Saturday, January 19, 2013

SONY YAZINDUA "SONY Experia Z" SIMU YENYE TEKNOLOJIA YA HALI YA JUU NA ISIYODHURIKA NA MAJI!




 Kampuni kubwa na maarufu kwa utengenezaji wa vifaa vya umeme kwa matumizi mbalimbali kamavile luninga,michezo ya vedeo"Video Games",redio,nk imezindua rasmi toleo jipya ya simu za Smartphone "SONY  Experia"na sasa ni "SONY  Experia  Z".Kifaa hiki kina mambo yafuatayo

•Inaweza kustahimili maji na vumbi bila madhara yoyote
•5-inch full Touch HD screen
•Inatumia Android 4.1 aka Jelly Bean
•2GB RAM na memory ya 16GB ndani huku inauwezo wa kuendesha memory card mpaka 32GB.
•Kama zilivyo iPhone 5,Samsung Galaxy S III na vifaa vingine vyenye uwezo mkubwa,inaruhusu 4G/LTE band kwa internet yenye kasi kubwa.
•Xperia Z inakuja na kamera ya megapixel 13.1 na kamera nyingine ya mbele yenye 2.2MP.Hii ni zaidi ya iPhone 5 na Samsung Galaxy S III,zote zenye kamera ya 8 megapixel .
 Toleo jipya kabisa la simu aina ya Smartphone kutoka SONY "Experia Z" ndio inayosifika kwa mwonekano mzuri kuliko simu zote za Smartphone!
 SONY Experia Z ikiwa katika maonesho huko Las Vegas,Marekani
 SONY Expria Z haisababishiwi matatizo yoyote na maji wala vumbi.
 Simu hii kutoka SONY inafanya kazi zake zote hata ndani ya maji bila kuleta hitilafu wala kuharibika.
 Picha,muvi na kitu chochote kwenye simu hii inaweza kuonekana kwenye luninga yako bila waya wowote ule!

Mahafali ya Kidato cha Sita shule ya Sekondari Azania Mstahiki Meya Jerry Silaa akiwa mgeni rasmi

Mgeni rasmi Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Silaa akibadilishana mawazo na baadhi ya Wanafunzi wa shule ya Sekondari Azania ambapo na yeye pia alikuwa ni miongoni mwa baadhi ya viongozi waliosoma shule hapo baada ya kuwasili kwenye hafla mahafali ya wanafunzi wa kidato cha sita.
   Picha ya chini ni  Mstahiki Meya Jerry Silaa akipunga mkono kwa wanafunzi wa shule ya sekondari Azania waliojipanga mstari kumlaki kwa furaha huku akiwa ameambatana na Mkuu wa Shule hiyo Bw. Bernard Ngoze na Makamu Mkuu wa Shule hiyo Bi. Elizabeth Ngoda (kulia).


Mgeni rasmi Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Silaa akisalimiana na kuwapongeza baadhi ya wanafunzi wa kidato cha Sita wa Shule ya Sekondari Azania
Mstahiki Meya Jerry Silaa akipokea heshima kutoka kwa vijana wa skauti wa Shule ya Sekondari Azania

DK. SHEIN AFUNGUA MKUTANO WA BARAZA LA BIASHARA LA ZANZIBAR ZBC

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akifungua Mkutano wa Saba (7) wa Baraza la Biashara la Zanzibar ZBC,uliofanyika leo katika Ukumbi wa Salama Bwawani Hotel Mjini Unguja,(kulia) Katibu Mkuu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi Dk.Abduhamid Yahaya Mzee,na Waziri wa Biashara, Viwanda na Masoko,Nassor Ahmed Mazrui,
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,(katikati) akifuatana na  Waziri wa Biashara, Viwanda na Masoko,Nassor Ahmed Mazrui,(katikati) na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Juliun Raphael,alipowasili katika Viwanja vya  Salama Bwawani Hotel Mjini Unguja,kuufungua Mkutano wa Saba (7) wa Baraza la Biashara la Zanzibar ZBC,uliofanyika leo.

