Tuesday, July 2, 2013

KWA HERI BARACK ABAMA....KARIBU TENA NA SAFARI NJEMA

MAZISHI YA MANDELA YAGOMBANIWA NA VYOMBO VYA HABARI PINDI ATAKAPOFARIKI

PICHA ZA WANANCHI TOKA UBUNGO WAKISUBIRI MSAFARA WA RAIS OBAMA

MFALME MSWATI WA SWAZILAND AAONDOKA NCHINI NA AMEWATAKA WATANZANIA WABADILIKE

MAREKANI KUFUNGUA UKURASA MPYA KATIKA UWEKEZAJI BARANI AFRIKA

GEORGE BUSH NA OBAMA WATAKUTANA ANA KWA ANA KATIKA ARDHI YA TANZANIA

TANZANIA YAUMBULIWA....GAZETI MAARUFU LA MAREKANI LAANIKA UKATILI UNAOTENDEKA NCHINI

PICHA ZA RAIS OBAMA ALIPOTUA KATIKA ARDHI YA TANZANIA

MMILIKI WA FACEBOOK NA WAFANYAKAZI WAKE WASHEREHEKEA KUPITISHWA KWA SHERIA YA NDOA YA JINSIA MOJA

MKE WA OBAMA ATEMBELEA WAMA FOUNDATION NA KUKUTANA NA MAMA SALMA KIKWETE

TUJIKUMBUSHE MAMBO MACHACHE YANAYOTENDEKA KUHUSU OBAMA AMBAYE TAYARI YUPO TANZANIA

Obama ameshatua Tanzania

Saturday, June 29, 2013

HATARI LAKINI SALAMA!

 Randy Miller akicheza na chui wake Eden.
 Chui Eden akiwa amemdondosha chini mwalimu wake Randy
 Randy akiwa chini baada ya kudondoshwa na Eden.
 Marafiki hao wawili wakiwa katika pozi.Taswira hapo juu zinamwonyesha Bwana Randy Miller (45) akicheza na chui wake aitwaye Eden ambaye amemfundisha

jinsi ya kufanya mashambulio yasiyo na madhara na ambaye amekuwa akimtumia katika kucheza filamu mbalimbali.

Mambo 20 ya kusisimua kuhusu Obama

RAIS wa Marekani, Barack Obama, anatarajia kutua Tanzania Jumatatu. Watanzania wengi wanamsubiri kwa hamu, lakini je wanayafahamu mambo yanayovutia kuhusu rais huyo? Makala hii inayachambua mambo 20 ya kufurahisha kuhusu Obama.

1. Asili
Obama ni mchanganyiko wa damu ya Kenya, Ireland na England.

2. Namba 44
Ni Rais wa 44 wa Marekani. Rais wa kwanza alikuwa, George Washington, ambaye alitawala kuanzia mwaka 1789 hadi 1797.

3. Anapenda TV
Obama anapenda kuangalia televisheni. Anapenda kipindi cha ‘The Wire’. ‘The Wire’ ni tamthilia inayorushwa kwenye televisheni na inahusu upelelezi wa polisi.

4. Wa Kwanza
Obama ni rais wa kwanza wa Marekani ambaye amezaliwa Hawaii.

5. Ndugu yake
Rais Obama ana dada mmoja tu, anaitwa Maya. Hata hivyo Obama na Maya wamechangia mama tu, baba ni tofauti.

SIMULIZI ZA MZEE MADIBA; MANDELA BONDIA ALIPOKUTANA NA BONDIA…!

Ndugu zangu, Kuna simulizi nyingi za Mzee wetu Madiba. Hakika, Nelson Mandela hajawahi kuwa mpenda makuu. Mzee Mandela yuko simple sana, ni tangu enzi za ujana wake. Lakini, kuna ambao hawajui kuwa Mandela anapenda sana mchezo wa ngumi, na kuwa , yeye mwenyewe aliwahi kuwa bondia.

