Saturday, April 13, 2013

PADRI ALIYEOA KWA SIRI AFUNGWA JELA MIEZI 6

KUSHOTO: Padri William akimbusu mkewe, Beverley. KULIA: Kanisa la Mt. Clara ambamo Padri huyo alibambwa akifanya uchavu wake kwa binti wa miaka 17.

Padri mmoja wa kanisa Katoliki ambaye alifunga ndoa kwa siri amehukumiwa kifungo cha miezi sita jela jana kwa kumsumbua msichana mdogo kwa kile jaji alichoelezea 'uvunjifu mkubwa wa uaminifu'.

William Finnegan, akifahamika kama 'Fadha Bill', alimpapasa binti huyo mwenye miaka 17 chini na kulazimisha kumbusu kwa nguvu katika Kanisa Katoliki la Mt Clara mjini Bradford siku ya Jumapili ya Pasaka mwaka jana.

Jaji Roger Thomas alisema kwamba Padri huyo mwenye miaka 60, alikiri wakati wa kesi hiyo kwamba alifunga ndoa kwa siri miaka 14 iliyopita.
Pia alitumia maneno makali kwa wanaparokia wa Finnegan ambao walikuwa upande wake licha ya mashitaka hayo, akisema: "Pengine baadhi yao wanaweza kuamini kesho jua litachomoza magharibi kesho kama akisema hivyo."

MWENYEKITI WA CHADEMA ATUPWA JELA MWAKA MMOJA KWA WIZI WA MIL. 1.2

Mwenyekiti wa chadema, mtaa wa isamilo kaskazini B wilayani nyamagana Philbert Bulinjiye amehukumiwa kifungo cha mwaka mmoja jela kwa kosa la kujipatia shs milioni 1,250,000 kwa njia ya udanganyifu.

Hukumu hiyo, imetolewa na hakimu Vaineth Mahizi wa mahakama hiyo, kufuatia kesi ya jinai namba 196/2012, iliyofunguliwa na Vedasto Mavubhi ambaye alimtuhumu mwenyekiti huyo kuchukua kwake kiasi hicho cha fedha, kwa ajili ya kumuuzia kiwanja.

Hakimu Mahizi katika hukumu yake, alidai ameridhika na ushahidi uliotolewa na upnade wa mlalamikaji, mashahidi pamoja na wazee wa baraza hivyo kumhukumu mwenyekiti kwenda jela.

Alisema mwenyekiti huyo pamoja na Balozi Robert Byagaye wanastahili kutumikia kifungo hicho cha mwaka mmoja jela kutokana na kutiwa hatiani.

"kitendo kilichofanywa na viongozi hawa, kuwaibia raia wanaowaongoza kiutapeli kwa kuwadanganya kuwauzia kiwanja na kisha kutafuta mtu bandia kwa madai kuwa kiwanja hicho kiko katika mtaa wanaouongoza, ni udanganyifu" Alisema hakimu na kuongeza kuwa Mwenyekiti huyo amehukumiwa kifungo hicho ili iwe fundisho kwa viongozi wengine matapeli.

NYARAKA NZITO ZA CCM ZAVUJA...

Taarifa za ndani kabisa zilizopatikana kutoka kwa Waandishi wa habari,Vyombo vya usalama na ndani ya CCM kwenyewe zinaonyesha sakata la Kuteswa kwa Kibanda na kufunguliwa mashtaka ya ugaidi Mkurugenzi wa usalama wa Chadema ndugu Alfred Lwakatare linachukua sura mpya na mapya yamefichuka kwa ushahidi.

Dennis Msacky ambaye ni mhariri wa Mwananchi aliyehusishwa na kuwa mojawapo wa watu waliopangwa kutekwa,amekua akifanya mawasiliano na Ludovick Joseph Lwezaura kama ifuatavyo

Tarehe 27/12/2012: Dennis Msacky kupitia simu ya mkononi namba 07643310**  aliwasiliana kwa simu na Ludovick Joseph kupitia simu namba 07539271**  akiwa Tamal hotel,Mwenge jijini dar-Es Salaam. Hii ilikua siku moja kabla ya mkanda wa video uliowekwa youtube kurekodiwa.mkanda ulionyesha kuwa ulirekodiwa kesho yake yaani tarehe 28/12/2013

