Wednesday, August 22, 2012

MATOKEO YA MECHI YA CHELSEA JANA PAMOJA NA WAFUNGAJI WAKE.


TTB yawatunuku Vyeti watanzania waliofanya vyema katika Utalii

Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii nchini Tanzania TTB Dk Aloyce Nzuki wa tatu kutoka kushoto akiwa katika picha ya pamoja na watanzania hao wakiwa wameshika vyeti vyao kushoto ni Wilfred Moshi, Respicius Baitwa wa pili kutoka kulia na Juma K. Nugaz aka Antonio Nugaz wa tatu kutoka kushoto wengine ni Geofrey Meena Meneja Masoko wa TTB na Devotha Mdachi Mkurugenzi wa Masoko wa pili kutoka kushoto.

Bodi ya Utalii Tanzania TTB leo imetoa vyeti kwa watanzania watatu walioipeperusha vyema bendera ya Tanzania katika masuala ya Utalii.

Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii nchini Tanzania Dk Aloyce Nzuki Akizungumza na waandishi wa habari kwa ajili ya tukio muhimu la kuwatunikia vyeti watanzania wa tatu amesema watanzania hao waliweza kupeperusha bendera ya Tanzania vizuri hasa katika masuala ya utalii, kwa hapa Tanzania na nchi za nje.

Watanzania hawa wameweza kufanya mambo makubwa ambayo kwa kiasi kikubwa sana yamechangia kwenye sekta ya utalii.Watanzania ambao tunaowapa tuzo leo ni pamoja na

    Mr. Respicias H. Baitwa
    Mr. Wilfred Moshi
    Mr. Juma K. Nugaz

1. Mr. Respicius BaitwaNi mtanzania wa kwanza ambaye ameweka rekodi ya Afrika kwa mwafrika wa kwanza anatarajia kupanda vilele saba virefu katika mabara yalioko duniani. Mr. Baitwa mpaka sasa ameshapanda vilele 4. Ameshapanda kilele cha kwanza Mt. Kilimanjaro zaidi ya mara 100, amepanda Elbrus kilele kirefu katika nchi za ulaya, Aconcagua, Argentina na Kosciusko Australia.

    2. Mr. Wilfred Moshi

Wilfred Moshi amekuwa mtanzania wa kwanza kupanda kilele kirefu kuliko vyote duniani kilele cha mlima Everest. Wilifred Mosha alipanda mlima Everest mwezi may 2012 na amekua mwafrika wa 3 kupanda na kufika kilele cha mlima Everest, na kupandisha bendera ya Tanzania kwa kufanya hivyo Wilifred Mosha ameweza kutangaza jina la Tanzania na kwenye mahojiano mbalimbali na vyombo vya habari duniani ameweza kutangaza vivutio vya utalii wa Tanzania kwa ujumla wake.

3. Mr. Juma K. Nugaz (Antonio Nugaz)
Juma Nugaz mtayarishaji wa kipindi cha utalii cha Kambi Popote kinachorushwa na clouds TV amekuwa mtangazaji bora katika kuhakikisha utalii wa ndani kwa mwaka 2012 tuzo iliytolewa na chama cha waandishi wa habari Tanzania.

Mr. Juma Nugaz amekuwa mstari wa mbele katika kuhamasisha utalii wa ndani kupitia kipindi cha kambi popote na amekuwa akitembelea bila kuchoka vivutio vya utalii na mwaka jana mwezi wa Disemba aliweza kurekodi kipindi maalum wakati wa zoezi la kupanda mlima kwa baadhi ya watanzania katika sherehe za kuazimisha miaka hamsimi (50) wa Tanzania bara ya Uhuru.Tunampongeza sana.

Bodi ya utalii Tanzania inawapongeza watanzania hawa kwa kufanya juhudi kubwa ya kutangaza vivutio vyetu vya utalii wa Tanzania na tutaendea kushirikiana nao kutangaza vivutio vyetu zaidi.

Pamoja na kuwazawadia cheti hiki vilevile tunawazawadia safari ya kitalii kwenda mbuga za wanyama za Selous kwa siku nne na familia zao.