Kuna wakati akiwa Ikulu kama Rais, Mandela alipata habari za bondia wa Afrika Kusini aliyetwaa taji la  kimataifa. Mandela alifurahishwa sana na habari hizo. Akataka ampongeze mwenyewe bondia  huyo.Siku moja akiwa na wasaidizi wachache sana, Mandela alikwenda hadi nyumbani kwa bondia huyo. Alihakikisha kuwa bondia huyo yuko nyumbani kwake. Alipofika, Mandela aliwaambia wasaidizi wake wakamwambie bondia huyo kuwa nje kuna mtu anayehoji ubingwa wake.  Wamwambie kuwa  mtu huyo ( Nelson Mandela) anadai kuwa yeye ndiye bingwa wa uzito huo katika Afrika Kusini ( Nelson Mandela!) Kwamba anataka mkutane mpange siku ya kupigana ili apatikane mshindi halali wa taji hilo.

Basi, bondia yule akapokea habari hizo na akatamani sana amwone huyo anayedai kuwa ana ubavu wa kupambana naye. Alipotoka nje akakutana na Nelson Mandela akiwa amesimama getini na amekunja ngumi yake. Akatania; “ Nimekuja kwako tuzipige ili dunia imjue bingwa halisi!”

Ikawa ni furaha kubwa kwa bondia yule. Hakuamini macho yake. Kuwa Rais wa nchi amekuja nyumbani kwake kumpongeza.  Kumpongeza kwa jambo kubwa alilolifanya kwa taifa la Afrika Kusini.

Na Mandela akawa tayari kuingia nyumbani kwa bondia huyo na kunywa nae chai!

What a Great Leader Of Africa! Yes, Nelson Mandela!

Maggid Mjengwa,

Iringa.

OBAMA, MANDELA SIRI NZITO!


MAMBO mawili ndiyo habari ya mjini kwa sasa; umahututi wa Rais Mstaafu wa Afrika Kusini, Nelson Rolihlahla Mandela ‘Madiba’ (94) na ziara ya Rais wa Marekani, Barack Husein Obama katika nchi tatu za Afrika.

NDEGE YA OBAMA NI NYUMBA INAYOTEMBEA AIR Force One ni ndege kubwa ya Rais wa Marekani. Ndege hii ina sifa nyingi kama ndege nyingine, lakini ina nyongeza ambayo kwenye ndege nyingine hakuna. Air Force One ambayo imewahi kuchezewa filamu iliyoitwa kwa jina hilohilo na staa wa muvi za Hollywood, Harrison Ford imeonekana ndiyo ndege yenye usalama zaidi duniani. SIFA KUBWA: Ndani ya ndege hiyo kuna ofisi ya rais, jiko, chumba cha mikutano, bafu, sehemu ya kuvalia nguo, eneo la kufanyia mazoezi ‘gym’ na chumba cha mawasiliano. Ndiyo maana inasemwa ni nyumba inayotembea. Pia kuna chumba cha maafisa wanaomlinda rais, sehemu yao ya kufanyia mkutano wakipata dharura na zahanati kama rais akiugua ghafla wakati ndege ipo angani. Si hayo tu, kuna chumba chenye simu 85 za mezani na Tivii 19 kwa ajili ya kupata habari za kidunia wakati ndege ipo juu. Ndege hiyo haikamiliki kuiita Air Force One bila kutambulisha sehemu maalum ambayo hutumika kijeshi kumkwepesha adui anayetaka kuilenga kwa lengo la kuilipua.

 AIR Force One ni ndege kubwa ya Rais wa Marekani. Ndege hii ina sifa nyingi kama ndege nyingine, lakini ina nyongeza  ambayo kwenye ndege nyingine hakuna.

Air Force One ambayo imewahi kuchezewa filamu iliyoitwa kwa jina hilohilo na staa wa muvi za Hollywood, Harrison Ford imeonekana ndiyo ndege yenye usalama zaidi duniani.
SIFA KUBWA:
Ndani ya ndege hiyo kuna ofisi ya rais, jiko, chumba cha mikutano, bafu, sehemu ya kuvalia nguo, eneo la kufanyia mazoezi ‘gym’ na chumba cha mawasiliano. Ndiyo maana inasemwa ni nyumba inayotembea.

