherland Kuwekeza Sekta Ya Afya Nchini

Kaimu mgaga mkuu wa serikali Dkt. Donan Mmbando akizungumza na ujumbe wa Biashara na Uwekezaji katika huduma za afya kutoka nchini Netherland  mara baada ya ujumbe huo kuwasili makao makuu ya Wizara ya Afya na Ustawi  wa jamii jana jijini Dar es Salaam.
 Watendaji wakuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii wakiwa katika picha ya pamoja na ujumbe wa Biashara na Uwekezaji katika huduma za afya kutoka nchini Netherland .

Dr.Slaa,Mbowe Na Lema Wakamatwa

Kwamba wanashikiliwa Central Dar.Tutawaletea habari kamili tutakapokuwa tumejuwa sababu ya wao kukamatwa.labda madai yao kuuawa na kukataa kupeleka madai polisi.

Taarifa Kwa Umma Juu Ya Hali Ya Utendaji Wa Viongozi Wa Bunge

CIVIL AND POLITICAL RIGHTS WATCH
The Citizens’ Parliament watch
Plot 522 Block E, Sinza Palestina, P. O. Box 522, Dar Es Salaam,
Telephone:0784417307,E-mail:ed.civilrights@yahoo.com; marcossy@yahoo.com Dated 18th JUNE, 2012.

TAARIFA KWA UMMA JUU YA HALI YA UTENDAJI WA VIONGOZI WA BUNGE
Taarifa hii ni matokeo ya ufuatiliaji wa shughuli za Bunge na mijadala ya Wabunge juu ya mahitaji ya umma kwao kwenye maendeleo, uongozi, kuimarisha utawala bora, uwajibikaji wa serikali na haki za binadamu na kuimarisha usimamizi wao kwa serikali kupitia mijadala yao katika vikao vya Bunge. Taarifa hii inahusika na utendaji wa viongozi wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mwaka 2011.

Kwa Ujumla:
Kumekuwa na upendeleo wa vyama katika kujadili na kuchangia hoja na kuonekana Mh Spika na Wenyeviti wa vikao kutumia vibaya kanuni za bunge kuwadhibiti wabunge kulingana na vyama vyao. Mfano ni pale Mh Spika alipomzuia Mh Tundu Lissu kumwuliza swali Mh Mizengo Pinda juu ya mauaji ya raia mikononi mwa vyombo vya dola kwa madai kuwa kuna kesi mahakamani juu ya hoja hiyo. Pamoja na Mh Lissu kujitahidi kufafanua tofauti zilizopo kati ya kesi inayomkabili yeye na wenzake na hoja anayoiulizia, bado Mh Spika ameendelea kuizuia hoja hiyo. Kulingana na maoni ya wabunge 36, Watendaji 22, wachambuzi 11 na wananchi 48 waliohojiwa, ubora wa uongozi wa bunge kwa mwaka 2011 ni kama ilivyo hapa chini:


NAFASI JINA SIFA YA KIPIMO ALAMA WASTANI MAONI YA WASHIRIKI
1 NDUGAI,
JOB
YUSTINO USIKIVU KWA WABUNGE 2.5 Amejitahidi sana kukwepa upendeleo wa kisiasa na kuilinda serikali; haoneshi utashi wake kumiliki mamlaka aliyopewa na Kanuni za Bunge anapoongoza vikao.
UZINGATIAJI KANUNI 2.625
UPENDELEO WA KISIASA 2.5625
UZINGATIAJI HOJA 2.375
USHABIKI BUNGENI 3
JUMLA KIWANGO 13.0625
WASTANI 2.6125
2 SIMBACHAWENE, USIKIVU KWA WABUNGE 2.125 Msikivu kwa Wabunge haswa wenye HOJA zenye maslahi kwa Taifa; Amejitahidi sana kukwepa upendeleo wa kisiasa na kuilinda serikali; Anayumbishwa na makundi au siasa.
GEORGE
BONIFACE UZINGATIAJI KANUNI 2.3125
UPENDELEO WA KISIASA 3.28125
UZINGATIAJI HOJA 2.09375
USHABIKI BUNGENI 3.4375
JUMLA KIWANGO 13.25
WASTANI 2.65
3 MAKINDA,
ANNE
SEMAMBA USIKIVU KWA WABUNGE 3.03125 Imara kwenye kanuni na kuzingatia hoja; Anayumbishwa na ushabiki kisiasa; si msikivu kwa wabunge.
UZINGATIAJI KANUNI 2.65625
UPENDELEO WA KISIASA 3.46875
UZINGATIAJI HOJA 2.75
USHABIKI BUNGENI 2.9375
JUMLA KIWANGO 14.84375
WASTANI 2.96875 Anajitahidi sana kuzingatia kanuni; Anayumbishwa na makundi kisiasa; si msikivu kwa wabunge.
4 MHAGAMA,
JENISTER
JOAKIM USIKIVU KWA WABUNGE 3.21875
UZINGATIAJI KANUNI 3.15625
UPENDELEO WA KISIASA 3.5
UZINGATIAJI HOJA 3.53125
USHABIKI BUNGENI 3.3125
JUMLA KIWANGO 16.71875
WASTANI 3.34375
5 MABUMBA,
SILVESTER
MASELE USIKIVU KWA WABUNGE 4.25 Haoneshi ushabiki wa wazi wa kisiasa; hushindwa kuhimili mivuto ya makundi na upendeleo wa kisiasa; Si msikivu kwa wabunge.
UZINGATIAJI KANUNI 4.25
UPENDELEO WA KISIASA 3.78125
UZINGATIAJI HOJA 3.90625
USHABIKI BUNGENI 3.25
JUMLA KIWANGO 19.4375
WASTANI 3.8875

