Friday, June 29, 2012

OMOTOLA AONDOKA WEMA AMZAWADIA MAPAMBO YA ASILI

 Mwigizaji Omotola Jalade wa pili kushoto akikabidhiwa zawadi na za khanga, shanga na viatu Wema Sepetu wakati akiondoka kuelekea Nigeria jana usiku. Wanaoshuhudia ni Mkurugenzi wa Kampuni ya One Touch Solutions, Petter Mwendapole ambao waliratibu ziara ya msanii huyo. Mwingine wa msanii Snura.


Omotola akijaribu bangili za kimasai alizopewa kama zawadi
Mwigizaji Wema Sepetu akimvalisha Khanga Omotola Jalade muda mfupi kabla ya hajandoka nchini kuelekea Nigeria.


 MWIGIZAJI  maarufu kutoka Nigeria Omotola Jalade Ekeinde aliondoka nchini jana usiku na kuahidi kusaidia soko la filamu nchini liweze kufikia ngazi za kimataifa.

Akizungumza na Mkurugenzi wa kampuni ya One Touch Solutions, Petter Mwendapole iliyoratibu ziara yake pamoja na mwigizaji Wema Sepetu aliyekuwa mwenyeji wake, Omotola alisema Tanzania ina kila sababu ya kuwika kimataifa katika filamu.

“Kwa Afrika Tanzania inaweza kuwa namba moja kama Nigeria, mna hali ya hewa nzuri, vivutio vya utalii na pia mna waigizaji ambao wana vipaji, hii inaweza kuwapeleka mbali yapo mambo madogo ya kurekebisha,” amesema.

Alisema kwa kuanzia atafanya kazi kwa karibu na Wema Sepetu ambaye ndiye alikuwa mwenyeji wake na kuhakikisha anafikia mafanikio ya juu katika tasnia hiyo kwa kimataifa.

Omotola mama wa watoto watatu, alisema kwa Nigeria yeye anafahamika kama Super Star hiyo alipoambiwa anakuja kuzindua filamu ya jina hilo alijiona kuwa ni muhisika wa moja kwa moja.
Tangu kuwasili kwake nchini vyombo mbalimbali vya habari vya Nigeria vimekuwa vikatangaza na kuzipa taarifa za uzinduzi wa filamu ya super star nafasi kubwa.

Akiwa nchini alitembelea kituo cha watoto yatima kinachohudumiwa na Tanzania Mitindo House, kabla ya kula chakula cha mchana na watoto hao nyumbani kwa Wema na jioni yake kuzindua filamu katika hoteli ya Giraffe. Pia alitembelea jengo la Quality Plaza ambapo alikwenda kuangalia sinema.

Wakati akiondoka, Omotola alikabidhiwa Khanga, viatu vya kimasai na shanga. Mbali na Wafanyakazi wa One Touch na Endless Fame na Image Professional mwigizaji mwingine maarufu nchini na Mkurugenzi wa 5 Effect, Gabriel Mtitu alikuwepo uwanjani hapo kumsindikiza na walizungumza mambo kadhaa.

HIVI KWELI KUNA MTU “ANASTAHILI” KITENDO HIKI?

Soma hii habari kuhusu kauli ya Mbunge wa Korogwe Vijijini,Steven Ngonyani(Maji Marefu) na kujiuliza hivi baadhi ya hawa watu tunaowaita wawakilishi wetu huwa wanaropoka tu au wakiwa kule Bungeni wanasema kile ambacho wananchi wao wamewatuma au kile ambacho wanaamini kabisa kitasaidia wananchi wa jimbo wanaloliwakilisha?

Hivi kweli katika dunia ya leo ambapo wote tunaongelea habari za ukomeshwaji wa mateso(torture) dhidi ya binadamu, yupo Mbunge ambaye anaweza kusimama na kusema kipigo kama alichokipata Dr.Steven Ulimboka alistahili? Yaani kwa mwakilishi huyu,case closed,justice has been served! Mbaya zaidi Mbunge huyu hakutolewa Bungeni!

    "Mbunge wa Jimbo la Korogwe Vijijini, Steven Ngonyani maarufu kwa jina la Profesa Maji Marefu (pichani), leo amesema bungeni kuwa kipigo alichopata Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari, Dk. Steven Ulimboka, kinastahili ili naye apate machungu wanayopata wagonjwa wengine mahospitalini.

