Saturday, March 30, 2013

Kwaya ya Ambassadors of Christ ‘Kwetu Pazuri’ la Kigali Rwanda kutua Dar es salaam


KUNDI la muziki wa kiroho la Ambassadors of Christ ‘Kwetu Pazuri’ la Kigali, Rwanda linatarajia kutua Dar es Salaam leo (Jumamosi) kwa ajili ya Tamasha la Pasaka kesho.

Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Tamasha la Pasaka, Alex Msama alisema Dar es Salaam jana kuwa kundi hilo pamoja na mambo mengine litazindua albamu yao iitwayo Kaeni Macho katika tamasha hilo litakalofanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

“Tayari mambo yetu yanaenda vizuri na Kwetu Pazuri watawasili Jumamosi wakiwa wamepania kufanya mambo makubwa kwenye tamasha letu,” alisema Msama na kuzitaja nyimbo zilizopo kwenye albamu hiyo kuwa ni Kaeni Macho, Mungu Wangu, Tugireurukundo, Ewe Ndugu, Tuombeane, Umwamini Yesu, Msalaba, Twawona, Okuswala na Huruma.

Alisema kundi hilo limefurahi sana kuja hapa Tanzania na ndiyo sababu wakaipa heshima Tanzania kuzindua albamu yao wakiwa na imani mashabiki wataipenda na kwamba hivi sasa wanatamba na albamu ya Mtegemee Yesu na wamemhakikishia watang’arisha tamasha la mwaka huu.

Alibamu yao hiyo ina nyimbo nane ambazo ni JY’ Ushima Uwite, Mtegemee Yesu, Ndifuza Kugerayo, Iyana Iby’ Isi, Yesu Niwe Mungeri, Parapanda, Abasaruzi na Nenda.

Licha ya kundi hilo, wasanii wengine wa nje ya Tanzania watakaotumbuiza tamasha hilo ni Sipho Makhabane wa Afrika Kusini, Ephraim Sekeleti wa Zambia na Solomon Mukubwa raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) anayeishi Kenya.

Wasanii wa Tanzania waliothibitisha hadi sasa ni Rose Muhando, Upendo Nkone,  Bonny Mwaitege, Upendo Kilahiro, John Lissu, kwaya ya Kinondoni Revival na kundi la Glorious Celebration.

Tamasha la Pasaka litafanyika Dar es Salaam kesho na litaendelea Aprili mosi kwenye Uwanja wa Sokoine Mbeya, wakati Aprili 3 ni Uwanja wa Samora Iringa na Aprili 6 Uwanja wa Jamhuri, Dodoma na siku inayofuata itakuwa Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza.

Magazeti ya leo Jumamosi ya 30th March 2013




RAIS KIKWETE ALIPOWASILI KWENYE ENEO AMBALO GOROFA LILIPOPOROMOKA JANA DAR ES SALAAM





Mkuu wa mkoa Said Meck Sadick akiwa na Rais Kikwete na Kamanda wa polisi kanda maalum Dar es salaam Suleiman Kova, picha zote kutoka kwa mwandishi wa habari Mtoki ambae pia ni mmiliki wa mrokim.blogspot.com

Watu 40 wahofiwa kufukiwa baada ya jengo la ghorofa 16 kuporomoka Dar

 Watu zaidi ya 40 wanahofiwa kufukiwa na kifusi baada ya jengo la ghorofa 16 lililokuwa linajengwa kuporomoka katikati ya Jiji la Dar es Salaam jana asubuhi.

Jengo lililoporomoka

Kuporomoka kwa ghorofa hilo lililokuwa katika Mtaa wa Indira Gandhi, kulizua huzuni, taharuki na simanzi kwa ndugu na jamaa waliofika kwenye eneo la tukio kutaka kufahamu nini kimetokea.

Shughuli mbalimbali katikati ya jiji hilo zilisimama kwa siku nzima baada ya jengo hilo kuanguka na kusababisha vifo vya watu watano, 13 kuokolewa huku zaidi ya watu 40 wakisadikiwa kufukiwa na kifusi cha udongo wa jengo hilo.

MUUAJI WA PADRE MUSHI - ZANZIBAR AMEKAMATWA LEO

                                                Father Evalist Mushi enzi za uhai wake
 Mtu anaesadikiwa kuwa ndie muuaji wa aliyekuwa Padre Evalist Mushi wa kanisa katoliki, visiwani zanzibar, amekamatwa leo alasili maeneo ya kariakoo, zanzibar.

Jeshi la polisi limethibitisha kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo, na kwenda nae kituo cha polisi kwa ajili ya mahojiano zaidi.