ANGALIZO LA VIWANGO:
1.00 – 1.49 = Uongozi Mzuri Sana,
1.50 – 2.49 = Uongozi Mzuri
2.50 – 3.49 = Uongozi wa Wastani
3.50 – 4.49 = Uongozi Dhaifu
4.50 – 5.0 = Uongozi Dhaifu Sana

Kwa Ujumla
Taarifa hii imeonesha mapungufu kadhaa kwenye uongozi na utendaji wa kazi wa viongozi wa Bunge na hivyo kutoa changamoto kwa viongozi wa Bunge na wabunge kuimarisha utendaji wao iwapo wangependa kutekeleza wajibu wao kwa jamii. Ni matarajio yetu kuwa wabunge watatumia taarifa hii kuimarisha mjadala wa bajeti ya 2012/13 unaoendelea, ikiwa ni pamoja na kendeha na kusimamia vema vikao na mijadala ya Bunge na kutoa changamoto kwa utendaji wa serkali kwa maslahi ya jamii.

Tunakumbusha pia kuwa bado Bunge limeendelea kutumia muda vibaya kwa wabunge kuendeleza vijembe, kebehi, shukrani, pongezi na salamu. Hata baada ya miaka miwili sasa baada ya Uchaguzi na Serikali kuundwa bado wabunge wameendelea kutoa shukrani kwa Rais, wapiga kura wao na wengineo. Matumizi haya ya muda yanapunguza mijadala na mwendelezo wa ushiriki wa wabunge kwa ufasaha.

Mapendekezo
1. Ipo haja ya wabunge kujiangalia kwa karibu uwezo na utayari wao kujadili maswala ya maslahi kwa taifa bila kuingiza ushabiki na maslahi binafsi.
2. Iangaliwe upya akidi ya wabunge katika kupitisha hoja (angalau iwe robo tatu na sio nusu ya wabunge kama ilivyo sasa).Hii iendane na haja kwa Mhe, Spika kujiridhisha bila kuacha shaka juu ya idadi ya kura za wabunge kwenye hoja husika, na haswa walioshiriki mjadala baadala ya kuingia kwa ajili ya kupiga kura tu;
3. Spika atumie mamlaka na kanuni za Bunge ili kudhibiti maudhui, mantiki na maana ya mijadala ya Bunge bila kuathiri maslahi ya taifa. Katika hili Mhe Spika, Naibu na Wenyeviti wa Bunge,wana dhamana ya kuhakikisha ushabiki wa kisiasa haupati nafasi kuvuruga Bunge
4. Tunaona ipo nafasi kubwa kwa Spika kusaidia na kuelekeza bunge ili lifanye kazi zake vizuri zaidi. Spika atumie nafasi hii baadala ya yeye kuangukia kwenye ushabiki na kuilinda serikali.

Imetolewa na Taasisi ya Raia ya Haki za Kisiasa na Mwenendo wa Bunge,

CIVIL AND POLITICAL RIGHTS WATCH
Marcossy Albanie
Mkurugenzi Mtendaji

HAWA NDIO WATOTO WENGINE WA P DIDDY.