Pia kuna chumba cha maafisa wanaomlinda rais, sehemu yao ya kufanyia mkutano wakipata dharura na zahanati kama rais akiugua ghafla wakati ndege ipo angani.

Si hayo tu, kuna chumba chenye simu 85 za mezani na Tivii 19 kwa ajili ya kupata habari za kidunia wakati ndege ipo juu.

Ndege hiyo haikamiliki kuiita Air Force One bila kutambulisha sehemu maalum ambayo hutumika kijeshi kumkwepesha adui anayetaka kuilenga kwa lengo la kuilipua.



Friday, June 28, 2013

Magazeti ya leo Ijumaa 28th June 2013





TASWIRA ZA MAPOKEZI YA RAIS OBAMA NCHINI SENEGAR








Pichani juu ni taswira za rais wa Marekani, Barack Obama alivyopokelewa na rais wa Senegal, Macky Sall jana jijini Dakar nchini Senegal. Rais Obama yupo ziarani barani Afrika ambapo atatembelea nchi za Senegal, Afrika Kusini na Tanzania.

Wednesday, June 26, 2013

Mzee Mandela afanyiwa maombi maalum

ASKOFU mkuu wa kanisa la kianglikana mjini Cape Town, Afrika Kusini, Thabo Makgoba, amejitolea kufanya maombi kwa niaba ya rais mstaafu Nelson Mandela ambaye anaugua sana hospitalini.

Kasisi huyo anamuombea Mandela aweze kupata nafuu na amewataka wananchi kumshukuru kwa yote aliyowafanyia.Jamaa za Nelson Mandela wamekutana nyumbani kwake huko Kunu, huku hali yake ya afya ikizidi kudorora hospitalini, Pretoria. Afya ya Bwana Mandela ilikuwa mbaya zaidi Jumapili.

Maombi hayo yalitolewa baada ya Askofuu huyo kumtembelea Mandela hospitalini ambako kiongozi huiyo wa zamani amekuwa akilazwa kwa wiki mbili na nusu zilizopita baada ya kuugua mapafu.

Vyombo vya habari nchini humo vinasema kuwa wajukuu wa rais huyo wa zamani wa Afrika kusini wanakutana nyumbani kwake kijijini katika mkoa wa Eastern Cape province, ambako viongozi wa kitamaduni wamealikwa.

Halikopta ya jeshi kadhalika zilionekana zikipaa karibu nyumbani kwa mandela. Afisi ya Rais jacob Zuma ilitangaza jumapili kuwa hali ya mzee Mandela ya afya ilikuwa mbaya sana.

Chanzo: bbcswahili

Magazeti ya leo Jumatano 26th June 2013






Mzee Mandela bado yuko hali mahututi

RAIS mstaafu wa Mandela Nelson Mandela, bado yuko hali mahututi ingawa madaktari wanadhibiti hali yake baada ya afya yake kuzorota mwishoni mwa wiki.Taarifa kutoka ikulu ya rais zinasema kuwa Mandela angali yuko chini ya uchunguzi wa madaktari ambao wameweza kuidhibiti hali yake.

 Anaugua maradhi ya mapafu na amelazwa hospitalini kwa zaidi ya wiki mbili sasa.Mapema leo familia yake ilimtembelea hospitalini, mzee Mandela ambaye anasifika kwa vita alivyopigana dhidi ya utawala wa wazungu nchini Afrika Kusini.

Amekuwa akiugua ugonjwa wa mapafu mara kwa mara na hii ni mara ya tatu kwa Mandela kulazwa hospitalini mwaka huu.Rafiki na jamaa wameendelea kukusanyika katika hospitali alikolazwa Mandela mjini Pretoria kumtakia afya njema mzee Mandela.

Mmoja wa waliomtembelea Mandela , mfanyabiashara Calvin Hugo, aliawachilia huru njiwa weupe, kama heshima yake kwa Mandela anaeyendelea kuugua hospitalini.Alisema kitendo chake kilikuwa ishara ya, hatua ya Mandela kuikwamua nchi ya Afrika Kusini kutoka kwa mkoloni.

Baadhi ya jamaa zake wamekusanyika nyumbani kijijini eneo la Qunu, kujadili kile wanachosema ni habari muhimu sana.