Simba yaogelea tatu Oman

MABINGWA wa Tanzania, Simba wameendelea kupokea kipigo nchini Oman baada ya jana kufungwa mabao 3-1 na timu ya Taifa ya Jeshi ya Oman.Kiungo wa Simba, Haruna Moshi alifunga bao la

kufutia machozi katika dakika ya 69 baada ya wenyeji Jeshi la Oman kufunga mabao yao kupitia Alabab Alnoaley (22), Yones Almushefrei (89) na Kassim Said.

Simba ilianza mchezo huo kwa kasi, lakini wenyeji walitumia vizuri udhaifu wa ngome wa mabingwa hao wa Tanzania katika kuokoa mipira ya kona kufunga mabao yao.

Kocha wa Simba Patrick Liewig alisema baada ya mechi hiyo kuwa mechi ni nzuri, lakini vijana wake wamezidiwa umakini.

“Inakera kwa sababu timu inacheza vizuri lakini mnafungwa kwa sababu ya uzembe.

“Yaani mtu anapiga kona anafunga mara mbili, ni tatizo, hata hivyo bora nimeliona hili mapema kwa ajili ya kulifanyia kazi.”

Kikosi

Simba: Juma Kaseja/Abel Dhaira, 2 Nassor Said ‘Cholo’/ Haruna Shamte, 3 Paul Ngalema/ Kigi Makassy, 4 Mussa Mudde, 5 Shomari Kapombe, 6 Jonas Mkude/ Abdallah Seseme, 7 Haruna Chanongo, 8 Mwinyi Kazimoto/ Amri Kiemba, 9 Felix Sunzu/ Abdallah Juma, 10 Mrisho Ngassa/Haruna Moshi na 11 Ramadhani Chombo.

Yaliyojiri leo Magazetini jumamosi ya 19th January 2013


IDADI KAMILI YA WALIO CHUKUA FOMU TFF NA KUREJESHA

Wanamichezo 50 kati ya 52 waliochukua fomu kuomba kuwania nafasi mbalimbali za uongozi katika uchaguzi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) utakaofanyika Februari 24 mwaka huu wamerejesha fomu hizo.

Waombaji ambao hawakurejesha fomu ni Geofrey Nyange aliyekuwa akiomba ujumbe wa Kamati ya Utendaji kuwakilisha mikoa ya Morogoro na Pwani, na Shufaa Jumanne aliyekuwa akiomba kuwakilisha Kanda ya Dar es Salaam.

Orodha kamili ya waombaji ambao wamerejesha fomu ni Athuman Nyamlani, Jamal Malinzi, Omari Nkwarulo na Richard Rukambura (Rais). Michael Wambura, Ramadhan Nassib na Wallace Karia (Makamu wa Rais).

JK aanza ziara ya kikazi ufaransa

RAIS wa Jamhuriya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete (pichani) anaanza ziara rasmi ya Kiserikali nchini Ufaransa leo, Jumamosi, Januari 19, 2013, kwa mwaliko wa Rais wa Ufaransa, Mheshimiwa Francois Hollande.

Rais Kikwete na ujumbe wake aliondoka nchini usiku wa kuamkia leo, Jumamosi, kwa ndege ya Shirika la Ndege la Uswisi kuelekea Ulaya kwa ajili ya ziara hiyo.

Mara baada ya kuwasili kwenye Uwanja waNdege wa Charles De Gaul mjini Paris leo jioni, Rais Kikwete ambaye anafuatana na Mama Salma Kikwete atapokelewa rasmi katika Ufaransa kwa gwaride na kupokelewa na Waziri wa Misaada ya Maendeleo wa Ufaransa, Mheshimiwa Paschal Canfin.

Miss utalii wawasili kambini

Washiriki wanao wanania Taji la Miss Utalii 2012/13 wakiwa katika picha ya pamoja muda mfupi baada ya kuwasili Kambini, Ikondolelo Lodge Hoteli iliyopo Kibamba Jijini Dar es salaam.

Jumla ya warembo arobaini kati ya sitini wa Miss Utalii Tanzania kutoka mikoa yote ya Tanzania.tayari wameripoti kambini leo,kuanza kambi Taifa ya siku 21  kuanzia leo. Kambi hiyo mwaka huu iko katika Hoteli ya Ikondelelo Lodge iliyoko Kibamba Dar es Salaam.