Saturday, September 29, 2012

SIMBA vs TANZANIA PRISONS Mechi Inaendelea Jion Hii

Timu za Simba na Tanzania Prisons zinapambana jioni hii Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 11 kamili jioni. Tayari makocha wa timu zote mbili Jumanne Charles (Tanzania Prisons) na Circo Milovan (Simba) wameshataja vikosi vyao.

Simba:  VS    Tanzania Prisons:
01.Juma Kaseja (c)                        18.David Abdallah
02.Nassoro Masoud                         03.Aziz Sibo
17.Amir Maftah                            05.Laurian Mpalile
15.Shomari Kapombe                        16 .Lugano Mwangama (c)
24.Juma Nyoso                             15.David Mwantika 
14.Mwinyi Kazimoto                        13.Khalid Fupi
28.Amri Kiemba                            07.Misango Magai
08.Ramadhan Chombo                        12.Fred Chudu
19.Edward Christopher                     14.Elias Maguri
10.Felix Sunzu                            17.Peter Michael
16.Mrisho Ngasa                           19.John Matei

Wachezaji wa akiba;
22.Wilbert Mweta                          01.Daudi Mwasongwe
23.Paul Ngalema                           04.Jumanne Elfadhili
20.Jonas Mkude                            09.Sino Augustino
12.Salim Kinje                            22.Julius Kwaga
04.Komanbil Keita                         08.Henry Mwalugala
13.Daniel Akuffor                         11.Hamisi Ally
05.Pascal Ochieng                         23.Jeremiah Juma

Refa: Paul Soleji (Mwanza)
Mwamuzi Msaidizi 1: Jesse Erasmo (Morogoro)
Mwamuzi Msaidizi 2: Mwarabu Mumba (Morogoro)
Mwamuzi wa Akiba: Israel Nkongo (Dar es Sala

RAIS KIKWETE AONANA NA UJUMBE WA MWAPORC IKULU, DAR ES SALAAM, LEO

 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na ujumbe toka kampuni ya Mwambani Port and Railway Corridor Company (MWAPORC) uliomtembelea leo Septemba 29, 2012 Ikulu jijini Dar es salaam kumweleza nia yao ya kutaka kuwekeza katika sekta ya reli.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiuonesha njia za reli katika  ramani ya Tanzania ujumbe toka kampuni ya Mwambani Port and Railway Corridor Company (MWAPORC) uliomtembelea leo Septemba 29, 2012 Ikulu jijini Dar es salaam kumweleza nia yao ya kutaka kuwekeza katika sekta ya reli.

PICHA NA IKULU

KIINGILIO MECHI YA YANGA, SIMBA SH. 5,000, LINE UPS ZA VIKOSI SIMBA NA PRISON

Kiingilio cha chini kwenye mechi ya Yanga (anae kipiga kiungo wa Rwanda Haruna Niyonzima) na Simba (anae chezea kiungo wa Tanzania Mwinyi Kazimoto) itakayochezwa Jumatatu (Oktoba 3 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kitakuwa sh. 5,000 kwa viti vya rangi ya kijani ambavyo ni 19,648 kwenye uwanja huo wenye uwezo wa kuchukua watazamaji 60,000.

Mechi hiyo namba 80 ya Ligi Kuu ya Vodacom itachezwa kwenye uwanja huo kuanzia saa 11 kamili jioni.

Watazamaji watakaotaka kuona mechi hiyo wakiwa wameketi kwenye viti vya rangi ya bluu ambavyo ni 17,045 watalipa sh. 7,000 kwa tiketi moja.

Viingilio vingine kwenye mechi hiyo ni sh. 10,000 kwa viti vya rangi ya chungwa ambavyo viko 11,897 wakati VIP C inayochukua watazamaji 4,060 itakuwa sh. 15,000.

Kwa upande wa VIP B tiketi ni sh. 20,000 na VIP A yenye watazamaji 748 tu kiingilio kitakuwa sh. 30,000.

SIMBA vs TANZANIA PRISONS LINE UPS
Timu za Simba na Tanzania Prisons zinapambana jioni hii Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 11 kamili jioni. Tayari makocha wa timu zote mbili Jumanne Charles (Tanzania Prisons) na Circo Milovan (Simba) wameshataja vikosi vyao.

