Tuesday, March 12, 2013

Magazeti ya leo Jumanne ya 12th March 2013





MTOTO WA MIAKA 8 AFUNGA NDOA NA JIMAMA LA MIAKA 61...

 Kijana huyo Sanele Masilela alisimama mbele ya watu 100 na kufunga ndoa na Bi Shabangu, mama mwenye watoto watano .

WAKENYA WAANDAMANA KUPINGA MATOKEO YA URAIS

Polisi wa kutuliza ghasia, wamelazimika kutumia mabomu ya machozi nchini Kenya, mji wa Kisumu kuwatawanya waandamanaji waliokuwa wakipinga matokeo ya urais ambayo mgombea wao, Raila Odinga alishindwa katika uchaguzi uliofanyika nchini humo.

Vurugu hizo ziliibuka, baada ya kutangazwa kwa matokeo ya urais yaliyompa ushindi Uhuru Kenyatta.

DOKEZO
Mahakama Kuu ya Kenya ndicho chombo pekee chenye uwezo wa kutengua matokeo ya urais yaliyotangazwa IEBC.

Jopo la majaji watano ndilo litakalosikiliza rufaa ya mgombea wa Cord, Raila Odinga; nao ni Jaji Mkuu, Dk. Willy Mutunga ambaye ni Rais wa Mahakama hiyo, wengine ni Majaji Dk. Smokin Wanjala, Njoki Ndung’u, Philip Tunoi, Jackton Boma Ojwang na Mohamed Ibrahim.

Source: Mwananchi, Jumatatu, Marchi 11, 2013

"BILA DIAMOND SINA MVUTO"...WEMA SEPETU

Wema Sepetu amefunguka kuwa anapenda kuvaa urembo wenye madini ya almasi (diamond) kwani humpendeza kuliko madini mengine.

Akizungumza na mwandishi wetu, Wema alisema amekuwa akivaa madini mbalimbali ila tangu alipoanza kuvaa ya ‘diamond’, watu wake wa karibu wamekuwa wakimsifia kuwa anatoka chicha.

“Ukiniambia nichague madini kati ya silver, gold na diamond mimi nitachagua diamond kwani yananipendeza sana, bila kuyavaa nahisi sijapendeza,’’ alisema Wema.