    Profesa Maji Marefu aliitoa kauli hiyo wakati akichangia hoja katika bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Bungeni Dodoma.

    Kauli hiyo ilisababisha tafrani kidogo bungeni, ambapo  Spika wa Bunge, Mhe. Anne Makinda  alilazimika kuingilia kati kumzuia Profesa Maji Marefu asiendelee kutoa kauli hiyo kwani jambo la madaktari bado liko mahakamani."

Chazo: blog ya Michuzi

MADAKTARI 72 WATIMULIWA KAZI MKOANI MBEYA


Mwenyekiti wa Bodi na Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Norman Sigara akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake kuhusu kufukuzwa kazi kwa madaktari hao.
                      Mkurugenzi wa Hospitali ya Rufaa jijini Mbeya, Dk E. Sankey akimsikiliza kwa makini  Kaimu  Mkuu wa Mkoa wa Mbeya.

BODI ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mbeya, imewasimamisha kazi madaktari 72 kwa kosa la kutoingia kazini kwa siku tano jambo ambalo ni kinyume cha makubaliano ya mkataba.

Imeelezwa kuwa madaktari hao ambao 54 ni wale wa mafunzo ambao waliingia mkataba wa miaka miwili na hospitali ya Rufaa na madaktari 18 ni wale walioajiriwa na Wizara ya

Akizungumza na waandishi wa habari, Mwenyekiti wa Bodi Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Norman Sigara, alisema kitendo cha madaktari kutoripoti kazini kwa siku tano ni ukiukwaji wa kanuni za utumisha wa umma toleo la 2009 kifungu namba F.16-F17 na F. 27.

"Hivyo kupitia kanuni hiyo madaktari hao wamesimamishwa kazi na kurudishwa kwa mwajiri wao ambaye ni Katibu Mkuu Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kwa hatua zaidi za kinidhamu,"alisema Sigara.

Kwa mujibu wa Mwenyekiti huyo wa Bodi, imeelezwa kuwa siku ya tarehe 23/6/2012 wafanyakazi 15 waliokuwa zamu(Intern Doctors 12 na Registrars3) hawakufika kazini na tarehe 24/6/2012 wafanyakazi 19(Intern doctors 15 na Registrars 4) hawakufika kazini.

Alisema, kuanzia tarehe 25/6/2012 hadi leo imethibitika kuwa Interns doctor 54 na Registrars 18 hawakufika kazini hadi leo tarehe 28/6/2012 ambapo tarehe 25/6/2012 bodi ya hospitali ilifanya kikao cha dharura kujadili hali ya utendaji kazi na utoaji huduma hospitalini na kutoa uamuzi.

Sigara, aliyataja maamuzi hayo kuwa ni Mwenyekiti wa Bodi akutane na madaktari ambao hawakufika kazini ili awasikilize sababu za kutofika na kujadili namna ya kumaliza matatizo hayo jambo ambalo madaktari hao waligoma.

Alisema, baada ya madaktari hao kukaidi ombi hilo, Bodi ya hospitali ili waandikia barua za kujieleza kwanini wasichukuliwe hatua za kinidhamu kwa kuvunja mkataba walioingia na hospitali na pia kukiuka kanuni za kudumu za utumishi wa umma nalo walilikaidi

"Iwapo madaktari ambao hawakuripoti au kueleza sababu za kuridhisha ifikapo tarehe 28/6/2012. Kwa kuzingatia kanuni za utumishi wa Umma, madaktari hao watasimamishwa kazi na kurudishwa kwa mwajiri wao ambaye ni Katibu Mkuu Wizara ya Afya na Ustawi wa jamii,"alisema.

Aidha, alisema kuwa kwa ujumala madaktari hao waligomea barua zote mbili yaani ya kuitwa kwenye kikao pamoja na ile ya kuwataka kujieleza hivyo Bodi imechukua hatua za kisheria za kuwafukuza kazi.

Hata hivyo Mwenyekiti huyo wa bodi, alisema kuwa tayari hospitali ya Rufaa kwa ushirikiano wa Mkurugenzi wa Jiji la Mbeya, madaktari watano wamepatikana ili kusaidia huduma kwa hospitali hiyo.