Simba:                                        Tanzania Prisons:
01.Juma Kaseja (c)                            18.David Abdallah
02.Nassoro Masoud                             03.Aziz Sibo
17.Amir Maftah                                05.Laurian Mpalile
15.Shomari Kapombe                            16.Lugano Mwangama (c)
24.Juma Nyoso                                 15.David Mwantika
14.Mwinyi Kazimoto                            13.Khalid Fupi
28.Amri Kiemba                                07.Misango Magai
08.Ramadhan Chombo                            12.Fred Chudu
19.Edward Christopher                         14.Elias Maguri
10.Felix Sunzu                                17.Peter Michael
16.Mrisho Ngasa                               19.John Matei

Wachezaji wa akiba;
22.Wilbert Mweta                              01.Daudi Mwasongwe
23.Paul Ngalema                               04.Jumanne Elfadhili
20.Jonas Mkude                                09.Sino Augustino
12.Salim Kinje                                22.Julius Kwaga
04.Komanbil Keita                             08.Henry Mwalugala
13.Daniel Akuffor                             11.Hamisi Ally
05.Pascal Ochieng                             23.Jeremiah Juma

Refa: Paul Soleji (Mwanza)
Mwamuzi Msaidizi 1: Jesse Erasmo (Morogoro)
Mwamuzi Msaidizi 2: Mwarabu Mumba (Morogoro)

Mwamuzi wa Akiba: Israel Nkongo (Dar es Salaam

ERMIE ATAMBULISHWA KUWA KOCHA WA YANGA

                                                Kocha Mpya wa Yanga katika utambulisho

Hatimaye leo hii klabu bingwa ya Afrika mashariki na kati Dar Young Africans imemtambulisha rasmi kocha wake mpya Mholanzi Ernie Brandts.

Kocha huyu ambaye miezi michache iliyopita alikuwa mwalimu wa klabu bingwa ya Rwanda, APR aliwasili jijini Dar es Salaam jana usiku na leo asubuhi ametambulishwa rasmi kwa waandishi wa habari na kusaini mkataba wa mwaka mmoja wa kuifundisha klabu hiyo ya Jangwani.

Brandts ambaye amewahi kuwa mchezaji wa timu ya taifa ya Uholanzi na klabu kubwa ya nchi hiyo PSV Eindhoven akicheza kwenye nafasi ya ulinzi, amekuja Yanga kuchukua nafasi ya mbelgiji Tom Saintfiest aliyetimuliwa wiki iliyopita baada ya kukaa kwenye klabu hiyo kwa siku 81.

SOURCE: Shaffihdauda.com

MAONYESHO YA SARAKASI YA MAMA AFRIKA YAENDELEA KURINDIMA NEW WORLD CINEMA DAR

                         "Karibuni watanzania wote muone sarakasi na utamaduni wa kitanzania".
 Trade Marketing Supervisor wa kampuni ya simu za mkononi ya TIGO ambao ndio wadhamini wakuu wa maonyesho ya 'Sarakasi ya Mama Afrika' yanayoendelea katika viwanja vya New World Cinema Bw. Christopher Mmbando akiwakaribisha wageni waliohudhudhuria onyesho hilo. kushoto ni Afisa Mahusiano wa TIGO.
 




 

 Pichani Juu na Chini ni mfululizo wa maonyesho ya sarakasi ya 'Mama Africa Circus'.

Picha Juu na Chini ni baadhi ya wadau walioshiriki maonyesho hayo wakifurahia.

Magazeti ya Leo Jumamosi 29th September 2012

Friday, September 28, 2012

Ufafanuzi wa kilichotokea Uchaguzi Meya Mwanza..CCM Yafanya "UMAFIA"

CCM wameshindishwa na mbinu za kisiasa amabzo uhalali wake kisheria linabaki kuwa suala la wanasheria wanaojua taratiu zikoje.

Baada ya mgawanyo wa h/shauri ya jiji na kuwa na h/shauri ya jiji inayoundwa na jimbo la Nyamagana na halmashauri ya ilemela inayondwa na jimbo la ilemela mwezi Julai mwaka huu mgawanyo wa madiwai ulikuwa hivi kwa nyamagana

Chadema -wa kata 5, viti ,maalum 2. mbunge mmoja, jumla wanakuwa 8
CCM - wa kata 6, viti maalum 1 jumla wanakuwa 7
Cuf - wa kata 1, viti maalum 1

Ilemela

Chadema -- wak kata 6, viti maalum 2 mbunge 1 jumla wanakuwa 9
CCM - wa kata 3, viti maalum 2 na mbunge 1 (wa viti maalum) jumla wanakuwa 6
CUF - MBUNGE WA viti maalum 1

Kilchotokea kwenye uchaguzi ni CCM kuhamisha diwani mmoja wa viti maalum (kwa barua ya CCM kwenda kwa mkurugenzi wa jiji ya tarehe 14, Septemba, 2012) na mbunge wa viti maalum toka Ilemela kuja nyamagana na hivyo kuongeza idadi ya kura zao kuwa 9, wakati huo huo Chadema walishakuwa hawaihehabu kura ya Diwani wa Igoma Chagulani ambaye wamemfukuza uanachama akalejeshewa na mahakama wao wanapugukiwa na kura 1 zao zinabaki 7 , aliyepungua Chadema akiwapigia CCM wanakuwa na kura 10 dhid ya 7 za Chadema.

