Monday, March 4, 2013

KUTOKA BBC KUHUSU UCHAGUZI KENYA MARCH 4 2013


Hii picha ni kutoka Daily Nation Kenya, baadhi ya wakazi wa Nairobi waliojitokeza kupiga kura.

PAPA AWAAGA RASMI WAUMINI WA KANISA CATHOLIC

 -UTUMISHI wake umekoma rasmi 28th ,02 ,2013, aaga kwa mawingu mazito, jua lawaka ghafla

ILE historia ambayo haijawahi kuwepo kwa miaka 600 iliyopita ya papa kujiuzulu inafikia tamati Alhamisi 28th February 2013 ambapo Papa Benedict XVI ameachia rasmi uongozi wa Kanisa Katoliki Duniani.

Jumapili iliyopita katika Uwanja wa Kanisa la Mtakatifu Petro, jijini Vatican, maelfu ya waumini wa madhehebu hayo walijitokeza kumuaga wakati alipowabariki katika ibada yake ya mwisho wa utumishi ambapo alisema ilikuwa Februari 28, 2013.