Padri Mushi aliuwawa kwa kupigwa risasi mwezi uliopitwa wakati akiwa kwenye gari lake kuelekea kanisani kwenye ibada ya jumapili.

"SIPO TAYARI KUJIUZULU KWA KUOGOPA MAJUNGU YA VYAMA VYA UPINZANI".....NAIBU WAZIRI WA ELIMU

Victoria fm ya mjini Mwanza jana asubuhi kipindi cha matukio wameripoti kuwa wamefanya mahojiano na naibu waziri wa elimu Bw.Philip Mulugo kuhusu tuhuma zinazomkabili ambapo amesema hawezi kujiuzulu kwa kuogopa majungu ya vyama vya upinzani wanaopika uongo juu yake ili kuwika kisiasa.

Mulugo amekanusha madai yote yaliyoandikwa na gazeti la Mwananchi na kudai kuwa kama kuna mwenye wasiwasi na elimu yake aende akamuoneshe vyeti vyake vya elimu ya sekondari hadi vya taaluma na chuo alichosoma

Thursday, March 28, 2013

BREAKING NEWS:MBUNGE WA CHAMBANI SALIM HEMED KHAMIS AFARIKI


 Mbunge wa chambani Bwana Salim Hemed Khamis baaday ya kuanguka jana ghafla hapo jana jijini Dar katika vikao vya mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa na kukimbizwa hospital ya taifa muimbili kwa matibabu ya haraka.Kwa habari zilizotufikia hivi punde zinaeleza kuwa mbunge huyo amefariki mchana huu.

Taratibu za kuusafirisha mwili wa marehemu kuelekea pemba kwa mazishi zinafanafanyika.Tutazidi kuwafahamisha zaidi.

MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU MAHALI PEMA PEPONI. AMINA

Magazeti ya leo Alhamisi ya 28th March 2013






MENEJA WA KAMPUNI YA NDEGE YA FASTJET ATIWA MBARONI

MENEJA wa Wafanyakazi wa Ndani ya Ndege wa Kampuni ya Fastjet Emma Donovan, alifikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala Dar es Salaam kujibu shtaka linalomkabili la kutoa lugha ya matusi.

Emma (40) alipandishwa kizimbani jana na kusomewa shtaka hilo na Wakili wa Serikali Nassoro Katuga, mbele ya Hakimu Joyce Minde.

Katuga alidai Machi 19 mwaka huu Emma alimtolea lugha ya matusi Samson Itinde jambo ambalo ni kinyume cha sheria.Emma alikana shtaka hilo ambapo Katuga alidai upelelezi umekamilika na kuomba kupangiwa tarehe kwa usikilizwaji wa awali.

Hakimu Joyce alisema kuwa dhamana ya mshtakiwa iko wazi lakini kwa kuzingatia vigezo vya dhamana vitakavyotolewa kwa kuwa mshtakiwa ni raia wa kigeni.Alitaja masharti ya dhamana kuwa mshtakiwa anatakiwa kuwasilisha hati yake ya kusafiria au kutoa fedha taslim sh milioni tano na pia awe na wadhamini wawili ambao ni Watanzania.
Kesi hiyo imeahirishwaa hadi Aprili 9 ili kupangwa tarehe ya kuanza kwa usikilizwaji wa awali.

BINTI WA MIAKA 16 ALAZIMISHWA KUNYWA MKOJO NA MAMA YAKE MDOGO HUKO IRINGA

Vituko mjini Iringa haviwezi kuisha kama jamii haitakubali kwa moyo mmoja kupambana na ukatili wa kijinsia. Huyu ni Binti ZAWAD KARIM miaka 16 mkazi wa mshindo nyuma ya banki ya NBC manispaa ya Iringa amepigwa na hatimaye kunyweshwa mkojo na mama yake mdogo aitwaye Ever ubamba.