Lakini pia CUF walishakubaliana na chadema kuungana mkono, kwa hiyo kwa kura 2 za CUF Chadema wangekuwa na kura 9, lakini inaonekana ama mwana Chadema mmoja kapigia CCM au CUF mmoja kapigia CCM na kufanya matokeo ya kuwa kuwa 11 kwa CCM dhidi ya nane za Chadema.

Hiyo ndiyo hali halisi ya jinsi mahesau ya kura yalivyochezwa, kama kuna uhalali katika mchakato huo au la ni suala la wataalamu wa masuala haya kutujuza.

Hayo yakiendelea uchaguzi wa Meya wa Ilemela meahirshwa katika mazingira tata, baada ya Mkurugeni kusoma Amri ya Mahakama iliyopewa tafsiri na mwanasheria wa jiji kuwa inakifanya kikao hicho kuahirishwa kwa kuwa Diwani wa Chadema Matata (pia alifukuzwa uanachama pamoja na wa igoma na anaendelea na udiwani kwa amri ya makahama) kuleta pia barua ya kutaka atambuliwe kaa mgombea.

Ukazuka ubishi kidogo juu ya hoja ya mgombea kuteuliwa na chama, mkurugenzi wa jiji akasema hiyo siyo sheria ni mwogozo, na kwa kuwa sheria na mwongozo zikigongana sheria ndiyo inatamalaki hatakia aingie katka mgogoro wa tafsiri ya sheria, akaahirisha kikao bila hata madiwani kujadili hoja hiyo.

Kwa mujibu wa mwanasheria wa wa Chadema, pingamizi hilo lilikuwa linawarejeshea haki yao ya uanachama na hivyo kuendelea na udiwani wao, na kutaka matata asizuiliwe kuendelea na mchakato wa kuomba umeya, Kwa hiyo matata ameomba lakini hakuteuliwa na chama na mahakama haiwezi kuwalazmisha chama wateue mgombea kwa amri ya mahakama, anadhani ni uhuni tu na njama za kisiasa zimefanyika kuahirisha uchaguzi huo.
Nadhani kidogo piacha itaeleweka kwa wanjamvi juu ya nini hasa kimetokea.

SOURCE: Kamnada Deus Bugaywa-Mchambuzi Raia Mwema

BIRTHDAY YA WEMA SEPETU.

                             Mungu akupe Miaka aliyotuahidi ya Biblia ila tu Kwa kuacha ya duniani
Hii kutoka kwa Sukari ya Warembo

JK: Afungua Mkutano Wa Kimataifa Wa African Green Revolution Mjini Arusha


 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na Mwenyekiti wa Alliance for a Green Revolution in Africa Dkt.Kofi Annan(kushoto) pamoja na Mkurugenzi wa Bill and Melinda Gates, Bibi Melinda Gates wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Kimataifa wa” Africa  Green Revolution Forum 2012,” uliofanyika katika ukumbi wa Ngurdoto mountain Lodge mjini Arusha.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akitoa hotuba yake ya ufunguzi wa mkutano wa Kimataifa wa”African Green Revoultionmjni Arusha.

CCM Yashinda Umeya Jimbo La Nyamagana

 Mgombea wa kiti cha umeya katika Halmashauri ya jiji la Mwanza kupitia CCM na diwani wa kata ya Mkolani Ndg Stanslaus Mabula, ameshinda kiti cha umeya kwa jumla ya kura 11 dhidi ya mgombea wa CHADEMA diwani wa kata ya Mahina Ndg Charles Chinchibera aliyepata kura 8.

TAMKO LA CHAMA KUKANUSHA SHUTUMA ZA CHAMA CHA CUF KUFANYIWA VURUGU NA CHADEMA.




  CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO – CHADEMA
MKOA WA ARUSHA

Ndugu wananchi na wanahabari,
Siku ya terehe 27 Alhamisi Septemba 2012 chama cha wananchi CUF walitoa taarifa ya malalamiko kwa vyombo vya habari na mitandao kuwa wanachama wa CHADEMA wamewafanyia vurugu kwa kuwapiga mawe na kuwa jambo hilo limehamasishwa na viongozi wa chama katika mkoa wa Arusha pamoja na Mhe Godbless Lema.

Wote tunafahamu kuwa siku hiyo hiyo katika viwanja vya soko la Kilombero wafanyabiashara ndogo ndogo walikuwa wamevamia na walikuwa wakijigawia maeneo, baada ya eneo la awali walilopewa la viwanja vya NMC kushindwa kuwachukua wafanyabiashara wote na halmashauri kushindwa kutoa majibu kwa wafanyabiashara hawa ambao waliwaambia wote waende NMC. 

Kwanza tunapenda kutoa pole kwa viongozi wa CUF kwa jambo hili lililowapata. Wao kama watu na Watanzania wenzetu tunawapa pole sana.

Pili, CHADEMA inakanusha kuhusika na jambo hili. Hii si tabia ya CHADEMA na kamwe haiwezi kuwa tabia ya CHADEMA kufanya siasa chafu za namna hiyo. CHADEMA tunajali sana amani na upendo, na hii ndiyo tabia na makuzi yetu Watanzania.

Katika mazingira haya, CHADEMA tunachukua fursa hii kuvikaribisha vyama vyote mathalani CUF, Arusha ni yetu sote na tutumie demokrasia vizuri kufanya kazi nzuri ya siasa kwa ajili ya kusababisha na kuleta matumaini kwa Watanzania hawa ambao serikali ya chama cha mapinduzi imeshindwa kuwaletea.
CHADEMA hatuna shida na ushindani wa kisiasa katika mazingira ya kidemokrasia kwa maana ndio wakati pia wa wananchi kupima na kujua nani mkweli na ama nani anafanya kwa dhati ya kweli. Hivyo tunawakaribisha CUF karibuni Arusha na wala wasitafute kisingizio cha kuegemea ili CUF ianze kutajwa tajwa kwa kutumia mgongo wetu.
Sambamba na hili, CHADEMA mkoa wa Arusha tumesikitishwa sana na tamko la CUF lilitolewa na Naibu Mkurugenzi wa Habari, Uenezi na haki za BInadamu Mhe Abdul Kambaya, tamko lenye matisho na lugha isiyofaa. Moja na maneno ya tamko hilo wamesema, nukuu “Uwezo wa kuwafanya tutakavyo tunao na kwa sababu wameanza tunaweza kumaliza”. Wakazi wa Arusha na Watanzania wapime na waone, haya si maneno yanayoweza kutoka kwenye kichwa cha mtu anayefikiri vizuri, mtu anayeipenda nchi yake na kuheshimu utawala wa sheria. Zaidi ya hapo tamko hilo limesema pia, “Ile ngangari kwa polisi tunaweza kuwahamishia wao wakose pa kukaa”.
 
Katika yote haya, niwaombe wakazi wa Arusha, Wanachadema na hata wanachama wa vyama vingine tuwapende na tuwakaribishe CUF Arusha na sote tufanye kazi ya siasa kwa nguvu za hoja. CUF wanaweza kufanya hicho wanachotaka kufanya lakini CHADEMA kamwe hatupo tayari kwa vurugu ya aina yoyote, aidha tunawakaribisha kwa moyo mmoja na kama wapo tayari basi tufanye siasa zenye tija na manufaa kwa wakazi wa Arusha.

Aidha nitoe onyo kali sana kwa mamluki ambao wamekuwa wakijifanya kondoo kumbe ndani ni mbwa mwitu. Mara kadhaa watu hawa wamekuwa wakisababisha fujo ili kukifanya CHADEMA kionekane kuwa ni chama cha vurugu. MAMLUKI ni sumu, tukimgundua na kumthibitisha mtu wa aina hiyo katikati yetu tutamtangaza mbele ya jamii kuwa yeye ni sumu na kuomba wananchi wamtenge maana anapingana kwa kuleta hila na unafiki kwenye kazi ya kuwakomboa Watanzania. Niwatangazie mamluki hamtatuweza na tutawagundua tu.