Chanzo: bbcswahili

UCHAGUZI WA ARUSHA WAAHIRISHWA TENA ILI KUIMARISHA HALI YA AMANI NA UTULIVU

TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imeahirisha tena uchaguzi wa madiwani kata nne za Arusha hadi Julai 14 kuruhusu kurejea utulivu baada ya mlipuko wa bomu kwenye mkutano wa kampeni wa Chadema ulioathiri uchaguzi huo wiki iliyopita.

Bomu hilo lilirushwa Juni 15 na mtu asiyejulikana katikati ya mkutano wa Chadema katika viwanja vya Soweto, mjini Arusha na kusababisha vifo vya watu watatu na wengine kujeruhiwa na uchaguzi huo wa Juni 16 kulazimika kuahirishwa.

Baada ya tukio hilo, Msimamizi wa Uchaguzi wa Arusha aliuahirisha hadi Juni 30, lakini jana Mwenyekiti wa NEC, Jaji Damian Lubuva alisema utafanyika Julai.

Kata zinazohusika ni Elerai, Kimandolu, Thani na Kaloleni. Akizungumza na waandishi wa habari, Jaji Lubuva alisema walipotangaza kuwa uchaguzi ungefanyika Juni 30 waliamini kuwa hali ya utulivu na amani ingekuwa imetengemaa.

ULINZI WA RAIS OBAMA JIJINI DAR NI BALAA....MITAMBO MBALIMBALI YA MAWASILIANO IMEFUNGWA UWANJA WA NDEGE WA KIA

Maandalizi ya ujio wa Rais wa Marekani, Barack Obama nchini yanazidi kupamba moto huku maofisa wa usalama wa Marekani wakipiga kambi katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam.

Aidha, kutokana na ujio huo, Serikali imeagiza mashirika yote ya ndege kubadili ratiba zao za safari Julai Mosi, siku ambayo Rais huo atatua nchini.

Jana, waandishi wetu walishuhudia pilikapilika za kuimarisha ulinzi katika uwanja huo jambo ambalo uongozi wa uwanja huo jambo wamelieleza kwamba halijawahi kutokea.

Ulinzi haujawahi kutokea

Mkurugenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Moses Malaki alisema jana kwamba ratiba za uwanjani hapo zitabadilika kutokana na uzito wa ugeni huo.

SERIKALI YATOA TAMKO KUHUSU KAULI YA WAZIRI MKUU...YADAI POLISI WANARUHUSIWA KUPIGA NA KUUA KISHERA

Serikali imetoa tamko bungeni kuhusu mauaji ya raia mikononi mwa polisi ikieleza kuwa sheria ya kanuni ya adhabu inaruhusu kutumia nguvu za kadiri hata kiasi cha kusababisha madhara au kifo.

Kauli hiyo imekuja siku chache baada ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kunukuliwa bungeni akiwataka polisi kuwashughulikia kwa kuwapiga watu wote wanaokaidi kutii sheria.

“…Nasema wapigwe tu, maana tumechoka sasa,” alisema Pinda alipojibu maswali ya papo hapo Alhamisi iliyopita.

Akisoma tamko hilo bungeni jana, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Pereira Ame Silima alisema kuwa kifungu cha 18(B) na 18(C) cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu kinatoa uwezo kisheria wa kutumia nguvu za kadiri hata ikibidi kiasi cha kusababisha madhara au kifo katika mazingira ya kisheria.

Tuesday, June 25, 2013

"TUTAIFUTA CHADEMA ENDAPO ITABAINIKA KUWA WALIRUSHA BOMU LA ARUSHA WENYEWE"....TENDWA

Msajili wa Vyama vya Siasa nchini John Tendwa,  amedai kuwa ikibainika kuwa CHADEMA ndio waliohusika katika kulipua bomu katika mkutano wao wa 15/06/2013 atakifuta.
Tendwa  ameyasema   hayo alipokuwa akizungumza katika kipindi cha Hot Mix cha East Africa Television akijibu swali la mtangazaji wa kipindi Adrian Stepp  kuhusu  hatua  zitakazochukuliwa...
Alipoulizwa kama itathibitika kuwa CCM ndio walihusika kulipua bomu hilo amedai kuwa hawezi kukifuta kwakuwa kwa kufanya hivyo itakuwa ni kufanya mapinduzi ya kalamu.