Tukio lilikuwa hivi:

SHIRIKISHO LA FILAMU TANZANIA LAMMPONGEZA WEMA SEPETU

SHIRIKISHO la Filamu Tanzania (TAFF) limempongeza msanii wa kike Wema Sepetu kwa moyo wa upendo aliouonyesha kwa msanii mwenzie Kajala Masanja kwa kumlipia faini ya sh. milioni 13 alizotozwa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kutokana na kupatikana na hatia katika kesi ya utakatishaji fedha iliyokuwa inamkabili mahakamani hapo

Akizungumza kwa niaba ya viongozi wengine rais wa shirikisho hilo Simon Mwakifwamba alisema kuwa imani na moyo wa upendo aliokuwa nao msanii Wema ndio uliomsukuma kumlipia kiwango hicho cha fedha bila ya kujiuliza mara mbili kitendo hiko kimeonyesha jinsi gani wanavyohitaji kushirikiana katika matatizo

Alisema kuwa wasanii wanatakiwa kujifunza kutoka kwake kwani wanahitaji kuwa kitu kimoja kujaliana kwenye matatizo na kutambua kuwa wao ni familia moja wanaojenga nyumba moja

Wednesday, March 27, 2013

RAIS KIKWETE AZINDUA TAARIFA YA UTAFITI WA VISAHIRIA VYA UKIMWI NA MALARIA MWAKA 2012

 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikata ukanda kuzindua rasmi taarifa ya utafiti wa viashiria vya ukimwei na malaria mwaka 2012 leo Machi 27, 2013 katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es salaam.

Kulia kwake ni Waziri Mkuu Mhe Mizengo Pinda na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Saidi Meck Sadiki. Kushoto kwake ni Mkurugenzi wa Tume ya Kudhibiri Ukimwi (TACAIDS) Mama Fatma Mrisho na

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), Mhe William Lukuvi.

KITABU CHA KIFO NI HAKI YANGU CHAZINDULIWA RASMI


 Mtunzi mashuhuri wa vitabu kutoka kampuni ya Mkuki na Nyota, Mzee Walter Bgoya, akikata utepe pamoja na mtunzi wa kitabu cha ‘Kifo ni Haki Yangu’, Eric James Shigongo (kulia) wakati wa uzinduzi wa kitabu hicho uliofanyika katika duka la vitabu la Tanzania Publishing House lililopo mtaa wa Samora jijini Dar es Salaam.
 Mtunzi Eric Shigongo akimpatia kitabu mtunzi mwenziye, mzee Walter Bgoya.

ALICHOKIANDIKA ZITTO KABWE KUHUSU HABARI ZA NJAMA ZA KUMUUA

BINTI ABAKWA MPAKA KUFA...ALIKUWA ANATOKA NACHINGWEA RESORT

Bint aliyejulikana Mariam amekutwa na mauti  baada ya kubakwa mpaka kufa....

Vijana hao waliokosa utu na kushindwa kumuogopa Mungu walifanya kitendo hicho mbele ya eneo la kanisa(Voda st)Nachingwea Lindi.

Marehemu alikuwa  na  mkasa   huo wakati akitoka Nachingwea Resort(NR) katika muziki siku ya ijumaa.Inasadikika marehemu amelewa  na wabakaji  alitoka nao muziki.

MSANII RADO ANUSURIKA KIFO BAADA YA KUPOKEA KICHAPO KIKALI MWANANYAMALA

 MSANII wa muziki na filamu Bongo, Saimon Mwapagata ‘Rado’ amenusurika kifo kutoka kwa vijana waliofunga njia maeneo ya Mwananyamala, jijini Dar Jumapili iliyopita.

Kwa mujibu wa rafiki wa Rado ambaye pia ni msanii wa filamu, Deogratius Shija, tukio hilo lilitokea usiku wakati Rado alipokuwa akirudi nyumbani kwake..

“Alikuta njia imefungwa na vijana watatu, alijaribu kuwapigia honi lakini hawakufungua njia.

“Rado alishuka kwenye gari na kuwauliza kwa nini wamefunga njia wakamjibu kwamba mmoja wao ameibiwa simu, hivyo wanamtafuta mwizi wao.
Shija alisema kwamba ghafla vijana wale walimvamia Rado  na kumshushia kipigo cha haja wakiwa na mapanga na marungu na kumjeruhi hadi akapoteza fahamu.

 “Nilipigiwa simu na msamaria  na kuambiwa kuwa Rado hajiwezi, sababu kuna watu wanaomjua maeneo yale alipelekwa Oysterbay Polisi kisha kukimbizwa Hospitali ya Mwananyamala ambako alishonwa, kifuani na mguuni,”

YULE MTOTO WA MIAKA 8 ALIYEOA BIBI WA MAIAKA 61 ADAI KUFURAHIA FURAHA KUITWA BABA

 KUSHOTO: Sanele akibusiana na mkewe, Helen siku ya harusi yao wiki mbili zilizopita. KULIA: Sanele na Helen walipata chakula cha usiku pamoja nyumbani kwa mkewe huyo.

