Saturday, November 26, 2016

Hi my people

Jamani tunaomba,radhi,kwa,kutokuwepohewanikwamuda,mrefu,ila,kwa,uwezo,wa,mungu,tumerudi,na,shetani,kashindwa.tunaendelezalibeneka,kama,kawaida

Thursday, February 4, 2016

ROYAL WEDDING YA WAHAYA……







Wamependeza hadi basi Mungu awatangulie Kwenye maisha Haya Mapya zidisheni upendo mzidi kupendeza

Kupendeza raha jamani call 0754 590 221 Arusha Town Upendeze






Wema Sepetu amekua Mtanzania wa pili kufikisha followers milioni moja Instagram


Ikiwa ni siku chache baada ya mwimbaji Diamond Platnumz kuwa msanii wa kwanza wa bongo fleva kuwa na wafuasi milioni 1 kwenye mtandao wa kijamii wa Instagram, mwigizaji Wema Sepetu ameiandika rekodi kwa kuwa staa wa pili Tanzania kufikisha followers milioni moja.

Huku Tanzania ikitajwa kuwa ya kwanza kwa utumiaji wa mtandao wa Instagram Africa, mastaa wengine wenye followers wengi ni pamoja na Vanessa Mdee mwenye zaidi ya laki nane na elfu 40, Jokate mwenye zaidi ya laki nane na elfu sitini na Ommy Dimpoz mwenye zaidi ya laki saba.

Msanii gani ukisikia nyimbo zake unahisi uwepo mungu


                                                                      Rozi Muhando
Christina Shusho

                                                                  Flora Mbasha

                                                                  Upendo kilahiro

Wednesday, February 3, 2016

RIP Kelvin Kaloosh

                                                                 Kelvin Kaloosh

 Ajali hii imetokea jijini Dar, karibu na Ubalozi wa Kenya

Poleni sana wafiwa na wote walioguswa na msiba huu Hasa wasanii na watu maarufu

Wema Sepetu Aelezea Kwa Kina Beef yake na Zari, ‘Sio Nasib Wala sio Mwanamke Wake, Wote Waniache’


Wema Sepetu amefunguka kwa mapana kuhusiana na ugomvi wake na Zari the Bosslady ulioshuhudia warembo hao wakibadilishana michambo kwenye Instagram.


Miss Tanzania huyo wa zamani alikuwa akihojiwa kwenye Ijumaa hii kwenye kipindi cha Ala za Roho cha Clouds FM. Alikuwa ameongozana na mpenzi wake, Idris Sultan.

Mimi nilivyoamua kuwa out of Diamond’s life niliamua hivyo and I am out of Diamond’s life. I don’t know why watu wanajaribisha sana kunibring back to his life wakati I have already like moved on,” alisema Wema.

“I accepted my break up with Diamond from the beginning and I never wanted anything to do with him, nilivyoamua kwamba this is is going to be it nikaamua. Mimi na Diamond tumeachana 2014 and I was the one who actually decided that it’s going to be over. Lakini wakati Diamond ameshamove on ameshakutana na girlfriend wake, mama wa mtoto wake mimi sikuwahi kujihusisha katika mambo yao. Lakini I think the girl (Zari) anakuwa kama ana kitu na mimi. I have been quite for a very long time, first year nimekaa kimya, second year nimekaa kimya, it’s like kama vile anataka kunichokonoa,” alifafanua.

Instagram kwa kukuza mambo ni shida


Etiii  mwanamuziki Diamond Platnumz na Idriss Sultan Waonyeshana Uanaume Laivu

Leo Diamond na Idriss Wameonyesha kuwe wenyewe ni wanaume pale ambapo Diamond Platnumz Amemuwish Happy Birthday Idriss na Idriss kujibu bila tatizo lolote huku kukiwa na fukuto la ugomvi mtandaoni kati ya wapenzi wao Wema Sepetu na Zari Hassan

Wabongo tujifunze kuwa na bifu na mtu mmoja sio wote ni wabaya kwako utapoteza wengi wanaokuhitaji naamini fans wenu wanajali sana mahusiano yenu ya wanawake waachieni wanawake jamani big up to all Platnumz na Idriss

Mtoto wa Taifa (Kampuni Tatu Zamtaka Mtoto wa Wema Sepetu Atakapozaliwa


Kampuni tatu zimejitokeza kutaka kumtumia kibiashara mtoto atakayezaliwa baada ya staa wa filamu Wema Sepetu kujifungua baadaye mwaka huu.

