Saturday, February 9, 2013

Tanzania yashiriki utalii hispania

 Ujumbe wa Tanzania ukiwa katika picha ya pamoja na Youssou Ndour Waziri wa Utalii na Utamaduni nchini Senegal  ambaye pia ni mwanamuziki maarufu duniani wakati alipotembelea banda la Tanzania katika maonyesho hayo , Youssou Ndour amewahi kufanya ziara ya kimuziki mara tatu nchini Tanzania kabla ya kuteuliwa kuwa Waziri wa Utalii na Utamaduni nchini mwake.

Miss Utalii Tanzania 2013 kutembelea Hifadhi za Taifa na vivutio vya utalii





    Miss Utalii Tanzania 2012/13 wiki ijayo wataanza ziara ndefu ya kutembelea Hifadhi za Taifa na vivutio vya utalii katika mikoa ya Dar es salaam,Morogoro,Mtwara,Lindi na Pwani. Vivutio hivyo ni pamoja na Hifadhi za Taifa za Mikumi, Udizungwa, Saadani, Selous, pia maeneo ya kihistoria ya Bagamoyo, Amboni, Kijiji cha makumbusho,Makumbusho ya Taifa, Pugu sekondari,maeneo mengine ni ufukwe wa kigamboni, soko la kimataifa la Magogoni, Uwanja wa Taifa, uwanja wa ndege wa  J.K.Nyerere Air Port, Soko la Kariakoo, Mashule ya sekondari na msingi, pia watatembelea manispaa za Ilala, Temeke na Kinondoni ambapo watakutana na viongozi wakuu wa wilaya, mikoa, na wabunge katika majimbo ya mikoa hiyo.

JK atua msumbiji Jana

 Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya nchi jumuiya ya Maendeleo ya Uchumi Kusini Mwa Afrika SADC Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akikagua gwaride la heshima muda mfupi baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Maputo.Rais Kikwete yupo nchini Msumbiji kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi za SADC

MAgazeti ya leo Jumamosi ya 9th February 2013




YALIYOJIRI BUNGENI

 Mh Kigwangalla alimalizia kwa kusema “naomba atumie uungwana yeye mwenyewe kusimama katika bunge hili.. aidha kuwaomba radhi Watanzania kwa kudanganya ama kutimiza wajibu aliousema hapa yeye mwenyewe wa kujiuzulu, uongo aliousema ni mkubwa sana.. naomba nitoe hoja kwamba Mh Mbatia aadhibiwe kwa mujibu wa kanuni ya 63, asihudhurie vikao visivyozidi 20 na aombe radhi kwa maandishi kwa Watanzania kwa kusema uongo bungeni”