Saturday, March 16, 2013

Uchaguzi wa Kamati za Bunge:Vita Lowassa,Membe yakolezwa

                                              Mbunge wa Jimbo la Monduli, Edward Lowassa

Dar es Salaam. Ofisi ya Bunge jana ilitangaza majina ya wenyeviti na makamu wapya wa Kamati za Kudumu za Bunge huku Mbunge wa Jimbo la Monduli, Edward Lowassa akichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

Kuchaguliwa kwa Lowassa kuongoza kamati hiyo kunaibua upya vita kati yake na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, kutokana na wote kutajwa kutaka kugombea urais katika uchaguzi mkuu ujao mwaka 2015. Awali

RAFIKI WA RAILA ODINGA AMPA TALAKA MKEWE KWA KUMSIFIA UHURU KENYATTA KUWA NI HANDSOME

 Rafiki wa karibu wa waziri mkuu wa Kenya Raila Odinga Jumatatu hii anadaiwa kumpa talaka mke wake baada ya kumsifia Rais mteule wa Kenya Uhuru Kenyatta ni ‘handsome’ mbele yake.

Kwa mujibu wa mtandao mmoja wa Kenya, mwanasiasa huyo wa chama cha CORD anayetokea magharibi mwa Kenya, alikuwa akitazama taarifa ya habari akiwa na mke wake na ndipo alipoonekena Uhuru Kenyatta kwenye TV akizungumza na wawakilishi wa nchi mbalimbali nyumbani wake.

AFYA YA LWAKATARE NI MBAYA.....BADO ANASHIKILIWA NA POLISI

Dar es Salaam. Hali ya afya ya Mkuu wa Usalama na Ulinzi wa Chadema, Wilfred Lwakatare anayeshikiliwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za kuwahamasisha watu kufanya vitendo vya uvunjifu wa amani kupitia mitandao ya jamii, imezorota.

Gazeti hili imemshududia jana akizungumza na wakili wake Nyaronyo Kicheere, huku akilalamikia hali yake kuwa si njema kutokana na ugonjwa wa kisukari alionao.

Alikuwa akitembea kwa kujivuta, na alidai kuwa ameshindwa kula chakula inavyotakiwa.

MGOGORO WA UCHINJAJI NYAMA BAINA YA WAKRISTOB NA WAISLAM HUKO GEITA WAPATA SULUHISHO

Baadhi ya viongozi wa Dini ya Kiislam na Kikristo kutoka Geita wamekaa pamoja na kuondoa tofauti zao hususan katika suala la uchinjaji wa nyama kwa ajili ya kitoweo, miongoni mwa makubaliano waliyofikia ni nyama yoyote inayochinjwa kwa ajili ya biashara wachinje waislamu lakini kwenye sherehe zinazowahusu waislam wachinje waislamu na sherehe zinazowahusu wakristo wachinje wakristo wenyewe. Hivyo sherehe zozote za kidini wasiingiliane kwenye taratibu za kidini kwa kila mmoja.

Shehe Ismail Ibrahim na Mchungaji Isaya Ikiri

Magazeti ya leo jumamosi ya 16th March 2013