Chanzo cha uhakika kilicho karibu na staa huyo, kimesema kampuni hizo ambazo hakuzitaja kwa kushindwa kukariri majina yake, zimeshafanya mazungumzo ya awali na Wema, kwani wanaamini mtoto huyo atakuwa kivutio kikubwa.

“Hivi ninavyokuambia licha ya kampuni hizo, tayari wengine wamejitokeza na kudai watamvalisha kwa muda wa mwaka mzima mtoto huyo,” kilisema chanzo hicho.

Ripota wetu ilimtafutamtafuta muigizaji huyo na kuulizia juu ya ishu hiyo, ambapo alicheka na kudai hayuko katika nafasi nzuri kwa muda huo ili kuzungumzia suala hilo hadi hapo baadaye.

“Kwa sasa ni mapema mno kuzungumzia hilo jambo, nitaweka wazi baadaye,” alisema Wema

Aunt Ezekiel Adaiwa kafunga ndoa Kwa siri

KUNASWA kwa msanii wa filamu Bongo, Aunt Ezekiel akiwa ndani ya gauni la harusi (shela) kumezua maswali tata huku wadau wakiamini alikuwa safarini kwenda ukumbini kwa ajili ya harusi yake.

Aunt alinaswa hivi karibuni akitoka ndani ya saluni moja iitwayo Wedding  Dover, Sinza Afrikasana akitoka akiwa ndani ya shela hilo.

Kwa mujibu wa chanzo chetu, baadhi ya watu waliamini Aunt alikuwa kwa ajili ya sherehe hizo kwani kuingia kwake saluni hapo mpaka kutoka akiwa amepambwa kulichukua saa moja.

AUNT EZEKIEL“Hizo picha mimi nimezipata akiwa ndani ya hoteli maarufu pale Sinza Afrikasana. Kila mtu alisema bibiye kafunga ndoa kwa siri na mzazi mwenzake, Iyobo (Moses) na harusi yake ni kwa siri,” kilisema chanzo.

Baada ya mwandishi kunasa habari hizo, alimtafuta Aunt ili aweze kuzungumzia kuhusu kuvaa gauni hilo ambapo alichenga na kusema kuwa muda utakapofika ataweka wazi kila kitu.

“Unajua kila mtu katika maisha yake na taratibu zake, sasa mimi bado sijapanga kulizungumzia hilo la kufunga ndoa ya siri mimi na Iyobo. Ila muda ukifika nitaweka wazi kila kitu. Hilo gauni lisikutishe ndugu yangu,” alisema Aunt.
Source-Global Publishers

Udaku wa Insta sikia hii


Mwigizaji Batuli Afunguka Kuhusu Kuzulimiwa na Ray Kwenye Movies Mpya ya Bosi Mfupi..Warushiana Maneno Insta

Waigizaji Batuli na Ray ni kama wana bifu la chini chini baada ya kurushiana maneno Instagram Picha ilianza pale Lemutuz alivyoshare Tangazo la Movie yao mpya iitwayo tajiri mfupi kwenye page yake ya Instagram ambapo Mwigizaji Batuli Aliandika kwenye picha hiyo maneno fuatilia udakus  ...

Friday, January 29, 2016

Idris na Wema watarajia mtoto mwezi July 2016


Akizungumza katika kipindi cha Amplifaya cha Clouds FM Jumanne hii, Idris alisema mpenzi wake huyo anatarajia kupata mtoto baada ya miezi 6 au 7 hali ambayo imetafsiriwa na wadau wa mambo kuwa huenda mwanadada huyo akawa na mimba ya miezi 3 au 2.
“Yes very soon natarajia kupata mtoto kama miezi 6 au 7 ijayo,” alisema Idris. Pia Idris alisema bado hajatambua jinsia ya mtoto anayetarajia kujifungua mpenzi wake.
“No hatujui mwenzangu anataka surprise. Mimi nataka kujua kabla kwahiyo bado hatujafikia muafaka, naogopa nisije nikawa nanunua vigauni akaja Wa kiume bure,” alisema.

Aliongeza, “Huwezi kuwazuia watu kuongea, waache waongee maana sometimes watu ni wagumu kupokea changes lakini siku zinavyoenda naamini wataelewa tu.”

Wema na Idris Wafunguka kuhusu mapenzi yao

Idris na wema wafunguka kuhusu mahusiano yao na zuri zaidi madaam anategemea kupata mtoto soon .  tunakuombea mungu akupe afya njema wewe naa familia yako kiukweli timu wema mmuacheni wema aapate muda wakutulia na kupumzika ili kumpa mtoto uwezo wa kukua na afya safi sana idris mungu akupe ujasiri wa kukubaliana na hali halisi we proud to have u &madaam