Wednesday, July 4, 2012

HAHAHAHAHAHAHAHAH................ AMKA,TUMERUDI KAZINI


RAIS KIKWETE AREJEA TOKA RWANDA NA BURUNDI

Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete wakiwasili Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam jana jioni
wakitokea Burundi na Rwanda walikohuidhuria sherehe za miaka 50 wa uhuru wa nchi hizo. Anayeongozana nao ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Saidi Mecky Sadik.
Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa na Inspekta Jenerali wa Polisi Afande Saidi Mwema na Mkuu wa Majeshi Jenerali Davies Mwamunyange baada ya kuwasili Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam jana jioni wakitokea Burundi na Rwanda walikohuidhuria sherehe za miaka 50 wa uhuru wa nchi hizo

PICHA NA IKULU

Banda la Wizara ya Fedha, lachukua ushindi wa pili kwenye Maonesho ya Sabasaba

Mchumi Mwandamizi wa Wizara ya Fedha, Idara ya Bajeti, Adam Msumule, akimpatia maelezo mwananchi aliyetembelea banda la wizara ya Fedha, kuhusu bejeti ya nchi, kwenye maonesho ya Biashara ya Kimataifa, viwanja vya J.K. Nyerere, barabara ya Kilwa, Dar es Salaam leo.
Baadhi ya wafanyakazi wa Wizara ya Fedha wanaotoa huduma ya kuwaelimisha wananchi kwenye banda la wizara hiyo, Viwanja vya Maonesho ya Biashara ya Kimataifa, wakipiga picha ya pamoja kwa ajili ya kumbukumbu ya maonesho hayo leo




Wananchi wakiingia kwenye banda la Wizara ya Fedha, leo kujionea na kupata huduma mbalimbali zitolewazo na wizara hiyo.

HIVI UMEMSIKIA KIPA SHABAN KADO ALICHOSEMA KUHUSU KURUDISHWA MTIBWA? UNAYAJUA MAONI YAKE KUHUSU KIPA MPYA YANGA ALIETOKA SIMBA?

                                           Kipa Shaban Kado kushoto mwenye jezi nyeusi
Kwa long time kidogo stori zimekua zikiandikwa kwenye magazeti, Radio na Tv kuhusu kipa wa Yanga Shaban Kado ambae club hiyo imetangaza kumrudisha kucheza kwa mkopo Mtibwa Sugar hivyo ikasajili kipa mwingine mpya ambae ni Bartez kutoka Simba.

Amesema “hizo taarifa nilianza kuzisikia kwenye vyombo vya habari bila mimi mwenyewe kuambiwa na uongozi lakini baadae nikafanya mawasiliano na boss wangu na sasa tuko kwenye mikakati ambayo ikikamilika ndio itajulikana Kado anakwenda wapi, inaweza kuwa sio Mtibwa”

Kuhusu Kurudi Mtibwa Kado amesema “kwa makubaliano ikitokea hivyo ninaweza kurudi kwa sababu ni timu yangu iliyonifanya kila mtu anasikia kuhusu Kado, sitakataa kurudi Mtibwa ila itategemea itahitajika nirudi vipi na kuhusu ishu ya mimi kuondolewa Yanga kuna sababu tu nazifaham ambazo baadae zitakuja kujulikana”

Kuhusu stori za kurudishwa Mtibwa kwa sababu kiwango chake cha uchezaji kimeshuka akiwa Yanga, Kado amesema  “katika mechi zote za Yanga nimepoteza mechi mbili au tatu, sasa utaniambiaje kiwango kimeshuka wakati kupoteza mechi ni kitu cha kawaida tu”

Kado ambae ni mmoja kati  ya wachezaji wa kibongo wanaotumia sana mtandao wa kijamii wa facebook amekubali kuzungumzia ishu za yeye kuhamia kwenye club nyingine ikiwemoa Simba ambayo inadaiwa kumuita kwa ajili ya kumpa mkataba.

Katika sentensi nyingine Kado amesema mpaka sasa hayuko tayari kuzungumza ni timu gani atakayokwenda kuichezea baada ya Yanga lakini amethibitisha kwamba kuna uwezekano akarudi Mtibwa au timu nyingine yoyote.

 Chanzo: millardayo.com

MKE MJAMZITO WA GAEL GLICHY NDIO HUYU.

Baada ya Mario Balotelli kutangaza kwamba anatarajia kupata mtoto na demu wake Raffaella, leo Gael Glichy amejitokeza mitaani na mkewe wake Charlene Guric ambaye sasa imegundulika ni mjamzito wa miezi minne.

Clichy na mkewe Charlene walionekana wakitembea kwenye maduka ya St.Lopez wakifanya manunuzi ya vitu mbalimbali siku mbili baada ya mchezaji mwenzie wa Manchester City Mario Balotelli na mchumba Modo Raffaella kutangaza kwamba wanatarajia kupata mtoto.

Inaonekana wachezaji wa City wamepania kutengeneza timu nyingine ya watoto wao sasa.

HUYU NDIO MISS DAR INDIAN OCEAN 2012, NA HII NI SEHEMU YA MAGUMU ALIYOYAPITIA.



                                                     Diana Hussein Miss Dar Indian Ocean 2012.
Kuna asilimia kubwa ya mastaa au watu maarufu unaowapenda au kuwafaham kupitia  TV, Magazeti, radio na internet lakini umaarufu walionao haujaja kirahisi.

Stori nyingi sana za mastaa kusikia alikoanzia, na ni mbali wengi sana wametoa jasho debe kufikia walipo mtu kama Sean Kingston ambae aliwahi kuja bongo kwenye KTMA aliwahi kufanya kazi ya kukata nyasi kwenye garden za watasha ili mwisho wa day zipatikane dola kwa ajili ya kula, nakumbuka mwaka jana aliandika kwenye twitter kwamba kazi ya kuwa msimamizi wa garnen aliichukia sana.

Tukirudi home bongo, wako mastaa kibao wameanza kwa kusota sana… au kupitia kwenye mambo magumu ya maisha pia akiwemo binti mrembo ambae juzi juzi ndio alivishwa taji la miss Dar Indian ocean Diana Hussein,  ni mrembo lakini mwenye makovu mengi ya kimaisha yasioyoonekana kwenye ngozi yake nzuri, ameanza kufanya kazi miaka mitatu iliyopita akiwa na umri wa miaka 17 tu kazi ambazo hakuzipenda kabisa lakini alifanya hivyo kwa sababu ya maisha.

Baada ya kukosa ada ya kuendelea na masomo ya sekondari ilibidi Diana aje Dar akitokea Tanga na kuanza kazi yake ya kwanza ya kuajiriwa kwenye duka la dawa, aliifanya hiyo kazi kwa mwaka mmoja na baadae huku akiwa na machungu ya kuisaidia familia yake kiuwezo aliamua kutafuta kibarua kingine na akafanikiwa kuwa mkaribisha wageni kwenye kampuni moja Dar es salaam, kazi zote hizo alizifanya lakini hakuwahi kuzipenda kabisa.

Japo bado hajatimiza ndoto zake lakini amefikia kwenye hatua ya kuridhisha baada ya kuacha kazi za kuajiriwa mwaka huu na kuanzisha biashara yake ya kuuza vitu vya warembo wenzake, kama mikufu, perfume na vingine…. huku mawazo yake yakimpa msukumo wa kufanya vizuri zaidi kwenye mashindano yanayofata ya juu zaidi.

Magazeti Ya Leo Jumatano 4th July 2012