CHANZO: http://mbeyayetu.blogspot.com/

HIVI ULISIKIA ALICHOSEMA WAZIRI MKUU JANA BUNGENI? KUHUSU KUJIUZULU NA MGOMO WA MADAKTARI? CHOTE KIKO HAPA..


Jana ndio siku ambayo waziri mkuu Mizengo Pinda aliahidi kutoa jibu la serikali bungeni kuhusu itakachofanya kuhusu mgomo wa Madaktari.

Kuhusu kujiuzulu kutokana na mgomo wa sasa likiwa ni swali kutoka kwa mbunge Tundu Lisu wa Singida Mashariki amesema “yako mazingira unaweza ukawajibika kwa njia hiyo lakini sio lazima yakawa yoote na mimi sioni kama hili ni moja ya maeneo ambayo unaweza ukasema kistahiki hivi unaweza kufikia hatua hiyo, ninachokubali tu ni kwamba tatizo hili ni kweli ni la muda mrefu na nimefanya kila njia kujaribu kulitatua kwa kiasi kikubwa sana, inabidi tukubali kwamba bado lina changamoto nyingi kwa sababu ya mambo mengi tu ambayo yameingiliana na mgogoro wenyewe”

Freeman Mbowe kiongozi wa kambi ya Upinzani bungeni alisimama na kumuuliza Waziri Mkuu kwamba “ulitoa kauli ambayo kama mzazi au kama baba imetia hofu kubwa sana katika taifa pale ulipokua unazungumzia mgomo wa Madaktari na hatimae ukasema na LITAKALOKUWA NA LIWE, vilevile zilipatikana taarifa nyingine kwamba rais wa Madaktari ametekwa juzi usiku, ameteswa, kavunjwa meno, kango’lewa kucha.. unalieleza nini taifa kuhusu kauli yako ya LITAKALOKUA NA LIWE? na serikali inafanya nini cha ziada?

Hili ndio jibu alilotoa Waziri mkuu kwa Freeman Mbowe: “Kwanza nikiri kwamba ni kweli nilitamka hivyo jana lakini kilichokua kinanisumbua kichwani ni kwa sababu nilijua jambo hili liko mbele ya mahakama kuu, kuhusu yaliyompata Dr Ulimboka naonyesha masikitiko yangu juu ya jambo hili na ninamtakia kila la kheri na apone haraka”

Kuhusu alichoahidi kukiongea leo kuhusu Mgomo unaoendelea Waziri Mkuu amesema “tumezungumza na vyombo mbalimbali ili tuone katika mazingira tuliyonayo ni namna gani tutawahudumia wagonjwa, tumewaomba wenzetu wa LUGALO tutumie hospitali ile kuhakikisha wagonjwa hawakosi hiyo huduma, hata hospitali zake nyingine ndogo zote tumeamue tuzitumie kwa njia hiyo, lakini pia tumeona ni vizuri kama kutakua na madaktari wengine waliostaafu na wengine waliopo wizarani pale wote tumeomba sasa watafutiwe njia mbalimbali ili warudi waweze kutoa hiyo huduma kwa Watanzania”

MAGAZETI YA LEO IJUMAA JUNE 29


RIPOTI KAMILI

     Dk Ulimboka akiendelea kupata matibabu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kitengo cha mifupa (MOI)  kwenye chumba cha wagonjwa mahututi (ICU).

   NYUMA ya kipigo alichopewa kiongozi wa madaktari ambao wako kwenye mgomo nchi nzima, Dk. Steven Ulimboka kuna siri nzito, Ijumaa lina ripoti kamili.

  Gazeti hili lilinyetishiwa mkanda mzima na mtu aliyekuwa na Dk. Ulimboka (jina tunalo ambaye naye ni daktari) usiku wa kuamkia Jumatano wiki hii kwenye Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni jijini Dar es Salaam.

   MUVI LA MATESO LAANZA
Jamaa huyo alidai kuwa, wakiwa viwanjani hapo wakipooza koo, walifika watu watano waliojitambulisha kuwa ni askari wakiwa na silaha ambapo walidai kuwa walimfuata Dk. Ulimboka na kumwambia anatakiwa Kituo cha Polisi Kati (Central).

