Monday, April 15, 2013

MECHI YA AZAM, SIMBA YAINGIZA MIL 66/-


Na Boniface Wambura, TFF

Mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Azam na Simba iliyochezwa jana (Aprili 14 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam imeingiza sh. 66,855,000 kutokana na watazamaji 11,458.

Viingilio katika mechi hiyo namba 155 iliyomalizika kwa timu hizo kutoka sare ya mabao 2-2 vilikuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 huku kila klabu ikipata mgawo wa sh. 15,587,177.45 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 10,198,220.34.

Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 7,925,683.45, tiketi sh. 3,818,890, gharama za mechi sh. 4,755,410.07, Kamati ya Ligi sh. 4,755,410.07, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 2,377,705.03 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 1,849,326.14.

 WATAZAMAJI 11,021 WAZISHUHUDIA YANGA, OLJORO

Magazeti ya leo Jumatatu ya 15th April 2013






ZITTO KABWE AIKANA NAMBA YAKE YA SIMU LIVE BAADA YA CHADEMA WENZAKE KUDAI NI GAIDI NA ACHUNGUZWE

 Sasa  nashawishika  kuamini  kuwa  CHADEMA  wana  lao  juu  ya  mipango  ya  kigaidi...

Jana  Mabere  marando  alitoa  tamko refu  sana   lenye  namba  za  simu  kibao  za  watu  mashuhuri  akitaka  mahakama  ichunguze  simu  zao  ikiwemo  ya  Zitto  Kabwe.....

SWALI  LA  KUJIULIZA:

-Kwanini Mabere Marando anatoa tamko muhimu kama hili bila kuhussisha viongozi wa juu kama Zitto?

-Matamko ya nini wakati kesi iko mahakamani?

-Kwanini chadema inaendelea kulizungumzia hili swala nje ya mahakama huku wanaharakati wa chadema kama Mwanakijiji wakiwa wameshaanzisha harakati za kutaka kesi ifutwe kwa swala kuzungumziwa nje ya mahakama?

 HUU  NI  UJUMBE  WA  ZITTO  AKIKANUSHA  KUHUSIKA  NA  UGAIDI

 ( HAPA  AMEANZA  KWA  KUNUKUU  SEHEMU  YA RIPOTI  YA MABERE:)

UGOMVI WA CHADEMA NA CCM WAFIKIA PABAYA......MABERE MARANDO AYAANIKANI MAWASILIANO NYETI YA VIONGOZI WA CCM

TAMKO LA CHADEMA KUHUSU NJAMA ZA KUKICHAFUA ZINAZOFANYWA NA GENGE LA VIONGOZI WAKUU WA CCM NA VYOMBO VYA DOLA, LIMETOLEWA JIJINI DAR ES SALAAM LEO, MACHI 14, 2013 NA MJUMBE WA KAMATI KUU NA MWANASHERIA WA CHAMA, MH. MABERE NYAUCHO MARANDO

Ndugu waandishi wa habari;
LEO tumewaita hapa ili kuwaomba mtufikishie ujumbe kwa Watanzania, kwamba nikiwa mwanasheria na mtu ambaye nimepata ujuzi wa kazi za ushushu, nimefanya uchunguzi matukio haya ya utekaji na utesaji na kugundua mambo mengi mno.

Uchunguzi huu nimeufanya kabla na baada ya kukamatwa kwa Mkurugenzi wetu wa Ulinzi na Usalama, Willifred Muganyizi Lwakatare, ambaye hivi sasa anashitakiwa mahakamani kwa tuhuma za kupanga ugaidi.

Nimefanya hivyo kwa kuangalia maslahi mapana ya taifa langu na chama changu. Katika uchunguzi wangu huo, nimegundua mambo mengi ikiwamo kuwapo kwa genge la watu ndani ya serikali na Chama Cha Mapinduzi (CCM), wanaopanga mipango hii ya kishetani na kisha kuwasingizia watu wengine.

Angalieni mfano huu: Unaoitwa na polisi na Mwigulu Nchemba, “mkanda wa Lwakatare” unadaiwa uliwasilishwa jeshi la polisi Desemba mwaka jana. Lakini jeshi hilo halikumkamata yoyote wala kumhoji, hadi pale Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri, Absalom Kibanda, alipovamiwa na kuumizwa.

KAULI YA MJENGWA BAADA YA KUKAMATWA NA POLISI MAKAO MAKUU KUHUSU KUTEKWA KWA KIBANDA

Ndugu zangu,
Kama alivyowataarifu kaka yangu Nyaroonyo Kichehere, ni kuwa, jana Jumamosi nilikuwa Makao Makuu ya Jeshi la Polisi kuanzia saa tano asubuhi ya jana mpaka saa tatu usiku. Ilihusu mahojiano ya Polisi na mimi kuhusiana na sakata la ndugu yetu Absalom Kibanda.