Makarani 800 Wagoma Kula Kiapo Cha Sensa

MAANDALIZI ya Sensa ya Watu na Makazi inayotarajiwa kufanyika Agosti 26, mwaka huu yameingia dosari baada ya matukio kadhaa ya kukwamisha kazi hiyo kujitokeza katika mikoa mbalimbali, ukiwamo Dar es Salaam ambako zaidi ya makarani 800 wamegoma kula kiapo cha utii na kutunza siri.

Habari zilizopatikana jana zimeeleza kuwa mbali na makarani hao, vipeperushi vyenye ujumbe wa kutaka watu wagomee Sensa vimesambazwa mkoani Arusha, huku mkoani Tanga kukiwa na tukio la Sheikh mmoja kutiwa mbaroni kwa kusambaza vipeperushi vya aina hiyo.

Makarani hao waligoma jana ikiwa ni siku yao ya mwisho ya mafunzo ya kazi ya kuhesabu watu na makazi. Makarani hao kutoka vituo mbalimbali kulikotolewa mafunzo hayo, walisema wameamua kugomea kiapo hicho kutokana na fedha zilizotengwa kwa ajili ya malipo ya kazi hiyo kuchakachuliwa kinyume na makubaliano.

Baadhi ya vituo ambavyo makarani wake wamegoma ni Shule ya Sekondari Makumbusho, Kambangwa, Shule ya Msingi Zawadi na vituo kadhaa vilivyopo maeneo ya Buguruni na Kawe.Baadhi ya makarani hao walionekana wakiwa katika makundi, muda ambao walipaswa kuendelea na mafunzo yao kabla ya kula kiapo cha kushiriki Sensa kwa uaminifu na ukamilifu.Baadhi ya makarani ambao waliomba majina yao yasitajwe gazetini, walisema imekiuka makubaliano ya awali.

“Serikali imesema imetenga Sh141 bilioni kwa ajili ya Sensa. Sisi tayari tuliingia makubaliano nayo kwamba tunatakiwa kulipwa Sh35,000 kwa siku, kwa muda wa siku saba jambo ambalo limegeuka na kuwa kinyume.”

“Ukipiga mahesabu fedha ambazo tungetakiwa kulipwa kwa siku hizo saba ni Sh245,000 lakini wao wamekuja hapa na kutupa Sh140, 000 tu. Hatuwezi kuendelea na kazi mpaka tulipwe fedha zetu.”
Karani mmoja katika Kituo cha Sekondari ya Kambangwa, alisema wameamua kugomea kiapo baada ya kuona kuwa mpaka mafunzo yanahitimishwa jana, baadhi yao hawajalipwa chochote.

RC Dar:Watalipwa
Akizungumzia madai ya makarani hao, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadiki alisema mpaka jana mchana makarani wote walipaswa kulipwa awamu ya pili ya fedha zao. Alisema awamu ya kwanza ya malipo hayo ilifanywa katika siku tano za mwanzo.“Kuna watu wamejichomeka katika zoezi hili, lakini kama kweli karani ameteuliwa lazima atalipwa pesa zake na kama imetokea amesahaulika basi afanye mawasiliano na mratibu wa Sensa wilaya anayotoka ili alipwe,” alisema.

Sheikh mbaroni
Katika hatua nyingine Sheikh Juma Koosa (52) anashikiliwa na polisi wilayani Morogoro akituhumiwa kutumia kipaza sauti kuwatangazia wananchi wasishiriki Sensa.

Sheikh huyo ambaye pia ni mwanafunzi wa mwaka wa pili wa Chuo Kikuu cha Kiislamu Morogoro, alikamatwa Agosti 19 mwaka huu alipokuwa kwenye Msikiti wa Miembeni, Mazinde mara baada ya kukaribishwa na wenyeji wake kuzungumza.Imedaiwa kuwa Koosa alitoa kitabu chenye kueleza sababu za kuwakataza Waislamu kutokushiriki Sensa mwaka huu.

Chanzo: http://www.mwananchi.co.tz

Magazeti ya Leo Jumatano 22th 2012