Huku miguu yake ikining'inia juu ya sakafu na sehemu yake ya chakula cha mtoto, inaonekana kama anakula chakula cha usiku na bibi yake.Ukweli ni kwamba Sanele Masilela, mwenye miaka 8, anafurahia chakula cha usiku na mke wake, baada ya kumuoa wiki mbili zilizopita, na inasemekana kwa sasa ameanza kujisikia kama mume kamili.

Magazeti ya leo Jumatano ya 27th March 2013




Tuesday, March 26, 2013

CHADEMA WAPOKEA MSAADA WA MILIONI 400

 Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimepokea msaada wa fedha shilingi milioni 400 kutoka Chama cha Upinzani nchini Denmark cha Conservative People’s Party (CPP), kwa ajili ya utekelezaji wa Mradi wa kuwajengea uwezo vijana pamoja na Wanawake Viongozi wa chama hicho.

Akizungumza wakati wa kutiliana saini Mkataba wa utekelezaji wa Mradi huo, Katibu Mkuu wa CHADEMA, DK. WILBROAD SLAA amesema awamu ya kwanza ya utekelezaji wa Mradi wa kuwajengea uwezo Wanachama wake kupitia Baraza la Vijana la Chama hicho, (BAVICHA), pamoja na lile la Wanawake (BAWACHA), inatarajiwa kuanza Machi, mwaka huu.

Kwa upande wake Mwakilishi wa Chama cha Conservative People’s Party (CPP), ROLF AAGAARD, anaelezea lengo la chama hicho kutoa msaada huo.

Nae Mwenyekiti wa Baraza la Vijana (CHADEMA), JOHN HECHE amesema msaada huo utawawezesha kutoa mafunzo kwa Viongozi wa Baraza hilo katika mikoa mbalimbali nchini.

Chama cha Conservative People’s Party (CPP), kilianzishwa mwaka 1915 na kimekuwa madarakani kwa kipindi kirefu hadi kiliposhindwa katika Uchaguzi Mkuu uliopita nchini.

ALIYEMGONGA TRAFIKI ENEO LA BAMAGA AFIKISHWA MAHAKAMANI

                 Waandishi wa habari wakimpiga picha (Simbo) wakati akiingia mahakamani...

 Jackson  Simbo anayedaiwa kumgonga kwa gari marehemu trafiki Elikiza Nko wiki iliyopita maeneo ya Bamaga-Mwenge  jijini Dar ss Salaam amepandishwa kizimbani leo katika mahakama ya Wilaya ya Kinondoni.

Mshitakiwa huyo ameachiwa kwa dhamana hadi kesi hiyo itakapo tajwa tena Aprili 15 mwaka huu

HUU NDO UTAJIRI WA WEMA SEPETU.....

                                                       Wema akiwa na Mama yake
 Well, well, well! Hiki ni kitu ambacho kila mmoja anapenda kukifahamu. Wema Sepetu ni tajiri kiasi gani? Ni ngumu kusema exactly mrembo huyu ana shilingi ngapi benki, lakini mambo anayofanya yanatupa jibu la wazi kuwa, Wema ana mkwanja mrefu. So hebu tuangalie mangapi makubwa yaliyohusisha fedha nyingi aliyoyafanya kuanzia mwezi June, 2012.

WANAFUNZI 10,000 WALIOKATA RUFAA YA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE-2012 WAMEFELI TENA

    MATOKEO YA RUFAA CSEE 2012 AWAMU YA I
    MATOKEO YA RUFAA QT 2012 AWAMU YA I

Taarifa ifuatayo, inahusiana na rufaa hizo, imenukuliwa kutoka kwenye gazeti la NIPASHE

Wakati tume ya kuchunguza matokeo mabaya ya kidato cha nne mwaka 2012 ikiendelea na kazi, imebainika kuwa wanafunzi waliokata rufaa kutaka mitihani yao isahihishwe upya wamefeli zaidi baada ya kusahihishiwa.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ambazo zimethibitishwa na baadhi ya maofisa, wanafunzi waliokata rufaa wamefeli zaidi na hata walioongezewa alama matokeo hayakubadilisha madaraja waliyopata awali.

MWANAFUNZI UDSM AJINYONGA HADI KUFA

 Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) mwaka wa pili Kitivo cha Sheria, Joseph Bernadina (25), amejinyonga kwa kutumia kamba na kukutwa ameifunga juu ya mti, katika eneo la Yombo chuoni hapo.

Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Utawala, Profesa Yunus Mgaya, alithibitisha  kutokea kwa tukio hilo na kwamba alipata taarifa hizo jana asubuhi.