                                               Jessie, D’Lila na Chance.
According to blog ya Necole ni kwamba jana ilikua siku ambayo Rapper/Producer wa longtime P DIDDY alipata time ya kuspend na watoto wake mapacha wa miaka mitano baada ya mama yao ambae ni longtime girlfriend wake (Kim Porter) kukubali manake alikua hataki kabisa mapacha wake wakutane hasa na dada yao mwingine aitwae Chance ambae alizaliwa miezi mitano kabla ya mapacha hao lakini kwa mama mwingine ambae ni Sarah Chapman.

P Diddy ni miongoni mwa mastaa wenye watoto wengi lakini ndoa bado haijafungwa, Diddy tayari mpaka sasa ameshapata watoto na wanawake zaidi ya watatu huku November 4 mwaka huu akifikisha umri wa miaka 43.
Pamoja na kwamba ana watoto wengi na kila mmoja ana mama yake, Diddy amevunja rekodi ya kuwa baba anaetimiza mahitaji yote… hataki lawama au mtoto wake kupata tabu anawajibika kila anapohitajika, hii ilikua ni siku nyingine wakati wa birthday ya Chance.

                          PichaYa chini Mama (Sarah Chapman) mtoto na baba.

Huyu wa katikati tena ni mtoto wake mkubwa sasa anaitwa Justine

Thanks Millard Ayo Blog.

MADAKTARI KUANDAMANA TENA?

                              Dr Rodrick Kabangila upande wa kwanza kulia.
Kutokana na kusitishwa kwa ujasili wa madaktari zaidi ya 400 waliokuwepo kazini na wale wa mafunzo kwa vitendo Chama cha Madaktari (MAT) kimesema kimeandaa maandamano ya amani yatakayoshirikisha wanachama wake nchi nzima lengo likiwa ni kudai haki zao.

Katibu mkuu wa MAT Dr Rodrick Kabangila amesema tangu kuanza kwa vuguvugu la mgomo wa Madaktari, mambo mengi  yamekua yakifanywa kinyume na taaluma yao hivyo wameamua kukutana kesho ili kupanga maandamano.

Amesema lengo jingine la maandamano ya amani ni kuiomba serikali kuunda tume huru kufuatilia ishu ya kutekwa na kuteswa kwa Dr Ulimboka ambae kwa sasa yuko Afrika Kusini akipatiwa matibabu kutokana na huo mkasa pamoja na kupinga dhuluma na uonevu unaoendelea dhidi ya taaluma ya udaktari na madaktari wenyewe.

KAULI YA CHAMA CHA WALIMU KUHUSU KAULI YA NAIBU WAZIRI.

Chama cha walimu Tanzania CWT kimesema kimeshangazwa na kauli iliyotolewa jana bungeni na Naibu waziri ofisi ya waziri mkuu TAMISEMI Kassim Majaliwa kwamba chama hicho hakina mgogoro wa kimaslahi na serikali huku akitambua kwamba hiyo ishu iko kwenye majadiliano chini ya tume ya usuluhishi.

Rais wa chama cha walimu Gratian Mukoba amesema hiyo kauli ni ya upotoshaji na ni kulidanganya bunge pamoja na Watanzania na kusisitiza kwamba nchi ya kuendeshwa kwa girba sio hii, kama girba za mwaka  70 zitaendelea kutumika 2012 ni kwamba unaishi na kichwa cha zamani katika ulimwengu mpya.

Amesema ” hizi girba hazitawasaidia kuwapa walimu mshahara, hazitawasaidia waliokata tamaa kurudisha ari ya kazi… kinachotakiwa ni kutafutwa ni ukweli utakaosaidia nchi kwenda mbele”

Kuhusu ishu ya walimu kuingia rasmi kwenye mgomo rais huyo wa Chama cha Walimu amesema hatua hiyo itafikiwa kama majadiliano yanayoendelea sasa hivi kati yao na serikali yatafikia pazuri.

Amesisitiza kwamba “katika mkutano wetu hatukumaliza majadiliano kwa sababu upande wa serikali wameomba siku mpaka tarehe 20 July 2012, ndio tutarudi mezani kuzungumza kama wametuletea tunachokihitaji na kama hatutakubaliana msajili atatupatia cheti kwamba tumeshindwa kukubaliana na tutaendelea na hatua inayofuata ambayo ni kupiga kura na kuingia kwenye mgomo”

Magazeti yaleo13th July 2012