  Ilidaiwa kuwa Dk. Ulimboka alishurutishwa kupanda kwenye gari leusi ambalo halikuwa na namba za usajili na kuondoka eneo hilo huku akiacha gumzo kuwa Central anapelekwa kwa ishu gani.
Ikadaiwa kuwa baada ya Dk. Ulimboka kuchukuliwa, marafiki zake walitoka spidi kuelekea Central kujua kulikoni na pia kumwekea dhamana.

  Jamaa huyo alidai kuwa marafiki zake walipofika Central hawakumkuta na wala hakukuwa na dalili za Dk. Ulimboka kufikishwa mahali hapo.

  Aliendelea kudai kuwa walianza kufanya mawasiliano usiku huo ili kujua rafiki yao alipelekwa wapi lakini jitihada hizo hazikuzaa matunda.

  SIMU HAIPATIKANI
Alidai wakiwa Central, askari mmoja aliwataka kutulia hadi asubuhi wangepata taarifa kamili kwani kwa wakati huo hata simu yake ilikuwa haipatikani.

  Jamaa huyo alidai kuwa saa 12:00 asubuhi alipokea simu kutoka kwa msamaria mwema aliyekuwa maeneo ya Mabwepande nje kidogo ya Jiji la Dar akamwambia kuna mtu amemkuta akiwa taabani ambaye alimtajia namba kwa shida ili aipige na kutoa taarifa ya hali yake.

  “Alisema alimtajia namba tu na hakumsesha tena,” alisema rafiki huyo wa Dk. Ulimboka.
Alidai kuwa baada ya kujulishwa habari hiyo alitaka aende mwenyewe lakini alipoomba ushauri watu walimsihi asiende peke yake.

  Jamaa huyo alisema alitafuta watu akaenda nao na walipofika huko walimkuta Dk. Ulimboka aliyechukuliwa akiwa mzima hajitambui na hakuwa na uwezo wa kuzungumza.

  Alisema kuwa baada ya kumuona mwenzao alivyochakazwa, wakamchukua na kumpeleka kwenye Kituo cha Polisi cha Bunju ambapo yule msamaria mwema alitoa maelezo jinsi alivyomkuta.

  Rafiki huyo wa Dk. Ulimboka alidai kuwa, katika maelezo ya yule msamaria mwema alisema kuwa alishtuka alipomkuta akiwa porini na hali mbaya huku akiwa amefungwa kitambaa cheusi usoni na kutapakaa madonda mabichi mwili mzima.

  Baada ya kuchukuliwa maelezo walipatiwa PF-3 ambapo walifanya jitihada za kumkimbiza katika Hospitali ya Muhimbili kwa kutumia ambulance ya AAR, alipofikishwa tu madaktari wenzake walianza kumpa matibabu ya hali ya juu ili kunusuru uhai wake huku mgomo wao ukiendelea.

 MTU ALA KIPIGO
Wakati anafikishwa Muhimbili tayari wanaharakati mbalimbali walishajitokeza ili kumpokea lakini mara baada ya kufikisha mtu mmoja aliyesadikiwa kuwa ‘njagu’ aliingia chooni na akasikika akizungumza na simu.

Ilidaiwa kuwa katika mazungumzo yake alisikika akisema kumbe jamaa hajafa, jambo lililoibua hisia kwamba alijua kilichoendelea.
Ilisemekana kuwa watu waliomsikia wakamchomoa na kumpa kipigo cha mbwa mwizi hadi Radio Call inayotumiwa na polisi ikamchomoka kwenye suruali kabla ya askari waliokuwa doria kumwokoa na kuondoka naye.

KOVA ATHIBITISHA
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova alithibitisha kutokea kwa tukio hilo linalodaiwa kuwa la utekaji na kuongeza kuwa uchunguzi unafanyika na sheria itachukua mkondo wake dhidi ya wahusika.

Wananchi waishauri serikali
Wakiongea na Ijumaa mara baada ya tukio hilo kutokea, baadhi ya wananchi wameitaka serikali kuhakikisha uchunguzi wa kina na wa haraka unafanyika na ripoti yake kuwekwa hadharani ili kuondoa utata uliotawala.

Imeandaliwa na Haruni Sanchawa, Issa Mnally na Makongoro Oging.

Kikazi Zaidi Jamani

Anatisha Wema Sepetu