Ukweli sikukamatwa mahali popote, bali niliitwa na Kamishna ( Upelelezi) Advocate Nyombi. Alhamisi nikiwa Iringa, tukakubaliana na kiungwana na Kamishna Nyombi kuwa nifike Makao Makuu hayo ya polisi Jumamosi saa tano. Ikawa hivyo.

Hapo nilipokelewa na Kamishna Nyombi. Baada ya mazungumzo mafupi ndipo akawaita maofisa wengine watano wa Upepelezi kufanya mahojiano nami.

Niliomba niwe na Mwanasheria, nikakubaliwa. Nilimpigia simu kaka yangu Nyaroonyo, naye, kwa vile ni Wakili pia wa Kibanda akanisaidia kuhakikisha napata wakili mwingine. Pamoja na kuwa ilikuwa ni Jumamosi, ndugu yangu Nyaroonyo Kichehere alifanya alivyoweza.

Ndani ya dakika 40 hivi alifika chumba nr 704 ghorofa ya saba akiwa na Wakili Jacquiline Rweyongeza na Legal Officer Dickson Mbonde. Nilimshukuru Kaka Nyaroonyo Kichehere. Na nilimuaga kwa kumwambia; “ Nenda ukaifahamishe jamii juu ya hiki kilichonitokea”.

Nachukua fursa hii pia kuwashukuru kwa dhati kabisa dada yangu Wakili Jacquiline Rweyongeza na kaka Dickson Mbonde kwa kuacha yote ya Jumamosi na kuwa tayari kuwa msaada kwangu.

Jacquiline alimuacha nyumbani mtoto wake wa miezi minne kwa ajili ya suala langu. Sina namna nyingine ya kumshukuru. Na hakika, msaada wao niliuhitaji sana.

Nawashukuru pia kwa dhati kabisa, ndugu zangu Saed Kubenea, Mbaraka Islam na wengine wote waliokuwa na utayari wa kunisaidia pale msaada wao ulipohitajika.

Kwa ufupi, nimetoa maelezo yangu bila shuruti wala kutishwa.

Na nimeweka wazi kuwa yanaweza kutumika Mahakamani kama yatahitajika au hata kama mimi nitahitajika, kwa namna yeyote ile.

Kesho saa mbili asubuhi nitaripoti Makao Makuu ya Polisi kupewa maelezo ya kitakachofuatia.Kwa mara nyingine tena, nawashukuru sana kwa kuwa nami katika muda wote huuMaggid,
Dar es Salaam.

MAJID MJENGWA NAYE AKAMATWA NA POLISI AKIHUSISHWA NA SAKATA LA KIBANDA

                                                                        Majid Mjengwa.
  MWANDISHI wa safu katika magazeti mbalimbali nchini, Majid Mjengwa amekamatwa na polisi kwa tuhuma za kuhusika na tukio la kushambuliwa kwa Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Absalom Kibanda.

Habari zilizoufikia mtandao huu jana mchana na baadaye kuthibitishwa na polisi zinasema Mjengwa alikamatwa muda wa asubuhi na kwamba alikuwa akihojiwa na makachero wa jeshi hilo hadi alasiri kuhusu tukio la kuteswa kwa Kibanda.

Msemaji Mkuu wa Polisi Advera Senso alisema kwamba:

“Ni kweli kwamba tunaye, tunaendelea kumhoji, tunachoomba ni kwamba mtupe nafasi ili tufanye kazi yetu na kukiwa na jambo lolote tutawajulisha.”

PICHA ZA MABAKI YA NDEGE ILIYODONDOKA JANA JIJINI ARUSHA



Eneo ambalo ndege iliyoanguka, kutoka eneo hilo mpaka landing truck ni kama 1km. Mbele ya mabaki hayo ya ndege kuna mti mmoja ambao unasadikiwa kuwa  ndege hiyo ilijigonga na kudondoka chini.

MBOWE AMKAANGA ZITO KABWE...ADAI KUWA LWAKATARE HATOFUKUZWA CHADEMA HATA KAMA NI GAIDI

 Katika hali ya kushitua,Mh.Mbowe akiongea na wanachama wa chadema leo Ubungo plaza amemkaanga  Zitto  kabwe  na  kudai  kuwa  chadema  haiko  tayari  kumtimua  Lwakatare  katika  chama  hata  kama  ni  gaidi....

"Eti nashangaa kuna watu wanataka CHADEMA kimuache Lwakatare na kumsimamisha uongozi kwa uzushi uliopandikizwa na CCM, Hilo halitafanyika"- alisema Mbowe.

IKUMBUKWE siku chache zilizopita naibu katibu Mkuu wa CHADEMA Mh. Zitto Kabwe alitoa mapendekezo ya kuomba Mshitakiwa mkuu kwenye kesi ya Ugaidi ambaye ni Ndugu Lwakatare aliyekuwa mkuu wa usalama wa chadema awajibike kisiasa...
 Kuwajibika kisiasa ni pamoja na kuachia ngazi ya ukurugenzi wa usalama ili kupisha uchunguzi salama na kukiacha chama salama.