Friday, August 24, 2012

Magazeti ya leo Ijumaa 24th August 2012








Simba, Azam Zajiandaa Kwa Ajili Ya Ngao Ya Hisani Septemba 8

                                                                 Kikosi cha Simba.
                                                                 Kikosi cha Azam.

KATIKA kujiandaa na mechi ya Ngao ya Jamii, mabingwa wa Tanzania Bara, Simba SC, Jumamosi watacheza mechi ya kujipima nguvu na Mathare United ya Kenya kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid Arusha.

Simba itamenyana na Azam katika mechi ya Ngao ya Jamii ya kuashiria kufunguliwa kwa pazia la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Septemba 8, mwaka huu, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.


Habari za ndani kutoka Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), zimesema kwamba, kuchelewa kwa mechi hiyo ambako kumeenda sambamba na kuchelewa kuanza kwa ligi hiyo, kumetokana na kuchelewa kufikiwa mwafaka mapema wa mkataba mpya wa udhamini wa Ligi Kuu.

Wakati huo huo, Mshindi wa pili wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara, Azam FC Jumamosi watamenyana na Transit Camp kwenye Uwanja wa Chamazi, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.

Kihistoria hiyo itakuwa mechi ya tano ya Ngao ya Jamii kuchezwa nchini na ya pili kuishirikisha timu nje ya wapinzani wa jadi wa soka ya Tanzania, Simba na Yanga.
Mtibwa ilicheza na Yanga mwaka 2009, baada ya Simba kugoma na ikashinda mabao 2-1 na kutwaa Ngao, wakati kabla ya hapo, mwaka 2001, Ligi Kuu ya Tanzania ikiwa bado inadhaminiwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), kupitia bia ya Safari Lager, ilichezwa mechi ya kwanza ya Ngao kihistoria.

Katika mechi hiyo, Yanga ilishinda mabao 2-1 dhidi ya Simba na mwaka juzi Yanga iliifunga tena Simba kwa penali 3-1 kufuatia sare ya 0-0 na mwaka jana, Simba ilitwaa Ngao ya kwanza katika historia yake, kwa kuifunga Yanga mabao 2-0.


MABINGWA WA MECHI ZA NGAO YA JAMII:
Mwaka Mshindi Matokeo
2001 Yanga 2-1 Simba
2010 Yanga 0-0 Simba (3-1penalti)
2011 Simba 2-0 Yanga

Chanzo: http://bongostaz.blogspot.com

Mama Shujaa Wa Chakula Yapata Mdhamini-NMB

 Afisa Mtendaji Mkuu wa NMB, Mark Wiessing (Kulia) akizungumza katika hafla hiyo (kutoka kushoto)ni Mkurugenzi wa Maisha Plus, Masoud Ally na Mkurugenzi Mkazi wa Oxfam, Monica Gorman.
 Mkurugenzi Mkazi wa Oxfam, Monica Gorman (Kulia) akizungumza katika hafla hiyo, kushoto ni Mkurugenzi wa Maisha Plus, Masoud Ally.
                            Meneja Mawasiliano wa NMB Josephine Kulwa akifafanua jambo.

Mpango wa Mama Shujaa wa chakula unaoratibiwa na shirika la Oxfam ulianziashwa mwaka jana hapa Tanzania. Dhumuni likiwa ni kuthamini, kuwahamasisha na kuwasaidia wanawake wote katika uzalishaji wa chakula.

NMB kwa kutambua kuwa kilimo ndiyo shughuli kuu ya uchumi Tanzania na ikiwa benki yenye mtandao mpana zaidi Tanzania imetoa shilingi milioni 50 kwa ajili ya kuunga mkono mpango huu wa Mama Shujaa wa chakula kupitia kipindi cha televisheni kiitwacho Maisha Plus kinakachotarajiwa kurushwa mapema Oktoba mwaka huu.

Akizungumza katika hafla hiyo, Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB Bw. Mark Wiessing alisema,

udhamini huo ni sahihi kutokana na kuwa utakuza kilimo na kuwasaidia wakulima wadogo katika maisha, mapambano dhidi ya njaa,umasikini na uhaba wa ajira miongoni mwa wanawake.

“Tumeamua kudhamini mpango huu kwa lengo la kuwasaidia kinamama ambao ni wazalishaji wadogo wa mazao mbalimbali,ili waweze kupiga hatua katika kilimo kupitia mpango huu wa Mama shujaa wa chakula”alisema Mark.

Katika kuchochea maendeleo ya kilimo, NMB ni benki ya kwanza kuanzisha akaunti maalum kwa ajili ya wakulima iitwayo NMB Kilimo Account. Pia imeanzisha huduma ya mikopo kwa ajili ya mazao mengi ya kilimo ikiwemo chai,kahawa,miwa,alizeti,korosho na mazao mengine.

Mbali ya kutoa fedha na kusaidia wakulima katika maeneo mabalimbali, NMB imeongeza mikopo zaidi katika sekta ya kilimo hasa kwa wasambazaji na watengenezaji wa chakula toka mzalishaji mdogo hadi wasambazaji wakubwa.Vilevile NMB imesaidia vyama vya ushirika zaidi 600 vyenye zaidi ya wakulima 500,000 ambao ni wanachama.

NMB kupitia mpango wa NMB Finacial Fitness unaolenga kuongeza uelewa wa matumizi mazuri ya fedha itapata fursa ya kuwaelimisha washiriki kuhusu huduma za kifedha, uwekaji akiba, kupanga matumizi, matumizi mazuri ya kifedha na mengine mengi.Kama msemo wa kiswahili unavyosema” Ukimwelimisha mwanamke umeelimisha Jamii” .NMB inaamini NMB financial Fitness itamwezesha kila mwanamke kuwa na matumizi mazuri ya kifedha na kuwa na msingi mzuri wa maisha.

Mkurugenzi Mkazi wa Oxfam ,Monica Gorman pamoja na Mkurugezi wa Maisha Plus kwa nyakati tofauti waliishukuru NMB kwa mchango wake wakiamini washiriki 15 wa Mama shujaa wa chakula na 15 toka Maisha plus watafaidika na mpango wa NMB Financial Fitness. Chanzo: www.fullshangweblo.com