Aliongeza kuwa Jumamosi iliyopita alipokea simu kutoka kituo cha polisi cha chuo hicho akielezwa kuwa kuna mwanafunzi alitishia kujiua, lakini aliwahishwa hospitali na kupatiwa ushauri kutoka kitengo maalum cha washauri wa chuoni hapo na kuruhusiwa Jumapili.

WABUNGE ZITTO KABWE NA AZAN WAMALIZA MAFUNZO YAO YA JKT KAMBI YA MGAMBO 835KJ LEO

                       Zitto Kabwe akijiandaa kwenda katika gwaride la mwisho na picha chini
Zito akiwa shambani pamoja na Mbunge mwenzake  Iddi Azan, Abdallah haji, Raya Ibrahim na Antony Mbassa kambi ya Mgambo 835KJ.

Mbunge wa Kigoma CHADEMA, Zitto Kabwe pamoja na Wabunge wenzake kadhaa vijana leo wakemaliza rasmi mafunzo yao ya awali ya JKT katika kambi ya Mgambo 835KJ kilichopo Mkoani Tanga.

Aidha Zitto Kabwe amesema anafuraha iliyo pitiliza kumaliza mafunzo hayo na ameweka historia ya kubwa katika maisha yake hii leo. Anapasha zaidi katika wakati wa Zoezi la kulenga shabaha alifanikiwa kulenga risasi 3 akiwa amelala, 3 akiwa amepiga magoti na 1 akiwa amesimama.

CHETI ALICHOTUMIA NAIBU WAZIRI WA ELIMU KUOMBEA KAZI YA UALIMU NI CHA RAFIKI YAKE...

 Imebainika kuwa mmoja wa watu ambao Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo (pichani)anadaiwa kutumia jina lake kutafuta kazi ya ualimu katika Shule ya Sekondari ya Southern mkoani Mbeya ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu kishiriki cha elimu Mkwawa (Muce), kilichopo mkoani Iringa.
Mhadhiri huyo ni Dick Aron Mulungu ambaye alisoma na Mulugo katika Shule ya Sekondari ya Songea Wavulana kati ya 1994 na 1996 na alijiunga na shule hiyo baada ya kuhitimu kidato cha nne katika Shule ya Sekondari ya Kafule, ambayo iko mkoani Mbeya.

Taarifa zinaonyesha kuwa Mulungu alijiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na kupata Shahada ya kwanza katika Elimu (BA Education) 2001 na baadaye alisoma na kupata Shahada ya Uzamili (MA Development studies ) 2007.
Alipotafutwa kupitia simu yake ya mkononi, mahojiano yalikuwa hivi:

MAHAKAMA YAAMURU MATOKEO YA URAIS KENYA YAHESABIWE UPYA KWA VITUO 22 KATI YA 33

Nairobi. Mahakama ya Juu (Supreme Court) ya nchini Kenya imeagiza kuchunguzwa kwa fomu 34 za matokeo ya uchaguzi wa rais kutoka katika vituo vyote 34,400, vilivyotumika kupigia kura katika Uchaguzi Mkuu wa nchi hiyo uliofanyika Machi 4, mwaka huu.

Kadhalika mahakama hiyo jana iliagiza kuhesabiwa upya kwa kura za urais katika vituo vya kupigia kura 22 kati ya elfu 33 vilivyolalamikiwa na aliyekuwa mgombea urais wa Muungano wa Cord, Raila Odinga.
Katika malalamiko yake yaliyowasilishwa katika mahakama hiyo kupinga Uhuru Kenyatta kutangazwa mshindi wa urais katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika Machi 4, Odinga alidai kuwa vituo hivyo 22 kura zilizopigwa zinazidi idadi ya wapigakura walioandikishwa.

Jamani Familia ya Sepetu Imebarikiwa Hawa Vimwana Wanne

                                                               WEMA SEPETU

 TUNNU SEPETU... YEYE NI MAMA WA MTOTO MMOJA.. ANAISHI NCHINI MAREKANI

 NURU SEPETU... NI MAMA WA WATOTO WATATU, MARRIED AND BASED IN DAR.


 SUNNA SEPETU: HUYU PIA ANAISHIA MAREKANI KWA KIPINDI KIREFU...








KIBONGO BONGO TUMEZOEA KUMUONA WEMA AKIMAKE HEADLINE BUT WENGI HAMJUI KAMA WEMA AMEZUNGUKWA NA DADA WATATU WALIOSIMAMA KIMAISHA NA WASIOENDA SPOTLIGHT...  LEO NAWAKUTANISHA NA WASICHANA WANNE WANAOKAMILISHA FAMILIA YA SEPETU.