MWANAMKE MPUMBAVU HUIVUNJA NDOA YAKE MWENYEWE NA SERIKALI PUMBAVU HUBOMOA NCHI"... MH. SUGU

Wakati akichangia bajeti ya PM, Mh Mbilinyi ametumia lugha kali sana dhini ya serikali na Mwigulu Nchemba akazua ubishi mkubwa kati yake na Speaker..
Ameanza kwa kusema kuwa "Mwanamke mpumbavu huvunja nyumba yake mwenyewe" na hivyo hivyo serikali pumbavu hubomoa nchi.
Akiwa  na  jaziba  nyingi, Joseph Mbilinyi 'sugu' amemchanachana Mwigulu kuwa ni mpumbavu na kudai  kuwa anafanya dili alafu anatumia m-pesa...
Baada  ya  kumvaa  Mwigulu, Sugu  alimgeukia waziri wa elimu Mulugo na  kudai  kuwa ana elimu ya kuungaunga na ni chenga tupu...
Sugu  anadai  kushangazwa  na  tabia  ya  usalama  wa  taifa  kuifuatilia Chadema na kung'oa watu kucha na meno.
Pamoja na kukalishwa mara mbili na spika ili atumie lugha ya staha bado aliendelea

FASTJET YAKANUSHA KUNYANG'ANYWA LESENI YAKE YA BIASHARA TANZANIA

 Kampuni ya ndege ya Fast Jet imezikanusha ripoti kuwa imenyang’anywa leseni yake ya biashara katika nchi kadhaa barani Afrika ikiwemo Tanzania.Kupitia website yake kampuni hiyo imeandika:

Licha ya taarifa za leo kwenye vyombo vya habari, ni biashara kama kawaida hapa fastjet. Madai kuhusu kunyang’anywa leseni ni uongo mtupu. Tunaendelea na safari zetu kutoka Tanzania na tunaendelea kuanzisha safari mpya kama ilivyopangwa.

Hii ni njama/hujuma ‘binafsi’ dhidi ya fstjet katika jaribio wazi lililotengenezwa kuharibu brand na sifa ya Fastjet.Ofisi zetu na matawi yetu bado zipo wazi kwa booking mpya na hakuna refund zozote.

NAULI MPYA NCHINI SASA NI VURUGU TUPU

Viwango vipya vya nauli za daladala na mabasi yaendayo mikoani zimeanza kutumika jana, huku wananchi wakizipinga wakidai zinawaumiza zaidi kiuchumi.

Wakati baadhi wakilalamikia kupanda kwa nauli za dalala katika maeneo yao, baadhi ya wafanyakazi wa mabasi yaendayo mikoani wameendelea kutoza nauli ya zamani.

Zoezi la kupandisha nauli nchini lililoanza jana limewagawanya wamiliki wa magari na kufanya baadhi ya safari za mikoani kupandisha nauli, huku nyingine zikiendelea kuwa kama zamani wakati nauli za daladala Dar es salaam zikipanda kama ilivyoagizwa.

Hatua hiyo ya kupandisha nauli ilizua tafrani baina ya makondakta na abiria waliokuwa wakisafiri katika safari mbalimbali ndani ya jiji, hususan wale waliokuwa hawajui kuwa jana ndiyo siku ambapo nauli zilitakiwa kupanda.

KITENDO CHA KUWANYANG'ANYA ARDHI WANANCHI WA LOLIONDO CHAMCHANGANYA RAIS KIKWETE

Sakata la mgogoro unaorindima kwa sasa kuhusu unyang'anywaji wa Ardhi ya Loliondo kwa lengo la kumpa mwekezaji wa kiarabu umemvuruga sana Rais Kikwete na kusita kujitokeza hadharani kulitolea kauli.

Hapo awali Kupitia kikao cha baraza la mawaziri iliamriwa kuwa WAKAZI WA LOLIONDO WANYANG'ANYWE ENEO HILO na kumtuma Waziri wa Maliasili na Utalii Hamisi Kagasheki kwenda kulisimamia kwa nguvu zote....

HUU NDO UFISADI MKUBWA WA JOHN CHEYO CHINI YA "KOFIA YA BUNGE"

 John Momose Cheyo mwanasiasa wa siku nyingi ametumia cheo chake cha Uenyekiti wa Kamati ya PAC, kujinufaisha kupitia kampuni ya mdogo wake anayejulikana kwa jina la Sylvester Maghembe Cheyo ambaye anamiliki kampuni inayoitwa ATLAS PLUMBERS AND BUILDERS LTD.

Kwa kipindi ambacho Mheshimiwa Cheyo amekuwa Mwenyekiti wa Kamati hii ya Bunge kampuni ya ATLAS Plumbers amd Builders imepata miradi ifuatayo katika mashirika ya Serikali ambayo yapo chini ya Kamati iliyokuwa inaoongozwa na Bwana Mapesa.

Magazeti ya leo Ijumaa ya 13th April 2013