MH. SUGU AMEACHIWA KWA DHAMANA BAADA YA KUKAMATWA NA POLISI

MBUNGE wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi (SUGU) amekamatwa na Jeshi la Polisi Mjini Dodoma na kuachiwa kwa dhamana.

Mwandishi wetu akiwa Mjini Dodoma anasema kwamba Mbunge huyo alikamatwa muda mfupi baada ya kutoka katika vikao vya Bunge.

Sugu alikamatwa na kupelekwa katika Kituo Kikuu cha Polisi Dodoma na baada ya kuhojiwa aliachiwa kwa dhamana na kutakiwa kuripoti kituoni hapo kesho asubuhi kwa mahojiano mengine.

Hata hivyo taarifa za awali za tukio la kukamatwa kwa Mbunge huyo wa Chama Cha Manedeleo na Demokrasia (Chadema) zinadai kwambwa inatokana na kosa la kutoa maneno ya uchochezi, matusi na dhihaka kwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mizengo Pinda.

SUGU AKAMATWA KWA KUMTUSI WAZIRI MKUU

Habari zilizotufikia hivi punde zinadai kuwa Mbunge wa Mbeya mjini Mh Joseph Mbilinyi amekamatwa kwa kile kinachodaiwa ni uchochezi na kumkashifu Waziri Mkuu Mzengo Pinda.   Hivi  karibuni, Mh. Sugu  alidai  kuwa  Tanzania  haijawahi  kuwa  na  waziri  mkuu  mpumbavu  kama  Mizengo  pinda. Tunaendelea  kufuatilia  undani  wa  habari  hii: 

Jeshi la Polisi limemjibu Joyce Kiria Je Majibu haya ni sawa kwa mama Huyu?

 Joyce Kiria akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam ambapo alidai hajui mume wake yuko wapi?
Inasikitisha kuona kwamba huyu mama Joyce Kiria anaingilia mambo ya kisheria na kutaka kupotosha jamii kwamba hajui mume wake yuko wapi pia nadhani analenga kuichochea jamii kwamba aliyetuhumiwa kutenda uhalifu akikamatwa familia yake iandamane, tendo ambalo pia ni kosa la jinai. Aidha anatakiwa kuheshimu haki za watoto na kuacha kuwatumia katika kinga ya kutetea watu wanaotenda uhalifu (Imetolewa na Advera Senso Msemaji wa Jeshi la Polisi Nchini Tanzania)

Mume wa Joyce Kiria Henry Kilewo akiwa ndani ya pingu na vijana wengine kwa tuhuma za ugaidi

  Bw.Henry Kilewo akiwa na watuhumiwa wenzake wa mashtaka ya Ugaidi yanayowakabili wakati walipofikishwa Mahakama ya Hakimu mkazi mkoani Tabora kwa mara ya kwanza
 Ulinzi katika Mahakama hiyo uliimarishwa ipasavyo.
 Wanachama wengine wa Chadema ambao wanahusishwa katika mashataka hayo ya Kigaidi ambapo imedaiwa kuwa watuhumiwa walifanya makosa hayo ya Ugaidi na kumjeruhi Bw.Mussa Tesha ambaye ni mwanachama wa CCM wakati wa kampeni za uchaguzi wa Ubunge wa jimbo la Igunga mnamo tarehe 9/9/2011 katika msitu wa Hanihani huko wilayani Igunga.
Kamanda Henry Kileo ndani ya pingu akiwa ndani ya gari pamoja na wtuhumiwa wenzake wanne wakisubiri kupelekwa Gereza la Mahabusu hadi watakapoletwa tena Mahakamani hapo mnamo tarehe 8/7/2013.