Mwisho, tunapoelekea kwenye marudio ya uchaguzi mdogo kwenye kata za Daraja II kwa Arusha mjini na Bangata kwa wilaya ya Arumeru Magharibi, nirudie kusema maneno ya Mhe Lema kuwa iwapo viongozi na watumishi wa umma watajihusisha na kushiriki kwa kufanya kampeni za kisiasa wakiwa wanatumia magari na vifaa vingine vya serikali watu hawa tutawakamata na tutawapeleka huko wanakostahili kupelekwa wezi na vibaka wengine. Hii ni tahadhari tunamaanisha kweli na wananchi wote wawe makini “wakamate mwizi” lengo likiwa ni kuweka adabu kwa watumishi na viongozi umma wanaovunja sheria ya utumishi wao kwa umma na matumizi ya rasilimali kwa namna isivyotakiwa kisheria. CHADEMA tutashiriki chaguzi hizi na tunawaomba wakazi wote wa maeneo haya tushiriki kwa utulivu na amani.

WANACHADEMA wote tuendelee kuwa majasiri, tusiwe waoga na tusimamie kweli na haki.
“Hakuna kulala Mpaka Kieleweke”

Amani Sam Golugwa

KATIBU WA CHADEMA MKOA  WA ARUSHA: golugwa@gmail.com

Barua zote ziandikwe kwa Katibu wa Mkoa
Ofisi ya Mkoa –  Mtaa wa NHC – Ngarenaro: Nyumba Na 8.
S.L.P. 12525, Arusha, Tanzania. Simu: +255 754 912 914,
Email: info@chademaarusha.com.     Tovuti: www.chademaarusha.com
Thanks Crashwise: JF

CUF YASHUTUMU WAFUASI WA CHADEMA KWA KUSHAMBULIA WAFUASI WAKE KATIKA VURUGU ZA ARUSHA






Angalia picha jinsi ya mambo yalivyokuwa wakati wamachinga wa jijini Arusha walivyopora kiwanja na kuanza kujipimia ili kufanyia biashara kabla ya polisi kuinguilia kati


CHAMA Cha Watu wananchi CUF kimetoa tamko kali kwa kuwatuhumu wafuasi sita wa Chadema jijini Arusha kwamba walihusika na vurugu za kulishambulia gari la matangazo na kisha kumpiga mawe mfuasi wao huku wakilitaka jeshi la polisi kuchukua hatua kali za kisheria.

 Akitoa tamko hilo leo  katika ofisi za chama hicho zilizopo kata ya Kaloleni jijini Arusha,mjumbe wa baraza kuu la uongozi taifa wa CUF, Mbarala Maharagande, alisema kwamba chama chao kina ushahidi  wa kutosha kwamba mfuasi wao, Athuman Abdulraham, alipigwa mawe na wafuasi wa Chadema wakati akiwa katika gari la matangazo.

Maharagande,alisema kwamba mfuasi wao alikuwa katika eneo la Levolosi karibu na eneo lililovamiwa na wamachinga na wakati akiwa ndani ya gari hilo wafuasi wa Chadema walianza kumyooshea alama ya vidole viwili kabla ya kuanza kumpopoa kwa mawe.

Hatahivyo,alisisitiza kwamba tayari mfuasi huyo ameshatoa tarifa kwa jeshi la spolisi mkoani hapa na kufungua faili nambari AR/RB/12419/012 na kulitaka jeshi hilo kuwakamata wafuasi hao wa Chadema  hadi kufikia septamba 30 mwaka huu na wakishindwa wao watachukua  hatua za kisheria wanazozijua.

 “Kijana amepigwa na wafuasi wa Chadema na tayari tunawajua wako sita tumeshatoa tarifa polisi wawachukulie hatua na kama wakishindwa basi sisi tutachukua hatua za kisheria tunazozijua”alisema Maharagande

 Alisema kwamba wana tarifa za kutosha kwamba Chadema wamefanya vurugu za kutaka kuharibu mkutano wa hadhara wa chama chao unaotaraji kuhudhuriwa na mwenyekiti wake,Prof Ibrahim Lipumba sanjari na makamu mwa kwanza wa Rais Zanzibar,Maalim Seif Sharif Hamad .

 Alisema kwamba wao wamekuja Arusha kufanya kazi za siasa zikiwa ni pamoja na kujiandaa na uchaguzi wa madiwani,ubunge pamoja na kueneza será ya V4C iliyoasisiwa hivi karibuni.

 Hatahivyo,alisisitiza kwamba wao hawapendi kupambana na Chadema kwa kuwa hawana serikali huku akisisitiza kuwa kama ni fujo wanazijua lakini kwa sasa wanaeneza será na kama Chadema wakitaka kupambana nao wakashindane kwa hoja majukwaani.