Thursday, May 9, 2013

Magazeti ya 9th May 2013




MTOTO WA MIAKA 9 AUAWA KWA KUPIGWA RISASI NA POLISI HUKO TARIME

Polisi mkoani Tarime wameua mtoto wa miaka 9, Deo Yakob, katika kilichoripotiwa kuwa pilikapilika za kukamata majambazi wanaoiba na kuua watu mpakani mwa Tanzania na Kenya.

Bado hakuna maelezo zaidi, kuhusu ni kitu kani kilichopelekea mtoto huyo kuuawa katika juhudi za polisi kukamata majambazi hayo. Pia haijafahamika kama polisi hao walifanikiwa  kuwakamata majambazi...

Pichani ni wananchi wakiwa na mwili wa mtoto huyo ambaye alikua ni mwanafunzi wa darasa la tatu katika shule ya msingi ya Mturu, mjini Tarime.

Mlipuko wa Kanisani Arusha: saba wapelekwa dar kwa matibabu zaidi

 Wagonjwa saba ambao ni majeruhi wa mlipuko wa bomu kwenye kanisa la Joseph Mfanyakazi eneo la Olasiti jijini Arusha wamehamishiwa kwenye Hospitali za Muhimbili na LUgalo jijini Dar es Salaam.

Majeruhi hao wamesafirishwa mchana majira ya saa tisa kwa ndege ya shirika la Hifadhi za taifa (TANAPA) kwenda kuendelea na matibabu zaidi baada ya hali zao kuonekana bado zinahitaji vifaa vyenye uwezo wa hali ya juu.

Miongoni mwa walisafirishwa wapo watoto watatu wakike wawili na wakiume mmoja huu wakina mama walisafirishwa wakiwa wawili na kinababa wawili ambao hali zao bado mbaya licha ya matibabu walikuwa wakiyapata tokea juzi.

Wasamaria wema kutoka makampuni mbali mbali wameendelea kutoa misaada mbali mbali ya hali na mali ikiwemo madawa na vifaa tiba na mablanketi na mashuka,na Magodoro iliviisaidie hospitali za Mt.Meru na St,Elizabeth.

SERIKALI YAPIGA MARUFUKU MIKUTANO YA DINI YENYE "VIRUSI" VYA UCHOCHEZI

Waziri wa MAmbo ya Ndani ya NChi, EMmanuel NChimbi, ameliagiza jeshi la polisi kuanzia IGP, RPC, OCD na OCS kuwachukulia hatua wale wote wanaoendesha mihadhara ya kidini yenye kuchochea vurugu na mifarakano katika jamii. ...

Nchimbi amesema kuwa kiongozi yeyote ambaye atabainika kutochukua hatua licha ya taarifa kuripotiwa kwake basi atakwenda na maji.. ...

Kauli  hiyo  ameitoa   jijini dar es salaam jana wakati akiongea na wawakilishi wa viongozi wa dini na vyombo jeshi la polisi mkoa wa dar es salaam

Waziri Nchimbi amewatahadhalisha vijana wanaoshinda kwenye mitandao na wanaotumia simu kutuma ujumbe wenye lengo la kuhamasisha chuki za kidini. Amesema kuwa kuanzia sasa serikali itachukua hatua   stahiki

Chanzo: taarifa  ya  habari ya TBC1

BRAKING NEWS: SHEIKH PONDA AHUKUMIWA KIFUNGO CHA MWAKA MMOJA CHA NJE

 Makahama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar Es Salaam leo  imemuhukumu Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda kifungo cha nje cha mwaka mmoja, huku washtakiwa wengine wote 49 wakiachiwa huru