Inaumiza kiukweli msikia Joyce kiria alichoandika katika facebook yake

Jana baada ya kufanya hili zoezi na familia yangu namshukuru Mungu Wakili wetu Peter Kibatala alinipigia sim majira ya alasiri akanitaarifu ya kwamba Mume wangu yupo Tabora na yuko salama. isipokuwa amepandishwa kizimbani na kusomewa mashitaka mawili, UGAIDI na KUM'MWAGIA MTU TINDIKALI....Am speechless familia yangu tunaitaji maombi yenu sana kuliko mnavyofikiria

Monday, June 24, 2013

Magazeti ya leo Jumatatu 24th June 2013







MWIGULU NCHEMBA NA MSIGWA NUSURA WATWANGANE NGUMI BUNGENI

Mbunge wa Jimbo la Iringa Mjini (Chadema), Mchungaji Peter Msigwa na mbunge wa Iramba Magharibi (CCM), Mwigulu Nchemba jana nusura wachapane makonde baada ya kutupiana maneno ya kashfa, wakituhumiana kuhusika na mlipuko wa bomu uliotokea Jumamosi iliyopita mkoani Arusha.

Tukio hilo lilitokea katika viwanja vya Hoteli ya St Gasper nje kidogo ya mji wa Dodoma, walipokwenda kwa ajili ya kuhudhuria semina ya wabunge wapambanaji na Ukimwi, ambapo baadhi ya wabunge wa Chadema walihudhuria, baada ya kutoonekana mjini humo tangu Juni 17 mwaka huu.

Wabunge hao wa Chadema hawakuhudhuria kikao chochote cha Bunge kutokana na kwenda mkoani Arusha kwa shughuli mbalimbali, kutokana na mlipuko wa bomu uliotokea katika mkutano wao wa kuhitimisha kampeni zake za uchaguzi mdogo wa udiwani katika viwanja vya Soweto, Juni 16 jijini humo.

HALI YA MANDELA NI TETE...ASHINDWA KUFUMBUA MACHO KWA SIKU KADHAA

Mzee Nelson Mandela ameendelea kuwa katika hali mbaya hospitalini jana baada ya kubainika kwamba gari la wagonjwa lililombeba Rais huyo wa zamani wa Afrika Kusini kwenda hospitali limeharibika.

Gari hilo la wagonjwa mahututi liliharibika wiki mbili zilizopita wakati Mandela alipokuwa akikimbizwa kwenye hospitali moja mjini Pretoria, na kumwacha 'njiapanda' kwa dakika 40.

Rais huyo wa zamani wa Afrika Kusini alihamishiwa kwenye gari jingine la wagonjwa la hospitali ya kijeshi kumalizia safari iliyobaki ya dakika 50 kati ya Johannesburg na Hospitali ya Moyo ya Medi-Clinic.

Msemaji wa Rais Mac Maharaj alisema: "Tahadhari zote zimechukuliwa kuhakikisha kwamba hali ya kiafya ya rais wa zamani Mandela haiathiriki na tukio hilo."

Saturday, June 22, 2013

TANZANIA NCHI BORA KWA SAFARI ZA KITALII AFRIKA

Baadhi ya watalii wakiwa katika hifadhi ya Taifa ya Serengeti kujioea wanyama mbalimbali ikiwemo makundi ya nyumbu wakati yakivuka mto Mara kurejea katika hifadhi hiyo kutoka Maasai Mara.

 NYOTA ya Tanzania katika sekta ya Utalii imeendelea kung’ara zaidi badaa ya hivi karibuni kuchaguliwa kuwa ndio nchi bora kwa watu mbalimbali kuweza kufanya safari za kitalii miongoni mwa nchi barani Afrika.

Kwa mujibu utafiti uliofanywa na kutolewa hivi karibuni na katika mtandao wa Kampuni ya marketplace  kwa ajili ya safari za Africa (marketplace for African safari tour)

Tanzania imepata kura nyingi zaidi ziliyotolewa kama maoni ya  watu kufuatia utafiti huo ambapo Safaribooking .com ilifanya mchanganuo huo kwa kupitia maoni 3061ya zaidi ya watalii na wasafiri waliohusishwa katika utafiti huo na kuhitimisha kuwa katika  nchi zote zilizopendekezwaa barani Africa,Tanzania ni zaidi.