Monday, May 13, 2013

LADY JAYDEE AFIKISHWA MAHAKAMANI

                                                        Judith Wambura 'Lady Jaydee'.

MWANAMUZIKI Mahiri wa Bongo Fleva, Judith Wambura 'Lady Jaydee' leo alifika Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam kufuatia kufunguliwa kesi ya madai katika mahakama hiyo. Katika hati ya madai hayo, mwanamuziki huyo anashitakiwa na viongozi wa Clouds Media Group ambao ni Ruge Mutahaba na Joseph Kusaga. Tuhuma za kesi hiyo zinatarajiwa kusomwa mahakamani hapo na Hakimu, Athuman Nyamrani Mei 27 mwaka huu. Jaydee aliwasili mahakamani hapo akiwa na mumewe Gadner G. Habash mishale ya saa 6 mchana na kuongoza moja kwa moja chumba cha makarani wa mahakama hiyo ambao aliwakabidhi hati ya mashitaka hayo.

Magazeti ya leo Jumatatu ya 13rd May 2013




MATOKEO MABOVU YA KIDATO CHA NNE YATACHELEWESHA MATOKEO YA KIDATO CHA SITA

Matokeo ya mtihani wa kidato cha sita yaliyotarajiwa kutangazwa mwezi  huu yatachelewa  ili kutoa nafasi kwa Baraza la Mitihani la Taifa (Necta),  kurekebisha matokeo mabaya ya mitihani  kidato cha nne ya mwaka jana yaliyofutwa na serikali  mwezi huu.

Matokeo ya kidato cha sita ambayo huwa yanatangazwa mwanzoni  mwa mwezi Mei mpaka sasa hayajatolewa  na kwamba hayatatangazwa mpaka matokeo mapya ya kidato cha nne yatakaporekebishwa rasmi.

Alipoulizwa  juu ya suala hilo, Naibu Waziri   wa Elimu na  Mfunzo ya Ufundi  Philipo Mulugo alisema ingawa wakati huu ndio unaopaswa yatangazwe matokeo ya kidato cha sita haitafanyika hivyo hadi yatangazwe matokeo mapya ya kidato cha nne baada ya kufutwa.

TAARIFA MUHIMU KUHUSU AFYA YA MZEE SMALL

Kwa wote walioguswa na kuumwa kwa nguli wa sanaa za maigizo hapa nchini, Mzee Small, taarifa ni kuwa amepata nafuu na anatembea japo kwa fimbo ingawa mkono wake bado umelemaa.

Changamoto kubwa kwake ni dawa za kuchua, takribani 30,000/= kwa mwezi pamoja dawa za kusaidia kuyeyusha damu iligundulika kuganda kichwani mwake, takribani 50,000/= kwa mwezi pamoja na mengineyo madogo madogo, ANAWASHUKURU SANA WOTE MNAOGUSWA NA KUMJALI, Kwa msaada wowote tafadhali wasiliana na mkewe.

Angalizo; Bi Kidude aliteseka mno na hata nyumba aliyokuwa akiishi kwa muda mrefu ilikuwa pagale, na bila aibu alipofikwa na umauti, Rais wetu wa Serikali ya Mapinduzi aliongoza ujumbe wa Serikali na mengi mazuri yalisemwa juu ya nyota hii iliyoachwa ikaadhirika, NAULIZA TU HIVI MPAKA LINI?????????
By Matukio Chuma.